Riwa
Platinum Member
- Oct 11, 2007
- 2,607
- 3,068
Sijui ni ajali gani wanaziongelea hapa...maana sijawahi sikia Dar Express imepinduka au kugongana na gari nyingine kusababisha vifo au majeruhi kadhaa! Kama unafungia Dar Express kwa mfano wa kugonga mpanda piki piki, sijui utafungia magari mangapi maana hawa jamaa wanagongwa kila siku na madereva wengi mnajua jinsi piki piki zinavyoendeshwa vibaya siku hizi na watu wasio hata na leseni wala kujua miongozo ya usalama barabarani! Kumekuwa na mlolongo wa jali mbaya za kutisha ambazo zimesababisha vifo vingi sana na vilema kibao, sijasikia Dar Express kuhusika hata kwenye ajali moja kati ya hizo...wala sijasikia hayo makampuni yaliyohusika kufungiwa!