Radash
Member
- Dec 12, 2012
- 41
- 16
Habarini za asubuhi mabibi na mabwana,
Hivi kuna nini kinaendelea kati ya PPF na SSRA? Ni hivi nilikuwa mwajiriwa katika taasisi flani ya binafsi hapa mjini. Nimefanya kwa miaka 5 huku nikiwa mwanachama wa PPF, baada ya mkataba kwisha nikaamua niachane na ajira niwe mjasiriamali.
Nikaamua ngoja nifatilie mafao yangu PPF ili kuongeza kamtaji kangu, PPF wakasema hawatoi kitu na hiyo ni order kutoka SSRA nikasema msinitanie nikaenda hadi ofisi za SSRA kuwauliza kulikoni wakasema ni kweli PPF walikuwa hawatoi mafao lakini wiki iliyopita waliwaita na kuwambia walipe watu mafao. Sasa narudi PPF makao makuu wanasema hawana taarifa yoyote ya kulipa kutoka SSRA na hawalipi kitu.
Sasa najiuliza nani mkweli kati ya SSRA NA PPF? Kwanini mnatunyanyasa na hela ni zetu? Magufuli tupia jicho SSRA na PPF wanakuhujumu hawa watu bado hawajakuelewa kabisa.
Ahsante.
Hivi kuna nini kinaendelea kati ya PPF na SSRA? Ni hivi nilikuwa mwajiriwa katika taasisi flani ya binafsi hapa mjini. Nimefanya kwa miaka 5 huku nikiwa mwanachama wa PPF, baada ya mkataba kwisha nikaamua niachane na ajira niwe mjasiriamali.
Nikaamua ngoja nifatilie mafao yangu PPF ili kuongeza kamtaji kangu, PPF wakasema hawatoi kitu na hiyo ni order kutoka SSRA nikasema msinitanie nikaenda hadi ofisi za SSRA kuwauliza kulikoni wakasema ni kweli PPF walikuwa hawatoi mafao lakini wiki iliyopita waliwaita na kuwambia walipe watu mafao. Sasa narudi PPF makao makuu wanasema hawana taarifa yoyote ya kulipa kutoka SSRA na hawalipi kitu.
Sasa najiuliza nani mkweli kati ya SSRA NA PPF? Kwanini mnatunyanyasa na hela ni zetu? Magufuli tupia jicho SSRA na PPF wanakuhujumu hawa watu bado hawajakuelewa kabisa.
Ahsante.