Je, Wajua? Mhimili wa Mahakama Usipotenda Haki Unaweza Kushitakiwa? Pongezi Jaji Mkuu wa Kusisitiza Usuluhishi na Sio Kukimbilia Kufungua Kesi

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,506
113,627
Wanabodi,

Kwa Maslahi ya Taifa ya Jumapili ya leo, 12 February, 2023

Screen Shot 2023-02-12 at 7.23.52 AM.png
Screen Shot 2023-02-12 at 7.24.32 AM.png

KONGOLE JAJI MKUU WA TANZANIA KUSISITIZA UMUHIMU WA USULUHISHI KUTATUA MIGOGORO, KUTAKUZA UCHUMI

Kwa Maslahi ya Taifa leo, inawachambulia sehemu ya hotuba ya Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Hamisi Juma kwenye Siku ya Sheria ya mwaka huu 2023 iliyofanyika katika uwanja wa Chinangali jijini Dodoma, na kwa vile mimi nawaandikia wananchi wa kawaida kabisa, baadhi ya vifungu vya sheria, nitaviacha na kuwaachia wanasheria, wananchi wa kawaida wanachotaka ni haki, kutendewa haki na haki kuonekana inatendeka.

Kauli mbiu ya siku ya sheria mwaka huu wa 2023 inasema “UMUHIMU WA UTATUZI WA MIGOGORO KWA NJIA YA USULUHISHI KATIKA KUKUZA UCHUMI ENDELEVU: WAJIBU WA MAHAKAMA NA WADAU”, Jaji Mkuu Prof. Juma amesema umuhimu wa usuluhishi katika utatuzi wa migogoro ni kwa mujibu wa Inara ya 107 ya Katiba inayoitaka Mahakama katika kutoa uamuzi wa mashauri, inatakiwa kuzingatia kukuza na kuendeleza usuluhishi baina ya wanaohusika katika migogoro. Kanuni hii ya Katiba inazingatia faida kubwa za matumizi ya usuluhishi katika utatuzi wa migogoro zikijumuisha kupunguza gharama na muda wa kuendesha shauri na kuendeleza undugu miongoni mwa wadaawa.

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1977) imeweka Kanuni mbili muhimu ambazo bado hazizingatiwi kikamilifu na mhimili wa mahakama wakati wa kusikiliza mashauri Mahakamani na hivyo kusababisha uchelewaji mkubwa wa mashauri na kuongeza gharama za uendeshaji wa mashauri. Ibara ya 107A (2) (d) imetamka kanuni inayoitaka Mahakama, wakati inasikiliza mashauri ya madai au jinai, kukuza na kuendeleza usuluhishi baina ya wanaohusika katika migogoro. Ibara ya 107A (2) (e) imetamka kanuni nyingine muhimu sana kuwa, katika kutoa uamuzi wa mashauri ya madai na jinai kwa mujibu wa sheria, Mahakama zitende haki bila kufungwa kupita kiasi na masharti ya kiufundi yanayoweza kukwamisha haki kutendeka.

Sio mara moja wala mbili tumeshuhudia wananchi wengi wakikosa haki zao mahakamani kwa kesi zao kutupwa kwasababu tuu ya makosa ya kiufundi, “legal technicalities”, na hili sio kosa na mhusika ni kosa la mawakili.

Mfano mzuri ni kesi ya mwanasiasa Zitto Kabwe alipovuliwa unachama wa Chadema aliwa ni Naibu Katibu Mkuu, (NKM), kwa mujibu wa Katiba ya Chadema, mamlaka ya nidhamu ya NKM ni Baraza Kuu, Kamati Kuu ya Chadema, ilipata wapi mamlaka na uwezo wa kumfuta uanachama NKM wakati sio mamlaka yake ya nidhamu?!.

Zitto alikimbilia mahakamani na kesi yake ikatupwa kwa makosa ya kiufundi!, hivyo kupoteza haki yake, na baada ya kushindwa kesi, katiba ya Chadema imeweka kifungu kinachokwenda kinyume na katiba ya JMT, kuwa mwanachama wa Chadema haruhusiwi kufungua shauri mahakamani dhidi ya chama, na akifungua, akishindwa anakuwa amejifukuzisha uanachama!, hivyo Zitto baada ya kushindwa kesi, akafungasha kwa kuliaga Bunge na kujitoa Chadema huku Chasema wenyewe wakishangilia kumtimua!. Niliwapa Chadema angalizo Opinion: Kung'atuka Kwa Zitto, CHADEMA, Msishangilie, Mkajisahau, Jiandaeni kwa "Karma!" bahati mbaya sana Chadema hawaijui karma, hivyo hawajui the consequences za kudhulumu haki za wanachama wake!.

Sasa hivi kuna kesi nyingine mahakamani dhidi Chadema kwa mazingira yale yale kama ya kesi ya Zitto. CC ya Chadema imekaa tena kama kawaida yake, as a kangaroo court na kumtimua Halima Mdee!, huyu ni Mwenyekiti wa Bawacha, mamlaka yake ya nidhamu ni Baraza Kuu, CC ya Chadema inapomtimua Mwenyekiti wa Bawacha, imepata wapi mamlaka hayo ya kumfuta uanachama mtu kama Halima Mdee, wakati CC hiyo sio mamlaka yake ya nidhamu?.

Mamlaka rasmi ya nidhamu ya Halima Mdee ni Baraza Kuu, Chadema ilishindwa kuitisha kikao cha Baraza Kuu kwasababu fulani, (naijua), thanks God, kukajitokeza Msamaria mwema fulani, (namjua), akawezesha kikao cha Baraza Kuu kikaitishwa, hii sasa ndio mamlaka sahihi ya nidhamu ya Halima Mdee, kwanini kikao cha Baraza Kuu kilipoitishwa shauri la Halima Mdee halikusikilizwa?, na badala yake kikao cha Baraza Kuu kilikaa kama mamlaka ya rufaa kwa wabunge waliotimuliwa na CC ya Chadema, lakini kwa mujibu wa katiba ya Chadema, mamlaka ya nidhamu ya Mwenyekiti wa Bawacha ni Baraza Kuu, na mamlaka yake ya rufaa ni Mkutano Mkuu. Chadema imekuwa ikitumia hizi loopholes za legal technicalities kuwahukumu wanachama wake kikangaroo court na kushangilia utimuaji huo bila kupima the consequences, amini nawaambia the karmic consequences za kuwatimua kama mbwa, watu waliokipigania Chadema kwa machozi, jasho na damu ni devastating!. Mpaka sasa Chadema wanayo chance ya usuluhishi na hao wabunge wao 19 waliowatimua Kikangaroo.

