Historia fupi ya Rambo ili iweze kuwa hamasa katika harakati zako

Eli Cohen

JF-Expert Member
Jun 19, 2023
1,309
4,017
Huko nyuma, Stallone (rambo) kabla ya kuwa muigizaji alipitia wakati mgumu sana. Wakati fulani, alifulia sana hivi kwamba aliiba vito vya mke wake na kuviuza. Mambo yalikuwa mabaya sana hata akaishia kukosa makao.

Alilala katika kituo cha basi cha New York kwa siku 3. Hakuweza kulipa kodi au kununua chakula. Hatua yake ya chini kabisa ilikuja pale alipojaribu kumuuza mbwa wake kwenye duka la pombe kwa mgeni yeyote. Hakuwa na pesa za kulisha mbwa tena. Aliiuza kwa $25 pekee.

Anasema aliondoka huku akilia. Wiki mbili baadaye, aliona pambano la ndondi kati ya Mohammed Ali na Chuck Wepner na mechi hiyo ilimpa msukumo wa kuandika maandishi ya filamu maarufu, ROCKY. Aliandika maandishi kwa masaa 20.

Alijaribu kuiuza na akapata ofa ya $125,000 kwa hati hiyo. Lakini alikuwa na OMBI MOJA tu. Alitaka KUIGIZA kwenye sinema. Alitaka kuwa MWIGIZAJI MKUU, Rocky mwenyewe. Lakini studio ilisema HAPANA. Walitaka NYOTA HALISI. Walisema "Alionekana hafai kuwa star wa movie kwa maana uongeaji wake ulikuwa mmbovu na muonekano wake pia ulikuwa mmbovu"

Aliondoka na script yake. Wiki chache baadaye, studio ilimpa $ 250,000 kwa script. Alikataa. Walitoa hata $350,000. Bado alikataa. Walitaka filamu yake, lakini SI yeye. Alisema HAPANA. Ilibidi awe KWENYE FILAMU HIYO. Baada ya muda, studio ilikubali, ikampa $ 35,000 kwa script na kumwacha aigize ndani yake! Mengine ni historia! Filamu hiyo ilishinda Picha Bora, Uongozaji Bora na Uhariri Bora wa Filamu katika Tuzo za Oscar maarufu. Hata aliteuliwa kuwa MWIGIZAJI BORA! Filamu ya ROCKY iliingizwa hata kwenye Rejesta ya Filamu ya Kitaifa ya Marekani kama mojawapo ya filamu bora zaidi kuwahi kutokea! Pia stallone alirudi kununua mbwa wake aliemuuza.

HAKUNA ANAYEJUA UNA UWEZO GANI ILA WEWE MWENYEWE! Watu watakuhukumu kwa JINSI unavyoonekana. Na kwa KILE ulichonacho. Lakini Pambana! Pigania nafasi yako katika historia. Pigania utukufu wako. USIWAHI KUKATA TAMAA! Hata ikimaanisha kudharalika kuipigania ndoto yako, NI SAWA!

MUDA UPO HAI HADITHI YAKO HAIJAISHA. Endelea Kupambana. Weka ndoto zako na matumaini hai. Chukua hatua.


Sent from my SM-A047F using JamiiForums mobile app
 
Hii imekaa kama fix fulani.
Yaani mtu mwenye njaa hivyo, apigwe pesa ndefu hivyo halafu agome kuuza script kisa anataka yeye aigize huku hakuwahi kuwa muigizaji.

Kama ni kweli basi sio kitu cha kuiga, ni hatari na ujinga.
Tofautisha kutafuta mafanikio yatakayodumu, na kuwa chawa usiye na malengo ya kesho na vizazi vyako. Huyu alikuwa na njaa ya mafanikio na aliamini mafanikio yake yataletwa na yeye mwenyewe. Wakati chawa wanaamini mafanikio yao yataletwa na mabos zao
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom