Slaa alipua kombora jingine

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
Na Mwandishi wetu - Tanzania Daima

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbord Slaa, amelipua kombora jingine kwa kuziweka hadharani kampuni zilizoshindwa kurejesha fedha za madeni ya malipo ya nje (EPA) kwa kile alichokiita kukingiwa kifua na vigogo wa serikali.

Hatua ya Dk. Slaa imekuja ikiwa ni siku mbili tu tangu alipomshukia Rais Jakaya Kikwete akimsakama kwa kushindwa kuwashughulikia watuhumiwa wa ufisadi na kutatua matatizo ya kiuchumi ambayo yameiyumbisha nchi.


Akizungumza na Tanzania Daima jana, Dk. Slaa alisema kuwa pamoja na kauli za ukali zilizotolewa na Rais Kikwete muda mrefu uliopita, akiwataka waliokwapua fedha za EPA kuzirejesha kwa hiyari yao wenyewe na kutishia kuwachukulia hatua za kisheria, hadi sasa ni kampuni nane tu kati ya 21 zilizorejesha fedha hizo.



Alisema kuwa ni jambo la kusikitisha kuwa Rais Kikwete amekaa kimya bila kuchukua hatua wala kusema chochote dhidi ya kampuni zilizodharau agizo lake na kwamba inaonyesha ni jinsi gani serikali na CCM imeelemewa na ufisadi na imeshindwa kuchukua hatua kwa kuwa ufisadi umejikita katika mfumo mzima unaowagusa pia viongozi waandamizi katika chama na serikali.



Alionya kuwa kwa kuwa serikali imeshindwa kutekeleza wajibu huo, namna pekee ya kusimamia uwajibikaji ni kwa kuunganisha nguvu za wananchi katika kutetea rasilimali za taifa.



Slaa alitaja kampuni zilizorejesha fedha hizo na kiasi katika mabano kuwa ni Bencon International Ltd iliyorejesha sh bilioni 7.96 kati ya bilioni 10.56 ilizokwapua; Njake Hotels and Tours & Njake Enterprises Ltd iliyorejesha fedha zote sh bilioni 2.225; na Ndovu Soap sh bilioni 1.548 ambazo ni kiasi chote ilichokuwa imekichukua.



Nyingine zilizorejesha fedha zote zilizokuwa zimechotwa ni pamoja na Kagoda Agriculture, (bilioni 34.781), VB & Associated (bilioni 9.227), VB Holdings Ltd (bilioni 5.148), Venus Hotels & Apartments Ltd (bilioni 4.050) na Bora Hotels & Apartments Ltd (bilioni 5.779).


Hata hivyo, alizitaja kampuni 13 ambazo zimegoma kurejesha fedha hizo (majina tunayo) na kwamba hazijalipa jumla ya fedha zote zinazokisiwa kufikia sh bilioni 50.


Dk. Slaa alidai kuwa CHADEMA ilitarajia kwamba mwaka 2011 ulikuwa wa kukamilisha uchunguzi na uchukuaji wa hatua dhidi ya wahusika katika kashfa mbalimbali ili kurejesha utamaduni wa uwajibikaji. Badala yake serikali imeendelea kuahirisha kuchukua hatua kamili serikalini, bungeni na hata ndani ya chama chenyewe.


Aliongeza kuwa katika hali ya kusikitisha Rais Kikwete katika hotuba yake kwa taifa ya Disemba 31, 2011 hakuzungumzia hatua ambazo serikali yake imefikia katika kushughulikia mafisadi.


Juzi akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na hotuba ya Rais Kikwete ya kufunga mwaka, Dk. Slaa alidai kuwa hali ya uchumi inazidi kudorora na serikali haionyeshi mikakati yoyote ya kulinusuru taifa.



Alisema kuwa badala yake, Rais Kikwete amekuwa akitoa majibu yanaisukumia lawama hali mbaya ya uchumi ya kidunia, wakati angeweza kufanya jitihada za kuondokana na hali hiyo, na hasa kuwachukulia hatua watu wote wanaotuhumiwa kuhujumu mali ya taifa.

