Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
WAZIRI wa Nishati na Madini, Willium Ngeleja amesema ni ngumu kujiuzulu kwa kuwa tatizo la umeme si la wizara yake pekee na kuwafumba midomo wale wanaotaka ajiuzulu licha ya Bajeti yake kukataliwa Bungeni |
Aliyasema hayo Mjini Dodoma wakati wabunge wengi wakitaka ajiuzulu mara tu bajeti yake ilipokataliwa bungeni kwa kuonekana hotuba hiyo haionyeshi tatizo la umeme Tanzania litaisha lini Hivyo Ngeleja alisema hawezi kujiuzulu kutokana na matakwa ya watu na kujitetea kuwa tatizo hilo si lake peke yake bali ni tatizo la serikali nzima Wabunge wanamtaka ajiuzulu ili kuwapisha watu wengine wanaoweza kukabiliana na wizara hiyo ili kuweza kuondoa tatizo la giza linaloendelea nchini ambao umeme linaonekana ni janga la kitaifa kwa kuwa watanzania hawana uhakika wa umeme Bajeti si ya wizara pekee, na mimi si ndiye niliyetenga kiasi cha fedha kinacholeta utata, muhimu tukae chini kwa muda tuliopewa kutafakari tufanye nini ili kuweza kulinusuru Taifa kuondokana na janga la umeme nchini, kuliko kunitaka kuachia ngazi alisema Ngeleja Wizara jhiyo imepewa muda wa wiki tatu kuja kutoa bajeti hiyo upya na kufafanua ni jinsi gani wamejipanga kukabiliana na tatizo la umeme linaloendelea nchini kote Tatizo la umeme ni janga sugu linaloendelea nchini Tanzania ambapo wajasiriamali wengi kuonekana kufunga ofisi zao kutokana na kukosekana kwa umeme kwa muda mwingi wakiwemo Saloon, Stationary, migahawa ya vinjwaji baridi, wanaotumia mashine mbalimbali ikiwemo na mashine za kusaga nafaka na hali hiyo kupelekea kuondoa ajira za watu waliokuwa wakiendesha ofisi hizo |
Chanzo: NIFAHAMISHE Tanzania news portal .: Habari za Tanzania :.