Sio bure, aliyemvuta mguu Kikwete jukwaani Mwanza alikuwa na ujumbe mzito

voicer

JF-Expert Member
Jul 13, 2020
5,553
11,885
Mtu yule huenda kama angepata watu wa kumsikiliza kabla na au baada ya kupelekwa gerezani.

Yawezekana alikuwa na ushuhuda mkubwa sana juu ya alichokuwa ameoteshwa kuhusu madhara ya lile Genge la wanamtandao lililokuwa nyuma ya Kampeni za Kikwete kwa wakati huo.

Ilikuwa ni katika uwanja wa CCM kirumba Mwanza. Kwenye kampeni za aliekuwa mgombea uraisi kwa tiketi ya CCM 2005,Ndugu Kikwete.

Ni tukio ambalo lilistusha na kushangaza wengi,kwa jinsi lilivyotokea baada ya mtu yule kuweza kujipenyeza hadi kufanikiwa kumfikia Kikwete pale jukwaa kuu.

Baadae alimng'ang'ania mguu akijaribu kumshusha jukwaani mgombea aliekuwa akiendelea na hotuba yake ya kampeni. Kabla ya kudhibitiwa na wanausalama na hatimae kukamatwa.

Mtu yule baadae alihukumiwa kwenda jela. Na baadae alimaliza adhabu yake na hatimae akarudi uraiani. Ingawa haikuchukuwa muda mrefu baadae iliripotiwa kwamba alifariki Dunia.

Binafsi ninashangazwa na habari hizo zote kutopatikana katika mitandao yote ya kijamii kwa sasa. Na hii inadhihirisha genge lile lilivyokuwa limejipanga.

Lakini kwa wale tulio na kumbukumbu za mambo ya siasa za nchi hii. Bado tukio lile tunalikumbuka vizuri sana.

Nimetafakari juu ya Ujio wa Kikwete na wanamtandao wake na jinsi nchi hii ilivyo na inavyoelekea.

Ndio nikamkumbuka huyo mwamba.

Samahani kama nitawakwaza baadhi yenu kwa kumbukumbu hii ya kitambo kidogo.
 
weka picha au videotuone uhalisia jamaa alikua na ujasiri wa hali ya juu
Mkuu kama umesoma andiko langu vizuri. Nimesema waliondoa kila kitu kilichohusiana na tukio lile kwenye mitandao hadi Google.
Wanamtandao walijipamga ipasavyo.
 
Ila mimi na shindwa kujua interest yenu na Raisi mstaafu kikwete ni ipi?

Ni wivu naona kuna juhudi za kumchafua mitandaoni ila mtashindwa yule ana superchata ya kupendwa, imagine imeandika nini hapo kwa kweli kama sio chuki tu.
 
Hujatukwaza Mkuu. Kukumbushana yaliyopita yanatusaidia kufikiri kwa uzuri yanayotokea leo hasa pale uliposema "...baada ya kutoka jela, akakaa muda mfupi uraiani, akafariki..."
 
Ila mimi na shindwa kujua interest yenu na Raisi mstaafu kikwete ni ipi? Ni wivu naona kuna juhudi za kumchafua mitandaoni ila mtashindwa yule ana superchata ya kupendwa, imagine imeandika nini hapo kwa kweli kama sio chuki tu.
Kwani nyinyi mnapomfuata Magufuli aliekufa inawasaidia nini?

Kikwete tunamfuata kwa sababu bado hataki kustaafu.
 
Nyota ya JK inazidi kuwaka ni mwanasiasa mwenye kila aina ya mbinu na ukongwe. Anatazama mbali siku zote kabla ya kufanya maamuzi.

Kuna muda unaweza kudhani ndio ameshapotea lakini anaibuka kutoka kusikojulikana na kutamba upya.

Samia anamtumia sana katika masuala yenye utata wa kisiasa na kuhitaji uzoefu, na anaonekana kuiweza nchi kwa kutegemea ushauri wa hazina ya wazee tulionao.

Hana kabisa papara, hana mihemko. Na hizo ni sifa mbili zinazompatia heshima miongoni mwa kundi fulani la wasomi wa nchi hii.
 
Kwani nyinyi mnapomfuata Magufuli aliekufa inawasaidia nini?

Kikwete tunamfuata kwa sababu bado hataki kustaafu.
Sio rahisi kustaadfu kama tunavyodhani. Ukishakuwa rais mstaafu huwezi kuachana na uongozi kwa namna moja ama nyingine.

JPM akiwa katikati ya utendaji wake aliandaa kikao akawaita wastaafu karibu wote na akaongea nao pale ikulu kwa uwazi kabisa.

Mawazo yao na maono yao aliyahitaji licha ya kuwa na uwezo mkubwa wa kiuongozi.
 
...kwa jinsi lilivyotokea baada ya mtu yule kuweza kujipenyeza hadi kufanikiwa kumfikia Kikwete pale jukwaa kuu.

Baadae alimng'ang'ania mguu akijaribu kumshusha jukwaani mgombea aliekuwa akiendelea na hotuba yake ya kampeni. Kabla ya kudhibitiwa na wanausalama na hatimae kukamatwa.
Clip tafadhali
 
Back
Top Bottom