 
Kiongozi hodari huwa hachoki kupigania haki za wanyonge.Hongera Dr. Kwa kutufungua macho wadanganyika
 
hatahivyo wanainchi waelimike maisha yamekuwa siyo kira kitu sasa juu 2015 chagueni chadema chadema hoooyeee
 
kikwete hawawezi wezi waliomuweka madarakani.....hawezi kuwafanya lolote.

Nazi yake ubwabwa.
 
Eee Mungu fanya lolote kwa ajil ya taifa la TZ, tuepushe na huu uongozi wa Kikwete! Mapenz yako yatimizwe juu ya serikal yake nzima.
Mpe nguvu na afya njema Baba ye2 na rais anaestahil kuiongoza nchi na s kuitawala Tz, Dkt SLAA! Shusha adhabu juu ya viongoz wote wala rushwa na wale wasio tenda haki. Eee Mungu ikumbuke Tz, kwan kwako tunakuja kwa ku2bu na kwa kunyenyekea. Kwa Jina lako takatifu naomba,.. wote tuseme!
Amen.....!
 
​ndo nini sasa kutaja zilizorejesha pesa na kutotaja ambazo hazijarejesha peasa?????arrrrrrggggggggghhhhh
 
piga keleleeeee! sema chadema, chadema, chadema, chadema, chadema, chadema, chadema, chadema, chadema,
 
Jamani Dr Slaa alianza kuyasema Bungeni hakurupukiiiii>>>>>> Kikwete kaa chonjo Saa ni mbaya hii..Watanzania tumechoka na Mibunge inatafuna mifwedha ya Nchi upo kimya,,Wanyama wameporwa upo kimya, Dhahabu Zinapelekwa nje upo kimya, Na hii mifisadi unaiangalia tuu kwani mifedha yote hii imakaliwa na watu kwa mifuko yao..utayajutia haya siku ya siku..
 
Huyu nae kesha choooka maana ukiona mtu anatupa makombora kila kuchapo bila ya kombora kulipuka na kuleta tija basi jua mtu huyo hajasomea vizuri namna ya kulipoa kombora!

Namshauri huyu padre apumzike tu kwa sasa na kazi hizi awaachie vijana kama zito, mbowe,mnyika nk...
 
Huyo ndie DR slaaaaaa Bana .hakuna kuzungumzia oooh sijui fulani kafukuzwa chama anaongelea vitu vyenye mashiko na umuhimu juu ya mustakabali wa Nchi yetu .hongera mzee
 
Na Mwandishi wetu - Tanzania Daima

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbord Slaa, amelipua kombora jingine kwa kuziweka hadharani kampuni zilizoshindwa kurejesha fedha za madeni ya malipo ya nje (EPA) kwa kile alichokiita kukingiwa kifua na vigogo wa serikali.

Hatua ya Dk. Slaa imekuja ikiwa ni siku mbili tu tangu alipomshukia Rais Jakaya Kikwete akimsakama kwa kushindwa kuwashughulikia watuhumiwa wa ufisadi na kutatua matatizo ya kiuchumi ambayo yameiyumbisha nchi.


Akizungumza na Tanzania Daima jana, Dk. Slaa alisema kuwa pamoja na kauli za ukali zilizotolewa na Rais Kikwete muda mrefu uliopita, akiwataka waliokwapua fedha za EPA kuzirejesha kwa hiyari yao wenyewe na kutishia kuwachukulia hatua za kisheria, hadi sasa ni kampuni nane tu kati ya 21 zilizorejesha fedha hizo.



Alisema kuwa ni jambo la kusikitisha kuwa Rais Kikwete amekaa kimya bila kuchukua hatua wala kusema chochote dhidi ya kampuni zilizodharau agizo lake na kwamba inaonyesha ni jinsi gani serikali na CCM imeelemewa na ufisadi na imeshindwa kuchukua hatua kwa kuwa ufisadi umejikita katika mfumo mzima unaowagusa pia viongozi waandamizi katika chama na serikali.