Kufuatia Zitto kushindwa kesi yake kwa legal technicalities, nikatoa angalizo The Voices From Within: "Mahakamani Watashindwa Tena!" Sababu ni Mawakili! Jee Tanzania Tuna Mawakili wa Calibre ya Murtaza Lakha?Jitokezeni Kusaidia! sasa angalau mahakama imekubali kuwasikiliza, natumaini safari hii mahakama itatenda haki. Ila hata kama mahakamani watashindwa na Chadema kufanikiwa kuwatimua, the consequences will be devastating for Chadema kama nilivyo eleza hapa Makamanda walioigharimia CHADEMA kwa machozi, jasho na damu, leo ni wakuitwa wasaliti? Karma Haitawaacha salama, itawatandika tu

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tayari limetunga sheria kufanikisha matumizi ya usuluhishi kwa kupitisha Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na.1 ya mwaka 2020 [Written Laws (Miscellaneous Amendments) Act No. 1 of 2020] iliyozifanyia marekebisho Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Madai (SURA YA 33) kwa kuongeza Kifungu kipya cha 64A, kinachotamka kuwa, wadaawa, sasa wana hiyari ya kutatua mgogoro wao nje ya Mahakama.

Endapo wadaawa watafikia makubaliano nje ya Mahakama, watayasajili katika ngazi husika ya Mahakama na makubaliano hayo yatakuwa na nguvu ya amri ya mwisho ya Mahakama katika mgogoro huo. Ni wajibu wa Majaji, Mahakimu, Mawakili wa Serikali na Mawakili wa Kujitegemea; kila mara kuwakumbusha wadaawa uwepo wa hiyo nafasi ya kutatua migogoro nje ya Mahakama kwa nia hiyo hiyo ya kuwataka wenye migogoro kutumia usuluhishi badala ya kukimbilia Mahakamani, hii iboreshwe zaidi kwa kutungwa sheria kuwa kesi zote za madai, lazima kwanza zianzie usuhishi ukishindikana ndipo ziende mahakamani.

Jaji Mkuu Prof. Juma, ameipongeza Wizara ya Katiba na Sheria kwa kuweka mazingira ya kisheria ya kusuluhisha migogoro nje ya Mahakama kwa kutoa orodha ya wasuluhishi. (d) Mihimili ya Bunge na Serikali Inatambua Usuluhishi ni Tiba ya Ucheleweshwaji wa Mashauri Mahakamani. Kauli mbiu hii, inatoa tahadhari kwa Majaji, Mahakimu, Mawakili wa Serikali na Mawakili wa Kujitegemea ambao ndio wahusika wakubwa wa uendeshaji wa mashauri Mahakamani. Mihimili ya Bunge na Serikali, tayari imeelewa kuwa dawa ya ucheleweshwaji wa mashauri Mahakamani ni usuluhishi ambao tayari umewezeshwa kwa kutungiwa Sheria nyingi katika maeneo mbali mbali ambayo usuluhishi unawezekana.

Mhimili wa Mahakama na wadau wake, wataonekana kuwa wameshindwa mtihani wa viapo vyao na wajibu wao kulinda na kutetea Katiba na Sheria za nchi wasipotekeleza wajibu wao wa kufanikisha Usuluhishi. Wananchi wanayo haki kuwashtaki mhimili wa Mahakama kwa mhimili wa Bunge, wakiona haki inachelewa kwa kujiuliza kwa nini Mhimili wa Mahakama hautumii Sheria zilizotungwa na Bunge, kuwasaidia wananchi kutatua migogoro kwa njia ya Usuluhishi?.

Mhimili wa serikali usipotenda haki unaweza kushitakiwa kwenye mhimili wa Mahakama na mahakama iakiamuru serikali kutenda haki, lakini ikitokea mhimili wa Bunge kutotenda haki kama Bunge letu kututungia sheria batili zinazokwenda kinyume cha katiba, na mahakama ikauthibitisha ubatili huo, kwanza ilipaswa Mahakama kuzibatilisha sheria batili hizo pale pale zilipothibisha ubatili wa kwenda kinyume cha katiba kwasababu anayebatilisha sheria batili zilizokwenda kinyume cha katiba, zinabatilishwa na katiba na sio Mahakama, kazi ya Mahakama ni kutangaza tuu ubatili huu, na ubatili ni ubatili wa void ab initio.

Bunge litunge sheria batili inayokwenda kinyume cha katiba, mahakama ikathibitisha sheria hiyo ni batili, kwanini Mahakama Kuu haikubatilisha sheria hiyo pale pale na badala yake kuiamuru serikali kuibadili na Mahakama ya Rufaa ikaurudisha ubatili huo kwa Bunge lile lile lililotunga ubatili huo ndio liuondoe hii imekaaje?.
Baada ya Bunge kutunga sheria batili ilitakiwa

1. Sheria batili ikiishatangazwa ni batili, ubatili huanzia hapo hapo na kubatilika pale pale!.
2. Bunge lilipaswa kuadhibiwa kwa kutunga sheria batili
3. Bunge kuamriwa kutunga sheria halali.

Lakini mfumo wetu wa utawala wa mihimili mitatu, hauna utaratibu wowote wa kuliadhibu Bunge letu linapokosea!.

Na mhimili wa Mahakama ni vivyo hivyo, mhimili wa Mahakama unapo wakosea wananchi kwa kutowatendea haki, ilibidi wananchi wawe na uwezo wa kuishitaki Mahakama kwa mhimili wa Bunge na Bunge kuwa na uwezo wa kuiadhibu mahakama pale ambapo mahakamani haijatenda haki kwa Watanzania, na mfano mzuri ni ile kesi ya Mtikila ya mgombea binafsi.

