Sisi ndio wanaume bwana!

Mhh hataree
Homer-08-june.gif
Homer-09-june.gif

Happy Friday Babu Asprin ..
 
Habari zenu waungwana.....


Huu ni waraka kwa vijana/wavulana wanaokaribia kuwa WANAUME. Kuwa MWANAUME si mchezo na si lelemama. Ushawahi kusikia Chama cha Wanaume, Umoja wa Wanaume, Umoja wa Wanasheria Wanaume, Umoja wa Madaktari wanaume etc?........ Hii inamaanisha MWANAUME ni Taasisi inayojitegemea.
Mwanaume kamili aliyekamilika si kama yule aliyozungumzia Bishanga kwenye sredi yake (kwa makusudi siweki link yake hapa)
Ili uwe MWANAUME yakupasa kwanza kabisa kumshukuru Mungu kwa kuumbwa jinsia ya kiume. Umepewa upendeleo lazima ushukuru. Halafu:

1. Uwe RIJALI na MMILIKI (hili halihitaji ufafanuzi) Ukishakuwa rijali unapaswa uwe na UMILIKI. Umiliki wa mwanaume rijali ni umiliki wa MWANAMKE/WANAWAKE. Iwe rasmi au vinginevyo. (Umiliki wa watoto pia ni muhimu japokuwa hili lategemea zaidi mapenzi ya Mungu). Ikumbukwe kuwa Mwanamke ni MALI ya mwanaume lakini watoto ni mali ya Mwanamke na Mwanamme.

2.Uwe na MAAMUZI. Usilegelege katika maamuzi yako. Mwanaume ndiyo kichwa cha familia, kichwa hakipaswi kuyumbishwa na mabega.....sawa? Kumbuka wewe ni taasisi!

3. MWAJIBIKAJI: Ni wajibu wako kuhakikisha Mwanamke UNAYEMMILIKI anatosheka na na kuridhika na huduma zako. Bioloji yake ipate habari yake sawa sawa, tumbo lake lipate chakula cha kutosha, mwili wake upate mavazi na miguu viatu. Mkipata watoto na mwanamke wako ni wajibu wako kuhakikisha wanapata mahitaji yote wanayostahili. Kama huna uwezo kwanini uzae kama kuku? Kulaaaleki!

4. Ukishafanikiwa kuyamudu yooote hayo hapo juu, usisahau kuwa duniani kuna wanaume wenzako. Tafuta muda wa kukutana na wanaume wenzako uongeze ujuzi na maarifa ya kuuishi uanaume. Hapo valuu, biya na nyama choma vinaruhusiwa kusikiliza maongezi yenu. Ukishapiga haya makitu rudi kwa mwanamke wako kampe haki yake kulaaleki. Ikumbukwe kuwahi kurudi nyumbani si sifa ya mwanaume. Mwache Mwanamke wako awe na muda wa kuwa huru na kulea watoto.

5. Inapotokea kwa namna yoyote na kwa sababu yoyote ile necha ikashika kasi ukajikuta unaenda nje ya MWANAMKE WAKO, hakikisha unaenda kwa uangalifu. MWANAMKE WAKO asijue! Kosa kubwa sana akijua, na hii si sifa ya mwanaume. Huo ni uvulana. Na huko ufanye kwa UANGALIFU. Usijemletea maradhi MWANAMKE wako.

Kuna wakongwe wenzangu, WANAUME wenzangu kibao wako hapa jamvini wanaweza kuendeleza huo mlolongo.

Au kama vipi, leo ni ijumaa, twaweza panga mkakati wa kukutana ili tuzungumzie uanaume wetu.

SISI NDIO WANAUME BANA! Wanaume ndio SISI.

Wanaume wengine hawa hapa wanaendeleza waraka.....
"Ikumbukwe kuwahi kurudi nyumbani si sifa ya mwanaume. Mwache Mwanamke wako awe na muda wa kuwa huru na kulea watoto."

Hilo nilikuwa silijui, huwa nawahi kurejea nyumbani. Itabidi nianze kuwa mtoro sana home.
 
Back
Top Bottom