Sugu ni Jiwe la MSINGI!

Amoeba

JF-Expert Member
Aug 20, 2009
3,289
781
Nawashangaa sana watoto wa bongofleva mnaoendekeza njaa!! Wengi wenu mnatakiwa mmwite kaka huyu jamaa, na wengine ni baba yenu kabsaa (kwenye mziki)! Ss mnapofunua vidomo vyenu vyenye lipustiki na kumponda mtu aliyeufinyanga huo mziki unaowapa maisha mnakuwa wakosefu wa shukrani!! Mnastahili bakora, pambf.
 
Kweli sugu ni nguzu wa muziki bongo hilo mbona halipingiki clauz wamembania mchiz kasonga,toka kushika mike mpaka kupiga story na pinda baaako, clauz aibu yao wanatamani walete shobo sugu kakaza huu ndo ukwel, watu mwanche selfish za kiswahili 2kubal mafanikio ya wenze2
 
Mtu aliyepata FOUR form FOUR naye atakuwaje jiwe la msingi? Kweli dunia haiishi maajabu.
 
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
wee una wazimu usio tibika. Sugu alikufanya nini? Au ndio ile hadithi ya demu wako, dada yako kisha akamaliza na wewe mwenyewe?
<br />
<br />
As a man of great probity, and for the sake of JF status, I have to refrain myself from using any billingsgate in return.
 
Sugu katoa muziki wa bongo mbali,time goes atafanikiwa katika harakati zake kwani wanamuzik walio kuwa hawajui sa ivi nao wanafunguka,
hofu yangu ni kwa wasanii wasio muunga mkono,je watakuwa upande wake badae?
 
Mtu aliyepata FOUR form FOUR naye atakuwaje jiwe la msingi? Kweli dunia haiishi maajabu.

Yaani Mwita Nashindwa kukuelewa kabisa ndugu yangu, inawezekana katika maisha yako hujaona watu ambao ni JIWE LA MSINGI na elimu ndogo!? Mzee wetu Rashid Kawawa wakati anachukua uwaziri mkuu alikuwa na elimu gani? Mzee wetu ambaye mpaka sasa tunamkumbuka kwa busara na uongozi thabiti Abeid Karume naye unamzungumziaje? hao wote hapo waliiongoza hii nchi mpaka ikawa ni mfano wa kuigwa. Angalia ambao ni wasomi Benjamin Mkapa, Jakaya Kikwete, Edward Lowasa, Andrew Chenge na wengine wengi wa aina hiyo wametupeleka wapi mpaka sasa.? Elimu ya Sugu sio iliyompatia Ubunge bali ni namna yake ya kujenga Hoja na Kuitetea. nitajie mwenye elimu kubwa katika chama chako cha magamba ambaye ameweza kutumia elimu yake kuwaokoa Watanzania katika matatizo kibao. Ndio, Elimu ni muhimu sana ktk maisha ya mwanadamu lakni kama CCM wameshindwa kuwapa elimu Watanzania wengi akiwemo SUGU unatazamia tutaongozwa na nani?

PUNGUZA DHARAU NDUGU YANGU, HIYO ELIMU YAKO ITUMIE KUELIMISHA WENGINE BADALA YA KUWAKEJERLI.
 
Sugu ni mmoja wa wapambanaji wa mwanzoni kwenye muziki wa kizazi hiki, hili halina ubishi!
Lakini mwisho wake kaharibu, amefilisika kimuziki na kifikra!
Kuona wenzake wanapanda juu na kupata promo hataki! Anataka aendelee tu kuenziwa!
Poor him!
Hint: Siasa nayo imemshinda! Akikosa ubunge 2015 ataanza tena kulitukana bunge
 
Mtu aliyepata FOUR form FOUR naye atakuwaje jiwe la msingi? Kweli dunia haiishi maajabu.
<br />
<br />
Elimu ya pro maji marefu,Nape na wameaminiwa kupewa nafasi kubwa tu,umesoma ila unaonekana hujui hata elimu ni nn,unaonekana umehitimu kwa madesa na vijiji vya ujamaa,punguza kiburi na elimu yako ndogo unayomiliki,whatever he is legend from am 2 fm,from jukwaa la muziki 2 mjengoni
 
<br />
<br />
As a man of great probity, and for the sake of JF status, I have to refrain myself from using any billingsgate in return.

Mkwara wa kizamani, eti "man of geat probity" huna lolote, mtaro wa maji machafu we!
 
Mtu aliyepata FOUR form FOUR naye atakuwaje jiwe la msingi? Kweli dunia haiishi maajabu.

Tuelimishane kidogo. Viwango vya elimu si ndio kipimo cha uwezo na uelewa wa mtu ingawa kwa baadhi ya watu inawasaidia ambao akili yao inahitaji kuamshwa zaidi. Tumepata madiwani hata wabunge ambao kiwango chao cha elimu ni shule ya msingi na wamefanya mazuri tu. Vinginevyo kama kiwango cha elimu ndio kigezo cha uwezo wa mtu kuongoza basi hata viongozi kitaifa kama rais wangepaswa kuwa na kiwango cha juu cha Phd. Lakini mambo hayaendi hivyo.

