Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,815
- 4,565
Upo msemo unaosema kuwa ili ndoa iweze kudumu kwa muda mrefu, mke usishike simu ya mme wako, na Mme usishike simu ya Mke wako.
Lakini kwa watu wengine Mke au Mme hushika na kuperuzi simu za wenza wao.
Mkuu wa Polisi Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu SSP. Selestino Sylvester kwa wenza, amefafanua usemi huo na kusema kuwa kushika simu ya mwenza wako na kuanza kuperuzi ni kosa la Jinai.
SSP Sylvester amesema hayo leo wakati wa maazimisho ya siku ya sheria yaliyo
fanyika katika viwanja vya Mahakama ya Wilaya hiyo, ambapo amewataka wenza kuacha tabia hiyo.