BURTON JNR
Member
- Jul 16, 2014
- 60
- 15
Waandishi wa habari na maafisa usalama wapo kufuatilia mgomo polisi unalinda nguvu ya umma.
Leo tarehe 19, Novemba 2014, wanafunzi wamegoma kuingia darasan kwa sababu zilizotajwa kuwa kikwazo kikubwa chuoni hapo kama: alama zake kuwa juu.
Wanafunzi kufelishwa maksud na kuombwa rushwa ya ngono kwa wasichana, upungufu wa viti, ubovu wa vyoo, ubadhirifu wa fedha za wanafunzi.
Walimu kutolipwa mishahara, kuonekana kwa majina ya walokufa zamani kwenye prospectus na kuingiliwa kwa serikali ya wanafunzi na uongozi wa chuo, W
Wanafunzi wote wameonekana kuzagaa uwanja wa mpira wa chuo hicho. Huku nyimbo za ROMA MKATORIKI NA NEY WA MITEGO zikilindima kwenye mitambo ya DJ MULLA.