Sumaye: Ukitumia kalamu kuingia Ikulu, utatumia risasi kung'ang'ania huko

Salaam wadau!

Matukio ya kutumia mabavu kwa wananchi

na vyombo vya dola kuhusika na mauaji ya raia

imenikumbusha kauli hiyo hapo iliyotolewa

na Waziri Mkuu F. Sumaye wakati wa mchakato

wa kutafuta mgombea wa CCM mwaka 2005

Serikali dhalimu huwa na tabia za kidhalimu kwa

wananchi wake.
 
Takribani kila baada ya miezi minne kunatukio kubwa linalogusa utawala huu wa awamu ya nne
 
Hii hi dhahiri kuna walakini katika uhalali wake

Dhuluma nyingi inapotendeka mafanikio au maendeleo huwa haba
 
JK angekuwa ni mtu wa kusoma alama za nyakati, angejiondoa tu kwenye kinyang'anyiro cha uraisi.
Hakuna haja ya kubaki madarakani kwa mtutu wa bunduki.

I agree. Naamini mwisho wa JK utakuwa mbaya sana tena sana zaidi ya ubaya aliowafanyia wenzake- Including Dr. Ulimboka
 
Wana jf habari;
nimejaribu kutafakari maneno ya waziri mkuu mstaafu mh.fredrick t.sumaye aliyosasema wakati wa kinyang'anyilo cha urais mwaka 2005 naona dalili zote za kutimia maneno yake alisema "anayefagia njia ya kwenda ikulu kwa kalamu na karatasi basi akifika huko atatumia risasi ili aweze kutawala"maneno haya aliyasema mzee sumaye baada ya kuchafuliwa na genge la wanamtandao ambalo lilikuwa linaongozwa na ;
  1. jakaya m.kikwete
  2. edward n.lowasa
  3. emmanuel nchimbi
  4. rostam azizi n.k

sumaye baada ya kuona anaandamwa sana na kashfa ambazo hazina kichwa wala miguu ilibidi aweke kumbukumbu kwa kutamka maneno hayo sasa toka wakati huo kumbukumbu zangu zinanionyesha yafuatayo yametokea;
  1. mauji ya wafuasi wa cdm arusha.
  2. kumwagiwa tindikali saed kubenea
  3. kuwekewa sumu dr,mwakyembe
  4. mauji ya songea
  5. mauji ya morogoro
  6. mauji ya daud mwangosi
  7. kutekwa kwa dr.ulimboka
  8. kuuwawa kwa padre evarist mushi
  9. kutekwa kwa absalom kiband n.k (ongeza matukio mengine ambayo yamesaulika hapa)
""je unazungumziaje maneno ya mh.sumaye na wakati huu ambao kumeibuka mtindo wakuteka waandishi wa habari na kuwang'oa kucha na meno bila ganzi"" karibu tujadili
 
Huu ni ujumbe mzito nitaufikisha mpaka kijijini kwetu ambako digitali haijafika wala analogia haikukanyaga hivyo wako gizani.
NAKUPENDA TANZANIA ILA WALAFI CCM WAMEKUBAKIZA FUVU inauma sana.
Nashukuru mkuu kwa uzi huu we are here to make history.
 
Yana ukweli lakini ni mazito sana. Mimi sijaamini sana kama serikali inahusika moja kwa moja na matukio yote haya. Wenye nchi wanapitia humu watatupa uhakika wa haya mambo.
 
Sumaye alikuwa ni kiongozi mwenye taswira ya mbali na muono wa taifa ya baadaye!Alichafuliwa lakini kakaa kimya hata hafunui kinywa chake kuongelea yanayotokea nchini!Nagu naye kamchafua nyumbani but amekaa zake kimya!hakika haya maneno tutayakumbuka maana yana ujumbe mzito!Uongozi wake ulitukuka siyo km hawa legelege wasiokuwa na misimamo na utekelezaji wa vitu wanavyoviongea!
 
Yana ukweli lakini ni mazito sana. Mimi sijaamini sana kama serikali inahusika moja kwa moja na matukio yote haya. Wenye nchi wanapitia humu watatupa uhakika wa haya mambo.
e

Hata kama wangehusika moja kwa moja huku wakijua hawawezi kukubali. Vinginevyo watakuwa wametangaza mapinduzi ya aina yake.

Lakini kwa vyoyote vile hata wakikataa hawawezi kuufuta ukweli kwamba yote haya ni matokeo ya udhaifu wa seriali vinavyopelekea vyombo vyake vya usalama kutokufanya kazi ama kwa makusudi ama kwa uwezo mdogo. Bado serikali haina njia ya kukwepa lawama katika hali hii.
 
