MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA KUMI NA TISA

★★★★★★★★★★★★★★★★


Mariam alikuwa na sauti nzuri, na hapo alipoongea alikuwa ameitoa yote. Hii ilimaanisha nini? Michezo tuliyokuwa tumeianza ilikuwa inamsaidia binti huyo kurejesha utaratibu mzuri kwenye ubongo wake, na hasa sasa nikawa nimetambua zaidi kwamba ni furaha aliyokuwa akiipata kwa kucheza hivi ndiyo iliyokuwa inafunika ile huzuni iliyosababisha akaanza kuumwa.

Wengine walikuwa wanamwangalia binti kwa kustaajabu, yeye mwenyewe asielewe kwamba hiyo ilikuwa ni pindi yenye kugusa nyoyo za wapendwa wake kwa kiwango kikubwa, naye akaushika mkono wa Miryam na kuanza kumvuta kuelekea pale Ankia alipokuwa amesimama.

Walipomfikia Ankia, Miryam akawa amesimama pembeni yangu, naye Mariam akamwambia Ankia, "Mwonyeshe."

Ke! Yaani sisi tulikuwa tumemezwa na butwaa la kuona binti ameanza kuongea vizuri lakini yeye alikuwa anataka tu kumwonyesha dada yake kilichofanya afurahi namna hiyo. Ankia akaninyooshea simu yangu ili nitoe lock, nami nikaiwekea kidole ili ifunguke. Ilipofunguka, Ankia akaweka ile video ya Shadya, naye Miryam akaanza kuiangalia.

Mariam akaendelea tu kucheka na makeup yake usoni, naye akasema, "Ona... anakimbia upande-upande kama bata!"

Oh Mungu! Nilijihisi vizuri sana aisee. Wiki moja tu nikawa nimefanikiwa kuanza kumkarabati vyema huyu binti.

Miryam akawa anacheka kwa pumzi, lakini kwa ile njia kama vile alikuwa anataka kulia. Najua video ilikuwa imemfurahisha lakini niliona furaha yake kuu kuwa kusikia mdogo wake akizungumza tena bila kujikwaa sana, naye akamwangalia usoni kwa hisia. Hata akacheka kidogo kwa pumzi, nami nikaona machozi yakimlenga.

"Mariam..." Miryam akamwita hivyo.

"Bee..." Mariam akaitika.

"Umenifurahisha sana. Nani ameku... nani amekuchora hivi halafu... ukamkimbiza shangazi?" Miryam akamuuliza tena.

Mariam akaniangalia na kunisonta, akionekana kutaka kusema jina langu lakini kukawa na ugumu fulani, hivyo akaishia kuachama tu.

"Ni wewe?" Miryam akaniuliza.

Nikamwambia, "Ni sisi wote tumechangia."

"Kasoro aliyekimbia kama bata," Tesha akasema hivyo.

Wanawake wengine wakacheka kidogo, naye Shadya akamwambia Tesha "Na we' nitafute sasa!"

Miryam akamshika Mariam usoni, kisha akamkumbatia kwa upendo.

Ilikuwa ni pindi yenye kugusa sana moyo ambayo kiukweli sikuwa nimetarajia ingefika hapa kwa muda mfupi namna hiyo. Yaani wazo langu mapema ilikuwa ni kufanya tu kioja pamoja na Mariam ili aendelee kuchangamka, lakini sikutarajia uchangamfu wake uonyeshe matokeo mazuri mapema mno kama haya ya sasa. Mama wakubwa walikuwa wanatokwa na machozi kabisa. Walikuwa watu wa hisia sana, nao wakawasogelea Miryam na Mariam kujiunga nao kwenye kumbatio.

"Jamani! Hadi raha," akasema hivyo yule mama mgeni.

"Umeona eh?" Shadya akamwambia hivyo huku akitabasamu.

Wanne hao wakiwa wameendelea kukumbatiana namna hiyo, Miryam akapandisha macho yake na kuniangalia. Nikawa namtazama kwa utulivu tu, naye akashusha pumzi na kuwaachia wenzake ili kumbatio hilo livunjwe hatimaye. Ankia akanisogelea na kunipiga kidogo begani kwa njia ya kusifia, naye Tesha akanipigia saluti ndogo ya kishkaji.

"Ahah... umependeza sana," Miryam akamwambia hivyo Mariam.

"Asante," Mariam akamjibu hivyo.

Sisi wengine tukacheka kidogo, na Tesha akasema, "Yaani dada ungekuwepo... ungegalagala kwa kucheka."

"Nataka kujua ilikuwaje. Nataka Mariam anisimulie," Miryam akasema hivyo kwa sauti yake tamu.

"Njoo... hapa..."

Mariam akamwambia hivyo Miryam na kumkalisha dada yake sofani. Akanivuta mkono pia ili nikae hapo hapo, hivyo nikawa nimekaa pamoja na dada hawa wawili, Mariam akiwa katikati. Akaanza kuongea.

Alijitahidi sana kuzungumza ijapokuwa maneno mengi aliyatafuta mno kichwani, na wote tulikuwa tukimsikiliza alipoongea kwa furaha na kufurahi pamoja naye. Miryam mpaka akajikuta anadondosha chozi kutokana na furaha aliyokuwa akihisi, naye Mariam akamalizia kumsimulia kwa kusema Tesha alicheka mpaka akakaa dhini.

"Yaani nyie ngojeni tu. Mmenigeuza kituko chenu leo ila na nyie nitakuja kuwaonyesha," Shadya akasema hivyo.

"Aaa, bado unalalama nini Shadya? Si pole umepewa?" Tesha akamwambia hivyo.

"Hata kama. Mnanicheka sana," Shadya akasema kwa njia ya kuudhika.

"Ahahah... Basi tunaacha kukucheka. Mamu... twende nikakusafishe uso uje ule. Unajua nimekuletea nini?" Miryam akaongea hivyo.

Mariam akatikisa kichwa kuonyesha hajui.

"Kitimoto," Miryam akamwambia.

Mariam akatabasamu kwa furaha, naye akasimama upesi.

Miryam akasimama pia, na ni wakati huu ndiyo akawa ametilia maanani uwepo wa yule mmama mgeni hapo ndani na kumsalimia, kisha akawasalimu na mama zake wakubwa na Ankia. Wakampa pole ya kazi, naye pia akaomba radhi kwa kuchelewa lakini wakamwambia kwamba haikuwa na shida.

Ankia akawa amemwambia Miryam kuwa mimi na yeye tungeondoka sasa kwenda kwetu, lakini Miryam akakataa. Akasema tutulie kwanza ili tupate chakula pamoja kisha ndiyo twende, kwa sababu alikuwa ameleta cha kutosha. Ankia na mimi tukawa wapole. Kwa hiyo akaondoka pamoja na mdogo wake baada ya kutuambia tutulie hapo, nasi tukakaa kuwasubiria.

Kilichofuata ilikuwa ni maongezi zaidi yenye kufurahisha kuhusiana na Mariam, na hata mara kwa mara Tesha angemtania Shadya, aliyekuwa amenuna kimasihara bado. Dada wale wawili wakawa wamerejea, wakati huu Miryam akiwa amevaa dera pana la zambarau na kilemba kilichofunika nywele zake kwa mbele, na Mariam alikuwa safi zaidi kwenye uso wake.

Miryam akaelekea jikoni, na Ankia akamfata kwenda kusaidiana naye kuandaa vyakula. Oh inaonekana bibie Miryam alikuwa ameleta vyakula vilivyotengenezwa tayari maana harufu nzuri ilikuwepo hewani baada ya wao kwenda kuifungua ile mifuko aliyokuja nayo.

Sisi tukiwa sebuleni tukiendelea kujaribu kumfanya Mariam aendelee kuzungumza, wanawake hao wawili ndiyo wakaanza kutuletea sahani za mmoja mmoja zenye vyakula pendwa kama chips kavu, kipande cha nyama ya kuku, na nyama za kitimoto kwa wingi. Na ilikuwa kama ameotea yaani kuleta msosi mtamu namna hiyo kwenye siku ambayo mdogo wake alikuwa ameanza kuzungumza tena, na baada ya kila mmoja kupewa yake na Ankia kutunawisha, makamuzi yakaanza.

Tukala huku tunapiga story, na hiki ni kitu ambacho lazima nikiseme kwa mkazo, kwamba kila mara ambayo ningemwangalia Miryam na yeye kunitazama, macho yetu yangetulia yakiangaliana kwa sekunde chache, kama vile yanatafakariana, na bibie ndiyo angevunja utizami huo na kuendelea kula taratibu.

Ilinifanya nione mtazamo mpya ndani ya mwanamke huyo kunielekea, yaani bado hakuwa ameniambia kitu chochote lakini macho yake tu yalitoa shukrani za dhati kwa yote niliyokuwa nafanya ili kumsaidia mdogo wake.

Nikawa najihisi vizuri sana rohoni, nikitazamia kwamba huenda hii hata ingeanza kutengeneza msingi mzuri wa urafiki baina yangu na huyo mwanamke, na sijui kwa nini tu lakini nilitamani sana tuwe marafiki. Tena hiyo ilikuwa ni kutokea mara ya kwanza kabisa nimekutana naye. Ningepaswa tu kusubiri kuona.

★★

Kwa hiyo tukawa tumemaliza msosi na kukaa hapo mpaka mida ya saa tano. Mariam alikuwa binti aliyezoea kulala mida ya saa tatu, saa nne, kwa hiyo hapo tayari alikuwa zake chumbani amesinzia muda mfupi tu baada ya sote kumaliza kula. Kwenye hii mida ya saa tano, yule mwanamke aliyekuja kuwatembelea mama wakubwa akaona aage hatimaye.

Alikuwa anafahamiana sana na marehemu mama yao wakina Tesha, na alikuwepo kusaidiana na akina Bi Zawadi na Bi Jamila katika kipindi ambacho wazazi wa ndugu hawa walikuwa wamepoteza maisha, na leo alikuwa amekuja kuwasalimia. Sikujua sana ila inawezekana hata huo mlo mtamu ambao Miryam aliuleta ulikuwa kwa ajili ya ujio wa mwanamke huyo.

Kwa sababu aliishi maeneo ya Toangoma, Miryam akawa amemwitia usafiri wa bodaboda fulani aliyejuana naye aje kumchukua na kumpeleka barabarani pale Mzinga ili mama wa watu akapande daladala. Mimi na Ankia tukatumia nafasi hii pia kuaga na kutoa shukrani kwa ukarimu wa familia hii, nao wakatupa heri nzuri ya usiku pia.

Wanawake hawa, hasa mama wakubwa, walikuwa wanapenda sana Tesha na mimi tulipoongea vitu vilivyowachekesha, nasi tukatoka nje baada ya yule bodaboda kufika tukiwa tunawafurahisha wote kwa story zetu. Yule mama akapanda zake boda, huyoo akasepa. Sisi, yaani mimi na Ankia, tukazungukia upande wetu huku tukiendelea kuzungumza na hawa majirani zetu kwa shauku.

Tulikuwa tumeshazoeana sana na mama wakubwa, walinipenda kweli, hasa kutokana na kuwa na utani pamoja nao wa kuwafanya wajihisi vijana. Kwa kuwa nafasi ilikosekana ya kuongea na Tesha kuhusiana na ishu yake na Winny, akawa ameniambia angenisimulia kesho, nami nikaridhia.

Sikuwa nimeongea lolote pamoja na Miryam kuhusiana na mdogo wake kwa wakati huu, kwa hiyo ningepaswa kusubiri tu maana najua alikuwa na nia ya kutaka kujua kiundani zaidi kuhusu maendeleo ya mdogo wake kutokea hapo. Nilifurahia sana usiku huu, yaani kama Ankia asingekuwa kipindi cha P, angekoma huko ndani!

Tukaingia zetu tu ndani na kwenda kujipumzisha, nikiwa na hamu na yale ambayo siku ya kesho ingeyakaribisha.


★★★


Pakakucha hatimaye, ikiwa ni Jumapili takatifu kwa wengi. Nilikuwa nimeamka mida ya saa kumi na mbili alfajiri lakini nikajirudisha tena usingizini, na sasa nikawa nimeamka mida ya saa tatu asubuhi. Sikutoka kitandani, bali nikavuta simu yangu iliyokuwa inaita kwa muda fulani sasa.

Nilikuwa nimeona uvivu tu kuichukua mapema, na sasa nilipoangalia mpigaji nikakuta ni Soraya. Kunipigia mapema ya saa tatu namna hii haikuwa kawaida yake, yaani hata hakuwa na kawaida ya kunipigia kwa sababu tulizoea kuwasiliana kwa sms, lakini nikapokea na kusikilizia.

"Halloo..." sauti yake ikasikika.

Nilikuwa nimelaza uso kwa upande huku simu ikiwa sikioni kwa juu, nami nikiwa nimefumba macho nikamjibu, "Halloo."

"JC jamani... mbona unanitesa?" akaongea kwa sauti ya kubembeleza.

"Ih, me nimekufanyaje tena?"

"Ina maana hujui?"

"Nisingeuliza."

"Sawa. Basi asubuhi njema," akasema hivyo.

"Na kwako pia," nikamwambia hivyo.

Akatulia kidogo, kisha ndiyo akakata simu.

Nikatabasamu kiasi na kuiweka simu pembeni.

Soraya alikuwa anafikiri ningeanza kumbembeleza lakini akawa amekosea namba. Siyo kwamba labda sikumtaka tena ila najua alikuwa ameshadata na mimi kwa hiyo hata kama ningefanya nini, najua angerudi mwenyewe tu. Nikaamua kunyanyuka ili nikafanye usafi wa mwili kisha mengine kama kunywa chai yafuate.

