Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
INAWEZA kuwa kama simulizi lakini ni ukweli mtupu. Baada ya kujikuta nikimuoa shangazi yangu kutokana na kufanya naye mapenzi kwa njia ya simu kwa muda wa mwaka mmoja.
Uhusiano wetu ulianza baada ya shangazi ambaye sasa ni mke wangu kukuta ‘missed calls' kwenye simu yake na kuamua kunipigia kutaka kujua mimi ni nani.
Lakini katika hali ya kushangaza sikupiga simu kwake kwa sababu tulikuwa hatujuani hata kwa sura.
Alipiga simu na kusema kuwa yeye yupo Arusha wakati mimi nipo Dar es Salaam. Nilimwambia kuwa sikumpigia simu kwa sababu sikumfahamu. Nilipomuambia hivyo alicheka na kukata simu.
Zilipita kama siku mbili shangazi alinitumia sms ya kunijulia hali nami nikamjibu. "Habari yako kaka, nimeona leo nikukumbuke kwani tangu siku ile hatujaongea tena, nimekukumbuka kweli."
"Usijali, tupo pamoja nami pia nimekukumbuka. Nilikuwa natafuta muda wa kukupigia simu lakini kutokana na kubanwa na majukumu nikashindwa."
"Oke, hakuna shida, nikutakie siku njema ila kuna swali nilitaka kukuuliza kabla sijakuaga."
"Swali gani tena hilo, wewe uliza tu nitakujibu usiwe na wasiwasi."
"Samahani kama nitakukosea maana simu ndiyo imetufanya tujuane."
"Kweli kabisa, nami nimekwambia usijali wewe uliza tu nitakujibu."
"Umeoa?"
"Hapana sijaoa, wewe umeolewa?"
"Bado, nashukuru kwa kutambua hilo, nakutakia siku njema."
"Oke, wewe pia Mungu akubariki kwa kazi uifanyayo."
Baada ya muda nilianza kujiuliza kwa nini aliniuliza swali la kama nimeoa. Mara mawazo ya kimapenzi yakaanza kuutesa moyo wangu.
Siku iliyofuata sms iliingia kwenye simu yangu kutoka kwa shangazi. "Hellow dear, mzima? Nimekukumbuka sana, natamani kuiona sura yako."
Ujumbe ule ulinifanya nishtuke kidogo, lakini kwa kuwa mawazo yangu yalikuwa yameanza kuelekea kumpenda kimahaba mwanamke yule niliamua kumjibu.
"Hellow sweat, mimi mzima hofu na mashaka ni kwako, nami pia natamani kukutana nawe ili niione sura yako."
Tulianza kutumiana sms za mapenzi tangu siku hiyo. Nilimuuliza jina lake alinitajia moja tu la Susan. Sikuwa na mawazo kama angeweza kuwa ni shangazi yangu.
Hali ya kutumiana sms iliimarisha penzi letu na kumfanya kila moja kuwa na shauku ya kumuona mwenzake.
Tukiwa katika hali hiyo ya kuchati kwa njia ya sms, ilifika kipindi tukawa tunatoshelezana kwa njia hiyo kwani miili ilikuwa ikisisimka kwelikweli.
Baada ya mwaka mmoja kuisha tulifanya taratibu za kukutana na tukafanikiwa kuonana na kuanza mikakati ya kuoana.
Habari za kwamba yeye ni shangazi yangu zilijulikana baada ya kwenda kujitambulisha kwao. Ndugu zetu walishangaa kuona nimekuwa na uhusiano wa kimapenzi kwa njia ya simu na shangazi yangu.
Kwa kuwa tulikuwa tayari tumeshamaliza kila kitu kwa njia ya sms, sikuona haja ya kusitisha uhusiano wetu, nikaamua kumuoa japo ndugu zetu wa pande zote mbili wameamua kututenga kwa madai kuwa tumewaaibisha
Chanzo: http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/sms-zimenifanya-nimuoe-shangazi-yangu
Uhusiano wetu ulianza baada ya shangazi ambaye sasa ni mke wangu kukuta ‘missed calls' kwenye simu yake na kuamua kunipigia kutaka kujua mimi ni nani.
Lakini katika hali ya kushangaza sikupiga simu kwake kwa sababu tulikuwa hatujuani hata kwa sura.
Alipiga simu na kusema kuwa yeye yupo Arusha wakati mimi nipo Dar es Salaam. Nilimwambia kuwa sikumpigia simu kwa sababu sikumfahamu. Nilipomuambia hivyo alicheka na kukata simu.
Zilipita kama siku mbili shangazi alinitumia sms ya kunijulia hali nami nikamjibu. "Habari yako kaka, nimeona leo nikukumbuke kwani tangu siku ile hatujaongea tena, nimekukumbuka kweli."
"Usijali, tupo pamoja nami pia nimekukumbuka. Nilikuwa natafuta muda wa kukupigia simu lakini kutokana na kubanwa na majukumu nikashindwa."
"Oke, hakuna shida, nikutakie siku njema ila kuna swali nilitaka kukuuliza kabla sijakuaga."
"Swali gani tena hilo, wewe uliza tu nitakujibu usiwe na wasiwasi."
"Samahani kama nitakukosea maana simu ndiyo imetufanya tujuane."
"Kweli kabisa, nami nimekwambia usijali wewe uliza tu nitakujibu."
"Umeoa?"
"Hapana sijaoa, wewe umeolewa?"
"Bado, nashukuru kwa kutambua hilo, nakutakia siku njema."
"Oke, wewe pia Mungu akubariki kwa kazi uifanyayo."
Baada ya muda nilianza kujiuliza kwa nini aliniuliza swali la kama nimeoa. Mara mawazo ya kimapenzi yakaanza kuutesa moyo wangu.
Siku iliyofuata sms iliingia kwenye simu yangu kutoka kwa shangazi. "Hellow dear, mzima? Nimekukumbuka sana, natamani kuiona sura yako."
Ujumbe ule ulinifanya nishtuke kidogo, lakini kwa kuwa mawazo yangu yalikuwa yameanza kuelekea kumpenda kimahaba mwanamke yule niliamua kumjibu.
"Hellow sweat, mimi mzima hofu na mashaka ni kwako, nami pia natamani kukutana nawe ili niione sura yako."
Tulianza kutumiana sms za mapenzi tangu siku hiyo. Nilimuuliza jina lake alinitajia moja tu la Susan. Sikuwa na mawazo kama angeweza kuwa ni shangazi yangu.
Hali ya kutumiana sms iliimarisha penzi letu na kumfanya kila moja kuwa na shauku ya kumuona mwenzake.
Tukiwa katika hali hiyo ya kuchati kwa njia ya sms, ilifika kipindi tukawa tunatoshelezana kwa njia hiyo kwani miili ilikuwa ikisisimka kwelikweli.
Baada ya mwaka mmoja kuisha tulifanya taratibu za kukutana na tukafanikiwa kuonana na kuanza mikakati ya kuoana.
Habari za kwamba yeye ni shangazi yangu zilijulikana baada ya kwenda kujitambulisha kwao. Ndugu zetu walishangaa kuona nimekuwa na uhusiano wa kimapenzi kwa njia ya simu na shangazi yangu.
Kwa kuwa tulikuwa tayari tumeshamaliza kila kitu kwa njia ya sms, sikuona haja ya kusitisha uhusiano wetu, nikaamua kumuoa japo ndugu zetu wa pande zote mbili wameamua kututenga kwa madai kuwa tumewaaibisha
Chanzo: http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/sms-zimenifanya-nimuoe-shangazi-yangu