Lucchese DeCavalcante
JF-Expert Member
- Jan 10, 2009
- 5,471
- 734
Msemaji wa kampuni ya Frontline inayoendesha mchezo wa SUPA PESA, Nancy Sumari (kulia) akiongea na wanahabari wakati wa uzinduzi wa Bahati Nasibu mpya ya SUPA PESA iliyozinduliwa leo Jumatatu katika Hoteli ya Sea Cliff jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Bahati Nasibu hiyo, Harm Fourie.
KAMPUNI mpya ya SUPA PESA leo imezindua Bahati Nasibu mpya iitwayo Supa PESA ambayo watumiaji wa mitandao ya Tigo, Zantel, Vodacom na Zain watatakiwa kutuma neno SUPA kwenda 155777 ambapo mshindi wa wiki atajinyakulia kitita cha shilingi milioni kumi (10,000,000/=). Kila Ujumbe utatozwa shilingi mia tano (500).
Mwandishi wa Kampuni ya Global Publishers, Issa Mnally (kulia) akikabidhiwa shilingi laki moja (100,000/=) na Mkurugenzi wa SUPA PESA, baada ya kujishindia kwenye droo ndogo iliyochezeshwa kwenye uzinduzi huo.
HIZI BAHATI NASIBU MIE NAONA NI WIZI MTUPU KAMA ILE YA VODACOM SHINDA MKOKO NYIE MWASEMAJE?