Sugu ameonesha ulimbukeni mkubwa sana kusema kuwa ameweka rekodi ya Dunia ya Muandamanaji aliyevaa vito vya thamani zaidi katika maandamano

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
15,305
9,734
Ndugu zangu Watanzania,

Kupitia mtandao wa Twitter Sugu ameandika kuwa katika maandamano ya hapo jana ameweka rekodi ya Dunia kama muandamanaji aliye vaa vito vya thamani zaidi,na kwamba rekodi hiyo aliiweka pale maandamano yalipofanyika mkoani Mbeya na sasa amevunja rekodi yake mwenyewe kwa maandamano ya hapo jana kwa kuvaa vito hivyo vya thamani.

Ndugu zangu Watanzania kwa maneno haya ya sugu mnaweza kuona ni namna gani jimbo la Mbeya mjini lilipata bahati mbaya sana ya kuongozwa na mhuni mhuni kwa miaka kumi mfululizo,jimbo lilikuwa katika mikono ya mtu asiyejitambua wala kuelewa kazi ya ubunge ilikuwa ni nini .ndio maana hapa majuzi wakati Dkt Tulia anagawa bure bima za afya elfu sita pamoja na kumkabidhi nyumba aliyomjengea ndugu Hosea,niliwaambia ya kuwa katika muda wote wa uongozi wa Sugu kama mbunge alikuwa ni kama mbunge hewa tu,hakuwahi kuwa na msaada wa aina yoyote ile kwa mwananchi yeyote yule wa jiji la mbeya zaidi ya maslahi yake binafsi.

Sugu aliomba ubunge na kuutaka tena ubunge kwa ajili ya kujineemesha yeye na familia yake. Mtu mwenye akili Timamu na unayejitambua na mwenye akili ya Kiutu uzima na unayeguswa na shida za watu unaanzia wapi kujitapa juu ya kuvaa vito vya thamani katika mwili wako? Hivi hiyo ni akili au matope? Huo ni ulimbukeni au utoto?

Sugu atakua na kukomaa lini akili yake? Mtu mwenye akili ya namna hii anaweza akagusa vipi maisha ya watu? Anaweza vipi wajali na kuwaonea huruma wajane, yatima,wazee na watu wasio jiweza na wanaohitaji msaada? Anaweza vipi wasaidia watu hawa? Anaweza vipi wapambania watu wakapata miradi ya maji safi na salama,miradi ya barabara,afya na elimu? Anaweza vipi pigania maendeleo katika jimbo wakati akili yake ipo katika kuwaza vito vya thamani ili kuwazidi na kuwalingishia wananchi anaowaongoza?

Kwa hiyo lengo la sugu na CHADEMA yake katika maandamano siyo yale wanayotamka katika ndimi zao,bali ni kuangalia ufukara wa watanzania,mavazi ya watanzania ,hali za wananchi pamoja na kuwalingishia utajiri wao waliouchuma kupitia viinua mgongo na maposho waliyovuna wakiwa wabunge. Hii ndio sababu wanawadharau watanzania na kuita kazi halali kuwa ni za laana kama alivyotamka lema hadharani.

Kumbe Wanawatesa watu katika mvua na safari ndefu za kutembea barabarani kwa ajili ya kuonyesha vito vyao vya thamani? Kwa hakika CHADEMA na viongozi wake imelaaniwa na ndio maana kwa upofu wa akili wanaandika ujinga huu katika mitandao ya kijamii.kwa sababu Mungu amewapiga upofu wa akili.maana kiongozi wa kamati kuu unayeguswa na maisha ya watu na mwenye dhamira ya kuwapigania wanyonge na unayetaka kuinua maisha ya watu siku ukipewa madaraka huwezi kujitapa kwa kuvaa vito vya thamani mwilini mwako .maana hiyo inamaanisha kuwa unapokuwa mstari wa mbele unakuwa unawakejeli waandamanaji kwa namna walivyo vaa vitu vya mitumba vilivyochoka na kuchakaa.

