yusufummaka
Member
- Apr 7, 2012
- 30
- 20
Kama mwanamichezo na mpenzi wa Yanga naahidi kwa moyo wangu wote kwamba sintakujasikiliza kipindi cha spoti cha Radio One. Sababu: Nilipoteza muda wangu mwingi kusubiri kipindi cha michezo cha radio one cha tarehe 16.07.2012 ili kusikia matokeo ya uchaguzi wa Yanga uliofanyika jana. Mshangao: Maulidi Kitenge na mwenzie hawakutangaza nafasi ya Mwenyekiti alishinda nani, badala yake walitoa matokeo ya nafasi ya makamu mwenyekiti na wajumbe wengine. Hakiya mungu njaa itatuumiza, kumbe vyombo hivi vya habari haviko huru namna hii? Kitenge ni mtangazaji anayeheshimika na anayependwa na wanamichezo wengi, lakini leo nimempuuza kupita maelezo na anajipalia makaa ya moto kwenye taaluma yake. Yanga ni club ya watu wengi, ilikuwepo, ipo na itaendelea kuwepo kuliko Manji na Mengi, hawa wanapita tu. Hivi kitenge una akili timamu? Hivi ulitegemea John Jambele angeweza kumshinda Manji katika uchaguzi ule? Manji size yake ni Mh. R. Mengi sio Jambele we vipi!!!. Kitendo cha kutowafahamisha wasikilizaji wako nani kashinda nafasi ya mwenyekiti kiliwafanya watu wasonye na kupoteza imani na kipindi chako na hatimae na Radio one.
Siku nyingine nakuomba umshawishi Mengi achukue fomu agombee sio kumtumia mtu size ya Jambale, hiyo ingekuwa hadithi ya Daudi na Gorieth wa bibilia. Yanga Oyeee!!!!
Siku nyingine nakuomba umshawishi Mengi achukue fomu agombee sio kumtumia mtu size ya Jambale, hiyo ingekuwa hadithi ya Daudi na Gorieth wa bibilia. Yanga Oyeee!!!!