Kwa nini wagombea nafasi mbalimbali za uongozi kuanzia ngazi ya rais hadi madiwani hupambanishwa kwenye midahalo? Kila mmoja wetu anajua ni kwa ajili ya kupima uwezo wao wa kujenga hoja, uelewa wao katika masuala ya uongozi, ukomavu wa kiakili na kifikra, ujenzi wa hoja za kutetea mambo ya msingi kwa maisha ya wananchi watakaowatumikia, na kujiamini kwao ili wananchi wawaaminishe kushika uongozi. Kama sio hayo kwa mtazamo wa Ndugu Mwita Elimu yao ingekuwa kigezo halali cha ubora wa uongozi, matokeo ya waliokwepa mdahalo ndo hayo sasa tunashuhudia wanavyoshindwa kusoma upepo baharini na mashua inaposhika kasi no control, nini sababu hawakukubali kupimwa na wananchi kwenye midahalo iliyo wazi kwa wapiga kura wao.

Kwa taarifa yako elimu yote ni kisomo cha shule ya msingi, baada ya hapo ni extension tu ya yale uliyosoma, hutasikia jipya zaidi ya yale uliyojifunza shule ya msingi ila sasa ni kwa upana zaidi. Kwa mwenye akili nzuri kiwango cha sekondari ni elimu nzuri sana kwa mantiki ya kwamba dunia yote utakuwa umeshaitalii kielimu.

Wanafalsafa mashuhuri kama akina
Sokrates na Aristatle wa jamii ya wayunani hawakuwa na kiwango cha Phd, bali walipanuana akili kule Ugiriki kwenye kilima cha Aleopago na yaliyojilia leo watu wanasomelea hadi kunyofoka nywele na wengine kurukwa akili ni kwa sababu ya kulazimisha kushindilia akilini kitu wakati capacity ya ubongo wao hairuhusu.

Kumbuka baada ya degree ya kwanza, Masters na Phd hakuna mfumo kama wa ilm yenye silabas na mkufunzi wako ndiye anayekuongoza na kukupa cheti cha ufaulu pamoja na wapambe wenzake kuridhishwa na hoja za utetezi wako. Ndio maana haitwi
teacher bali instructor kwa maana ya kwamba ni mtoa maelekezo na kazi wewe mwenyewe unaifanya. Kinachoendelea huko kwenye Masters na Phd ni mabishano kama watu wanywapo pombe kubishana kwa hoja, au wazee wetu walivyokuwa wanakutana siku za mapumziko na kupimana nguvu za kufikiri ambapo mawazo yao mengi yaliibuka na kuibua ubunifu fulani.

Nikupe mfano mmoja fulani, baada ya kutoka chuo na kupewa kazi ya kuendesha
Roscam Robotica Interface System kwa miaka miwili aliamua kuacha kwa hiari baada ya kuona ni mtumwa wa mtambo ambao akili yangu haifanyi kazi ila mtumwa wa robot na kiwango chake cha kufikiri kinazidi kudumaa. Bora kazi ya umachinga inakupa fulsa ya kuchanganya akili yako na ya wengine namna gani nipange biashara ya kuuza ubuyu aliouokota kwenye mbuyu wa kule Bwaga-moyo. Kwa mantihi hiyo kufikiria kufanya kazi kutokana na ulichosoma darasani ni utumwa na mara nyingi hakuna mafanikio. Darasa linakusaidia kufungua namna ya kutumia akili yako hapo ndio utakuwa umeelimika, lakini kufanya kwa kutegemea yale uliyoyasoma maana yeke we mtumwa wa mawazo ya mtu fulani.

Kwa hiyo kufikiri kwamba elimu ndio kiwango cha mtu kuweza kuongoza au kufanya vizuri ni ufinyu na pengine ni sababu ya kutotambua akili za watu zinavyofanya kazi, na pengine mtazamo binafsi mtu akauchukulia kama ndio kigezo kwa mambo ya watu wengine kitu ambacho sivyo. Kumbuka wagunduzi wa awali walipata wapi Phd? Akina Thomas Edson huko West Orange, NJ, nchini USA aliyevumbua bulb karne moja iliyopita alikuwa na elimu gani kama si utundu wa kutumia akili yake na kutokukubali kushindwa kwa kufanya majaribio kadhaa hadi afanikiwe? Na alikuwa halali nyumbani, kitanda chake kingali pale pale workshop alipokuwa anafanyia majaribio yake, akichoka analala huku anaota kazi yake na ndoto ikimfikia papo hapo huamka na kuendelea na majaribio yake. Hata majaribio yake ya kutengeneza gari litumialo umeme angefaulu kama kifo kisingemkatisha.
 
AROOO!nikisema up lala chini na nikisema down inuka juu.mimi ndiyo afande mwita nimesoma pare sekondari ya jangwani secondary school.tehe tehe tehe tehe.

SCHOOLING IS USELESS BECAUSE SCHOOLS ARE MAKING PEOPLE MORE STUPID AS HOSPITALS ARE MAKING PEOPLE MORE SICK-IVAN ILLICH
(1926-2002)
 
Back
Top Bottom