Alionya kuwa kwa kuwa serikali imeshindwa kutekeleza wajibu huo, namna pekee ya kusimamia uwajibikaji ni kwa kuunganisha nguvu za wananchi katika kutetea rasilimali za taifa.



Slaa alitaja kampuni zilizorejesha fedha hizo na kiasi katika mabano kuwa ni Bencon International Ltd iliyorejesha sh bilioni 7.96 kati ya bilioni 10.56 ilizokwapua; Njake Hotels and Tours & Njake Enterprises Ltd iliyorejesha fedha zote sh bilioni 2.225; na Ndovu Soap sh bilioni 1.548 ambazo ni kiasi chote ilichokuwa imekichukua.



Nyingine zilizorejesha fedha zote zilizokuwa zimechotwa ni pamoja na Kagoda Agriculture, (bilioni 34.781), VB & Associated (bilioni 9.227), VB Holdings Ltd (bilioni 5.148), Venus Hotels & Apartments Ltd (bilioni 4.050) na Bora Hotels & Apartments Ltd (bilioni 5.779).


Hata hivyo, alizitaja kampuni 13 ambazo zimegoma kurejesha fedha hizo (majina tunayo) na kwamba hazijalipa jumla ya fedha zote zinazokisiwa kufikia sh bilioni 50.


Dk. Slaa alidai kuwa CHADEMA ilitarajia kwamba mwaka 2011 ulikuwa wa kukamilisha uchunguzi na uchukuaji wa hatua dhidi ya wahusika katika kashfa mbalimbali ili kurejesha utamaduni wa uwajibikaji. Badala yake serikali imeendelea kuahirisha kuchukua hatua kamili serikalini, bungeni na hata ndani ya chama chenyewe.


Aliongeza kuwa katika hali ya kusikitisha Rais Kikwete katika hotuba yake kwa taifa ya Disemba 31, 2011 hakuzungumzia hatua ambazo serikali yake imefikia katika kushughulikia mafisadi.


Juzi akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na hotuba ya Rais Kikwete ya kufunga mwaka, Dk. Slaa alidai kuwa hali ya uchumi inazidi kudorora na serikali haionyeshi mikakati yoyote ya kulinusuru taifa.



Alisema kuwa badala yake, Rais Kikwete amekuwa akitoa majibu yanaisukumia lawama hali mbaya ya uchumi ya kidunia, wakati angeweza kufanya jitihada za kuondokana na hali hiyo, na hasa kuwachukulia hatua watu wote wanaotuhumiwa kuhujumu mali ya taifa.


Najuta kukichagua Chama Tawala,kila mtu hata watoto wadogo ongea nao wanachukia uamuzi wa watanzania walio wengi kukipa kura 2010,2015 bado ni mbali sana lakini hata wao hawastuki.Kila kukicha oooh mara wanajivua gamba,oooh mara wanawalazimisha wapiga kura wapige mbizi,mwingine huku Rombo yeye kipindi fulani alitulazimisha tule majani fasta tulimtungua,muulizeni lakini hata sijui kesi yake iko wapi.
 
Huyu nae kesha choooka maana ukiona mtu anatupa makombora kila kuchapo bila ya kombora kulipuka na kuleta tija basi jua mtu huyo hajasomea vizuri namna ya kulipoa kombora!

Namshauri huyu padre apumzike tu kwa sasa na kazi hizi awaachie vijana kama zito, mbowe,mnyika nk...

Kama waliochoka wanatakiwa wawaachie vijana, huyu anayelalamikiwa kwa kushindwa kuwachukulia hatua wezi unampa ujumbe gani?
 
Na Mwandishi wetu - Tanzania Daima

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbord Slaa, amelipua kombora jingine kwa kuziweka hadharani kampuni zilizoshindwa kurejesha fedha za madeni ya malipo ya nje (EPA) kwa kile alichokiita kukingiwa kifua na vigogo wa serikali.

