Tekelinalokujia
JF-Expert Member
- Sep 9, 2010
- 353
- 40
Usiku mmoja majira ya saa mbili hivi washkaji wawili walikua wanatoka kwenye kibarua chao cha kuchimba kisima wanaelekea makwao, walikua wamevuta bangi kabla hawajatoka eneo la kazi, sasa wakiwa wanakatiza vichochoroni watokee barabara kubwa wapate basi, siku hiyo ilikua na mbalamwezi, mmoja akamuuliza mwenzake, hivi lile ni jua? akimaanisha ule mwezi ulioandama, yule mwenzake akauangalia ule mwezi kwa makini kidogo akitafakari alafu akamjibu rafiki yake, kwa kweli sina uhakika maana mimi maeneo haya sio mwenyeji. wakaendelea na safari yao.