Hiyo wiki yote iliyoisha sikuwa nimefanya mzunguko mwingine wowote mbali na Mbagala zaidi ya nilipokwenda kukutana na yule askari mpelelezi Ramadhan, kwa hiyo nikawa nafikiria labda leo ingefaa kama nikitoka kwenda sehemu kupiga mbili tatu pamoja na Ankia na Tesha. Uzuri kulikuwa na mechi ya Simba kwa hiyo kwenda kuitazama na kuburudika pamoja na hao marafiki zangu lilikuwa wazo zuri.

Ankia tayari alikuwa ameshaamka na kufanya usafi, na wakati huu alikuwa akikanda unga wa ngano ili atengeneze mkate mkubwa. Tena angeukaangia, sijui kuubanikia, kwenye sufuria, nami nikampongeza na kusema nasubiri kwa hamu kunywa chai pamoja na mautashi yake ya kupika.

Nikaendelea kukaa sebuleni kwa muda fulani mpaka pale marafiki wawili wanawake wa Ankia walipokuja kumtembelea sijui, ama labda kwa biashara zao wajuazo wenyewe. Mimi nikaingia chumbani bila hata ya kuonana nao maana nilitoka sofani wakiwa ndiyo wameukaribia mlango, kwa hiyo nikajichimbia chumbani kwangu na simu yangu nikisoma mambo fulani.

Nilipomaliza, nikaweka tu simu pembeni na kuamua kutafakari vitu. Upande wa vita yangu dhidi ya tatizo la Mariam ulionekana kuanza kunipa ushindi, lakini kwa upande wa vita yangu dhidi ya mke wa Chalii Gonga bado ulisua. Mara kwa mara askari Ramadhan alikuwa amenitafuta kuuliza kama kuna maendeleo yoyote au jambo jipya, nami nilimjulisha kwamba bado kumetulia.

Ila huu ukimya wa Bertha uliniwazisha kiasi. Inawezekana alikuwa akifuatilia mambo fulani kuhusu mimi bila mimi kujua, huenda kwa hizo siku chache zilizopita akiwa ametumia watu wake kunichunguza. Nilikuwa na uhakika kabisa kwamba hakuna sehemu yoyote ile ambayo ningejikamatisha vibaya kwa lolote, kwa hiyo hata kama angenifatilia hangeona nuksi yoyote. Hata makutano yangu na huyo askari yalikuwa ya siri na yaliyopangwa kwa akili.

Ingekuwa rahisi kusema ah ninajipa presha tu bila maana yoyote lakini huwezi kuwa na hakika sikuzote kwamba mambo yatakuwa sawa tu na kutofikiria njia mbadala za kuepuka matatizo ambayo hufikirii yatatokea, kwa hiyo nikawa nawaza nini nitafanya hiki kikitokea, au nini nifanye kile kisipotokea. Hata yale madawa niliyotengeneza nilikuwa nimeyaweka sehemu salama na kwa kificho ili Bertha akiyaomba tu, ayapate, na kutokea hapo ndiyo mipango ianze kazi kwa kasi.

Bwana, nikiwa nimejilaza tu kitandani hapo simu yangu ikaanza kuita, na mpigaji alikuwa ni Bi Zawadi. Nikapokea na kumsalimia, naye akaniuliza ikiwa nilikuwa na kazi. Nikakanusha hilo, ndiyo akaniomba niende hapo kwao sasa hivi maana kuna jambo la muhimu alikuwa anataka ashiriki nami. Nikamwambia anipe dakika chache tu nami ningekuwa nimeshafika. Simu ikakatwa.

Nilikuwa nawaza kwamba bila shaka jambo hilo lingekuwa linamhusu Mariam, na kwa kufikiria pale nilipomwacha binti huyo kihali hiyo jana, ingekuwa muhimu kwenda kuona hali yake iko vipi kwa sasa. Hivyo, nikatia nguo safi mwilini na kujitengeneza vyema kama kawaida yangu, nami nikatoka chumbani.

Hapo sebuleni nikakuta Ankia akiwa amekaa pamoja na wale marafiki zake wawili. Wote sikuwahi kuwaona kabla; mmoja alikuwa mweusi wa maji ya kunde, mwingine alikuwa mweupe. Na nadhani wote walikuwa waislamu maana walivaa hijab vichwani, na nguo ndefu kama mabaibui au kanzu za kike. Wee!

Hawa nawajua. Huwa wanavaa kitakatifu kwa nje ila ndani sasa! Tena na hako keupe kalikuwa kameweka na pini iliyozunguka tobo moja la pua, ndiyo nikajua hapo kwisha kazi!

Lakini mimi nikawa makini tu na kufika usawa wa sofa alilokalia Ankia, nami nikamwambia, "Natoka."

"Ih, wapi tena?" Ankia akauliza.

"Warembo wangu wananiita," nikamjibu hivyo.

Ankia alielewa namaanisha mama wakubwa hapo jirani, naye akasema, "Chai je?"

"Ngoja nikawasikilize kwanza. Mambo vipi?" nikasema hivyo na kuwasalimu hao wadada.

"Safi..."

"Poa..."

Wakajibu huku wakiniangalia kwa umakini.

Nikamwangalia Ankia na kusema, "Badae.'"

"Haya," akanijibu.

Mimi huyoo nikatoka hapo kama vile najali muda. Sijui hao wanawake walifika hapo wakiwa na dhumuni lipi lakini macho yao yalionyesha kutaka masilahi fulani. Ah potelea pote, akili yangu ikakazia zaidi mwito wa warembo wangu Bi Zawadi na Bi Jamila.

Nilipotoka na kufika getini kwao Tesha, nilimwona yule Fatuma wa dukani akiwa amekaa kwenye kiti hapo nje pamoja na mwanaume kijana, wakionekana kuongea, nami nikagonga geti na kusubiri lifunguliwe.

Nikamwona huyo Fatuma akiwa anamwonyeshea huyo kijana kwa kidole kunielekea mimi, kisha akaanza kucheka huku huyo kijana akinitazama. Kwa haraka nilitambua kwamba alikuwa anamsimulia kile kituko cha usiku wa jana, nami nikakaza tu na kutazama muda kwenye simu.

Ikiwa inaelekea kuingia saa tano sasa, mlango mdogo wa geti hilo ukafunguka, na ni Tesha ndiye aliyekuwa amenifungulia. Tukasalimiana vizuri sana kirafiki, nami nikaingia na kukuta pickup ya Miryam ikiwa hapo nje, kisha tukaanza kuelekea ndani pamoja. Tesha akawa amegusia kwangu kuhusu kwenda kuitazama mechi ya siku hii baina ya Simba na Singida, nami nikampa uhakika kwamba tungekwenda kuiona kwa pamoja baadaye.

Tulipoingia tu ndani hapo, nikakuta mama wakubwa wakiwa wamekaa sofa moja, na Mariam akiwa amekaa kwenye lingine pamoja na bibie Miryam.

"Ah warembo wangu hao! Shikamoo ziende kwenu jamani," nikawapa salamu.

Wakaniitikia huku wakitabasamu kwa furaha, na baada ya Mariam kuniona, akatoka sofani na kunifata mpaka niliposimama huku akitabasamu.

"Vipi Mamu?" nikamwambia.

"Poa. Sh..kamoo," akaniamkia.

"Marahabaa. Hi-five," nikasema hivyo na kunyanyua kiganja changu juu.

Mariam akagongesha kiganja chake hapo kirafiki.

Nikamwangalia Miryam na kuona anatutazama huku akitabasamu kiasi, nami nikamwambia, "Za asubuhi?"

"Safi. Karibu," akanijibu.

Hako kasauti sasa! Na alikuwa amependeza kweli kwa nguo aliyovaa ingawa hakuonekana kutaka kutoka kwa siku hii.

"Karibu ukae baba," Bi Jamila akaniambia hivyo.

Nikaketi kwenye sofa pembeni yake Tesha, naye Mariam akakaa kwenye mkono wa sofa hilo hilo karibu nami. Nadhani alikuwa na hamu ya kuona tungefanya michezo ipi kwa leo. Kulikuwa na harufu ya nyama niliyovuta upesi baada ya kukaa hapo, nami nilielewa ilitokea jikoni.

"Shadya ametoka?" nikawauliza.

"Aende wapi wakati sasa hivi anatrend tiktok? Yuko jikoni anajua akitoka tu nje atavamiwa na paparazzi," Tesha akasema hivyo.

Mara ghafla Shadya akatokea jikoni akiwa ameshika kijiko cha kupakulia mboga na kusema, "Halafu Tesha naomba unitoe mdomoni mwako, sawa?"

Wote tukacheka kidogo, naye Tesha akasema, "Si ni JC ndiyo kakuulizia jamani?"

"Si ungemwambia tu niko jikoni, paparazzi wametokea wapi? Wewe! Nitakukoa na hili likijiko!" Shadya akamwambia hivyo Tesha huku akimnyooshea kijiko kweli.

Tukacheka tena kwa pamoja maana inaonekana vita ya Tesha na Shadya bado haikuwa imeisha.

Miryam akawa anacheka bila kutoa sauti, naye Bi Zawadi akamwambia Tesha, "Mwache mwenzio bwana, atakuja akukoe kweli."

"Yaani hili!" Shadya akasema hivyo.

"Ahah... shikamoo," nikamsalimu Shadya.

Akasonya kidogo kuondoa kero ya Tesha, kisha akaniambia, "Marahaba mwaya. Karibu."

"Asante," nikamjibu hivyo.

Tesha akaniangalia machoni kwa njia ya kuudhika lakini kikejeli, nami nikamwelewa. Ni ile kwamba mimi ndiyo niliyekuwa msababishi wa kumfanya Shadya awe kituko jana, lakini Tesha ndiyo alikuwa anarushiwa vijembe kwa kumtania kidogo tu halafu mimi mastermind nikawa natendewa vizuri.

Nikatabasamu kidogo na kumwambia, "Siyo makosa yangu, we' ndo' unamchokoza sana."

"Aa wapi, we' umemkuna tu jana kwa kale kamsimbazi ndo' maana anakufagilia," akanijibu hivyo.

Ilikuwa kidogo tu nimwambie 'acha ujinga,' lakini nikajituliza na kumwangalia Bi Zawadi. "Cheupe wangu vipi?" nikamsemesha.

"Safi tu," akanijibu hivyo.

"Haya niambie. Kuna ishu gani mpya weye? Ama... ni ya sisi wawili tu, tutaongea baadaye?" nikamuuliza hivyo.

Bi Zawadi akacheka kidogo, naye Tesha akasema, "Ishu gani tena? Mtufahamishe."

"Hamna wala. Nilikuita tu... uje tunywe supu pamoja. Shadya anatengeneza makongoro. Unayajua?" Bi Zawadi akaniuliza.

"Ahaa... ee nayajua. Basi nikafikiri labda kuna tatizo," nikasema hivyo.

"Hapana baba, tunapenda tu ukiwepo hapa. Umetusaidia sana kurudisha sehemu kubwa ya furaha kwenye hii nyumba," Bi Jamila akaniambia hivyo kwa upole.

Nikatabasamu na kumwangalia Miryam, ambaye alikuwa ameweka macho makini kwenye simu yake. Ni kama vile akili yake ilikuwa mbali kiasi kwa sababu fulani, kwa hiyo nikarudisha umakini wangu kwa mama wakubwa.

"Wengine wakajaribu na kushindwa mpaka kulegea, eti ooh mwanenu ni chizi, kichaa, aende wapi wapi sijui... si huyu hapa umemsaidia? Tena hata mwezi haujaisha," Bi Zawadi akasema hivyo.

"Kweli. Kila daktari na dawa yake, halafu ya JC ndiyo original sasa. Kama masihara tu kaanza, cheki sasa hivi! Nakubali sana mwanangu. Sana," Tesha akaniambia hivyo.

"Ah usiwaze... tuko pamoja," nikamwambia hivyo.

"Siyo rahisi kupata mtu kama wewe siku hizi ambaye... ambaye anaweza kujitoa, akatumia muda wake kufanya mambo mengi kama unayofanya kwa ajili ya Mamu bila kutegemea malipo. Yaani... JC umenigusa sana. Jana Mariam kuanza kuongea... ni kitu nilichokuwa nasubiri kwa hamu kuja kukiona. Kama umeweza kumfikisha hapo basi ina maana utamfikisha mbali zaidi. Unastahili malipo makubwa zaidi ya yale yote ambayo Mimi alitoa kujaribu kumsaidia mdogo wake lakini watu wakamfanyia ulaghai tu... baba, yaani tunakushukuru sana," Bi Jamila akaongea hayo kwa hisia.

Nikajikuta hadi nakosa la kusema na kubaki nikitazama tu chini, nikiwa nahisi amani sana moyoni kupokea shukrani hiyo ya dhati.

Tesha akasema, "Ni kweli bro. Wote hapa tunakukubali sana. Mama zetu hawa, Mamu, mimi hapa, Mrs. Paparazzi kule..."

Sote tukacheka kidogo.

"Na Miryam pia. Tena dada anakukubali kichizi yaani, usimwone amekaa tu hivyo amebunda, anakuelewa sana. Huwa anasema hapa 'yaani JC ni jembe kali sana!'"

"Tesha..." Miryam akamwita hivyo kwa sauti ya chini kama kumwonya.