Hatua ya Dk. Slaa imekuja ikiwa ni siku mbili tu tangu alipomshukia Rais Jakaya Kikwete akimsakama kwa kushindwa kuwashughulikia watuhumiwa wa ufisadi na kutatua matatizo ya kiuchumi ambayo yameiyumbisha nchi.


Akizungumza na Tanzania Daima jana, Dk. Slaa alisema kuwa pamoja na kauli za ukali zilizotolewa na Rais Kikwete muda mrefu uliopita, akiwataka waliokwapua fedha za EPA kuzirejesha kwa hiyari yao wenyewe na kutishia kuwachukulia hatua za kisheria, hadi sasa ni kampuni nane tu kati ya 21 zilizorejesha fedha hizo.



Alisema kuwa ni jambo la kusikitisha kuwa Rais Kikwete amekaa kimya bila kuchukua hatua wala kusema chochote dhidi ya kampuni zilizodharau agizo lake na kwamba inaonyesha ni jinsi gani serikali na CCM imeelemewa na ufisadi na imeshindwa kuchukua hatua kwa kuwa ufisadi umejikita katika mfumo mzima unaowagusa pia viongozi waandamizi katika chama na serikali.



Alionya kuwa kwa kuwa serikali imeshindwa kutekeleza wajibu huo, namna pekee ya kusimamia uwajibikaji ni kwa kuunganisha nguvu za wananchi katika kutetea rasilimali za taifa.



Slaa alitaja kampuni zilizorejesha fedha hizo na kiasi katika mabano kuwa ni Bencon International Ltd iliyorejesha sh bilioni 7.96 kati ya bilioni 10.56 ilizokwapua; Njake Hotels and Tours & Njake Enterprises Ltd iliyorejesha fedha zote sh bilioni 2.225; na Ndovu Soap sh bilioni 1.548 ambazo ni kiasi chote ilichokuwa imekichukua.



Nyingine zilizorejesha fedha zote zilizokuwa zimechotwa ni pamoja na Kagoda Agriculture, (bilioni 34.781), VB & Associated (bilioni 9.227), VB Holdings Ltd (bilioni 5.148), Venus Hotels & Apartments Ltd (bilioni 4.050) na Bora Hotels & Apartments Ltd (bilioni 5.779).


Hata hivyo, alizitaja kampuni 13 ambazo zimegoma kurejesha fedha hizo (majina tunayo) na kwamba hazijalipa jumla ya fedha zote zinazokisiwa kufikia sh bilioni 50.


Dk. Slaa alidai kuwa CHADEMA ilitarajia kwamba mwaka 2011 ulikuwa wa kukamilisha uchunguzi na uchukuaji wa hatua dhidi ya wahusika katika kashfa mbalimbali ili kurejesha utamaduni wa uwajibikaji. Badala yake serikali imeendelea kuahirisha kuchukua hatua kamili serikalini, bungeni na hata ndani ya chama chenyewe.


Aliongeza kuwa katika hali ya kusikitisha Rais Kikwete katika hotuba yake kwa taifa ya Disemba 31, 2011 hakuzungumzia hatua ambazo serikali yake imefikia katika kushughulikia mafisadi.


Juzi akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na hotuba ya Rais Kikwete ya kufunga mwaka, Dk. Slaa alidai kuwa hali ya uchumi inazidi kudorora na serikali haionyeshi mikakati yoyote ya kulinusuru taifa.



Alisema kuwa badala yake, Rais Kikwete amekuwa akitoa majibu yanaisukumia lawama hali mbaya ya uchumi ya kidunia, wakati angeweza kufanya jitihada za kuondokana na hali hiyo, na hasa kuwachukulia hatua watu wote wanaotuhumiwa kuhujumu mali ya taifa.


Ziko wapi?
 
Back
Top Bottom