Mahakama Kuu imetamka wazi shurti la kudhaminiwa na chama cha siasa kugombea uongozi ni shurti batili linakwenda kinyume cha katiba na kuamuru mgombea binafsi rukhsa na kuiamuru serikali kuandaa utaratibu. Mahakama ya Rufaa ukawakosea sana Watanzania kwa kulirejesha suala hili Bungeni, hakuna utaratibu wowote rasmi wa kuishitaki mahakama pale mahahama isipotenda haki, zaidi ya kuwatuma wabunge wetu kulalama tuu Bungeni la Bunge haliwezi kuufanya chochote mhimili wa Mahakama!.

Upo ushahidi kuwa Mihimili ya Bunge na Serikali ina ufahamu mkubwa kuhusu manufaa ya usuluhishi. Mhimili wa Mahakama na Wadau wake tukiwemo sisi mawakili, tutajiweka katika mazingira hatari mbele ya macho ya wananchi, endapo hatuzitumii Sheria zinazotoa nafasi za usuhishi na Sheria zinazotuzuia kutumia kanuni za kiufundi kuchelewesha haki.

Tukutane wiki ijayo kwa muendelezo wa makala hii kuhusu umuhimu wa usuluhishi na jinsi Rais Samia anavyotumia usuluhishi kuliponya taifa letu kisiasa hivyo kujikuta tunajiponya kiuchumi na kijamii.

Wasalaam

Paskali
 
... keywords - USULUHISHI, KULIPONYA TAIFA, MIGOGORO, KUKOSA HAKI; kwanini hayo yalitokea in the recent past na sio kabla? Mwl. Nyerere alituasa sana sana sana kwamba kwa Katiba hii akiinuka mwendawazimu, ole ni wenu! Ni bahati mbaya sana naye aliishia kuasa tu bila ku-take action ya maana kuhusu Katiba ya nchi.

Kiini cha tatizo ni ukosefu wa chombo madhubuti kinachowapa uwezo wananchi ku-regulate matendo ya viongozi na badala yake madaraka yote ya nchi wamerundikiwa wachache na kinga juu; hizo nyingine hadithi tu! Kama hatujajifunza kwa yaliyotokea, tutakuwa na kasoro kubwa.
 
Sina imani na mahakama zetu hasa pale unapokuwa na mgogoro na serikali.majuzi tu kesi iko mahakamani walitaka kutubomolea na kututoa kwa nguvu ktk maeneo yetu tunayoishi.mahakama zetu hazina nguvu ila ina nguvu kwa wezi wahalifu na kusuluhisha migogoro midogo
 
Nawe ! Unaandikaga nini sasa?
Mkuu Retired , hujaona chochote katika hili?, basi kuna mawili, ni ama hoja za bandiko hili zimekuzidi kimo hivyo umetoka patupu, na kwasababu hili ni mada muendelezo labda usubirie part 2, labda utaambulia kitu!.

Pili na mimi ni binadamu tuu, hivyo naweza kukosea kuwaandikia vitu vya juu sana yaani too big chunk kuliko uwezo wa the normal comprehension ya an ordinary people to bite and chew.

Hivyo nini wajibu wa ku break down into small small pieces so that everyone can be able to bite, chew and swallow na kwavile pia watu hatulingani uwezo, vitu vingine ni vigumu kwa uwezo wa uelewa wa baadhi yetu hivyo sometimes kuna baadhi ya vitu vigumu kutafuna, wagumu wanakomaa navyo kwa kula wenyewe na kutafuna hivyo hivyo kiugumu ugumu, lakini kwa walaini ni unawapikia, unawapakulia, anawatafunia, una wa spoon fed, wao kazi yao ni moja tuu!, kumeza!.

Usubirie part two next week, ukishindwa kutafuna, nitakutafunia, na nitakulisha, wewe kazi yako itakuwa ni kumeza tuu!.
P
 
Wanabodi,
Kwa Maslahi ya Taifa ya Jumapili ya leo, 12 February, 2023
View attachment 2514352View attachment 2514353
KONGOLE JAJI MKUU WA TANZANIA KUSISITIZA UMUHIMU WA USULUHISHI KUTATUA MIGOGORO, KUTAKUZA UCHUMI

Kwa Maslahi ya Taifa leo, inawachambulia sehemu ya hotuba ya Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Hamisi Juma kwenye Siku ya Sheria ya mwaka huu 2023 iliyofanyika katika uwanja wa Chinangali jijini Dodoma, na kwa vile mimi nawaandikia wananchi wa kawaida kabisa, baadhi ya vifungu vya sheria, nitaviacha na kuwaachia wanasheria, wananchi wa kawaida wanachotaka ni haki, kutendewa haki na haki kuonekana inatendeka.

Kauli mbiu ya siku ya sheria mwaka huu wa 2023 inasema “UMUHIMU WA UTATUZI WA MIGOGORO KWA NJIA YA USULUHISHI KATIKA KUKUZA UCHUMI ENDELEVU: WAJIBU WA MAHAKAMA NA WADAU”, Jaji Mkuu Prof. Juma amesema umuhimu wa usuluhishi katika utatuzi wa migogoro ni kwa mujibu wa Inara ya 107 ya Katiba inayoitaka Mahakama katika kutoa uamuzi wa mashauri, inatakiwa kuzingatia kukuza na kuendeleza usuluhishi baina ya wanaohusika katika migogoro. Kanuni hii ya Katiba inazingatia faida kubwa za matumizi ya usuluhishi katika utatuzi wa migogoro zikijumuisha kupunguza gharama na muda wa kuendesha shauri na kuendeleza undugu miongoni mwa wadaawa.

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1977) imeweka Kanuni mbili muhimu ambazo bado hazizingatiwi kikamilifu na mhimili wa mahakama wakati wa kusikiliza mashauri Mahakamani na hivyo kusababisha uchelewaji mkubwa wa mashauri na kuongeza gharama za uendeshaji wa mashauri. Ibara ya 107A (2) (d) imetamka kanuni inayoitaka Mahakama, wakati inasikiliza mashauri ya madai au jinai, kukuza na kuendeleza usuluhishi baina ya wanaohusika katika migogoro. Ibara ya 107A (2) (e) imetamka kanuni nyingine muhimu sana kuwa, katika kutoa uamuzi wa mashauri ya madai na jinai kwa mujibu wa sheria, Mahakama zitende haki bila kufungwa kupita kiasi na masharti ya kiufundi yanayoweza kukwamisha haki kutendeka.

Sio mara moja wala mbili tumeshuhudia wananchi wengi wakikosa haki zao mahakamani kwa kesi zao kutupwa kwasababu tuu ya makosa ya kiufundi, “legal technicalities”, na hili sio kosa na mhusika ni kosa la mawakili.

