Sitta kuongoza shughuli za Serikali Bungeni wiki hii

Pinda anaogopa mishale ya CDM, pia anakwenda nje ya nchi ili apate posho ili azigawe kwa ndugu zake, maslahi ya nchi hakuna ki2 hapa, we utaona ujumbe atakao ongozana nao.
 
Hii ndiyo nafasi iliyomgombanisha Sitta na EL. Nadhani Mh Pinda hakufurahishwa na comments za EL siku chache zilizopita alipokuwa akichangia kwenye hotuba ya bajeti ya ofisi ya WM. Siasa za Nchi hii tamu kwelikweli.
. mh sitta ana deserve ku-act nafasi ya waziri mkuu,huyo ni senior minister,kwani kabla ya hapo mh mohamed seif ndiye aliyekuwa akikaimu
 
WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta atakahimu nafasi Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuongoza shughuli za Serikali bungeni kwa kuwa anatarajiwa kuondoka nchini wakati wowote kwenda Brazil kikazi.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu na Bunge mjini Dodoma, ziara ya Pinda ina lengo la kuvutia uwekezaji wa nishati ya gesi kwa ajili ya kuzalisha umeme.

Taarifa hiyo iliongeza kwamba tayari Brazil imeonyesha dhamira ya kutafiti nishati ya gesi katika Ukanda wa Kusini na katika mpango huo nchi hiyo imekusudia kuweka mtambo mkubwa wa kutafiti gesi ukanda wa Mtwara ili kumaliza tatizo la nishati ya umeme.

Kufuatia ziara hiyo ya kiserikali, Waziri Sitta atakaimu nafasi yake bungeni kwa wiki nzima mpaka Julai 11, mwaka huu.Mkutano wa Bunge unatarajiwa kuendelea baada ya mapumziko ya mwisho mwa wiki na wabunge leo watapokea makadirio ya bajeti katika wizara mbili zilizopo chini ya Ofisi ya Rais.

Wizara zinazotarajia kuwasilisha hotuba zao ni pamoja na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu ambazo mjadala wake utakwenda pamoja.

Wiki iliyopita wabunge walipitisha makadirio ya matumizi katika wizara na idara zilizo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Sh 197 bilioni zilipitishwa.

Leo wabunge wataanza kupokea makadirio ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hawa Ghasia kabla ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu, Stephen Wassira kuwasilisha na zote zitajadiliwa kwa siku mbili.

Jumatano mpaka Ijumaa Bunge litakuwa likijadili makadirio ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) ambazo zitajadiliwa kwa muda wa siku tatu mfululizo.
What is so special about kukaimu kwake.
 
Hivi w/mkuu kaambatana na ujumbe wa watu wangapi vile?...na je, gharama ya ziara yake ni kiasi gani vile?.....
Wakati mwingine ni bora kujua kidogo kuliko kutokujua kabisa
 
Asile goodtime kama bosi wake. Ajabu mkulu mwenyewe hajaamua kwenda kuwasaka hao waezuaji uchumi wetu. Wanatoa moja wanachukua mia moja na moja.

Ukiona hivyo Kikwete ana safari nyingine ndio maana amemwachia Pinda. Sidhani kama angeachia chance hii ya kwenda Brazil kuchekacheka na kubembea.
 
Hii ndiyo faida ya kuwa na mtoto wa mkulima,,,,,,,,,nchi ambazo hazina mtoto wa mkulima km wetu zinapata shida sana..................tehe chichiemu bana.....wanaifilisi nchi kwa miziara yao yenye kuambatana na ujumbe wa watu wengi na gharama kubwa
 
Angemkaimisha Lowassa bana!!! maana ana uzoefu na kazi hiyo.
 
Jamani hivi Membe anafanya kazi gani. Mbona hizi ndo kazi nadhani anatakiwa kushughulikia sasa Jk anaingilia kazi zake, safari hii mpaka Pinda nae kazamia, hii nchi u@£nge umezidi sio rais sio Pm hakuna mwenye msimamo.
 
so 6 anaweza kuyafanya yale maamuzi magumu na jamaa atakaporudi anakuta mabadiliko hawezi kuyatengua sasa wakati wa six kuonesha uzalendo wake au uhalisia wake
 
Kweli Wabunge Mnyika,Tundu lissu na Halima Mdee ni Hazina ya Kutunza kwa ajili ya Mustakbali wa Taifa Hili.Ukisikia watu wa Kazi ndio wale
Jioni hii nilikuwa nafatilia kipindi cha Bunge hasa Kipengee cha Kupitia Budget ya Wizara ya Nchi ofisi ya Makamu wa Rais(Muungano) iliyowasilishwa na Waziri Samia Suluhu baadae kujibu hoja kisha kupitiwa Kifungu kwa Kifungu!Kila waheshimiwa Mnyika na Lissu wakijenga hoja zao baada ya Kutoa Shilingai,Sita Anapotokea Akisimama kutete serikali Anaonekana kupwaya kwa kutoa Majibu ya Kuwaridhisha watoa Shilingi!Hadi hatua ya Mwenyekiti kuamua kura na ndipo hoja ya Shilingi inaposhindwa na Kura za Ndiyo na Hapana zile Makelele nafikiri Itikadi zinachangia ndio kushinda.Sita alikuwa anashindwa kufafanua jambo kwenye suala moja la Ukaguzi ktk Masuala ya Mazingira hadi Mh.Mnyika Akamlipua kwa kusema analidanganya Taifa!Afu Mnyika Akadadavua swala lenyewe!
Nae Mh.Ndugai Hayupo vizuri ktk ufafanuzu wa kikanuni za Bunge! alikuwa anababaika na Kutoa maelekezo kijujuu tu!Kazi Ipo kama hawa ndio Reserve ya Uongozi wa Serikali na Bunge basi Kazi tunayo!Manake jioni hii wote ni Wasaidizi wa Spika na wa PM!
Kazi ipo!Bora sisi wakulima tuliozoea yate!Mvua Kiduchu na Jua Kibao
 
Mkuu nimefuatilia kwa ujirani sana Mzee Sitta katolewa umaana na mnyika hadi akawa mdogo kama pilitoni. Viva John Mnyika
 
Kwanza Sitta hajawahi kuwa Naibu Kiongozi wa Serikali Bungeni ila wiki iliyopita ali-Kaimu Uongozi wa Serikali Bungeni.

Nikirudi kwenye mada ni kwamba ni vigumu mno mno kuitetea serikali ya JK ukafaulu. Ndiyo sababu watu makini walimshauri Sitta na Mwakyembe wajitoe kwenye Baraza hilo la Mawaziri lakini wao wamekomaa tu.
 
Back
Top Bottom