Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 16,559
- 41,078
Majukumu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzanua, na maheshi mengune yote, yameainishwa kisheria.
Ni Amiri Jeshi Mkuu pekee ndiye anaweza kulielekeza Jeshi la Wananchi wa Tanzania kufanya shughuli nyingine nje ya shughuli ya msingi, kama kuna dharula, na anaona kuna haja ya kufanya hivyo. Mamlaka hayo anayo Amiri Jeshi Mkuu, siyo Chalamila wala Mkuu wa Mkoa mwingine yeyote. Wakuu wa mikoa kuwa wenyeviti wa kamati za Ulinzi na usalama mikoani mwao, haimaanishi wamekuwa wakuu wa majeshi yote yaliyopo mikoani mwao.
Tusiwafanye askari wa JWTZ kuwa ni watu wa kupewa amri na kila mtu. Tukiruhusu upuuzi wa namna hiyo kuendelea, kuna siku Wakuu wa Wilaya nao watawapa amri askari kufagia ofisi zao. Baadaye na watendaji wa kata watawaamrisha askari waliopo kwenye maeneo yao ya kiutawala kwenda kufagia maeneo ya shule za msingi.
Kama tunaona ni busara, kazi mojawapo ya kila jeshi ni kufanya usafi wa miji, basi mswada upelekwe Bungeni ili kubadilisha au kuongeza majukumu ya msingi ya majeshi yote kuwa ni pamoja na kufanya usafi kwenye miji. Na hilo likifanyika, Wizara ya TAMISEMI itoe maelekezo kwa majiji, maspaa na halmashauri za miji kufuta kandarasi zote zilizoingiwa na makampuni ya kufanya usafi kwa sababu kazi hiyo sasa ni ya JWTZ, Police, Mgambo na JKT. Na hilo litaifanya Tanzania kuwa nchi ya pekee na ya ajabu iliyoamua kutothamini kazi ya askari wake.
Chalamila anathubutu kueleza kuwa magari ya JWTZ ambayo hayajatengenezwa rasmi kwaajili ya kusomba takataka, eti tarehe 23 na 24 yatatumika kusomba takataka. Yaani magari ambayo huwa yanatumika kubeba askari na mizigo mbalimbali yakatumike kubeba kila aina ya takataka vikiwemo vinyesi vinavyotupwa kwenye mifuko ya plastic, halafu gari hilo hilo kesho yake liwabebe askari, tena wakati ambao kipindupindu kinaendelea kupiga hodi mikoa mbalimbali!
Ushauri: Siasa zisitupofushe kiasi cha kukosa hekima. Rais utakuwa umelipa heshima ambayo jiji la Dar es Salaam linastahili kama ukiwapa Mkuu wa Mkoa ambaye anaendana na hadhi ya jiji la Dar es Salaam. Aliyepo, bila kupepesa macho, viatu vya ukuu wa mkoa ni vikubwa mno kwake. Labda kuna mahali anafaa, lakini siyo kwenye nafasi zinazohitaji hekima.
Ni Amiri Jeshi Mkuu pekee ndiye anaweza kulielekeza Jeshi la Wananchi wa Tanzania kufanya shughuli nyingine nje ya shughuli ya msingi, kama kuna dharula, na anaona kuna haja ya kufanya hivyo. Mamlaka hayo anayo Amiri Jeshi Mkuu, siyo Chalamila wala Mkuu wa Mkoa mwingine yeyote. Wakuu wa mikoa kuwa wenyeviti wa kamati za Ulinzi na usalama mikoani mwao, haimaanishi wamekuwa wakuu wa majeshi yote yaliyopo mikoani mwao.
Tusiwafanye askari wa JWTZ kuwa ni watu wa kupewa amri na kila mtu. Tukiruhusu upuuzi wa namna hiyo kuendelea, kuna siku Wakuu wa Wilaya nao watawapa amri askari kufagia ofisi zao. Baadaye na watendaji wa kata watawaamrisha askari waliopo kwenye maeneo yao ya kiutawala kwenda kufagia maeneo ya shule za msingi.
Kama tunaona ni busara, kazi mojawapo ya kila jeshi ni kufanya usafi wa miji, basi mswada upelekwe Bungeni ili kubadilisha au kuongeza majukumu ya msingi ya majeshi yote kuwa ni pamoja na kufanya usafi kwenye miji. Na hilo likifanyika, Wizara ya TAMISEMI itoe maelekezo kwa majiji, maspaa na halmashauri za miji kufuta kandarasi zote zilizoingiwa na makampuni ya kufanya usafi kwa sababu kazi hiyo sasa ni ya JWTZ, Police, Mgambo na JKT. Na hilo litaifanya Tanzania kuwa nchi ya pekee na ya ajabu iliyoamua kutothamini kazi ya askari wake.
Chalamila anathubutu kueleza kuwa magari ya JWTZ ambayo hayajatengenezwa rasmi kwaajili ya kusomba takataka, eti tarehe 23 na 24 yatatumika kusomba takataka. Yaani magari ambayo huwa yanatumika kubeba askari na mizigo mbalimbali yakatumike kubeba kila aina ya takataka vikiwemo vinyesi vinavyotupwa kwenye mifuko ya plastic, halafu gari hilo hilo kesho yake liwabebe askari, tena wakati ambao kipindupindu kinaendelea kupiga hodi mikoa mbalimbali!
Ushauri: Siasa zisitupofushe kiasi cha kukosa hekima. Rais utakuwa umelipa heshima ambayo jiji la Dar es Salaam linastahili kama ukiwapa Mkuu wa Mkoa ambaye anaendana na hadhi ya jiji la Dar es Salaam. Aliyepo, bila kupepesa macho, viatu vya ukuu wa mkoa ni vikubwa mno kwake. Labda kuna mahali anafaa, lakini siyo kwenye nafasi zinazohitaji hekima.