Wengine wakacheka kidogo, nami nikashindwa kujizuia kutabasamu na kucheka kidogo kwa pumzi. Nilijua Tesha alikuwa anaongeza chumvi tu, lakini alionyesha kwamba uthamini wa familia yake nzima kunielekea aliujua.

Mariam akanishika begani, nami nikamwangalia. "Tutacheza... mm..muziki... baadaye?" akaniuliza hivyo.

Nikatabasamu na kumwambia, "Leo tutapumzika, sawa? Mpaka kesho. Nataka nikufundishe mchezo mwingine kesho. Utaupenda... sawa?"

Akatabasamu na kutikisa kichwa kidogo kuonyesha uelewa.

"Hamtacheza leo?" akaniuliza hivyo Bi Zawadi.

"Ee, leo mapumziko, kesho tutaendelea. Nimemnywesha-nywesha maziwa akayazoea, sasa hivi nitaanza kumpa msosi mgumu kidogo ili akae sawa zaidi. Si mnaelewa?" nikawaambia hivyo.

"Ndiyo baba, inaeleweka. We' endelea tu na utaratibu wako, ujue sisi tutakupa support yote," Bi Jamila akaniambia hivyo.

"Da' Mimi, mbona uko kimya tu? Mpe maua yake mwana huyu, tena mpe ya kimombo. Oya, dada anajua kiingereza huyo!" Tesha akasema hivyo.

"Usinambie," nikatoa jibu hilo.

Mama wakubwa wakacheka kidogo, nami nikamtazama Miryam machoni na kuona ananiangalia kwa macho yenye utafakari. Niliona wazi kwamba akili yake ilikuwa imemezwa na jambo tofauti na hili lililokuwa likiendelea hapa japo alikuwa msikivu wa mada nzima, na hakuna mtu yeyote ambaye aliona hilo isipokuwa mimi.

Nikiwa bado namwangalia mwanamke huyo, sauti ya Shadya ikasikika kutokea jikoni ikisema, "Mimi... tayari."

Nikajua tu kiongozi wa mapishi ndiyo alikuwa anaitwa ili kwenda kusababisha zaidi huko jikoni, naye Miryam akanyanyuka tu na kupita upande wangu kuelekea huko. Ah mwanamke alikuwa na mguu huyu! Niweke tu heshima pembeni aisee, yaani Miryam alikuwa moto!

Moja kati ya wale wanawake waliobarikiwa karibia kila kona ya miili yao halafu sasa alijua kujitunza. Harufu yake iliyopitishwa na upepo aliponipita ikanifanya hadi nifumbe macho kuisikilizia zaidi, ila nikajitoa mbali kote huko kifikira na kuirudisha ile heshima niliyokuwa nimeiweka pembeni kwa muda mfupi. Kama nilivyokuwa nimesema awali, huyo alikuwa wa kumwacha tu hivyo hivyo.

Kwa hiyo sisi wengine tukaendelea kuongea mambo kadha wa kadha kupisha muda, na tukimsaidia Mariam aendelee kutia jitihada ya kuongea, ndipo Shadya pamoja na Miryam wakaanza kuleta supu za nyama ya kongoro kwenye mabakuli mapana ya udongo.

Walianza kwa kuwapatia mama wakubwa supu zao na ya Mariam, nao wakaamua kushuka chini na kukaa ili wanywe kwa kujinafasi, naye Mariam akaenda kukaa pamoja nao hapo chini pia. Shadya na Miryam wakatuletea supu mimi na Tesha; Shadya akimpa Tesha yake, na Miryam akinipatia ya kwangu.

Alipokuwa ameinama kiasi kunipatia bakuli hilo, nikalipokea huku nikimtazama usoni kwa umakini, na macho yake mazuri yakaniangalia pia. Ilikuwa kama nimemezwa na hali ya kutaka kupata maana yoyote ile ya utizami wake kwangu mpaka nikawa sikazii fikira ni jinsi gani bakuli hilo lilikuwa likiunguza viganja vyangu. Sikuona ujumbe wowote ule kwenye macho yake zaidi tu ya uzuri yaliyokuwa nao, naye akaacha kuniangalia na kurudi tena jikoni.

Ni hapa sasa ndiyo nikahisi jinsi mikono yangu ilivyochomwa. Woi! Nikaliweka bakuli kwenye mkono wa sofa na kujikausha, nikiwa nakaza maumivu, ndiyo baada ya kutulia nikaanza kunywa thupu. Na ilikuwa "thupu" tamu sana.

Miryam na Shadya wakarudi sebuleni tena wakiwa na mabakuli yao pia na kuketi pamoja kwenye sofa la pembeni. Nyama za kongoro zilikuwa nyingi, naye Tesha akawa ameniambia kwa sauti ya chini kwamba Shadya ndiye aliyekuwa ameagiza ziletwe ili wazipike, akihisi huenda mwanamke huyo alitumia hela yake kujumuisha na pole niliyompatia jana kuzinunua.

Ilikuwa nyama nyingi sana yaani ilikuwa ni kunywa, kutafuna, na kushiba kabisa kama kiamsha kinywa. Ilivyo laini na yale mamifupa sasa! Tukaendelea kujinoma taratibu, na niligundua kwamba bibie Miryam alikuwa amejiwekea kiasi kidogo sana, hivyo yeye ndiyo akawa amewahi kumaliza na kurudisha chombo chake jikoni.

Kidogo tu nikawa nimetumiwa ujumbe kwenye simu, nami nikautazama na kukuta ni Ankia ndiye aliyeutuma. Alikuwa ananifahamisha kwamba ametoka pamoja na wale marafiki zake kwenda mahala fulani, na alikuwa amerudishia tu mlango wa kule ndani si kuukaza kwa funguo. Nikamjibu tu poa, tutaonana baadaye, nami nikaweka simu pembeni.

Tukaendelea kufurahia supu na maongezi mepesi ndani hapo, huku nikiwa makini kutambua mbadiliko mwingine wowote wa kitabia kwa binti Mariam kadiri alivyoendelea kula, na ndipo tukasikia geti huko nje likigongwa.

Tesha akataka kuacha kula ili aende kuona ni nani yupo huko nje, lakini Miryam akamzuia na kusema yeye ndiyo angeenda kufungua. Alitoa kauli ya kwamba anaenda kufungua, siyo kuona ni nani yupo huko nje, na hiyo ikanifanya nitambue kwamba kuna mtu aliyekuwa anamtarajia afike hapo; labda mgeni wake.

Akatoka ndani, sisi tukiendelea tu kutulia hapo na mama wakubwa, kisha baada ya sekunde chache bibie Miryam akarudi tena. Alianza kuingia yeye, kisha nyuma yake wakafata watu wawili. Kila mmoja hapo ndani, hata mimi, tulishangaa sana baada ya kumwona Joshua akiwa hapo! Yaani ilikuwa ni ujio mmoja wa ghafla sana ambao hakuna yeyote hapo alikuwa ameutegemea kabisa.



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
Hii story ni moja kati ya story zenye uhalisia zaidi.Tofauti na wale utakuta geti la kuzimu limefunguka mara sijui malaika akamsemesha.
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA ISHIRINI

★★★★★★★★★★★★★


Joshua alikuwa amefika hapo pamoja na mwanamke mwenye mwonekano wa umri usio mbali sana na wa Ankia, mweusi wa maji ya kunde, mrefu kiasi cha kumfikia Joshua, naye alikuwa amevaa gauni la kijani lililoubana mwili wake na kuishia magotini.

Alikuwa na mwili ule wa umenawiri-haujanawiri hivi, kawaida tu yaani, lakini alikuwa na hips nene zilizoonyesha alikuwa na ujazo wa kutosha huko nyuma. Miguu yake ilionekana kung'aa kwa mafuta lainishi, alikuwa amevalia wigi la nywele fupi kichwani kama za wakorea, na midomo yake ilikuwa minene. Joshua yeye alikuwa amevaa T-shirt la njano pamoja na suruali ya jeans, na wakati huu alikuwa amenyoa ndevu zake zote kidevuni.

Tesha akasimama kutoka sofani, naye Mariam akasimama kutoka chini. Mama zao wakubwa na hata Shadya wakasimama pia wakiwa wanawatazama wageni kama vile ni wageni sana kwao, nami nikaendelea kuwaangalia kwa umakini. Sasa nikawa nimeelewa kilichofanya Miryam aonekane kutekwa kiakili muda mfupi nyuma. Alikuwa anasubiria ujio wa hawa watu.

"Karibuni jamani," Miryam akawaambia hivyo wawili hao.

"Asante sana. Shikamooni," mwanamke huyo mgeni akaongea hivyo na kuwasalimu mama wakubwa huku akionyesha ishara ya kupiga magoti kiasi.

Bi Jamila na Bi Zawadi wakaitikia salamu yake kwa kusema 'marahaba.'

Joshua pia akasema, "Shikamooni," lakini wanawake hao hawakumjibu na kubaki wamemwangalia tu kwa umakini.

"Mimi, huyu anafanya nini hapa? Ameleta tena fujo zake? Aisee... ngoja nimpigie mzee Hamadi," Tesha akasema hivyo huku akitoa simu yake.

Shadya akatoka upande huo waliokuwa wamesimama wageni pamoja na Miryam, naye akaenda kusimama pembeni yake Mariam.

"Tesha hapana... hebu tulia. Mimi ndiyo nimewakaribisha... weka simu chini," Miryam akamwambia hivyo.

Tesha akamwangalia na kuuliza kwa sauti ya chini, "Nini? We' ndiyo umewaita?"

Hali hapo ilikuwa imeanza kujenga uzito, nami nikamwona Mariam akianza kubabaika kwa ule mtetemo wake wa kichwa. Agh, hiyo haikupaswa kutokea! Presha yoyote ambayo ingemwingia msichana huyu ingesababisha tuanze kurudi nyuma tena wakati alikuwa anaonyesha maendeleo, na ni wazi kilichosababisha hilo ilikuwa ni woga wake kumwelekea Joshua.

Nikasimama na kumgusa Shadya mkononi, naye aliponiangalia nikamwambia kwa sauti ya chini, "Naomba umpeleke Mamu chumbani."

Kwa kunielewa vizuri, Shadya akamshika binti mkono na kuanza kwenda pamoja naye chumbani kweli.

"Mimi, wewe ndiyo umewaleta hapa? Ili iweje?" Tesha akamuuliza hivyo dada yake tena.

"Tesha nakuomba ushushe hiyo sauti. Hawa ni wakubwa... wamekuja tuongee. Naomba ukae tuzungumze," Miryam akaongea kwa utulivu.

Mwanamke huyu akawaonyesha wageni masofa ili wakae, kistaarabu sana. Kiukweli hata mimi pia nilikuwa nashangaa, iweje iweje mpaka huyo jamaa akaja tena sehemu hiyo na kukaribishwa vizuri. Na huyo mwanamke alikuwa nani?

"Tuzungumze? Tuzungumze nini na huyu mbwa, Miryam?" Tesha akasema hivyo kwa hasira.

"Tesha!" Miryam akasema hivyo kama kumzuia.

"Jamani Tesha... tumekuja tu kuongea vizuri. Haina haja ya magomvi..." huyo mwanamke akasema hivyo.

"Magomvi? Unayajua magomvi aliyokuwa ameyaleta hapa huyo mume wako?" Tesha akamwambia hivyo.

"Tesha niangalie..." Miryam akasema hivyo.

Tesha akamwangalia kweli, na ni muda huo ndiyo Shadya akawa amerejea peke yake.

Nikawa nimetulia tu usawa aliosimama Tesha sasa, huku nikiona namna ambavyo huyo mke wa Joshua alinitazama sana.

"Ninakuomba ukae chini. Nisikilize... kuwa na adabu... kwa ajili yangu," Miryam akamwambia hivyo mdogo wake.

"Miryam nakuheshimu sana. Sana. Lakini hii kitu... siwezi kukubali. Amekuja kuongea nini? Hivi kweli... ma' mkubwa... hii ina-make sense? Miryam amekuwaje?" Tesha akaongea kwa hisia.

"Ndiyo utulie mwanangu tusikilize kilicholetwa hapa..." akasema hivyo Bi Zawadi.

"A-ah... hapana. Siwezi me kukaa na mtu aliyewashushia nyie heshima mbele ya watu kwa kusema hamna faida yoyote hapa! Anawajua? Kamtukana mpaka na dada halafu anamleta hapa? Ili iweje? Nisikilize nini labda atakachosema huyu mjinga?" Tesha akamwambia hivyo Bi Zawadi kwa hasira.

Mama wakubwa wakawa wametulia tu.

"Tesha mdogo wangu... usiwe hivyo. Mimi nimekuja tukae chini tuongee ili..." Joshua akawa anaongea kwa upole.

"Toka hapa mjinga wewe!" Tesha akamfokea.

"Tesha!" Miryam akamwita kiukali.

"Nini Miryam? Nini? Mbona unakuwa kama umerogwa?" Tesha akasema hivyo kwa hasira.

"Tesha hebu acha!" Bi Zawadi akasema hivyo.

Miryam akawa anamtazama mdogo wake kwa mkazo.

Nikamshika Tesha mkononi na kumwambia, "Oy, hebu jitulize. Siyo fresh, uko mbele ya mama zako."

"Ah... JC mwanangu, labda unisaidie kuelezea hii kitu. Hivi hata inaeleweka kweli? Huyu mbwa mpaka anamwita mdogo wangu taahira, anamwita Mimi dada nusu, halafu nimkaribishe eti nini... kisa kashusha sauti leo?" Tesha akaendelea tu kulalamika.

