Mbugi
JF-Expert Member
- Jan 7, 2011
- 1,488
- 257
jiwe la msingi lipo kwa kila kundi kwani kwa vilaza sugu ni strong base yao. lakini kinyume na hapo samahanini na mtuwie radhi, tunajuta kipofu kushika taa na kuwaongoza wenye machoYaani Mwita Nashindwa kukuelewa kabisa ndugu yangu, inawezekana katika maisha yako hujaona watu ambao ni JIWE LA MSINGI na elimu ndogo!? Mzee wetu Rashid Kawawa wakati anachukua uwaziri mkuu alikuwa na elimu gani? Mzee wetu ambaye mpaka sasa tunamkumbuka kwa busara na uongozi thabiti Abeid Karume naye unamzungumziaje? hao wote hapo waliiongoza hii nchi mpaka ikawa ni mfano wa kuigwa. Angalia ambao ni wasomi Benjamin Mkapa, Jakaya Kikwete, Edward Lowasa, Andrew Chenge na wengine wengi wa aina hiyo wametupeleka wapi mpaka sasa.? Elimu ya Sugu sio iliyompatia Ubunge bali ni namna yake ya kujenga Hoja na Kuitetea. nitajie mwenye elimu kubwa katika chama chako cha magamba ambaye ameweza kutumia elimu yake kuwaokoa Watanzania katika matatizo kibao. Ndio, Elimu ni muhimu sana ktk maisha ya mwanadamu lakni kama CCM wameshindwa kuwapa elimu Watanzania wengi akiwemo SUGU unatazamia tutaongozwa na nani?
PUNGUZA DHARAU NDUGU YANGU, HIYO ELIMU YAKO ITUMIE KUELIMISHA WENGINE BADALA YA KUWAKEJERLI.