dega
JF-Expert Member
- Dec 18, 2012
- 3,138
- 3,042
Endelea mkuu pamoja sanaSasa hapa umekuja kufanya nini?
Ulilazimishwa kusoma??
Endelea mkuu pamoja sanaSasa hapa umekuja kufanya nini?
Ulilazimishwa kusoma??
SEHEMU YA PILI
ILIPOISHIA…
Kamwe hakutegemea kama tukio lile alilolifanya miaka saba iliyopita, ambalo alimini siri ile kamwe isingejulikana kwakuwa hapakuwa na yeyote aliyekuwa akifahamu uhusiano wake na mke yule wa waziri zaidi ya wao wawili.
“Sasa nani amevujisha siri hii kwa hiki kirusi cha Instagram??” Stanley alinon’gona.
Akiwa bado katika taharuki, simu yake iliiita, alipoangalia kwenye kioo cha simu ile akaona mpigaji ni Scora Mtinika, mke wa waziri
ENDELEA NAYO…
Akasita kuipokea simu ile akawa akaitizama kama vile ndani ya kifaa kile kulitegeshwa bomu, simu iliendeleakuita kiganjani mwake.
Akakata shauri akabofya kitufe cha kupokelea nakuweka simu sikioni.
“Hallow” sauti nyembamba ilisikika
“Nakusikia”
“Umeona ?” scola, mke wa waziri mtinika alimuuliza.
“Nani ametufanyia huu unyama?”
“Sijui” scola alijibu.
Stanley akapiga kimya huku simu ikiwa bado ipo sikioni. Kisha akauliza kwa kwa sauti ya unyonge.
“Tunaweza kuonana?”
“Nini!!” Scola akahamaka kwa mshangao
“Tunaweza kuonana?” Stanley akauliza tena.
“Ili?”
“Tulizungumze hili”
“Hapana stanley, naogopa”
“Maji yamekwisha mwagika hatuna budi kuyaoga, Unapoendelea kuishi katika hofu ndivyo unayoikaribisha zaidi hatari maishani mwako” Alisema Stanley.
ukimya mwingine ukapita, kisha scola akazungumza simuni kwa sauti ya unyonge.
“Hatuwezi kuzungumzia kwenye simu?”
“Lakini kwanini hutaki tuonane?”
“Hebu kuwa mwelewa Stanley, kila kona sasa hivi wanazungumza jambo hili, kitendo cha kuonekana tukiandamana pamoja mtaani ni kuzidi kudhihirisha kile kinacho sambaa mtandaoni.
“Hufikirii ni hatua gani atachukua mume wangu dhidi yetu? Huna hofu kabisa na jambo hili Stanley, usisahau kabisa kwamba mimi ni mke wa waziri, na usijifanye hujui kwamba jambo hili limemdhalilisha mume wangu kwa kiwango kikubwa sana, na usidhani kwamba atalipuuza tu kama mwendawazimu, mimi na wewe kuanzia wakati huu hakuna ambaye yupo salama”
Scola alisema, Stanley alishusha pumzi ndefu, kwa mara nyingine alihisi tumbo likipata joto, hofu kubwa ikamvaa, alitamani ardhi ipasuke atumbukie ndani yake. Maneno ya Scola yalimwingia sawia mvulana yule chakalamu.
“Sasa naomba unisikilize kwa makini” Stanley alimwambia.
“Nakusikiliza” Scola akajibu.
“Waandishi wa habari wamekwisha kupigia kukuliza juu ya jambo hili.?” Stanley akamuuliza.
“Wamenipigia sana, lakini hadi sasa sijapokea simu yoyote, na sijaongea na mtu yeyote”
‘Vizuri sana, sasa unachotakiwa kufanya ni kulikanusha jambo hili kwa nguvu zote, likanushe kwa waandishi wa habari na kwenye akaunti zako mbalimbali za miotandaoni” Stanley alisema.
“Nitasema nini sasa wakati video iko wazi ikinionyesha mimi na wewe tukifanya uchafu ule”
“Unatakiwa useme picha hizo za video zimetengenezwa, shikilia msimamo huo,” stanley alisisitiza.
Ukimya mwingine ukapita baina yao, hatimaye scola akatikia kwa sauti ya taratibu:
“Sawa, nitafanya hivyo”
“Vizuri, hata mimi huo ndio utakuwa msimamo wangu, nitakukana popote pale niendapo”
Wakakubaliana hivyo.
Masaa machache badaye tukio la kuvuja kwa video ya Scola mke wa waziri na Stanley wakiwa katika mahaba motomoto ilikuwa gumzo nchi nzima.
Kila kona mada kuu ilikuwa ni kitendo hicho, vituo vya redio na runinga viliripoti jambo lile kadiri walivyoweza.