Alikuwa na haki kabisa ya kutenda namna hiyo, kwa sababu hata kama ingekuwa ni mimi nisingeweza kujihisi amani kukaa sehemu moja pamoja na mtu kama Joshua aliyefanya mambo mengi mabaya sana kwa hii familia. Sijui Miryam alikuwa na moyo wa aina gani!

Tesha alikuwa amekasirika mpaka jasho likaonekana kumtoka, naye Miryam akamwambia, "Nimekuomba ukae kimya kwa kuniheshimu mimi, lakini umekataa, si ndiyo?"

"Mimi, usitumie kiwango cha heshima nilichonacho kwako kunifanya nionekane jackass. Hata ufanye nini, hata useme nini... siwezi kupoteza muda wangu kumsikiliza wala kuongea na huyu mjinga..."

"Tesha! Mimi ni kaka yako..." Joshua akamkatisha.

"Wewe ni mpumbavu sana! Yaani kama unajiweza, niko tayari kuvuruga hii sebule nikipigana na wewe mpaka kukuua, lakini never siwezi kukuita wewe kaka yangu! Umeshakufa kwangu," Tesha akamwambia hivyo.

Dah! Hii kitu ilitia sana huruma.

Niliwaangalia mama wakubwa na kuona namna ambavyo hata wao walihisi maumivu aliyohisi Tesha japo walijikaza na kutosema lolote, na Miryam alikuwa amekosa la kusema na kubaki akimtazama mdogo wake kwa kuvunjika moyo.

"Tesha... tutoke kidogo," nikamwambia hivyo kwa sauti ya chini.

"Ee mwanangu, twende tuondoke. Hapa siyo," Tesha akasema hivyo na kuanza kuuelekea mlango kwa kasi.

Ilikuwa kasi iliyofanya mke wa jamaa asogee pembeni kwa woga kiasi mpaka kumpamia Miryam, naye Tesha akampita Joshua na kuufungua mlango kwa nguvu, kisha akatokomea nje. Aisee!

Nikawaangalia mama wakubwa na kusema, "Warembo wangu... mimi naenda. Mamu akishtua kwa lolote niiteni."

"Sawa mwanangu. Mwangalie basi na huyo, eti?" Bi Zawadi akasema hivyo, akiwa amemaanisha Tesha.

"Hamna shida. Tutaonana baadaye," nikamjibu.

Wakakubali kwa kutikisa vichwa vyao, nami nikaanza kuelekea mlangoni.

Sikuwasemesha wala kuwatazama wageni hata kidogo, na ile nilipoufikia mlango nikamwangalia Miryam na kuona amejishika tu kiunoni huku akitazama upande mwingine kwa kuvunjika sana moyo, nami nikatoka tu ndani hapo.

Hali ya hewa ilikuwa imebadilika ghafla, na Tesha alionyesha ni jinsi gani alivyokuwa na hasira kali sana kumwelekea ndugu yake. Yaani alikuwa anatamani hadi kumuua, na nilijua hilo kuwa kweli maana aliwahi kusema kwamba kwa ajili ya dada yake angeweza kuua mtu yeyote. Ila hilo lisingekuwa jambo la busara kufanya, nami ningepaswa kuhakikisha namwangalia kwa ukaribu ili asije kwenda kuua mtu huko kweli!

Hakuwepo hapo ndani ya geti, nami nikatoka nje na kumkosa pia. Mh? Ankia hakuwepo kwa hiyo Tesha asingekuwa ameenda kule ndani kwetu hasa kwa sababu nilimuuliza Fatuma hapo nje ikiwa amemwona jamaa anapita upande huu, lakini akakataa. Huyu angekuwa ameondoka, nami nikaona nimtafute kwa simu. Piga karibia mara tano, wapi. Zote hakupokea.

Nikaamua niende kumtafuta Masai, lakini nako nikamkosa. Ikawa wazi kwamba alikwenda sehemu nyingine isiyofahamika kwangu, kwa hiyo kama nisingempata kwa simu basi ndiyo nisingeweza kufanikisha zoezi la kuangalia usalama wake.

Nikaamua kurudi pale kwa Ankia na kwenda kukaa tu sebuleni, nikingoja kupata taarifa yoyote kuhusu alipokuwa huyo kijana kutoka kwa watu niliowaulizia pale Masai; yaani kama angefika hapo biashara ikianza kazi. Sijui kwa nini tu lakini nilikuwa nahisi kuishiwa pozi kabisa kwa sababu ya kujua mambo yaliyokuwa yakiendelea kwenye hiyo familia.

Bila shaka, Miryam alikuwa anajaribu kutafuta amani, lakini ilionekana kuwa ngumu mno kwa yeyote kukubaliana na njia yake ya kuona mambo; hata mimi sikumwelewa kwa kweli. Ni kitu gani kilichokuwa kinamfanya afumbie macho mambo mengi mabaya ambayo Joshua alikuwa amefanya na kujaribu kumweka karibu yao tena?

Ni lazima kulikuwa na kitu kilichomsukuma atende hivyo, lakini najua haingekuwa rahisi kwa ndugu zake kukubaliana naye. Hata Mariam tu alisumbuliwa mno na uwepo wa mwanaume huyo karibu nao, na hilo lilikuwa tatizo ambalo ningepaswa kuzungumza na Miryam kulihusu.

★★

Nikaendelea kukaa sebuleni nikiwa nasubiri lolote lile, na kiukweli niliweza kuhisi hali ya msongo kichwani iliyonifanya nijihisi mzito kiasi. Feni ilikuwa inanipuliza lakini bado nilihisi joto. Akili yangu ilikuwa katikati ya mambo mengi ya kufikiria kiasi kwamba mpaka nikawa nahisi kukosa amani.

Sikujua ni yapi yaliyokuwa yanaendelea kwenye hiyo nyumba baada ya kumwacha Joshua pamoja na wapendwa wangu, sikujua Tesha alikuwa wapi, na huyu Ankia na yeye aliona aondoke tu wakati ambao nilihitaji company kidogo. Nikaona uhitaji wa kufanya jambo lenye kuchangamsha kiasi, lakini sikuwa na wazo zuri lisilo lenye kuboa.

Ikiwa imekwishafika mida ya saa saba mchana sasa, nikawa nimempigia Ankia kumuuliza kama angerudi mapema, naye akaniambia alikuwa amekwenda mtaa wa eneo wanaloliita Emirate sijui, nadhani kwa mashoga zake, na akasema akitoka huko ilikuwa ni kupitilizia saluni kwanza ili atengeneze nywele zake.

Akaniuliza ikiwa kulikuwa na shida, nami nikamwambia nilikuwa nimemkosa tu kwa sababu ya kuboeka kukaa mwenyewe ndani. Akiwa hajui kuhusiana na mambo yaliyokuwa yametokea kwa majirani zetu, akaniambia nimwite Tesha tu ili anipe ushirika wake, nami nikaona nisianze kumsumbua kwa kumwambia hali ya huku kwa wakati huu, kwa hiyo nikamkubalia na kukata simu.

Kukosa lolote jipya kutoka kwa Tesha baada ya kumpigia na kumkosa kwa mara nyingine tena kukanifanya niamue kwenda kulala tu ili muda upite. Nikaingia jikoni kwanza na kuuangalia mkate aliokuwa ametengeneza Ankia. Ulikuwa mkubwa, umbo la duara kufatisha sufuria, na sehemu fulani ilikuwa imekatwa kwa pembetatu pana kuonyesha kwamba Ankia na marafiki zake walikuwa wamekula kabla hawajaondoka. Nikakata kiasi na kuanza kumega, nami nikarudia sofa tena sebuleni ili nikimaliza kuula ndiyo nielekee chumbani kulala.

Niliposhika simu, nikakuta ujumbe mfupi kutoka kwa Soraya.

'JC mim naumia san. Sielew kwnn umenitup namn hii. Au kun sehm nmekosea? Nambie nijirekebishe'

Ukasomeka hivyo. Dah! Huyu Soraya huyu! Alinifanya nihisi sauti yake kabisa ikiwa imesema maneno hayo, na sasa akawa mpaka ananifanya nijihisi kuwa mwenye hatia. Kwamba namwonea.

Unajua huyu alikuwa mwanamke aliyeolewa na hata kama hangekuwa ameolewa, sikuwa na lengo la kudumisha uhusiano wa kimwili niliokuwa nimeanzisha pamoja naye; hasa baada ya haya mambo mengine huku kuongezeka. Ni kama tu nilivyokuwa nimemweleza Ankia kuhusu namna navyoendesha maisha yangu kwa upande wa mapenzi, na hiki ni kitu ambacho nilitaka Soraya pia akielewe ili asije kunizoea mno mpaka akaanza kushindwa kupumua akiwa na familia yake.

Nikamjibu hivi kwa sms, 'haujakosea, nina mamb mengi tu dear'

Akajibu, 'mamb mengi JC? mamb gn? Si uliniambia uko likizo? ama umepat mwnmk mwngn?'

'Nikisema ndyo?'

'lkn JC'

'Kwan we unatak iweje Soray? Unatak nn hasa?'

'natak kuw na ww'

'Soma hii uelewe vyema Soraah. Wewe na mimi siyo wapenz pekee, ni wapenz marafiki. Una mume, na mimi nina mtu wangu. Usitarajie labd niwajibike kwako % zote, unaelewa?'

'kwan me nimekuomb uwajibike JC? me natak tukutan2.. nimekumiss'

Nikaisoma sms hiyo kwa ufikirio, nami nikamjibu, 'Saw. Tukutane wap?'

'nakusikiliza2 ww,' akajibu hivyo.

'Uko free saiz?'

'ndy'

'Saw. Naingia hapo Mbagala muda so mref. Ukuje pale pale pa sikuile, si unapakumbuk'

'ndy'

'Ee uje. Kwanz uko wapi?'

'nyumban'

'Watoto je?'

'nawaacha na mtu'

'Poa. Jiandae tukutane fasta,' nikamwandikia hivyo, kibabe yaani.

'aya'

Mpango wangu wa kwenda kulala ukawa umevurugwa, lakini si ningeenda kujinoma bwana? Hata hivyo mwanzoni nilikuwa nikitaka kufanya jambo lenye kuchangamsha ili niondoe msongo uliokuwa umeanza kuniingia, kwa hiyo ni kama Soraya alikuwa amekuja kuwa ukombozi.

Nikaona uhitaji wa kujimwagia maji tena, kisha nikatia pamba nyepesi na kuvaa kwa mara ya kwanza zile ndala nzito na mpya nilizonunua siku ile Kariakoo. Nikawa nimekaa fiti kimwonekano na kunukia fresh, kisha nikamjulisha Ankia kwa ujumbe kwamba hata mimi ninatoka pia hivyo ninafunga mlango kwa funguo, halafu ningeziacha zake kwa majirani zetu pale kwa kuwa hakuondoka na funguo zake za ziada.

Nikiwa nimeshatoka na kufunga kabisa ndiyo akawa amenijibu kwa kusema ameelewa, nami nikaelekea pale kwao Tesha. Nikagonga geti, na baada ya sekunde kadhaa Shadya akawa amefungua. Akanisifia kwa kupendeza na kuuliza nilikokuwa naenda, nami nikamwambia nafika hapo Mbagala mara moja kuonana na rafiki.

Akamuulizia na Tesha, ndiyo nikamwambia tu kwamba tuliachana baada ya kuwa ameondoka kwao ila sikujua alipokuwa amekwenda kwa sasa, lakini nikamhakikishia kwamba angekuwa sawa. Nikamkabidhi funguo za nyumba yake Ankia na kumwambia ikiwa ningechelewa kurudi kabla yake basi angezikuta hapo, naye akawa amekubali.

Nikaona niulize tu hali ilikuwa vipi hapo ndani, naye Shadya akasema yaani kulikuwa na bonge moja la maigizo kutoka kwa Joshua na mke wake. Akaniambia jamaa hadi alipiga magoti kabisa na kuishika miguu ya Bi Jamila na Bi Zawadi akiwa anaomba msamaha, na sasa walikuwa wakiendelea kuzungumza kuhusu mengi waliyohitaji kufanya ili kurudisha amani kwa familia nzima, hususani kumshawishi Tesha awe mpole.

Ila hata Shadya akaonyesha bado hamwamini huyo mwanaume, na mimi nikamwambia tu aendelee kusikilizia hali. Nikamwambia aende ndani na kuwapa warembo wangu salamu yangu ya kuaga, na ikiwezekana tungeonana baadaye, kisha ndiyo nikaondoka.

★★

Dakika chache baadaye nikawa nimefika Mbagala, nami nikakunja mguu mpaka kufikia Zakhem na kuingia kwenye hoteli ile niliyomtandikia Soraya penzi la maana siku ile mpaka sasa akawa analililia tena. Nikalipia chumba cha elfu thelathini, nami nikawa nimeomba kuingia kwenye kile kile nilichotumia siku ile baada ya kukuta kiko bila mteja.

Nikakaa kitandani na kumsubiria mja wangu. Nikajaribu kumpigia Tesha simu tena bila mafanikio, nami mpaka nikaingiwa na hasira na kuamua kuachana naye. Kama hakutaka kunijibu, basi, na hata hamu ya kwenda kutazama mechi tayari ilikuwa imeshakata hasa kwa kuwa hapa nilikuja kucheza yakwangu mwenyewe.

Nikaweka simu pembeni na kuwasha TV ndogo iliyokuwa humo. Zilikuwepo chaneli kadhaa za king'amuzi cha Azam, nami nikaitafuta chaneli ambayo ingeonyesha mechi ile niliyokuwa nimeisusia, nami nikaipata.