Mfano mzuri ni kesi ya mwanasiasa Zitto Kabwe alipovuliwa unachama wa Chadema aliwa ni Naibu Katibu Mkuu, (NKM), kwa mujibu wa Katiba ya Chadema, mamlaka ya nidhamu ya NKM ni Baraza Kuu, Kamati Kuu ya Chadema, ilipata wapi uwezo wa kumfuta uanachama NKM wakati sio mamlaka yake ya nidhamu?!.

Zitto alilimbilia mahakamani na kesi yake ikatupwa kwa makosa ya kiufundi!, hivyo kupoteza haki yake, na baada ya kushindwa kesi, katiba ya Chadema imeweka kifungu kinachokwenda kinyume na katiba ya JMT, kuwa mwanachama wa Chadema haruhusiwi kufungua shauri mahakamani dhidi ya chama, na akifungua, akishindwa anakuwa amejifukuzisha uanachama!, hivyo Zitto baada ya kushindwa kesi, akafungasha kwa kuliaga Bunge na kujitoa Chadema huku Chasema wenyewe wakishangilia kumtimua!. Niliwapa Chadema angalizo Opinion: Kung'atuka Kwa Zitto, CHADEMA, Msishangilie, Mkajisahau, Jiandaeni kwa "Karma!" bahati mbaya sana Chadema hawaijui karma, hivyo hawajui the consequences za kudhulumu haki za wanachama wake!.

Sasa hivi kuna kesi nyingine mahakamani dhidi Chadema kwa mazingira yale yale kama ya kesi ya Zitto. CC ya Chadema imekaa kama a kangaroo court na kumtimua Halima Mdee!, huyu ni Mwenyekiti wa Bawacha, mamlaka yake ya nidhamu ni Baraza Kuu, CC ya Chadema imepata wapi mamlaka kumfuta uanachama Halima Mdee?.

Kufuatia Zitto kushindwa kesi yake kwa legal technicalities, nikatoa angalizo The Voices From Within: "Mahakamani Watashindwa Tena!" Sababu ni Mawakili! Jee Tanzania Tuna Mawakili wa Calibre ya Murtaza Lakha?Jitokezeni Kusaidia! sasa angalau mahakama imekubali kuwasikiliza, natumaini safari hii mahakama itatenda haki.

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tayari limetunga sheria kufanikisha matumizi ya usuluhishi kwa kupitisha Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na.1 ya mwaka 2020 [Written Laws (Miscellaneous Amendments) Act No. 1 of 2020] iliyozifanyia marekebisho Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Madai (SURA YA 33) kwa kuongeza Kifungu kipya cha 64A, kinachotamka kuwa, wadaawa, sasa wana hiyari ya kutatua mgogoro wao nje ya Mahakama.

Endapo wadaawa watafikia makubaliano nje ya Mahakama, watayasajili katika ngazi husika ya Mahakama na makubaliano hayo yatakuwa na nguvu ya amri ya mwisho ya Mahakama katika mgogoro huo. Ni wajibu wa Majaji, Mahakimu, Mawakili wa Serikali na Mawakili wa Kujitegemea; kila mara kuwakumbusha wadaawa uwepo wa hiyo nafasi ya kutatua migogoro nje ya Mahakama kwa nia hiyo hiyo ya kuwataka wenye migogoro kutumia usuluhishi badala ya kukimbilia Mahakamani, hii iboreshwe zaidi kwa kutungwa sheria kuwa kesi zote za madai, lazima kwanza zianzie usuhishi ukishindikana ndipo ziende mahakamani.

Jaji Mkuu Prof Juma, ameipongeza Wizara ya Katiba na Sheria kwa kuweka mazingira ya kisheria ya kusuluhisha migogoro nje ya Mahakama kwa kutoa orodha ya wasuluhishi. (d) Mihimili ya Bunge na Serikali Inatambua Usuluhishi ni Tiba ya Ucheleweshwaji wa Mashauri Mahakamani. Kauli mbiu hii, inatoa tahadhari kwa Majaji, Mahakimu, Mawakili wa Serikali na Mawakili wa Kujitegemea ambao ndio wahusika wakubwa wa uendeshaji wa mashauri Mahakamani. Mihimili ya Bunge na Serikali, tayari imeelewa kuwa dawa ya ucheleweshwaji wa mashauri Mahakamani ni usuluhishi ambao tayari umewezeshwa kwa kutungiwa Sheria nyingi katika maeneo mbali mbali ambayo usuluhishi unawezekana.

Mhimili wa Mahakama na wadau wake, wataonekana kuwa wameshindwa mtihani wa viapo vyao na wajibu wao kulinda na kutetea Katiba na Sheria za nchi wasipotekeleza wajibu wao wa kufanikisha Usuluhishi. Wananchi wanayo haki kuwashtaki mhimili wa mahakama kwa mhimili wa Bunge, wakiona haki inachelewa kwa kujiuliza kwa nini Mhimili wa Mahakama hautumii Sheria zilizotungwa na Bunge, kuwasaidia wananchi kutatua migogoro kwa njia ya Usuluhishi?.

Upo ushahidi kuwa Mihimili ya Bunge na Serikali ina ufahamu mkubwa kuhusu manufaa ya usuluhishi. Mhimili wa Mahakama na Wadau wake tukiwemo sisi mawakili, tutajiweka katika mazingira hatari mbele ya macho ya wananchi, endapo hatuzitumii Sheria zinazotoa nafasi za usuhishi na Sheria zinazotuzuia kutumia kanuni za kiufundi kuchelewesha haki.

Tukutane wiki ijayo kwa muendelezo wa makala hii kuhusu umuhimu wa usuluhishi na jinsi Rais Samia anavyotumia usuluhishi kuliponya taifa letu kisiasa hivyo kujikuta tunajiponya kiuchumi na kijamii.

Wasalaam

Paskali
Si kweli. Utaushitaki wapi wakati mwisho wa siku muhimili wenyewe ndiyo unaotoa uamuzi wa mwisho? Hakuna mahakama ya kuhukumu mahakama duniani mwanangu Pasco. Nashauri usome sheria ambapo kisheria muhimili huu hujiita ex-debito justiciae yaani chemi chemi ya haki japo practically si kweli.
 