Mke wa waziri Mtinika, Scola mtinika alipopigiwa simu kutoa ufafanuzi juu ya ile sintofahamu alikana Kwa nguvu zote huku akiliweka tukio hilo katika muktadha wa kisiasa.
“Hizi ni hila anazofanyiwa mume wangu na maadui zake wa kisiasa kwa kunitumia mimi, kwakweli siwezi kukubali jambo hili linichafue kwa kiwango hiki, nimekwisha ongea na mwansheria wangu kwa ajili ya kupeleka jambo hili mahakamani. Na nina wahakikishia mange kimambi nitamtia adabu” Scola alijitetea mbele ya waandishi wa habari.
“lakini video inaonesha ni wewe, ukweli wa jambo hili ukoje?” mwandishi mmoja akauliza.
“Niwajibu mara ngapi kwamba hii ni hila ya mange kimambi, video hiyo ni ya kutengeneza, mtu ninaye husishwa naye simjui, na ifahamike mimi ni mke wa kiongozi mkubwa, kamwe siwezi kufanya uchafu wa kiwango hiki.” mwanake yule alizidi kujitetea.
Kwa upande wa waziri mtinika ambaye alikuwa ziarani nchini Marekani, alipotafutwa na waandishi wa habari kwa njia ya simu ajabu simu yake ilikuwa haipatikani, hata Scola, mke wa waziri huyo naye alipojaribu kumtafuta mumewe ili amweleweshe juu ya bomu lililolipuliwa na Mange Kimambi, hakumpata simuni.
“Mungu wangu nini kimempata mume wangu, kwanini hapatikani na siyo kawaida?” Scola alijiuliza kimoyomoyo.
Ndani ya muda huohuo mara simu yake ya mkonoi ilianza kuita, alipocheki kwenye kio cha simu akaona namba ya Stanely, moyo wake ukamdunda maana walikwisha kubaliana kutotafutana.
Simu iliita hadi ikakatika, mpigaji akapiga tena, mwisho alikata shauri akaona acha apokee:
“Hellow” alisema baada ya kupokea simu
“umeona kitu kingine alichoposti hiki kirusi”
“Kirusi gani?”
“Si Mange Kimambi”
“Kaposta nini tena?”
“ingia uangalie, alichoposti safari hii ni kibaya kuliko alichopost awali”
“Mungu wangu!!” Scola aliogopa.
ITAENDELEA
Sipend mahadithi ya namna hii mm.kwanza sijasoma..endelea kwa wengine
[/QUOpTE]p
Za wanafunzi
Mzee baba umeruka sehemu ya tatu!!SEHEMU YA 4
“Nkrii! Nkrii! Nkrii!!!” simu ya Scola iliita kwa nguvu.
Alipungaza spidi ya gari akaitizama simu simu iliyokuwa kando, macho yake yalipotua kwenye kioo cha simu ile hakuamini macho yake..
Mtu aliyekuwa akimpigia alikuwa ni Stanley Massawe, tumbo lilimkata, kila alipoona simu ya mwanaume yule kulikuwa na bomu jingine lililolipuka.
Akafikiria kama anatakiwa kupokea simu ile mwisho akaona kwakuwa amekwisha chukua maamuzi ni kheri kutotizama nyuma. Akaacha kupokea simu ile.
Hata hivyo, hazikupita dakika nyingi baada ya simu ile kukatika, mara simu nyiingine ikaingia, alipoangalia, akaona mpigaji ni mumewe!! Mheshimiwa waziri, Hassan Mtinika.
TOBA!!
Endelea nayo…
Scola akawa njia panda, hakujua achukue maamuzi gani, apokee simu ya mumewe, ama achane nayo. Kadhalika akaendelea kuijiuliza, kwa nini tangu kuibuka kwa lile songombingo mume alikuwa hapatikani? Wakati huu ambapo anatorka ndipo mwanaume huyo anapompigia simu?
Swali kuu likawa, je mumewe amekwisha baini kila kitu juu ya kuwa alikuwa akitoroka na Rolland, ama laa?
Simu iliendelea kuita kwa nguvu hadi ikakatika, pamoja na kwamba gari lile lilikuwa limefunguliwa mashine za kupoza joto, lakini mwili wa Scola ulindelea kutokwa na jasho kiasi cha kulowanisha shati na kuacha baka kubwa.
Haukupita muda mwingi mara simu ile ilianza kuita tena, mpigaji akiwa ni mumewe, baada a kutafakari kwa kina mwisho akaamua kuipokea ile simu.
“He…llow” alisema kwa kitetemeshi
“Uko wapi?” sauti nzito iliyojaa kisirani ilisikika upande wa pili, alikuwa ni Muheshimiwa waziri, Hassani Mtinika.