Nikaendelea tu kutulia hapo kama nusu saa hivi, ndipo simu yangu ikaita. Soraya huyo. Nikapokea kumsikiliza, naye akasema ameshafika Zakhem kabisa, hivyo nikamwambia aanze kuingia kwenye hoteli hiyo na mimi ningekutana naye ngazini. Alikuwa hana aibu wakati huu inaonekana maana alikubali haraka, kisha akakata simu.

Nikanyanyuka na kutoka ndani hapo, nami nikaenda kusimama kwenye kingo ya ngazi na kumsubiri. Mtoto huyo akafika. Alikuwa anapanda ngazi taratibu, nami nikatumia sekunde chache kumchora kwa macho.

Alikuwa amevaa yale magauni wapendayo kuvaa wanawake waislamu ambayo huvaliwa na suruali ya skinny kwa ndani, yaani miguuni, na kufikia mikononi nguo hiyo inakuwa ya mtindo huo huo wa skinny kama hako kasuruali. Lilikuwa jeupe, lililoubana kiasi mwili wake na kuuchoresha vizuri sana, na kichwani alivalia ushungi uliopendezesha sana uso wake mweupe. Oh, na chini miguuni alivaa kiatu kirefu chenye rangi ya samawati.

Wanaume aliokuwa anapishana nao walimwangalia kwa macho yenye uchu kwelikweli, naye akawa amemaliza kupanda ngazi na kuja upande wangu. Nilikuwa namwangalia kwa macho makini tu, lakini yeye akashindwa kujizuia kutabasamu na kuangalia chini kwa haya huku akitembea kwa mdundo wake wa kianamke.

Akanifikia karibu, akiwa ameshika pochi ngumu ya njano mkononi, naye akasema, "Mambo?"

"Mambo yamefanyaje?" nikamuuliza hivyo nikiigiza kuwa makini kweli.

Akacheka kwa pumzi na kuubana mdomo wake huku akiniangalia kwa uvutio.

"Em' njoo hapa..." nikamwambia hivyo na kumshika mkono.

Nikaanza kukielekea chumba nikiwa namvuta taratibu mpaka tukaingia pamoja. Ni baada tu ya kuingia na kuufunga mlango ndiyo nikakishika kiuno chake kutokea mgongoni na kumvuta kwangu kwa nguvu. Nikambana na kuanza kubusu upande wake mmoja wa shingo, naye akaangusha pochi yake chini.

"Hhh... JC..." akanena kwa kunong'oneza.

Sikutaka kelele. Yaani hapa nilichokuwa nataka ilikuwa kufuata ushauri wa wimbo wake Darassa; acha maneno, weka muziki!

Ndani ya sekunde chache Soraya akajikuta hana nguo, hana viatu, mpaka ushungi nikamtolea na kumwacha na nywele zake laini alizoziwekea kibanio kisogoni. Na chenyewe kikatupwa! Nikamrusha kitandani, kisha nikaanza kumpa tomasa na kumnyonya viamsha hisia mpaka akaanza kuchemka.

Nikatoa nguo zangu pia, nami nikampa pipi anyonye, naye hakupinga. Hisia zangu zilikuwa karibu mno kwa wakati huu yaani ilikuwa kidogo tu nimwagilie mdomo wake, lakini nikajizuia na kumweka aruke kichura; yaani mimi nilale, yeye aendeshe. Na kalijitahidi kweli siku hii.

Alipochoka ndiyo nikaanza kazi. Piga, piga, piga, mitindo miwili tu, akaanza kutetemeka miguu.

"Nakojoa... nakojoa...."

Akawa anaongea kwa presha kweli, nami nikaendelea kumshindilia mpaka akamwaga shukani! Leo alikuwa amepagawa kweli yaani alitoa malalamiko ya raha kwa sauti yake yote. Nilipenda sana jinsi alivyojiachia, kale kaupole kake aliamua kukapotezea.

Alionekana kushangaa namna ambavyo niliendelea kumtandika tu bila kutua mzigo wangu hata mara moja, nami nikamwambia nilikuwa sitaki kujiachia mapema kwanza kwa hiyo nilikuwa najikaza. Lakini baada ya dakika chache mwili ukashindwa kujizuia tena, nami nikajiachia ndani ya mwanamke huyo kwa raha zote!

Soraya alikuwa anaonyesha kupenda sana jinsi nilivyomwogesha ndani kwa ndani, kwa kuwa aliendelea kunibana kwake mpaka nilipomaliza. Na nilijisikia vizuri kweli baada ya kumaliza kazi kiaina hiyo. Tukaendelea kulala pamoja tu kitandani hapo, na nilipoona mechi imeanza, nikatambua ilikuwa ni saa kumi jioni sasa.

Nikiwa nimeegamia mto huku Soraya akiwa amelalia kifua changu, nikamuuliza, "Vipi mommy, unahisi njaa?"

Akasema, "Njaa yangu ilikuwa kwako JC, ninachohisi sasa hivi ni furaha kwa sababu umenishibisha."

Nikatabasamu na kusema, "Haya bwana. Ni fresh kama umefurahi."

"Sana. Yaani na ulivyo na mapigo matamu, halafu kama hauchoki!"

"Ahahah... afya kwa mazoezi tu."

"Kumbe? Mpaka nikafikiri labda unatumia dawa."

"Kwa nini? Kwani mzee wako huwa anatumia?"

"Hapana. Yaani JC... mume wangu ni mchovu tu... akienda mara mbili amechoka..."

Nikacheka kidogo.

"Ana mahaba ya kuku jamani! Halafu siyo fundi kama wewe ulivyo," akaniambia hivyo.

"Kwa nini usiongee naye? Labda akabadilika. Ama hampendani?"

"Hamna, ananipenda. Tunashirikiana kuwahudumia wanetu, sema tu ndo' hivyo... ameacha kuchangamka. Nilikuwa naogopa kutoka nje ya ndoa ingawa nimeshawishiwa sana na wanaume wengi, lakini wewe... nikashindwa kujizuia."

"Sasa mimi nina nini kwani? Hiki kibamia ndo' useme kinakuzuzua hivyo?"

"We! Hiyo yote unaiita kibamia? Acha kufuru. Sumaku yako imenivuta kwa nguvu sana JC, unayajua kweli yaani. Natamani hata nikumiliki," akaniambia hivyo.

Umeona? Kule kule kwa Ankia.

Nikasema, "Najua, lakini..."

"Usijali JC... naelewa. Umeshanielewesha. Hata wewe una mtu wako kwa hiyo hapa tuko kusaidiana tu. Please... tuyaweke hayo pembeni. Tufurahie tu wakati huu, sawa?"

Aliongea kistaarabu sana mpaka nikawa namwonea huruma kiasi. Lakini kukaza ilikuwa lazima. Sababu nilizijua mimi mwenyewe.

Kwa hiyo tukaendelea tu kulala hapo pamoja huku nikiangalia mechi na kumpigisha mwanamke huyu story, naye akaniomba tucheze mechi fupi tena. Sikumnyima. Na alikuwa ameniomba fupi tu ili ndiyo tuondoke hapo lakini nikampa ndefu ili aende kwake akiwa ametosheka kwa leo. Nilimvuruga mno huyu mwanamke mpaka akasema imetosha, ningemuua!

Kwa hiyo angalau mechi zangu na Soraya zikawa zimemalizika kwa ushindi, na Simba nayo ikawa imeshinda kwa magoli mawili kwa moja dhidi ya Singida; na walikuwa ugenini kama vile tu ambavyo na mimi nilikuwa nashinda mechi za ugenini huku Mbagala!

Ikawa imefika saa kumi na mbili na nusu hivi jioni, giza likianza kulivaa anga huko nje, nasi tukaoga pamoja na mimi kumtandika kidogo tena mwanamke huyo cha bafuni, kisha ndiyo tukavaa na kuondoka hapo.

Soraya alikuwa amenipa ahadi kwamba hangesahau kamwe penzi nililokuwa nampatia kuambatana na furaha aliyokuwa akihisi ingawa alikwenda kinyume na sheria za dini yake, naye akasema ikiwa 'majaaliwa' yangekuwa upande wake, basi tungekuja kukutana kwa mara nyingine tena. Sikuwa na neno, nasi tukaachana na kuelekea sehemu za makazi yetu.

★★

Nilifika pale nyumbani mida ya saa moja na kukuta Ankia akiwa bado hajarudi. Nikaamua kufungua tu milango hapo na kwenda ndani ili nipumzike kidogo. Funguo niliyokuwa nimeiacha kwa kina Tesha ilikuwa ile ya Ankia, niliyofungulia wakati huu ikiwa ni ile ya ziada aliyokuwa amenipatia, kwa hiyo nikafikiria labda hiyo yake ingefatwa baadaye.

Nikakaa zangu tu sebuleni na kuanza kuchat na Soraya, ambaye hakutaka kuacha kunisifia kwa mapenzi motomoto niliyotoka kumpatia masaa machache nyuma, nami nikawa nimemwambia ajitahidi sana kuwa mwangalifu ili asije kukamatwa na mumewe; nisije kuwekwa katikati ya chanzo cha ndoa yake kugeuka kuwa matatizo. Sawa alikuwa mtamu, lakini mimi hiyo kitu nilifanya kujichangamsha tu, ohoo!

Muda ukaendelea kutembea, mpaka inafika saa tatu usiku bado nilikuwa ndani tu nikisubiri kusikia chochote kuhusu Tesha, lakini simu yake haikupatikana wala hakukuwa na mtu mwingine aliyenipa taarifa za jamaa kuonekana Masai. Hata Bobo mwenyewe hakujua.

Nikawaza labda sijui alikuwa amesharudi hapo kwao, na huenda kutoka kwenda kumwangalia lingekuwa jambo la muhimu kufanya. Ilikuwa ni hali tu ya kujali iliyonifanya nihisi kuwajibika kwa huyo kijana, kana kwamba alikuwa mdogo wangu kabisa.

Ankia hakuwa amerudi bado kutoka saluni, na mara kwa mara nilikuwa nikizungumza na marafiki kwenye simu na kuchat na Soraya pia, na ilipogonga tu saa nne kamili nikaamua kutoka ndani hapo ili niende kwa jirani yetu kumwangalia rafiki yangu.

Nikavaa masai zangu miguuni kwa kuwa zile ndala mpya nilikuwa nimeshazirudisha chumbani, nami nikaanza kuelekea upande wa nje, lakini kabla sijalifikia geti letu dogo, nikawa nimekanyaga kitu fulani kigumu kilichosababisha masai yangu moja mguuni ivutwe, na hivyo nikawa nimejikwaa na kusukumwa mbele kwa mshtuko huo.

Ilikuwa kwa nguvu, na hilo likasababisha hicho kiatu changu kikatike sehemu ya kuingizia kidole gumba cha mguu, lakini sikuumia. Ah nikaisogelea masai yangu nikiwa peku mguu mmoja, na sikupenda kweli kukanyaga chini, nami nikachuchumaa ili kuangalia kilichonikwaa.

Ilikuwa ni msumari, ukiwa umepigiliwa chini na kubaki umechungulia juu kiasi, nami nikaelewa hilo kuwa utundu wa watoto ambao wangeingia mpaka sehemu hiyo ya mwanzo getini na kufurahia michezo yao, na sasa wakawa wamenisababishia hasara. Ingebidi kumwambia mwenye nyumba wangu ili awaonye la sivyo tungekuja kukatika vidole.

Nikauchomoa msumari huo na kusimama, lakini kwa ule mpigo wa haraka wa macho baada ya kugeukia ukuta, nikawa nimemwona Joshua kupitia matundu ya ukuta akitoka kule ndani, simu ikiwa sikioni, na akiwa kama anakuja upande wangu. Nikachuchumaa tena na kuusogelea ukuta, nami nikauegamia na kutulia.

Sikufikiri kwamba bado huyu jamaa na mke wake walikuwa hapo, lakini kumwona ametoka ndani ili aje huku kote kuzungumza na simu kuliamsha mashaka. Nilikuwa tu nimeingiwa na ile hisia ya kipelelezi, nikitaka kujua aliongea na nani na kuhusu nini; fikira za kwanza ikiwa masuala ya wanawake wengine.

Nikasikia vizuri hatua zake zikikaribia ukuta kwa upande wa pili, na maongezi yake yalikuwa kwa sauti ya chini lakini yenye msisitizo mkali.

"...unapiga, unapiga, unapiga, nimekwambia niko kwenye kikao... mbona huelewi?" akawa anasema hivyo.

Nikaweka umakini wangu zaidi.

"Sa... saawa... naelewa. Kwani we' hofu yako iko wapi? Hunijui?.... Muda, muda kitu gani... si ilikuwa juzi tu? A-ah... usilete masuala yako bwana... unanielewa? Nisikilize. Acha kulalamika, hau... hauna haki ya kulalamika nimekucheleweshea kwa sababu zoezi lenyewe hukulikamilisha.... lakini hata hivyo si bado nilikuahidi ningekulipa?... Ndiyo... wiki zimepita sawa.... ah... unazingua. Oya, me nitakutafuta, nimekwambia... nimekwambia niko kwenye kikao, mbona huelewi?... Mambo magumu kwangu pia... ndiyo bado.... bado niko kwenye harakati za kutafuta.... Ah... usilalamike Yohana... kwanza yote haya ni makosa yako!... Makosa yako ndiyo, kama ungekuwa umemgonga hiyo siku sasa hivi si tungekuwa tushapata hizo hela?"

Macho yangu yakakaza zaidi baada ya kusikia maneno hayo, moja kwa moja nikiwa nimeelewa maana yake.