Si kweli. Utaushitaki wapi wakati mwisho wa siku muhimili wenyewe ndiyo unaotoa uamuzi wa mwisho? Hakuna mahakama ya kuhukumu mahakama duniani mwanangu Pasco. Nashauri usome sheria ambapo kisheria muhimili huu hujiita ex-debito justiciae yaani chemi chemi ya haki japo practically si kweli.
Mkuu Father of All , kwanza ni kweli Mahakama isipotenda haki hakuna popote pa kuishitaki zaidi na kuwatuma wawakilishi wetu kulalama tuu Bungeni.

Naomba nikushukuru sana wewe na kushukuru JF kutukutanisha humu, maana mimi licha ya kusoma sheria miaka 4 na sasa ni miaka 16 baada ya kuhitumu, amini usiamini, hili neno "ex-debito justiciae" ndio nimelisikia leo kutokea kwako hivyo wewe kwangu ni mwalimu, kama member mwingine huyu Mkuu Ngambo Ngali
aliyenifundisha neno "quo warranto"
Thanks.
P
 
Mkuu Father of All , kwanza ni kweli Mahakama isipotenda haki hakuna popote pa kuishitaki zaidi na kuwatuma wawakilishi wetu kulalama tuu Bungeni.

Naomba nikushukuru sana wewe na kushukuru JF kutukutanisha humu, maana mimi licha ya kusoma sheria miaka 4 na sasa ni miaka 16 baada ya kuhitumu, amini usiamini, hili neno "ex-debito justiciae" ndio nimelisikia leo kutokea kwako hivyo wewe kwangu ni mwalimu, kama member mwingine huyu Mkuu Ngambo Ngali
aliyenifundisha neno "quo warranto"
Thanks.
P
Siku mkijua kuwa HAKI NI TOFAUTI NA NENO SHERIA NDIYO MTAKUWA MMEANZA KUPATA AKILI ......hayo yote unayoandika ni upuuzi mtupu kwa sababu tanzania sheria ipo juu ya HAKI ....NA WATANZANIA WENGI NI WAPUMBAV NDIYO MAANA UTAWASIKIA WANASEMA WANATAKA UTAWALA WA SHERIA..PIA UTAWASIKIA WANASEMA KUVUNJA SHERIA NI KOSA SASA KATI YA SHERIA NA HAKI NI KIPI KIKUU HAPO ?
Je mtu avunjae sheria kwa ajili ya kutenda haki na mtu avunjae haki kwa ajili ya kutenda sheria ni yupi aliye mpumbavu ?
SIFA MOJAWAPO YA BINADAMU BORA NA MZALENDO NI KUWA TAYARI KUVUNJA SHERIA AU KATIBA KWA AJILI YA HAKI
 
Mahakama ya Rufaa unaenda kuishitaki wapi?
Mkuu Bujibuji Simba Nyamaume , baada ya mimi kuwa wakili sasa, ndio na explore matundu na udhaifu wa katiba yetu na kuzungumza na wabobezi na wabobevu what's a way forward, kama katiba ni mali ya wananchi of the people, by the people and for the people, hii maana yake Mwananchi ndio the supreme, yuko juu ya katiba, na hiyo katiba ni yake, to serve him, serikali ni yake, Bunge ni lake na mahakama ni yake, lazima mwananchi huyu, ana uwezo wa kuishitaki serikali mahakamani isipomtendea haki, na mahakama ikaiamuru serikali kutenda haki kupitia vitu vinavyoitwa writs viko 6 ambavyo ni nimevitaja hapa Hoja ya Udikteta wa Magufuli: Tundu Lissu isn't Right. Haupingwi kwa kupaza sauti kupiga tu Kelele! kupitia
Court Review kupitia mamlaka ya Mahakama Kuu kutoa kitu kinachoitwa Prerogative Orders ziko 6, ila maarufu zaidi ni 3.
  • certiorari, an order by a higher court directing a lower court to send the record in a given case for review;
  • mandamus, an order issued by a higher court to compel or to direct a lower court or a government officer to perform mandatory duties correctly;
  • prohibition, directing a subordinate to stop doing something the law prohibits;
  • habeas corpus, demands that a prisoner be taken before the court to determine whether there is lawful authority to detain the person;
  • quo warranto, requiring a person to show by what authority they exercise a power.
  • procedendo, to send a case from an appellate court to a lower court with an order to proceed to judgment) mtanisamehe sizijui Kiswahili chake.
Lakini inapotokea Bunge halijatenda haki kama Bunge letu kukutungia sheria batili zinazokwenda kinyume cha katiba, Mahakama inaweza kutoa amri ya kuamuru tuu kuwa sheria fulani ni batili lakini haina uwezo wa kuubatilisha ubatili huo!. Tunataka Mahakama yenye meno ambayo ikikuta Bunge limetunga sheria batili, sio tuu Mahakama litamke tuu ubatili huo na kulibembeleza Bunge ndio lirekebishe ubatili huo, bali Mahakama ibatilishe ubatili huo na kuliadhibu Bunge kwa kuvunja katiba yetu.

Mwananchi awe na uwezo wa kuishitaki mahakama na iadhibiwe kwa kukuika haki za wananchi. Mfano Mahakama ya Rufaa ilipotoa ule uamuzi wa ajabu kuruhusu katiba yetu inajisiwe na Bunge letu, ni kutowatendea haki kabisa wananchi!, sasa kwa vile wananchi ndio wenye katiba a serikali, Bunge na Mahakama nazo ni mali za wananchi, serikali Bunge na Mahakama ziweze kuwajibishwa na kuadhibiwa.
P
 
Pumba as usual
Mkuu ampersand, kwanza asante kuchangia uzi wangu huu, ubarikiwe sana!.
Pili next time ukikutana na pumba save your time, wakati wengine wanapepeta mchele na pumba wanatupa, wakati wengine hizo pumba wanapepeta na kupata chenga, ambazo zinasagwa na kupata unga wa vitumbua, mabaki ya pumba za mpunga ni tandiko banda la kuku ambapo baadaye zinageuka mbolea na pumba za mahindi ni chakula cha kuku!.
Hivyo hiii hii mada ambayo kwako ni pumba tupu, kwa mwenzako ni kama ganda la mua la jana...
P
 
Huyu jaji alikuwepo tangu kipindi cha mwendazake!
ndio kipindi kilichojaa maovu, uonevu na unyimaji haki ktk mahakama zake huku yeye akishangilia!
Bora angekaa kimya kwani kama ni heshima basi yeye yupo ktk list of shame ya majaji wa Tz.
 