“Sa..sa…Sasa…. Hivi?” Scola naye akamuuliza kwa kitetemeshi.
“Uko wapi?” sauti ya amri ikasika tena, safari hii sauti ile ikiwa ya kutisha zaidi ya awali.
“Nakwenda,…nakwenda.., nipo Kariakoo” mwanamke yule alitoa majibu ya uongo huku akiwa mwingi wa hofu.
“Unafanya nini?’
“Nimekuja tu mara moja”
“Una uhakika?”
“Ndio”
“Rolland mpo naye?” waziri yule aliendelea kumuuliza maswali ya mtego mwanamke yule.
“Ndio”
“Kwanini umekwenda kumchukua shule wakati si muda wa likizo?” swali lile likamfanya Scola ajawe na mate mepesi mdomoni.
Akajikuta anaikata simu ile na kuizima. Mambo yalikuwa yamekwisha haribika, alikwisha tambua mumewe alikwishatambua kila kitu juu ya nyendo zake.
Aliikumbuka ile namba mabayo mume alimpigia akabainiilikuwa ni namba ya Tanzania.
“Inamaana maana kisha rujea nchini” alinong’oa.
Hata hivyo ndani ya muda umfupi uliofuatia aliliona Gari jeusi aina ya Nissan likija kwa kasi ya kimbunga nyuma yake.
Gari lile lilimpita kwa kasi kisha likaenda kama mita 200 na kusimama katikati ya barabara.
Watu wawili wenye bastola walishuka ndani ya gari lile na kulipungia mkono gari la Scola kumtaka asimame.
Lilikuwa ni shambulio baya mno kwa Scola, alitambua fika mambo yamekwisha haribika, na alikuwa kwenye vita kubwa kati yake na mumewe.
Aliogopa sana, hakutaka kabisa kupingia mikononi mwa wale watu wawili waliomsimamisha mbele yake, alipofikira suala la kutotii kusimama, aliona dalili za kifo aidha yeye ama mwanaye kutoka kwa wale wavamazi zipo waziwazi.
Alikanyaga breki na kusimamisha gari, wale wavamizi wakalizunguka gari na kuwataka wateremke yeye na mwanaye.
Rolland alianza kulia, hakuna alichojua kwa wakati huo, kila kitu kwakwe ilikuwa ni ‘suprize’
“shukeni wote kabla hatujamwaga damu ya mtu” jamaa alisema kwa ukali.
“Fanya haraka we Malaya” mtu wa pili alifoka alipoona Scola anababaika kushuka.
“Kuna nini jamani mbona hivyo?” Scola aliuliza
“usituulize maswali ya kipuuzi, utakwenda kujua tukifika Dar”
Scola hakuwa na la kufanya, watekaji wale, walichofanya ni kumfunga kamba mwanamke yule, pamoja na mwanaye, kisha wakawaweka katika siti za nyuma za gari lilelile, jamaa mmoja akaketi kwa dereva huku mwingine akiweka ulinzi upande wa Scola na mwanaye Rolland.
Hapo Scola akatambua watu wale hawakuwa wawili tu, bali zaidi ya wawili, maana pindi walipoanza safari ya kurudi Dar, ile Nissan waliyokuja nayo wale jamaa nayo iliunga tela kwa nyuma, hilo likamfanya atambue kuwa wavamizi wale walikuwa na wenzao walikuwa wamebakia kwenye lile gari dogo.
Safari ya Dar ilipoanza, Scola aliona ule ndio ulikuwa mwisho wa maisha yake, aliamini pasina shaka kwamba mambo yale yalikuwa yakiratibiwa na mumewe. Lakini pia hakutaka kabisa kujidanganya kwamba mambo yale hayakuwa ni matokeo ya post za Mange Kimambi kufumua siri zake za maisha ya nyuma.
Alianza kusali sala zake za mwisho, kwani alitambua kivyovyote mumewe asingeweza kumwacha hai endapo angethibistha ukweli wa mambo yote yaliyosewa dhidi yake.
Kumsaliti na kumbambikia mtoto ilikuwa jambo baya ambalo linachukiwa na wanaume kwa kiwango cha mwisho.
Mange kwa nini umenipa dhabu hii, kwa nini huku post watu wenye wenye matatizo ya umeme hadi ufumue siri hii” Scola alilalama kimoyomoyo.
Alianza kusali sala zake za mwisho, hakuamini kabisa kama wale watekaji, watu wasiojulikana wanaweza kumwacha salama.
“Mange Kimambi umenikomesha” aliongea peke yake kama mwendawazimu
Itandelea…
Sehemu ya tatu hujaweka mzee baba/mama
Sehemu ya 3 iko wapi?
Tumekuambia hujaweka sehemu ya tatu umeamua kutupuuza?Muendelezo huuuuoooooooo