"... ndo' utulie Yohana... hilo dili limeshafeli... Eee... we' tulia, niko nao huku nimeanza kubembeleza, taratibu nitapata njia ya kuzoa hela hapa, kwani we' hunijui? Ndo' usikilizie muziki sasa... nimerudi...."

Ah! Haki ya Mungu! Yaani alinifanya nihisi kuchoka.

"Tatizo unakuwa na presha mno... we' nipe tu wiki wala usijali, kwanza hilo gari si lilikwanguka tu, ina maana mwenye nalo ndo' anakusumbua akili namna hiyo? Aa wapi wewe... tulia. Nitakupa, halafu ndiyo tukamilishe hiyo ishu ya shamba... taratibu tu... aina hiyo. Usipige tena mpaka nikutafute, kichwa wewe! Hahahah... kafie huko Bunju!"

Nadhani hapo ndiyo akawa amemaliza maongezi yake hayo ya siri, isipokuwa tu hiyo siri na mimi nikawa nimeinakili.

Hatua zake za kuondoka hapo zikanifanya nisimame, nami nikamtazama kupitia matundu ya ukuta kumwona akirudi kule ndani; bila shaka kuendeleza unafiki wake. Ah Mungu mkubwa jamani! Yaani hata ufanye mabaya na kuyaficha jinsi gani, akiamua kuyafunua utapatikana tu!

Nikabaki hapo nikiwa natikisa kichwa kwa kuhuzunika. Huyu mwanaume hakuwa mtu kabisa. Yaani alikuwa hafai. Kusikiliza maneno hayo yote kulikuwa kumenifanya nitambue namna gani alivyokuwa mbinafsi, tena kupindukia. Mara ya kwanza nimekutana naye alinifanya nikamkasirikia, lakini wakati huu, nikawa nimemchukia.

Kumbe ni yeye ndiye aliyetengeneza ajali ile ya gari iliyokusudiwa kumwondoa binti Mariam, tena mdogo wake wa damu kabisa, ili tu afanikishe mipango yake ya kuchukua mali iliyoachwa kwa ajili ya huyo binti. Hilo zoezi liliposhindikana ndiyo akaunda kale kampango ka wizi kupitia hati bandia za kimahakama, na tena na hapo akafeli.

Kwa hiyo sasa alikuwa anatengeneza mbinu nyingine tena ili aje kuivuruga hii familia, tena ni familia yake kabisa! Alikuwa anautumia upendo wa Miryam kwa familia yao ili kuingia ndani, awadanganye-danganye halafu puuf... awamalize. Hakufaa kabisa!

Unajua kwa jinsi ambavyo mambo yalikuwa yamekwenda tokea ile siku nimemwokoa Mariam asigongwe kwa gari, nilikuwa nimeshaanza hadi kusahau kwamba kweli tukio lile lilikuwa la kupangwa, na sasa ndiyo Joshua akawa amethibitisha kuwa yeye ndiyo mfumaji wa hiyo mipango. Sijui kama na huyo mke wake alimuunga mkono kwa haya mambo lakini kiukweli ilikuwa imepita kiasi.

Nisingeweza kuwaacha waiharibu amani ya familia hiyo ambayo niliona wazi ilikuwa imeanza kuwa imara zaidi kutokea kwa binti Mariam aliyekuwa ameanza kuonyesha dalili za kupona, na kama ingehitajika nijiunge na Tesha ili kumwondoa huyo mtu aliyejiita kaka yao, ningefanya hivyo. Alikuwa mtu mchafu sana, nami ningehakikisha anakomeshwa kwa kutupwa kwenye kiroba cha uchafu alipostahili kuwa!



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA

★★★★★★★★★★★★★★★★★


Nikiwa nafikiria kurudi ndani kwanza kutokana na kiatu changu kukatika, Ankia ndiyo akawa amerejea. Alipendeza sana kichwani kwa kusuka nywele ngumu zenye mtindo wa mawimbi kama tambi, na zilikuwa nyekundu. Mkononi alishika mfuko mdogo ulioonyesha kitu kama karatasi, au bahasha nyeupe iliyotuna.

Alipofika karibu zaidi akasimama huku akitabasamu. "Vipi JC? Mbona umesimama hapa?" akaniuliza.

Nikiwa na uso makini, nikamwambia, "Nilikuwa nataka kutoka... ndala ikakatika. Inabidi nianze kuvaa zile mpya."

"Ee... pole."

"Umependeza."

"Asante. Zimenikaa vizuri?"

"Sana. Shi'ngapi hapo?"

"Elfu ishirini na tano."

"Ahaa... umependeza sana. Leo lazima nikutekenye," nikamtania.

"Ahahah... haya twende ndani. Nimeleta chips, saa nne sa'hivi, nisingeweza kuja kupika. Au? Ulikuwa unaenda wapi?" akaniuliza.

Alikuwa anaongea huku akitembea kuelekea kule ndani, lakini nikabakia hapo nikiwa nimeweka uso makini. Bado akili yangu ilikuwa imetekwa na suala la muda mfupi nyuma kuhusu Joshua.

"JC... vipi?" Ankia akarudi na kuuliza hivyo.

Nikamwangalia na kusema, "Poa. Namtafuta tu Tesha."

"Kumbe hamkuwa wote? Labda
atakuwa Masai... si kulikuwa na mechi leo?"

"Hapana. Masai hayupo."

"Kwao je?"

"Ndo' nilikuwa nataka niende ila... nimeahirisha," nikasema.

"Kwa nini? Kuna nini kwani?" akauliza.

"Twende ndani, nitakwambia," nikasema hivyo na kuanza kuelekea upande wa ndani pamoja naye.

Kweli nikawa nimemwelezea Ankia kilichotokea baada ya Joshua na mke wake kufika hapo nyumbani kwao Tesha, nami nikamjulisha kuwa bado watu hao walikuwa hapo ndiyo maana sikutaka kwenda nilipogundua hilo. Nilikuwa tu nataka kuhakikisha Tesha yuko poa maana mpango ulikuwa niondoke pamoja naye lakini akawa ameniacha tu, ikionekana ni hasira ndiyo zilimlemea.

Ankia akanituliza kwa kusema huyo kijana angekuwa poa tu maana alikuwa mjanja; labda alienda kwa mademu zake ama huko Mbagala kunywa pombe. Lakini na mwanamke huyu alishangaa sana suala la Miryam kumleta Joshua hapo baada ya kila kitu alichokuwa amewafanyia, ila akanishauri niachane na mambo ya hiyo familia maana hayakunihusu. Ila mimi sasa!

Tayari nilijua rangi za kweli za huyo Joshua, vitu vibaya sana ambavyo hata Ankia sikumwambia. Nisingeweza kuacha kujali hali ya Mariam huku nikijua kabisa kwamba kaka yake alikuwa na mpango wa kumuua, sijui na wakati huu alikuwa amepanga nini! Je kama alitaka kumuumiza Tesha? Mama wakubwa? Miryam?

Ningehitaji kuhakikisha naukomesha huo mchezo wake upesi ili asije kuleta shida kwa watu hao niliokuwa nimeanza kuwajali sana, yaani kwa maneno mengine, ningejitahidi kuilinda familia hiyo dhidi ya Joshua. Si alitaka watu wausikilizie muziki wake? Wakwangu angeucheza!

★★

Baada ya Ankia kuandaa vyakula mezani, tukala pamoja, chips kavu na mishikaki mitano-mitano. Ah hiki ni chakula pendwa na chepesi sana kupata kila kona ya eneo lolote, na angalau baada ya kushiba nikawa nimetulia zaidi kimwili. Nilikuwa nahisi uchovu-uchovu tu uliotokana na njaa, joto, bila kusahau mechi niliyocheza na Soraya pia, hivyo nikaamua kwenda kujimwagia ili kupunguza fukuto baada ya msosi kukaa mahali pake.

Mpaka inafika saa sita, sikuwa nimempata Tesha. Bi Zawadi alinipigia simu kuniuliza ikiwa nilikuwa na mwanaye huyo, lakini nikamwambia hapana. Walimpenda sana na walitaka kuhakikisha yuko salama, kwa hiyo nikawahakikishia angekuwa vizuri tu na angerudi, kwa hiyo wasijali.

Lakini mimi ndiyo nilikuwa najali zaidi, siyo kuhusu Tesha tu, ila wote hapo kwao. Nilikuwa nimemuuliza Bi Zawadi kama Joshua na mkewe waliendelea kuwepo hapo kwao, lakini akaniambia walikuwa wameondoka mida ya saa nne usiku huo, kumaanisha si muda mrefu sana uliokuwa umepita tokea nilipomsikia jamaa akiongea na jambazi mwenziye kwenye simu, ndiyo akawa ameondoka.

Nikaulizia tu na hali ya Mariam kwa muda huo, nami nikajulishwa kuwa binti alikuwa ameshapumzika usingizini. Sikutaka kuuliza mengi sana yasiyonihusu, kwa hiyo tuliachiana hapo tu.

Tesha sikuweza kumpata kabisa kwa simu. Bora hata mwanzoni ilikuwa ikiita mpaka kukata, lakini wakati huu haikupatikana kabisa. Dah! Sikuwa na namna ila kusubiri tu, nami nikakaa sebuleni mpaka saa nane kasoro usiku ndiyo hatimaye jambo jipya likaja.

Niliweza kusikia geti likigongwa huko nje, nami sikuwa na uhakika kama lilikuwa letu au la jirani, kwa hiyo nikatoka ili kwenda tu kuangalia ikiwa ilikuwa ni Tesha. Ankia alikuwa chumbani kwake lakini inaonekana alikuwa macho bado, kwani nilipoanza kufungua mlango wa kuingilia ndani hapa akawa ametoka chumbani na kuja kuniuliza naenda wapi. Nikamwambia naenda kuangalia ikiwa Tesha ndiyo amerudi, naye akasema poa.

Nikatoka mpaka nje, nikachungulia upande wa pili wa nyumba na kumwona bibie Miryam, ndani ya nightdress, akiwa hapo nje kwenye ubaraza wao. Alikuwa ndiyo ametoka ndani nafikiri, akitaka kwenda kufungua geti, nami nikadhani bila shaka ni kwake ndiyo paligongwa. Lakini geti lilipogongwa tena, nikatambua lilikuwa la kwetu.

Miryam akaonekana akienda kwenye geti lao na kufungua, kisha akaenda nje kabisa. Geti letu likaendelea kutoa kelele tu, nami nikaenda hapo na kukuta ni Tesha. Lakini hali niliyomkuta nayo haikuwa nzuri kabisa.

Alikuwa amechafuka kwenye suruali, huku akiwa anayumba kilevi na kofia yake kama kibandiko kichwani. Kuangalia jinsi alivyokuwa akiyumba lakini kwa kupindia upande mmoja kukanifanya nitambue kwamba alikuwa amepigwa.

Nikamwona Miryam akitokea pembeni yake na kumshika mkono, ikiwa wazi anataka ampeleke kwao, lakini Tesha akagoma.

"Hhh... sss... JC... kaka nifungulie..." Tesha akasema hivyo.

Hakuwa akitoa machozi, lakini alikuwa analia. Ile kulia ya kiume siyo kwa sababu umeumia mwilini, ila moyoni.

Miryam akaniangalia kifupi, kisha akamwambia mdogo wake, "Tesha... twende ndani. Ni usiku sasa hivi, na mimi hii tabia siipendi. Twende!"

"Niachie Mimi... nenda mwenyewe. Si unawajali hao mbuzi zaidi yetu... waambie wakae hapo... basi..." Tesha akasema hivyo.

Ikanibidi nirudi ndani upesi kwenda kuchukua funguo za hili geti letu, naye Ankia akawa ameniuliza kulikoni. Nikamwambia Tesha amerudi, lakini alikuwa vibaya, nasi sote tukatoka tena na kwenda nje. Tulikuta Miryam akiwa anamfokea mdogo wake lakini kwa sauti ya chini, nami nikafungua geti na kutoka.

"...maneno gani? Hebu jiangalie Tesha. Unafanya maisha yako yawe mabaya kisa hasira, unafikiri itakufikisha wapi?" Miryam akaendelea kumwambia hivyo.

"Mimi... niache... wewe fanya mambo yako... maana haujali hisia zangu..."

"Mimi sijali hisia zako Tesha? Unaniambia hivyo?" Miryam akamuuliza kwa hisia.

Nikamshika Tesha mkononi na kuuliza, "Tesha nini kimetokea?"

"Ah... sss... mwanangu..." akasema hivyo na kupiga ulimi mdomoni.

"Ulikuwa wapi? Umeanguka?" Ankia akamuuliza hivyo.

Tesha akawa anababaika, akionekana kuwa na maumivu.

"Umefanyaje? Nani amekupiga?" nikamuuliza hivyo kwa uthabiti.

"Amepigwa? Umepigwa Tesha?" Miryam akamuuliza hivyo na kusogea karibu zaidi.

"Ah... mwanangu nimekabwa... njiani..." Tesha akasema hivyo.

"Na vibaka? Sehemu gani?" nikamuuliza.

"Si huko Mbagala mwanangu... nilikuwa narudi... ah... mwanangu wamechukua simu yangu..." Tesha akaongea kwa kukaza hisia.

"Umetembea kutokea Mbagala?" Ankia akamuuliza hivyo.

"Jamani! Tesha umeona sasa mambo ya usiku? Nikwambie mara ngapi unisikilize?" Miryam akasema hivyo kwa huzuni.

