Siri nzito inanitafuna. Nifanye nini?

ZamdaIssa

JF-Expert Member
Nov 10, 2015
879
1,456
Salaam wanajamvi!Natumai mu wazima wa Afya!

Poleni wote munaopitia changamoto mbalimbali M/Mungu awafanyie wepesi

Niende moja kwa moja kwenye mada husika. SIRI NZITO!!

Wiki mbili zilizopita nilikua Nimeamshwa na kelele za kuku nyuma ya nyumba kwenye banda la kuku!

Nikaenda kagua mazingira,ilikua ni asubuhi yapata saa 11:15 hivi!

Naishi kwenye nyumba ya kupanga, hapa nilipo ni mtaa mpya nimehamia yapata miezi 2 nyuma.

Wakati nakagua kuku nilikua nimeinama kwa kua banda ni fupi.

Wakati zoezi likiendelea nilisikia gari imesimama upande wa pili wa nyumba kule nilikokua mimi kwa kasi sana kwa speed ile na muda ule ilinishtua kidogo ikabidi nisimame kuchungulia, Umbea uliniponza!!

Nilishuhudia mtoto mdogo wa miaka 4 jinsia ya kiume akiwa amebebwa na mama yake pamoja na mwanaume mwingine mweupee! alibebwa mpaka kwenye ile gari, yule mama na huyo mtoto nawafahamu kwa kua ni majirani zangu nyumba ya 4!

Alibebwa mpaka kwenye gari akiwa amevalishwa trucksuit za Adidas na kufunika kichwa chake kupitia lile koti la juu!Gari ikaondoka kwa kasi!!Hakuna alieniona kati yao!!

Baada ya gari kuondoka mama pekee ndie alirudi ndani huku akikimbia!nilishangaa kidogo ila sikujali niliona hayanihusu!

Baada ya siku 2 kupita,nilisikia mtoto amepotea!!ni yule yule niliemuona akiingizwa kwenye gari!nilipata mshangao nikaenda kwa mama mtoto aliepotelewa na mtoto! Nikamkuta analia hajiwezi!

Baada ya kumuhoji akasema mtoto amepotea wakati anaenda shule!anasema alimuandaa vizuri akamuacha aende mwenyewe kwakua alijisikia homa,muda kidogo akapigiwa simu na mwalimu kwamba mtoto hajafika shule na hawana taarifa!Siku anayosema mtoto amepotea ni ile ile siku nimemuona akimpakiza mtoto wake kwenye gari na yule mbaba mwingine!!NILISHANGAA SANA ILA NILIKAA KIMYA!

Kwa ufupi, huyo mama ameolewa na ana watoto 3, wakiume 2 na wakike 1, wakiume mmoja ndio huyo amepotea…anaishi na mumewake, siku ya tukio la mtoto kupotea mwanaume alikua amesafiri jana yake.

Yule mama ni mweupe kiasi tu (maji ya kunde) mumewe ni mweusi kabisaa! Yule mtoto aliepotea ni mweupe sanaaaa!na yule mbaba alokua amembeba anampandisha kwenye gari nae alikua mweupe sanaaaa! Kwa kuwa ilikua ni alfajiri sikuweza kuiangalia sura yake kwa utambuzi wa mfanano!

Nilichogundua ni kwamba yule mtoto hakua wa mumewe!yule baba alimchukua siku ile ndie baba yake.

Mume amerudi safari hajiwezi kwa Huzuni ya mtoto, masikini ya mungu hajui kama mtoto amechukuliwa na babayake wa kweli.

Naogopa kufungua mdomo wangu, siri hii inanitafuna sana! Najuta kushuhudia tukio lile!natamani kodi iishe hata kesho ili nihame hapa labda nitapata nafuu kidogo

Nifanye nini wanajmvi?
 
Salaam wanajamvi!Natumai mu wazima wa Afya!

Poleni wote munaopitia changamoto mbalimbali M/Mungu awafanyie wepesi

Niende moja kwa moja kwenye mada husika. SIRI NZITO!!