Siku mkijua kuwa HAKI NI TOFAUTI NA NENO SHERIA NDIYO MTAKUWA MMEANZA KUPATA AKILI .....
Mkuu Lwiva , kwanza ni kweli sheria na haki ni vitu viwili tofauti, Watanzania wanapaswa kuelimishwa tofauti ya sheria na haki, na hii kazi inabidi ifanyike.
.hayo yote unayoandika ni upuuzi mtupu
Sii kweli kuwa yote ninayoandika ni upuuzi!, ya kipuuzi yapo lakini ya pia yenye substence pia yapo.
Kwa sababu tanzania sheria ipo juu ya HAKI ....
Hili ni kweli na ni kosa!. Mara kibao watu wanakosa haki zao kwa vyombo vya utoaji haki kuangalia sheria tuu!. Mwaka jana nilipandisha bandiko hili humu JF Ukosekanaji wa Haki kwenye Mhimili wa Mahakama, kunaweza kuwa kunachangiwa na Majaji/Mahakimu wenye uwezo mdogo kubaini haki?
Bandiko hilo liliwaibua majaji akiwemo Jaji Kiongozi, soon Rais Samia akafanya uteuzi wa Majaji na siku anawaapisha akawapa maelekezo sio tuu ya kuhukumu kwa kufuata sheria tuu bali pia watumie nafsi zao kutoa uamuzi wa haki, na juzi kati siku ya sheria Rais Samia akatoa mrejesho Rais Samia ana nia njema Watanzania wapate haki, ila Watanzania hawajui Haki! Je, Tumsaidie kuelimisha umma Katiba, Sheria na Haki au?
Hoja hii imeleta matokeo chanya ambayo nimeyaeleza hapa
Msikilize Rais Samia anesema nini kuhusu majaji
P

NA WATANZANIA WENGI NI WAPUMBAV
Usitukane watu bure kuwa ni wapumbavu!. Watanzania ni wajinga na sio wapumbavu, mjinga ni asiyejua anayehitaji kuelimishwa ili wajue, na kuwa werevu, mpumbavu ni yule asiye elimishika!.
NDIYO MAANA UTAWASIKIA WANASEMA WANATAKA UTAWALA WA SHERIA..PIA UTAWASIKIA WANASEMA KUVUNJA SHERIA NI KOSA SASA KATI YA SHERIA NA HAKI NI KIPI KIKUU HAPO ?
Haki ndio Kuu!, ndio the bottom line!, sheria inatumika ili kutoa haki.
Je mtu avunjae sheria kwa ajili ya kutenda haki
Huyu atabarikiwa!.
na mtu avunjae haki kwa ajili ya kutenda sheria
Huyu atalaaniwa!.
ni yupi aliye mpumbavu ?
Hakuna mpumbavu ni mjinga tuu!.
P
SIFA MOJAWAPO YA BINADAMU BORA NA MZALENDO NI KUWA TAYARI KUVUNJA SHERIA AU KATIBA KWA AJILI YA HAKI
Naunga mkono hoja, na hiki ndicho JPM alichokifanya, na akina sisi washauri huru tulimshauri Kama sio udikteta, Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria, ongoza kwa 'presidential decrees'!
P
 
Wanabodi,
Kwa Maslahi ya Taifa ya Jumapili ya leo, 12 February, 2023
View attachment 2514352View attachment 2514353
KONGOLE JAJI MKUU WA TANZANIA KUSISITIZA UMUHIMU WA USULUHISHI KUTATUA MIGOGORO, KUTAKUZA UCHUMI

Kwa Maslahi ya Taifa leo, inawachambulia sehemu ya hotuba ya Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Hamisi Juma kwenye Siku ya Sheria ya mwaka huu 2023 iliyofanyika katika uwanja wa Chinangali jijini Dodoma, na kwa vile mimi nawaandikia wananchi wa kawaida kabisa, baadhi ya vifungu vya sheria, nitaviacha na kuwaachia wanasheria, wananchi wa kawaida wanachotaka ni haki, kutendewa haki na haki kuonekana inatendeka.

Kauli mbiu ya siku ya sheria mwaka huu wa 2023 inasema “UMUHIMU WA UTATUZI WA MIGOGORO KWA NJIA YA USULUHISHI KATIKA KUKUZA UCHUMI ENDELEVU: WAJIBU WA MAHAKAMA NA WADAU”, Jaji Mkuu Prof. Juma amesema umuhimu wa usuluhishi katika utatuzi wa migogoro ni kwa mujibu wa Inara ya 107 ya Katiba inayoitaka Mahakama katika kutoa uamuzi wa mashauri, inatakiwa kuzingatia kukuza na kuendeleza usuluhishi baina ya wanaohusika katika migogoro. Kanuni hii ya Katiba inazingatia faida kubwa za matumizi ya usuluhishi katika utatuzi wa migogoro zikijumuisha kupunguza gharama na muda wa kuendesha shauri na kuendeleza undugu miongoni mwa wadaawa.

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1977) imeweka Kanuni mbili muhimu ambazo bado hazizingatiwi kikamilifu na mhimili wa mahakama wakati wa kusikiliza mashauri Mahakamani na hivyo kusababisha uchelewaji mkubwa wa mashauri na kuongeza gharama za uendeshaji wa mashauri. Ibara ya 107A (2) (d) imetamka kanuni inayoitaka Mahakama, wakati inasikiliza mashauri ya madai au jinai, kukuza na kuendeleza usuluhishi baina ya wanaohusika katika migogoro. Ibara ya 107A (2) (e) imetamka kanuni nyingine muhimu sana kuwa, katika kutoa uamuzi wa mashauri ya madai na jinai kwa mujibu wa sheria, Mahakama zitende haki bila kufungwa kupita kiasi na masharti ya kiufundi yanayoweza kukwamisha haki kutendeka.

Sio mara moja wala mbili tumeshuhudia wananchi wengi wakikosa haki zao mahakamani kwa kesi zao kutupwa kwasababu tuu ya makosa ya kiufundi, “legal technicalities”, na hili sio kosa na mhusika ni kosa la mawakili.

