SAKATA la tuhuma za ufisadi bungeni limeingia katika hatua mpya, baada ya Spika wa Bunge, Anne Makinda kuamua kuunda Kamati ndogo ya watu watano kuchunguza tuhuma za baadhi ya wabunge kuhongwa, kwa lengo la kushawishi uamuzi unaofaa kuchukulia katika chombo hicho cha kutunga sheria.
Uamuzi huo ambao Spika aliutangaza jana baada ya kipindi cha maswali na majibu Bungeni, unauweka kando ule wa awali, ambao ulikuwa ni kulipeleka suala hilo katika Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, ambapo alikuwa ameahidi kuwaengua wote watakaoonekana kuwa, wana mgongano wa kimaslahi na suala linalotakiwa kuchunguzwa.
<<<<HABARI KAMILI>>>>