"Ni kweli Tesha, usiku siyo mzuri... jamani, tuingieni ndani..." Ankia akasema hivyo.

"Twende Tesha ukalale..." Miryam akamwambia hivyo na kuuvuta mkono wake, lakini Tesha akaweka mgomo.

"Tesha... msikilize dada'ako..." Ankia akasema.

"Mbona yeye hanisikilizi? Anawaleta... ah... Ankia, sister anazingua... ona mpaka nimejikuta kwenye hii hali..." Tesha akasema hivyo.

"Yaani unanilaumu mimi kwa sababu ya upuuzi wako? Me nilikutuma uende huko? Ukoje wewe?" Miryam akasema hivyo na kusukuma kichwa cha mdogo wake kwa kidole.

"Miryam..." nikamwita hivyo kwa sauti ya chini.

"Nini?" akaniitikia hivyo.

"Nitaenda kulala naye. Yuko vibaya kama unavyoona... mwache tu, mtaongea asubuhi. Sawa?" nikamwambia hivyo kwa upole.

Miryam akamtazama mdogo wake, nikiona machozi yakiwa yamemlenga.

"Oya... twende ndani..." nikamwambia hivyo Tesha na kuanza kumvuta.

"Dah... JC, simu yangu..." akasema hivyo kwa huzuni.

"Twende kwanza upumzike... tutatafuta nyingine..." nikamwambia hivyo.

Nikamkokota vizuri mpaka ndani, Ankia na Miryam wakiwa wanatufata kwa ukaribu, nasi tukafika chumbani kwangu. Tesha akajitupia kitandani na kulala kifudifudi, huku uso wake akiugeuzia ukutani, na mwili wake ungeshtua kila mara kwa ile njia ya kulia kwa pumzi.

Nikawa namtia moyo tu ajikaze, na nikiangalia kama kuna sehemu aliyokuwa ameumia vibaya, huku wanawake wakiwa wanatutazama tu pale mlangoni, nami nikamwomba Ankia aifate feni sebuleni na kuileta huku, kisha aiwashe mpaka mwisho.

Akatii na kuileta, akiiwasha na kuielekeza upande aliolala Tesha, nami nikatoka kitandani na kusimama kumtazama dada mtu. Alikuwa anamwangalia mdogo wake hapo kitandani kwa macho yaliyojaa huzuni, na nilitambua kuna kiasi cha machozi kilichokuwa kimemtoka lakini akawa ameyafuta macho yake.

"Tumwache alale sasa, pombe ikimtoka mambo yataeleweka zaidi, eti Miryam?" Ankia akamwambia hivyo.

"Muda mwingine natamani hata nimkate masikio," Miryam akasema hivyo kwa sauti ya chini.

Ankia akatabasamu na kuniangalia.

Nilikuwa namwangalia Miryam kwa uelewa mwingi sana, naye aliponitazama machoni, nikasema, "Najua unawaza sana kuhusu hali yake, ila usijali. Hajaumia sana. Hao vibaka wamemkwarua kidogo tu."

"Na simu yake wamebeba," Ankia akasema.

"Kama angekaa kwa kutulia, haya yote yasingetokea... ah..." Miryam akasema hivyo kwa huzuni.

Ankia na mimi tukatazamana tu machoni, kisha tukamwangalia tena dada mkubwa.

"Sitaki akuletee shida Ankia jamani, ikiwa..."

"Hapana, hapana, Tesha siyo shida Miryam. Ni rafiki yetu, kwa hiyo lazima tumsaidie. Mbona we' umenisaidia kwa mengi magumu Miryam... sasa hiki tu ndo' kinipe shida? Hebu acha kuwaza hivyo bwana. Nenda kapumzike... asubuhi mambo yatakuwa sawa," Ankia akasema hivyo kwa upole.

Nikawa namwangalia tu Miryam, naye akashusha pumzi na kutoa shukrani, kisha akaanza kuondoka. Nikahakikisha namtoa mpaka nje na kumwacha kwenye mazingira salama mpaka alipoingia getini kwao, tukiwa hatujaongea chochote kabisa, nami nikarudi upande wetu.

Ankia akaanza kuniambia ni namna gani maisha ya hapo yalivyokuwa yakitengeneza drama moja baada ya nyingine, na hili suala la Tesha kupenda mno pombe mpaka anajikuta kwenye matatizo lingemfikisha pabaya mno ikiwa asingeangalia.

Akaniaga na kwenda kulala chumbani kwake, nami nikabaki chumbani pamoja na rafiki yangu mpya. Tayari usingizi ulikuwa umeshambeba zamani sana, si unajua alikuwa amegusa pombe? Kwa hiyo nikakaa hapo kwanza kutafakari vitu kidogo.

Alichosema Ankia kilikuwa sahihi. Tesha alikuwa kijana mzuri sana, lakini naona kuna kitu fulani kilichokuwa kikimsukuma apende mno pombe na kumfanya awe tofauti na alivyotakiwa kuwa. Kiuhakika, sisi wote tulikunywa, lakini hata sisi wengine tungeweza kuona kwamba alikuwa akipita kiasi.

Labda shauri ya msongo wa mawazo uliosababishwa na kitu fulani nisichofahamu ndiyo jambo lililofanya awe hivi, na kwa sababu nilikuwa namjali, nilitaka kuhakikisha namsaidia kwa ushauri, ikiwa ingewezekana, ili ajiepushe na mambo ambayo huenda yangekuja kumwingiza kwenye matatizo mabaya zaidi kuliko hata ya leo.

Sikutaka vitu vibaya zaidi vije kumpata huyu kijana, kwa hiyo darasa huru lingeitishwa siku ikishakucha ili kweli nisaidie kumweka huru.


★★★


Siku ikakucha. Niliamka cha kwanza ikiwa ni saa moja kasoro, nao usingizi bado ukawa unanivuta niendelee kulala. Kwa kuwa nililala na Tesha kwa kupishana miili, nilimchungulia tu na kuona kwamba bado alikuwa amesinzia, hivyo nami nikaingia usingizini tena.

Ndoto moja, mbili tena, nami nikaamka kwa mara nyingine. Zamu hii nilipoangalia muda nikakuta inakimbilia saa tatu asubuhi, nami nikamwangalia mwenzangu na kuona bado amelala kitandani, lakini macho yake yalikuwa wazi.

Tesha alitazama kuelekea juu, ikiwa kama vile anatafakari mambo fulani, nami nikampiga kidogo mguuni kwa mkono wangu.

"Oy, oy..." akasema hivyo kwa sauti ya chini.

"Uko macho muda?" nikasema hivyo na kupiga mihayo.

"Hamna... nimekata dakika 10 tu. Ankia kaja, akanicheki, ameenda sokoni kufata nyama. Wewe unalala kama umekufa mwanangu, hata hukumsikia," akaniambia hivyo.

"Ah wapi! Hahah... nimeamka kabla yako, nikakucheki, nikaona bado uko Dreamland, kwa hiyo na mi' nikarudi kulala pia..." nikasema hivyo.

"Dah, nimekunywa jana! Nashangaa sijapotea njia ya kurudi," akasema hivyo.

"Mlevi hata alewe vipi, hawezi kusahau kwake," nikamwambia.

"Ahahah... uhakika. Na mimi navyolalaga vibaya hivyo, sijakupiga mateke kweli?"

"Hamna... ila sema unajamba sana..." nikamtania.

"Aa, acha hizo mwanangu..."

Sote tukacheka kidogo.

"Unajisikiaje?" nikamuuliza.

"Dah! Kichwa kinagonga. Mbavu zinauma, hao wajinga jana walinipiga kabaroho la hatari," akaniambia.

"Kwani ulikuwa unatokea wapi kabisa? Jana nilikupigia kweli afu' baadaye ndiyo ukawa hupatikani kabisa..."

"Dah! Mwana me nilikuwa nimekasirika sana... ile ishu, si unaelewa?"

"Yeah."

"Nikaona niende zangu Tandika. Kule kuna demu wangu... anaitwa Happy... ananielewa sana. Nikaenda kwake, nikakaa pale wee... badae', jioni pale mechi imeisha, nikamwacha. Ah, afu' linapenda kunyonywa chenza!" akaniambia hivyo.

"Ahahahah... usinambie'!"

"Ah, siyo poa. Nimelila, likanigei na hela ya bia maana... linafanya kazi kwenye hoteli, kuna shift ya usiku kwo' lenyewe likaenda huko, nami ndo' nikaanza kurudi Mbagala..."

"Mm-hmm..."

"Basi mwanangu, nikaenda zangu pale Highway. Piga bia zangu kama nne hivi, wenye kushoboka wakaja, wakaongeza, nikaendelea kupiga tu. Nimekunywa jana! Halafu zilikuwa kama haziishi..."

"Haukufahamiana na hata mmoja?"

"Hamna, chawa tu zisizojulikana. Walikuwa wanafikiri me mtu mwenye hela ndo' maana..."

"Ikawaje?"

"Nimekunywa, nimekunywa, kuna demu akawa anataka niende naye Lodge ya hapo, ila me sikuwa na hela. Afu' lilikuwa la moto!"

"Wewe!"

"Acha mwanangu, bonge la pisi! Ningekuwa na 15 nisingerudi huku kabisa, ningelala nalo..."

Nilikuwa nasikiliza kwa umakini namna ambavyo kijana huyu aliongea, nikijaribu kuisoma saikolojia yake. Niliweza kutambua mambo fulani kuhusu utu wake kutokana na jinsi alivyozunguka kwenye maneno aliyotumia ili kufika kwenye pointi ya kile nilichotaka kujua. Alipenda ukweli wa mambo yote aliyofanya uelezeke mwanzo mwisho kwa msikilizaji, ili kumwaminisha zaidi.

"Nikatoka hapo, saa sita mwanangu, nikasema ah... si unajua na pombe? Nitembee tu... yaani napaona skani kama hapo tu. Nilikuwa hata siyumbi kivile mwanangu... mdogo mdogo tu mpaka lile eneo pale karibiaa... nanilii... kale ka-guest... Lasanga..."

"Ee..."

"Eee pale mbele mbele ukikaribia sasa kwenye lile dampo la machupa ya kuuzwa. Pale si ndiyo pamekaa vizuri kukojoa, nikasogea nishushe mvua. Ah!"

"Ndo' wakakuvamia hapo?"

"Yaani sijui hata walitokea wapi kaka!"

"Walikuwa wengi?"

"Kama watatu hivi. Wawili walinishika, mmoja akiwa amenikaba, afu' nikasikia nimepigwa kiunoni... hapa kwenye mbavu, ah! Isingekuwa ya pombe ningeruka nao! Wakachukua simu na wallet mwanangu, ila haikuwa na kitu hiyo..."

"Hakukuwa hata na kadi za maana? Vitambulisho?"

"Hamna. Uzuri sikuwa nimevibeba jana. Si ile nimeondoka kwa hasira, nilikuwa na buku tatu tu... ahahaha... mpaka kwa Happy huko Tandika, ndo' na yeye akanitoa kidogo baadaye. Ndiyo hivyo bro... wamenitia hasara hao wakuda..." akasema hivyo kwa kuudhika.

"Inabidi uje kwenda polisi... masuala ya laini, si unajua?"

"Ah! Nimeshachoka akili. Yaani kama nikija kukutana nao tena! Nitafanya kitu mbaya sana," akaniambia hivyo.

Nikajinyanyua na kukaa, yeye bado akiwa amelala chali huku mguu mmoja akiukanyagisha kitandani na mkono wake akiuweka kwenye paji la uso.

"Hiyo ni kama utakutana nao tena, na ni kitu kigumu sana. Hao ni watu wa kubadilisha maeneo, na wewe haukuwa target ya moja kwa moja. Walikuotea tu," nikamwambia hivyo.

"Ah... ndo' hivyo kaka. Mtihani wa kutafuta simu nyingine ni wangu... na ni mgumu kinoma," akasema hivyo.

"Unajua Tesha... nakuelewa. Vizuri sana. Wewe unavyoona mambo, ni tofauti na jinsi ambavyo dada yako au mama zako wakubwa wanayaona, kwa hiyo migongano lazima itokee msipokubaliana kwa jambo fulani, lakini...."

"Mimi ndo' nacholilia JC! Hivi kweli mwanangu, si na wewe ulikuwepo ile siku huyo mbwa ameitukana familia yetu? Tena we' hapo ilikuwa ni mara ya kwanza... me mwanangu namjua huyo mtu toka tupo wadogo, yaani hafai! Ni mchoyo, mkuda, mpumbavu, yaani ah! Halafu analeta ***** zake hapo afu' eti nimpokee 'njoo, karibu sana'? Yaani siwezi JC. Sijui Mimi anafikiria nini... ah..." akaongea kwa hisia sana.

"Hujaingia kwenye akili ya dada yako Tesha, na najua hamwezi kufanana kwa kila kitu. Unajua... we' ni mdogo wangu, sawa? Nakuelewa. Ninaelewa hasira uliyonayo haiko kwa familia yako, ila una hasira juu ya kitu kingine ambacho... ndiyo kinakufanya upende zaidi kujistarehesha... wanawake... pombe sana... ili ujipe njia ya kupotezea hizo hisia. Lakini Tesha... ushawahi kusikia kwamba huwezi kuepuka matatizo yote kwa kuyakimbia?" nikamwaongelesha hivyo kwa upole.

Akawa ananiangalia kwa macho yenye subira.