Mfano mzuri ni kesi ya mwanasiasa Zitto Kabwe alipovuliwa unachama wa Chadema aliwa ni Naibu Katibu Mkuu, (NKM), kwa mujibu wa Katiba ya Chadema, mamlaka ya nidhamu ya NKM ni Baraza Kuu, Kamati Kuu ya Chadema, ilipata wapi uwezo wa kumfuta uanachama NKM wakati sio mamlaka yake ya nidhamu?!.

Zitto alilimbilia mahakamani na kesi yake ikatupwa kwa makosa ya kiufundi!, hivyo kupoteza haki yake, na baada ya kushindwa kesi, katiba ya Chadema imeweka kifungu kinachokwenda kinyume na katiba ya JMT, kuwa mwanachama wa Chadema haruhusiwi kufungua shauri mahakamani dhidi ya chama, na akifungua, akishindwa anakuwa amejifukuzisha uanachama!, hivyo Zitto baada ya kushindwa kesi, akafungasha kwa kuliaga Bunge na kujitoa Chadema huku Chasema wenyewe wakishangilia kumtimua!. Niliwapa Chadema angalizo Opinion: Kung'atuka Kwa Zitto, CHADEMA, Msishangilie, Mkajisahau, Jiandaeni kwa "Karma!" bahati mbaya sana Chadema hawaijui karma, hivyo hawajui the consequences za kudhulumu haki za wanachama wake!.

Sasa hivi kuna kesi nyingine mahakamani dhidi Chadema kwa mazingira yale yale kama ya kesi ya Zitto. CC ya Chadema imekaa tena kama kawaida yake, as a kangaroo court na kumtimua Halima Mdee!, huyu ni Mwenyekiti wa Bawacha, mamlaka yake ya nidhamu ni Baraza Kuu, CC ya Chadema inapomtimua Mwenyekiti wa Bawacha, imepata wapi mamlaka hayo ya kumfuta uanachama mtu kama Halima Mdee, wakati CC hiyo sio mamlaka yake ya nidhamu?.

Mamlaka rasmi ya nidhamu ya Halima Mdee ni Baraza Kuu, Chadema ilishindwa kuitisha kikao cha Baraza Kuu kwasababu fulani, (naijua), thanks God, kukajitokeza mtu, akawezesha kikao cha Baraza Kuu kikaitishwa, hii sasa ndio mamlaka sahihi ya nidhamu ya Halima Mdee, kwanini kikao cha Baraza Kuu kilipoitishwa shauri la Halima Mdee halikusikilizwa?, na badala yake kikao cha Baraza Kuu kilikaa kama mamlaka ya rufaa kwa wabunge waliotimuliwa na CC ya Chadema, lakini kwa mujibu wa katiba ya Chadema, mamlaka ya nidhamu ya Mwenyekiti wa Bawacha ni Baraza Kuu, na mamlaka yake ya rufaa ni Mkutano Mkuu. Chadema imekuwa ikitumia hizi loopholes za legal technicalities kuwahukumu wanachama wake kikangaroo court na kushangilia utimuaji huo bila kupima the consequences, amini nawaambia the karmic consequences za kuwatimua kama mbwa, watu waliokipigania Chadema kwa machozi, jasho na damu ni devastating!. Mpaka sasa Chadema wanayo chance ya usuluhishi na hao wabunge wao 19 waliowatimua Kikangaroo.

Kufuatia Zitto kushindwa kesi yake kwa legal technicalities, nikatoa angalizo The Voices From Within: "Mahakamani Watashindwa Tena!" Sababu ni Mawakili! Jee Tanzania Tuna Mawakili wa Calibre ya Murtaza Lakha?Jitokezeni Kusaidia! sasa angalau mahakama imekubali kuwasikiliza, natumaini safari hii mahakama itatenda haki. Ila hata kama mahakamani watashindwa na Chadema kufanikiwa kuwatimua, the consequences will be devastating for Chadema kama nilivyo eleza hapa Makamanda walioigharimia CHADEMA kwa machozi, jasho na damu, leo ni wakuitwa wasaliti? Karma Haitawaacha salama, itawatandika tu

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tayari limetunga sheria kufanikisha matumizi ya usuluhishi kwa kupitisha Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na.1 ya mwaka 2020 [Written Laws (Miscellaneous Amendments) Act No. 1 of 2020] iliyozifanyia marekebisho Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Madai (SURA YA 33) kwa kuongeza Kifungu kipya cha 64A, kinachotamka kuwa, wadaawa, sasa wana hiyari ya kutatua mgogoro wao nje ya Mahakama.

Endapo wadaawa watafikia makubaliano nje ya Mahakama, watayasajili katika ngazi husika ya Mahakama na makubaliano hayo yatakuwa na nguvu ya amri ya mwisho ya Mahakama katika mgogoro huo. Ni wajibu wa Majaji, Mahakimu, Mawakili wa Serikali na Mawakili wa Kujitegemea; kila mara kuwakumbusha wadaawa uwepo wa hiyo nafasi ya kutatua migogoro nje ya Mahakama kwa nia hiyo hiyo ya kuwataka wenye migogoro kutumia usuluhishi badala ya kukimbilia Mahakamani, hii iboreshwe zaidi kwa kutungwa sheria kuwa kesi zote za madai, lazima kwanza zianzie usuhishi ukishindikana ndipo ziende mahakamani.

Jaji Mkuu Prof. Juma, ameipongeza Wizara ya Katiba na Sheria kwa kuweka mazingira ya kisheria ya kusuluhisha migogoro nje ya Mahakama kwa kutoa orodha ya wasuluhishi. (d) Mihimili ya Bunge na Serikali Inatambua Usuluhishi ni Tiba ya Ucheleweshwaji wa Mashauri Mahakamani. Kauli mbiu hii, inatoa tahadhari kwa Majaji, Mahakimu, Mawakili wa Serikali na Mawakili wa Kujitegemea ambao ndio wahusika wakubwa wa uendeshaji wa mashauri Mahakamani. Mihimili ya Bunge na Serikali, tayari imeelewa kuwa dawa ya ucheleweshwaji wa mashauri Mahakamani ni usuluhishi ambao tayari umewezeshwa kwa kutungiwa Sheria nyingi katika maeneo mbali mbali ambayo usuluhishi unawezekana.