Once yr a bushman, you will never change. point yako haina mshiko. Mchonganishi mkubwa wewe.
Mwenzio kasema karibu tujadiri.... Sasa wewe hapo ndo umejadiri nini? Halafu what is the defn ya bushman kwako? Maana kwangu mimi bushman ni mtu yeyote anayetoka nje ya mada pale anapotakiwa kuchangia mada.

BAck to the topic, Maneno ya Sumaye ni makubwa sana, lakini najuwa watu wengi hawtaliona hili hadi yatokee mengine... NYERERE ALISHAWAHI KUSEMA KUHUSU DHAMBI YA UBAGUZI, EIDHA KWA KUMTAZAMA MWENZIO NI BUSHMAN NA WEWE NI TOWNMAN, SIKU HAO UNAOWAONA KUWA NI MABUSHMAN WATAKAPOISHA, UTATAFUTA NAMNA YA KUWATENGA HAO WATTOWN WENZIO.

SASA YA UTENGANO NDO TUSHAANZA NAYO, WAZANZIBAR NA WAZANZIBARA, TUKISHATENGANA HATUTAKUWA SALAMA TENA. TUTAANZA WAPEMBA NA WAUNGUJA... n.k. Hivyo basi maneno ya Sumaye yatafuata mtindo huo..Kama ilivyokuwa kwa Nyerere, hatukuliona alilolisema kwa wakati ule, lakini sasa hali ndo hiyo... TUSUBIRI YA SUMAYE NAYO TUTAYAONA KAMA HAYA YANAYOTOKEA SASA HATUONI KAMA YANATOSHA KUWA KIELELEZO CHA ALIYOYASEMA
 
Yana ukweli lakini ni mazito sana. Mimi sijaamini sana kama serikali inahusika moja kwa moja na matukio yote haya. Wenye nchi wanapitia humu watatupa uhakika wa haya mambo.

Mkuu ni vyema ukafahamu serikali ya nchi yoyote ile ina mkono mrefu sana; kwa mfano nchini Tnzania kuna Usalama wa Taifa (UWT), Jeshi la wananchi (JWTZ), Polisi, Askari magereza, na mashushu kibao, amini usiamini hata hapo ulipo wapo.

Hivyo basi likitokea tukio linalo husiana na kutoa uhai wa binadamu, kisha wahusika wasifahamike na kuchukuliwa hatua stahiki, hamna haja ya kusumbua kichwa chako, kwani mhusika mkuu atakuwa ni serikali. Jiulize kwa nini wahusika waliochomoa uhai wa kamanda Barlow walitiwa mbaroni ndani ya siku mbili baada ya tukio? kwa nini isiwe vivyo hivyo kwa matukio mengine yanayo fanana na hayo? Je ulisoma makala ya Kubenea kuhusiana na sakata la kutekwa na kuteswa kwa Dk. Ulimboka? Je kwa nini Ramadhani Ighondu ambaye alitajwa na Dk. Ulimboka mwenyewe hakamatiki?

Mkuu in short maswali ni mengi sana kuliko majibu.
 
Once yr a bushman, you will never change. point yako haina mshiko. Mchonganishi mkubwa wewe.

kakuchonganisha na nani, (uchochezi, uhaini, kuhatarisha amani ya nchi ni verified vichaka vya maficho ya ccm)
 
Wana jf habari;
nimejaribu kutafakari maneno ya waziri mkuu mstaafu mh.fredrick t.sumaye aliyosasema wakati wa kinyang'anyilo cha urais mwaka 2005 naona dalili zote za kutimia maneno yake alisema "anayefagia njia ya kwenda ikulu kwa kalamu na karatasi basi akifika huko atatumia risasi ili aweze kutawala"maneno haya aliyasema mzee sumaye baada ya kuchafuliwa na genge la wanamtandao ambalo lilikuwa linaongozwa na ;
  1. jakaya m.kikwete
  2. edward n.lowasa
  3. emmanuel nchimbi
  4. rostam azizi n.k

sumaye baada ya kuona anaandamwa sana na kashfa ambazo hazina kichwa wala miguu ilibidi aweke kumbukumbu kwa kutamka maneno hayo sasa toka wakati huo kumbukumbu zangu zinanionyesha yafuatayo yametokea;
  1. mauji ya wafuasi wa cdm arusha.
  2. kumwagiwa tindikali saed kubenea
  3. kuwekewa sumu dr,mwakyembe
  4. mauji ya songea
  5. mauji ya morogoro
  6. mauji ya daud mwangosi
  7. kutekwa kwa dr.ulimboka
  8. kuuwawa kwa padre evarist mushi
  9. kutekwa kwa absalom kiband n.k (ongeza matukio mengine ambayo yamesaulika hapa)
""je unazungumziaje maneno ya mh.sumaye na wakati huu ambao kumeibuka mtindo wakuteka waandishi wa habari na kuwang'oa kucha na meno bila ganzi"" karibu tujadili