Wiki mbili zilizopita nilikua Nimeamshwa na kelele za kuku nyuma ya nyumba kwenye banda la kuku!

Nikaenda kagua mazingira,ilikua ni asubuhi yapata saa 11:15 hivi!

Naishi kwenye nyumba ya kupanga, hapa nilipo ni mtaa mpya nimehamia yapata miezi 2 nyuma.

Wakati nakagua kuku nilikua nimeinama kwa kua banda ni fupi.

Wakati zoezi likiendelea nilisikia gari imesimama upande wa pili wa nyumba kule nilikokua mimi kwa kasi sana kwa speed ile na muda ule ilinishtua kidogo ikabidi nisimame kuchungulia, Umbea uliniponza!!

Nilishuhudia mtoto mdogo wa miaka 4 jinsia ya kiume akiwa amebebwa na mama yake pamoja na mwanaume mwingine mweupee! alibebwa mpaka kwenye ile gari, yule mama na huyo mtoto nawafahamu kwa kua ni majirani zangu nyumba ya 4!

Alibebwa mpaka kwenye gari akiwa amevalishwa trucksuit za Adidas na kufunika kichwa chake kupitia lile koti la juu!Gari ikaondoka kwa kasi!!Hakuna alieniona kati yao!!

Baada ya gari kuondoka mama pekee ndie alirudi ndani huku akikimbia!nilishangaa kidogo ila sikujali niliona hayanihusu!

Baada ya siku 2 kupita,nilisikia mtoto amepotea!!ni yule yule niliemuona akiingizwa kwenye gari!nilipata mshangao nikaenda kwa mama mtoto aliepotelewa na mtoto! Nikamkuta analia hajiwezi!

Baada ya kumuhoji akasema mtoto amepotea wakati anaenda shule!anasema alimuandaa vizuri akamuacha aende mwenyewe kwakua alijisikia homa,muda kidogo akapigiwa simu na mwalimu kwamba mtoto hajafika shule na hawana taarifa!Siku anayosema mtoto amepotea ni ile ile siku nimemuona akimpakiza mtoto wake kwenye gari na yule mbaba mwingine!!NILISHANGAA SANA ILA NILIKAA KIMYA!

Kwa ufupi, huyo mama ameolewa na ana watoto 3, wakiume 2 na wakike 1, wakiume mmoja ndio huyo amepotea…anaishi na mumewake, siku ya tukio la mtoto kupotea mwanaume alikua amesafiri jana yake.

Yule mama ni mweupe kiasi tu (maji ya kunde) mumewe ni mweusi kabisaa! Yule mtoto aliepotea ni mweupe sanaaaa!na yule mbaba alokua amembeba anampandisha kwenye gari nae alikua mweupe sanaaaa! Kwa kuwa ilikua ni alfajiri sikuweza kuiangalia sura yake kwa utambuzi wa mfanano!

Nilichogundua ni kwamba yule mtoto hakua wa mumewe!yule baba alimchukua siku ile ndie baba yake.

Mume amerudi safari hajiwezi kwa Huzuni ya mtoto, masikini ya mungu hajui kama mtoto amechukuliwa na babayake wa kweli.

Naogopa kufungua mdomo wangu, siri hii inanitafuna sana! Najuta kushuhudia tukio lile!natamani kodi iishe hata kesho ili nihame hapa labda nitapata nafuu kidogo

Nifanye nini wanajmvi?
☹️ Hao ndio walimwengu.
 
Kama unamuonea hurumaa huyo Mwanaume,tumia njia zingine umwambie mkewe anajua kila aende police watampa ushirikiano wazee wa rungu za ugoko moja tu atasema wanawake hawana uvumilivu usema haraka.
Na mimi nakazia huu ushauri, kwa amani ya moyo wake ila sasa kama Baba na Mama lao moja watamtafuta na kumkata koromeo anyamaze maisha yote.
 
Back
Top Bottom