Mhimili wa Mahakama na wadau wake, wataonekana kuwa wameshindwa mtihani wa viapo vyao na wajibu wao kulinda na kutetea Katiba na Sheria za nchi wasipotekeleza wajibu wao wa kufanikisha Usuluhishi. Wananchi wanayo haki kuwashtaki mhimili wa Mahakama kwa mhimili wa Bunge, wakiona haki inachelewa kwa kujiuliza kwa nini Mhimili wa Mahakama hautumii Sheria zilizotungwa na Bunge, kuwasaidia wananchi kutatua migogoro kwa njia ya Usuluhishi?.

Mhimili wa serikali usipotenda haki unaweza kushitakiwa kwenye mhimili wa Mahakama na mahakama iakiamuru serikali kutenda haki, lakini ikitokea mhimili wa Bunge kutotenda haki kama Bunge letu kututungia sheria batili zinazokwenda kinyume cha katiba, na mahakama ikauthibitisha ubatili huo, kwanza ilipaswa Mahakama kuzibatilisha sheria batili hizo pale pale zilipothibisha ubatili wa kwenda kinyume cha katiba kwasababu ubatili huu ni ubatili wa void ab initio.

Bunge litunge sheria batili inayokwenda kinyume cha katiba, mahakama ikathibitisha sheria hiyo ni batili, kwanini Mahakama Kuu haikubatilisha sheria hiyo pale pale na badala yake kuiamuru serikali kuibadili na Mahakama ya Rufaa ikaurudisha ubatili huo kwa Bunge lile lile lililotunga ubatili huo ndio liuondoe hii imekaaje?.
Baada ya Bunge kutunga sheria batili ilitakiwa
1. Sheria batili ile kubatilishwa pale pale
2. Bunge lilipaswa kuadhibiwa kwa kutunga sheria batili
3. Bunge kuariwa kutunga sheria halali.
Lakini mfumo wetu hauna utaratibu wowote wa kuliadhibu Bunge letu linapokosea!.

Na mhimili wa Mahakama ni vivyo hivyo, mhimili wa Mahakama unapo wakosea wananchi kwa kutowatendea haki, ilibidi wananchi wawe na uwezo wa kuishitaki Mahakama kwa mhimili wa Bunge na Bunge kuwa na uwezo wa kuiadhibu mahakama pale ambapo mahakamani haijatenda haki kwa Watanzania, na mfano mzuri ni ile kesi ya Mtikila ya mgombea binafsi.

Mahakama Kuu imetamka wazi shurti la kudhaminiwa na chama cha siasa kugombea uongozi ni shurti batili linakwenda kinyume cha katiba na kuamuru mgombea binafsi rukhsa na kuiamuru serikali kuandaa utaratibu. Mahakama ya Rufaa ukawakosea sana Watanzania kwa kulirejesha suala hili Bungeni, hakuna utaratibu wowote rasmi wa kuishitaki mahakama pale mahahama isipotenda haki, zaidi ya kuwatuma wabunge wetu kulalama tuu Bungeni la Bunge haliwezi kuufanya chochote mhimili wa Mahakama!.

Upo ushahidi kuwa Mihimili ya Bunge na Serikali ina ufahamu mkubwa kuhusu manufaa ya usuluhishi. Mhimili wa Mahakama na Wadau wake tukiwemo sisi mawakili, tutajiweka katika mazingira hatari mbele ya macho ya wananchi, endapo hatuzitumii Sheria zinazotoa nafasi za usuhishi na Sheria zinazotuzuia kutumia kanuni za kiufundi kuchelewesha haki.

Tukutane wiki ijayo kwa muendelezo wa makala hii kuhusu umuhimu wa usuluhishi na jinsi Rais Samia anavyotumia usuluhishi kuliponya taifa letu kisiasa hivyo kujikuta tunajiponya kiuchumi na kijamii.

Wasalaam

Paskali
Mimi tangu aliyekuwa Jaji Mkuu Chande alipomlalamikia Magufuli aliyekuwa Rais kuhusu mahakama kukwazwa na vimemo vya maamuzi ya kesi, nikajua kuwa kumbe kuna likangaruu likubwa kuliko ka Chadema, hili tumelishuhudi kwenye mienendo ya kesi nyingi na Rais Samia amewahi kuliongelea hili, tumebaki tukiandika kuonesha umahili wetu kwenye kuchambua mambo bila kuchukua hatua!
 
... keywords - USULUHISHI, KULIPONYA TAIFA, MIGOGORO, KUKOSA HAKI; kwanini hayo yalitokea in the recent past na sio kabla?
Mkuu dudus , naunga mkono hoja, ila mambo ya kuhitaji usuluhishi sio kuwa ndiyo yametokea in the recent past, yalikuwepo tangu zamani ila watu walikuwa hawajui haki zao as a result kunakuwa kama hakuna migogoro.
Mwl. Nyerere alituasa sana sana sana kwamba kwa Katiba hii akiinuka mwendawazimu, ole ni wenu! Ni bahati mbaya sana naye aliishia kuasa tu bila ku-take action ya maana kuhusu Katiba ya nchi.
Ni kweli Mwalimu Nyerere, alizungumzia hili la katiba ya kidikiteta na mimi niliwahi kuuliza humu Udikiteta ni dhana tu au ni real? Lets call a spade a spade. Dikteta ni mtu mwenye tabia hizi
Kiini cha tatizo ni ukosefu wa chombo madhubuti kinachowapa uwezo wananchi ku-regulate matendo ya viongozi na badala yake madaraka yote ya nchi wamerundikiwa wachache na kinga juu;
Naunga mkono hoja, hivyo nataka tuibue mjadala, kama katiba ni ya wananchi, serikali, Bunge na Mahakama ni mali ya wananchi, hivyo wananchi, lazima wawe na uwezo wa kuiwajibisha serikali Bunge na Mahakama pale inapowakosea.
hizo nyingine hadithi tu! Kama hatujajifunza kwa yaliyotokea, tutakuwa na kasoro kubwa.
Kiukweli kama ni kujifunza kwa yaliyotokea, tumejifunza sana tuu.
P
 
Watawala wanapowashauri watawaliwa watumie usuluhisho ni kuwa wao wameshindwa kuzilinda mahakama zitende haki kwenye maamuzi ya mashauri bila kuziingilia.
 
Back
Top Bottom