Japo wengi tunamlaumu Mh Rais kwa kukaa kimya muda mrefu linapotoke jambo nikitofautisha na Ally Hassan Mwinyi (Rais Mstaafu), Mh Benjamin W Mkapa (Rais Mstaafu na yule Muasisi wetu Mh. Dr. Julius K. Nyerere,
Hoja yako ya kumshutumu moja kwa moja Rais Kikwete, nakaa pembeni siungi mkono. Inawezekana ni watendaji wake wanayakoroga mambo haya, tafakari, chukua hatua.

Ushauri wangu kwa Mh. Rais, japo si jambo jema wewe kama Mh. Rais kufanya kazi kwa kuombwa na vyombo vya mawasiliano, mimi nakushauri tu kwamba inapotokea jambo uwe unatoa TAMKO MAPEMA usisubiri mwisho wa mwezi, maana wakati mwingine tukio linatokea tarehe 2 ya mwezi kukaa na jambo hadi tarehe 31 inakuwa inatia wasi wasi.
 
Mkuu ni vyema ukafahamu serikali ya nchi yoyote ile ina mkono mrefu sana; kwa mfano nchini Tnzania kuna Usalama wa Taifa (UWT), Jeshi la wananchi (JWTZ), Polisi, Askari magereza, na mashushu kibao, amini usiamini hata hapo ulipo wapo.

Hivyo basi likitokea tukio linalo husiana na kutoa uhai wa binadamu, kisha wahusika wasifahamike na kuchukuliwa hatua stahiki, hamna haja ya kusumbua kichwa chako, kwani mhusika mkuu atakuwa ni serikali. Jiulize kwa nini wahusika waliochomoa uhai wa kamanda Barlow walitiwa mbaroni ndani ya siku mbili baada ya tukio? kwa nini isiwe vivyo hivyo kwa matukio mengine yanayo fanana na hayo? Je ulisoma makala ya Kubenea kuhusiana na sakata la kutekwa na kuteswa kwa Dk. Ulimboka? Je kwa nini Ramadhani Ighondu ambaye alitajwa na Dk. Ulimboka mwenyewe hakamatiki?

Mkuu in short maswali ni mengi sana kuliko majibu.
Mkuu, kuna watu huwa hawaamini kwa common reasoning, eidha kwa makusudi au kwa kutoelewa mambo, yaani hadi na yeye awe muhanga wa tukio kama hilo ndo ataamini.
 
Japo wengi tunamlaumu Mh Rais kwa kukaa kimya muda mrefu linapotoke jambo nikitofautisha na Ally Hassan Mwinyi (Rais Mstaafu), Mh Benjamin W Mkapa (Rais Mstaafu na yule Muasisi wetu Mh. Dr. Julius K. Nyerere,
Hoja yako ya kumshutumu moja kwa moja Rais Kikwete, nakaa pembeni siungi mkono. Inawezekana ni watendaji wake wanayakoroga mambo haya, tafakari, chukua hatua.

Ushauri wangu kwa Mh. Rais, japo si jambo jema wewe kama Mh. Rais kufanya kazi kwa kuombwa na vyombo vya mawasiliano, mimi nakushauri tu kwamba inapotokea jambo uwe unatoa TAMKO MAPEMA usisubiri mwisho wa mwezi, maana wakati mwingine tukio linatokea tarehe 2 ya mwezi kukaa na jambo hadi tarehe 31 inakuwa inatia wasi wasi.
Kwenye bold, HIVI UKIHARIBU OFISI, ANAYETAKIWA KUKUPA ADHABU NI NANI KAMA SI BOSI WAKO AU HR? Sasa kama HR kimya, bosi wako kimya na wewe ndo unaendelea kuharibu, wengine tusemeje wakati uharibifu wako unatuumiza wengine ?? KWENYE KUMTETEA YES TUMTETEE... PINDA ALISHAWAHI KUSEMA, KAMA INGEKUWA NI UWEZO WAKE ANGEMFAYA MTU FULANI HIVI WAKATI RAIS AKIWA AFRIKA KUSINI LAKINI ALISHINDWA KWA SABABU MWENYE MADARAKA YALE ALIKUWA RAISI ... Usimtetee, hapo anaonyesha udhaifu
 
Back
Top Bottom