Hoja yangu siyo kumshambulia sugu kuwa asivae hivyo vito vya thamani ambavyo amejinunulia kwa pesa zake.bali ni kupinga ulimbukeni wake na kukosa kwake busara ,hekima na kutokujitambua kwake kwa kuanza kulingia vito vya thamani mbele ya waandamanaji anaowaona kuwa wamevaa vitu vya hovyo hovyo.hii ndio sababu CHADEMA inaendelea kupuuzwa na watanzania kwa kuwa ni mkusanyiko wa viongozi wahuni wahuni wasio na uchungu na maisha ya watanzania wala kuguswa na maisha ya watu zaidi ya kutafuta milango ya kupatia madaraka yatakayowapa fursa ya kuvuna pesa pasipo jasho ili baadaye waje wawatapikie matusi Watanzania.

Akili na mawazo haya ya sugu ndio waliyonayo viongozi karibu wote wa CHADEMA.wakishapata vijisenti kidogo tu wanaanza dharau,matusi, kejeli,ulimbukeni na utoto utoto tu na kusahau waliowafikisha hapo walipo. CHADEMA ni laana mbele ya watu waliostaarabika. Ni chama kinachopaswa kupingwa sana maana kinaweza kuleta ubaguzi mkubwa sana katika jamii na kuwafanya watu wengine wajione hawana thamani wala hadhi katika Taifa lao.wanaweza chochea hasira kubwa katika mioyo ya wananchi ambao wanaweza kuamua liwalo na liwe kuliko kudharaulika.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
 
Wewe na Sugu nani Limbukeni?

1.Mwenzio anamiliki Hotels
2.Mwenzio anapesa
3.Mwenzio ameishi Marekani
4.Mwenzio amekuwa mbunge
5.Mwenzio anamke mzuri


Wewe unamiliki yafuatayo

1.Huna hela
2.Wewe ni chawa
3.Unamiliki mbupu tu hapo ulipo
4.Huna akili timamu( Hakuna mtu mwenye akili timamu anayemfungulia mwanaume mwenzie uzi kisa cheni)
5.Kutwa kushinda mitandaoni
6.Kwenu masikini


Kijana pambana kwa ajili ya familia yako na Kizazi chako,Acha UJINGA,UJUHA,UZWAZWA
 
Lucas,kuna uzi kuhusu hii reli yetu au unajifanya huuoni?,serikali ya ccm haina cha kujivunia zaidi ya kuiba kura za uchaguzi, PM yupo mkoani Mara na hotuba yake imejaa ufisadi wa level ya juu, pale mkoani kuna RPC, RCO RSO, TAKUKURU, na wapuuzi wengine ila ufisadi ule hawakuujua!,RPC akiambiwa tia ndani yule kazi yake ni kusimama kinafiki na salute ya kipuuzi, next time PM anza kuwatia ndani RPC na wenzie, BUT uende kwanza ukafungue docket police
 
Mnahangaika nn Sasa,na Bado ataendelea kuwasugua huko ofisi za ccm hakukariki Sorokoto nyie.
Mbona hujaweka namba mkuu.
Dawa imeanza kuwaingia mdogomdogo.
Maisha yalivyo Toka uhuru,ilitakiwa uone aibu.
Walioko ccm akili ndogo,ila wanataka kuendesha akili kubwa.
Mmebaki majungu,tunataka umeme,maji,sukari,na maisha Bora Kwa Kila Mtanzania,na sio maisha Bora Kwa wateuliwa wa Ccm.
Maana hakuna uchaguzi mliwahi kushinda tangu 1995 Kwa
Lwatonga Mlema.
 
Mnahangaika nn Sasa,na Bado ataendelea kuwasugua huko ofisi za ccm hakukariki Sorokoto nyie.
Mbona hujaweka namba mkuu.
Dawa imeanza kuwaingia mdogomdogo.
Maisha yalivyo Toka uhuru,ilitakiwa uone aibu.
Walioko ccm akili ndogo,ila wanataka kuendesha akili kubwa.
Mmebaki majungu,tunataka umeme,maji,sukari,na maisha Bora Kwa Kila Mtanzania,na sio maisha Bora Kwa wateuliwa wa Ccm.
Maana hakuna uchaguzi mliwahi kushinda tangu 1995 Kwa
Lwatonga Mlema.
Endeleeni na ujinga wenu na huo ulimbukeni wenu.majibu yake mtayapata katika sanduku la kura katika chaguzi zijazo.
 
Back
Top Bottom