Super stars wa bongo land

Hakuna Super star hata m1 kati ya uliowataja!!!!! Superstar gani anakula kwa mama ntilie? Super star gani anaendesha gari la Toyota? Super star gani akitembea mfukoni hana zaidi ya elfu 15?(Hasheem ashawahi kumsaidia adam mchomvu pale mlimani alimpa elfu 15 tu wakati adamu alikuwa anadaiwa zaidi ya hiyo hahahaha),super star gani hana hata nyumba ya kukaaa? yes namaanisha nyumba na si banda? wote hao ni waganga njaa tu!!! SUperstar gani ana bishara ya daladala??(AY ana daladala mbili hahahahaha) WOTE NI WAGANGA NJAAAA TUUUU..
Mkuu kama unazungumzia pesa nadhani utakuwa hujamtendea haki Hasheem Thabeet wa Houston Rockets maana hakuna mwananmichezo au mwanamuziki yeyote katika Africa mashariki na kati anaye-mzidi kwa fedha anazopata. Mshahara wake kwa mwaka ni karibia Tsh billioni 6 (zaidi ya dola za kimarekani million 4.7) kwa mwakaAngalia link hii hapa chini inayoonyesha wanamichezo wanaolipwa zaidi kwa kila nchi:ESPN The Magazine - The Money Issue - The best-paid athletes from 182 countries - ESPN
 
super stars wangu ni hawa
nyerere...anajulikana na kila mtanzania, hata mwenye miaka saba anamfahamu huyu kwa mazuri
filbert bayi na suleimani nyambui...walitupaisha katika riadha si mchezo miaka ileeee
mzee mwanakijiji...michango yake si mchezo...ni raia wa kawaida lakini yuko midomoni hata mwa wanasiasa wakubwa, kutokana na umakini wa hoja zake

kwenye burudani kina ay, jd hawana tofauti na wenzao wote kina chid benz, mabeste, ray c, prof jay etc...wote wana umaarufu wa vipindi, yaani kuna muda huwa hawasikiki na kuna nyakati wanasikika
huyo hashim thabeet kweli kafanikiwa kuingia NBA, that is all, huku nyumbani si maarufu kama unavo taka kutuaminisha, zaidi ni maarufu dar es salaam na baadhi ya miji mikubwa na maredioni, huku mawilayani hell no hajulikani kabisaaaa

Kuwaita Nyerere na Mzee mwanakijiji kuwa ni super star ni kuwashushia hadhi kwa kiwango cha juu sana, inabidi uombe radhi, Nyerere..Nyerere unamwita super star muasisi wa Taifa hili sasa anaitwa super star kweli tunafikiri kwa kutumia masaburi. kwa hiyo basi Nelson Mandela ni super star, Obote super star, kenyata super star, Saed Kubenea super star, crap
 
kibongo bongo superstar ni yule akiingia maeneo full kutupiwa macho kwa shobo za raia,kama yupo facebook watabe wengi humtumia friend request na akiaccept hao makiza husikia raha,kama ni mwanaume vicheche wakimuona full shobo....kwa tafsiri hii bongo kuna masuperstar wengi sana si hao tu!
 
Back
Top Bottom