"Mimi ni rafiki yako, na nimeshakusoma. Nimeelewa kwamba kuna kitu kinachokuumiza, lakini hautaki kuki-face... unakiepuka... kwa kuishi ile... kujiachia. Inaeleweka mwanangu, sawa? Hata mimi nimeshapita kwenye nyakati za namna hiyo... kwa hiyo nakuelewa. Lakini nitakwambia kitu. Ikiwa utaendelea kuiepuka hiyo hisia na kujifikirisha kwamba uko sawa, kwamba hauna tatizo... ndiyo itaendelea kukua zaidi. Inakuwa kama unapokuwa na kinyongo na mtu... lakini unaigiza kwamba ah mko fresh. Hiyo kitu inakuwa inakutafuna ndani kwa ndani, ndiyo maana unakuwa unafanya vitu kwa njia isiyo yako kabisa, hasa... hasa kama utakasirishwa na jambo hata dogo linalohusiana na hiyo hisia uliyoificha. Unanielewa rafiki yangu?"

Tesha alionekana kuzama ndani ya hisia fulani nzito sana baada ya kunisikia nikimwambia hivyo, naye akatikisa kichwa kuonyesha uelewa.

"Sisi siyo wakamilifu mwanangu. Hakuna mtu msafi yaani. Lakini tunapoona mwenzetu anajichafua haimaanishi tumwache tu. Tunakuwa tunasaidiana hivyo hivyo, uongo?" nikamwambia hivyo.

"Ni kweli," akajibu.

"Ee. Ila sasa... kuna watu kama Joshua. Sikupingi Tesha. Huyo kaka yako... hafai. Yaani ana ule uchafu sugu kwenye utu wake hata kuusugua kwa Jik wala msasa hautoki. Sawa?"

"Kwa hilo hupingwi JC..." Tesha akasema hivyo.

"Yeah. Ndivyo hali ilivyo, haipingiki. Lakini tukija kwa dada yako... Miryam ni mtu tofauti Tesha. Anajaribu kuona kitu fulani ndani ya mtu hata kama hakipo, na hiyo inamfanya awe mtu mwelewa sana... mpole... anayetaka amani hata kama nafasi ipo kidogo sana ya kuipata. Hayo siyo makosa yake, ndivyo alivyofundwa. Na dada yenu... anawapenda sana. Nadhani anataka kufanya kila kitu kuwaunganisha, maana anajua hatakuwa nanyi siku zote..." nikaeleza hivyo.

Tesha akaendelea kunisikiliza tu kwa utulivu.

"Ma' mkubwa wako alinielewesha kuhusu huo utu wa dada yako, kwa hiyo nimemwelewa namna hiyo. Anataka kutafuta amani hata na mtu kama Joshua kwa sababu ni ndugu yenu, sawa, huyo ni Miryam. Ila wewe ni Tesha. Ukishamwelewa kwamba 'dada yuko hivi,' we' kubaliana naye, kwa njia yake ya kuona mambo, lakini unakuwa unahakikisha kwamba uko macho kwa njia yako mwenyewe ya kuona mambo ili ukiona kwamba anakaribia kuanguka... unawahi kumdaka. Maana hata yeye anaweza akawa anakosea, si ndiyo?" nikamwambia hivyo.

"Ni kweli," akajibu.

"Ee, hawezi kuona vitu kama Bi Zawadi na Bi Jamila, ama Shadya na mashoga zake. Alivyo ndivyo alivyo tayari, we' mwelewe tu, halafu utulize hisia zake hata kama bado zako zinaruka-ruka. Si unaelewa mwanangu?"

Akatikisa kichwa kukubali.

"Ee. Haumwamini kaka yako, sawa, simama na hilo. Nenda na biti la dada yako la kutafuta amani lakini jicho lako makini lisitoke kwa huyo mtu unayejua anaweza kubadilika muda wowote. Si unanipata?" nikamwambia.

"Ee mwanangu, unasema kweli. Ah... mi' nakuwa sitaki hata awe karibu yetu maana..."

"Hata akiwa mbali Tesha, uwezekano wa kufanya mambo mabaya kwenu anao. Hicho ni kitu ambacho unatakiwa uwe nacho akilini. Kwa hiyo la muhimu kuangalia ni wale unaowapenda... basi. Wewe Tesha ndiyo mwanaume hapo... hebu, i-face hiyo hisia uliyoificha... ipe za uso... kitoe hicho kitu kinachoisumbua roho yako ili uache kujikimbia we' mwenyewe... ndiyo utaona umuhimu wa haya yote niliyokwambia ili uwe namna unavyotakiwa kuwa. Simaanishi utakuwa mtakatifu, ila najua utaanza kujitahidi kutotanguliza fikira zako tu na kuangalia faida za wapendwa wako zaidi. Hilo ndo' la muhimu. Au siyo?" nikamwambia hivyo kwa busara.

"Dah! Ahahah... kaka unaongea wewe! Fungua chaneli ya documentary..."

Akasema hivyo, nasi tukacheka kidogo.

"Me nimekuelewa JC. Uko sahihi. Unajua kuna kitu..."

Kabla hajamaliza kuongea, sote tukasikia mlango wa kuingilia ndani ya sebule ukigongwa, kuashiria mgeni kafika. Ah ingekuwa Ankia ndiyo karudi si angepita moja kwa moja? Huyo hakuwa yeye.

Nikaona nitoke tu kitandani na kuchukua T-shirt la kuvaa ili nikaone ni nani, maana nilikuwa kifua wazi na nimevaa pensi tu.

"Ankia kachelewa kweli kuleta supu," Tesha akasema hivyo.

"Labda ndo' katuma mtu ailete. Ngoja nikaone ni nani," nikamwambia huku nikivaa.

"Halafu mwana una kabode simple tu, ila kifua chako kiko mbele! Unaingiaga gym?" akaniuliza.

"Kitambo, niliacha. Ila nataka nije nianze tena kujenga kinga," nikamwambia hivyo.

"Na mimi nataka nianze pia, maana nilishakuwa legelege mpaka nakabwa kijinga," akasema hivyo.

Nikatabasamu kiasi, nami nikatoka chumbani na kwenda kufungua mlango.

Macho yangu yalikuwa na uzito kiasi, lakini baada ya kumwona bibie Miryam hapo nje ikawa kama yamepata wepesi. Alikuwa amevaa nguo kama dera, ya kijani, iliyokuwa imefungwa kwa mkanda laini sehemu ya kiuno. Kichwani alizibana nywele zake ndefu alizosuka kwa juu, na uso wake usiokuwa na virembesho vya aina yoyote ulipendeza sana kwa asubuhi hii.

"Za asubuhi?" akanisalimu kwa sauti yake nzuri.

"Salama. Vipi wewe?" nikamjibu.

"Safi tu. Huyo ameamka?"

"Ee yuko macho, ila... bado yuko kitandani... ingia..."

"Hapana, mwite tu. Nataka aje nyumbani."

"Bado ni mzito, Ankia ameenda kumfatia supu pia. We'... ingia tu umwone angalau. Tafadhali," nikamwomba hivyo.

Akaniangalia kwa macho yenye utathmini, kisha akavua ndala zake na kuingia ndani. Ngozi yake nyeupe iliyoonekana nyuma ya shingo yake ilipita hadi weupe wangu yaani, ikionekana kuwa nyororo sana.

Nikaacha kumtazama baada ya yeye kufika mbele zaidi na kunigeukia, nami nikaufunga mlango na kuelekea chumbani kwangu huku nikimwambia aje. Nikakuta Tesha akiwa amejilaza bado, nami nikamwambia dada yake amekuja.

Akajinyanyua na kuketi kitandani, huku dada yake akiwa anaingia chumbani sasa, nami nikaichukua simu yangu.

"Ngoja niwapishe kidogo... njoo ukae," nikamwambia hivyo Miryam.

"Hapana..."

Tesha akasema hivyo, nasi tukamwangalia.

"Usiondoke JC. Kuna vitu nataka niongee na we' usikie," akasema hivyo tena.

Nikamwangalia Miryam na kuona jinsi alivyomtazama mdogo wake kwa hisia, naye Tesha akasimama usawa wangu.

"Mimi... dada yangu... naomba unisamehe," Tesha akaanza kwa kusema hivyo.

Miryam akaingia ndani zaidi na kumfikia mdogo wake, akamshika mkono huku akimwangalia kwa hisia, naye akasema, "Usijali Tesha. Yameshapita. Wewe... twende nyumbani kwanza uka..."

"Hapana, Mimi, nataka unisikilize kwanza," Tesha akasema hivyo.

Miryam akabaki kimya.

Tesha akaanza kujipiga kifuani kwa kidole chake na kusema, "Kuna vitu vingi sana hapa dada. Nimejikaza muda mrefu mno. Unajua nikwambie kitu? Yaani kama ingekuwa... ingekuwa ni kuzaliwa kwenye maisha mengine... ningechagua kuwa na kaka wa damu kama JC... siyo Joshua."

Miryam akanitazama usoni, nami nikamtazama tu Tesha.

"Isingekuwa ya huyu kaka, leo nisingetambua kwa nini nimekuwa hivi. Mimi, hata wewe unajua sikuwa hivi... na japo... japo umeniacha tu niishi kama navyoishi sasa hivi lakini najua huwa nakuumiza sana. Najifumbisha tu macho... lakini ni kitu nachohisi... na roho inaniuma sana kwa sababu sipendi uumie..." Tesha akaongea kwa hisia.

Miryam akaanza kulengwa na machozi.

"Lakini... iko hivyo kwa sababu... yaani... nimekuwa hivi kwa sababu... kwa sababu uliniumiza Miryam..." Tesha akasema hivyo.

Miryam akamwangalia kwa njia iliyoonyesha hakuelewa, nami nikawa makini zaidi ili kuweza kuelewa sasa funguko la huyu kijana.

"Dada una moyo. Una moyo mzuri, sawa? Lakini Joshua siyo! Siyo mtu. JC... wazazi wetu wamekufa, sawa? Kwenye ajali. Walituachia kila kitu chao... wakatugawanyishia... lakini Joshua akawa anataka hadi na vya kwetu..."

"Tesha..." Miryam akasema hivyo kama kumzuia.

"Subiri kwanza Mimi, ngoja niongee. Mwanangu... Joshua alipewa vingi kuliko hata sisi, maana mama alikuwa anampendelea sana yaani. Lakini akavitumia vibaya, halafu ndiyo akageukia kwenye vyetu. Nilikuwa nimeachiwa shamba, nalimisha na Mimi, tunapata hela zinatumika kwenye maendeleo yangu, Mariam, na ndugu zetu wengine, lakini Joshua akaliiba... akaliuza serikalini!" Tesha akasema hivyo kwa sauti ya chini.

Hiki ni kitu ambacho nilifahamu, lakini nilidhani kwamba yeye Tesha hakujua. Nilipomtazama Miryam, alikuwa anamwangalia mdogo wake kwa njia iliyoonyesha hata yeye hakutarajia hilo.

"Da' Mimi alijua, lakini hakuniambia. Alikuwa anajaribu kulinda amani, kama ambavyo sikuzote anafanya, lakini nilipojua... niliumia sana kaka! Nilihisi kama vile na yeye anampendelea, ana... anakuwa kama mama..."

"Tesha..." Miryam akamwita hivyo huku machozi yakianza kumtoka.

"No, Mimi usilie, sikulaumu. Nakuelewa, sawa?" Tesha akasema hivyo na kumfuta dada yake machozi.

"Tesha..." Miryam akaita tena.

"Usijali. Nilikuelewa, ndiyo maana nikakaa kimya. Sasa... ah... JC ndiyo kanifungua macho leo. Hiyo kitu iliniumiza mno japo nilikuelewa... ndiyo maana nikawa namna hii. Kama ulivyoniambia mwanangu... nikawa naikimbia hiyo hisia. Ila me ni mtu mwenye hasira sana kaka, na nilikuwa sitaki ziende kwa Mimi. Nampenda mno..." Tesha akasema hivyo huku machozi yakionekana machoni mwake.

Nikaingiwa na simanzi baada ya kuwa nimemwelewa vizuri sasa. Unaona? Kadarasa huru nilikompa kakawa kameleta hiyo faida.

"Kwa hiyo dah! Me... Miryam siwezi kumchukia. Lakini ninakiri leo kwamba... kulikuwa na kitu hapa... kinanisukuma nimkasirikie... ndiyo maana nikaanza kunywa sana pombe, unajua inaweza ikawa ngumu kuelewa lakini... hii kitu ipo. Mimi... wewe ni mtu mmoja nayempenda sana. Nikikwambia naweza kuua mtu kwa ajili yako, namaanisha hata Joshua! Nikimwona anakuja hapo nyumbani... nakumbuka! Nakumbuka kila kitu... ndiyo maana nafanya mambo vibaya. Eh! Nisamehe dada'ngu. Kwa jana... ah, nisamehe tu..." Tesha akasema hivyo huku amemshika Miryam mabegani.

Dada mtu akawa anamwangalia tu mdogo wake kwa huzuni.

"Ila unajua nini? Sasa hivi... nimeshaliondoa hili kaa la moto rohoni. Sitaki tena. Sitaki... hasira niliyonayo iniongoze vibaya. Nakuahidi dada, nitabadilika. Labda... ila bia nitakuwa nakunywa kidogo tu, siyo mbaya..."

Kauli hiyo ikamfanya Miryam acheke kidogo kwa pumzi ingawa alikuwa na huzuni, nami nikatabasamu pia.

"Tuyaachie haya mambo hapa. Mimi... nakuahidi. Sitakuvunja moyo. Sawa? Amani unayoitaka utaipata... tena inaanzia kwangu, yaani usikonde," Tesha akasema hivyo kwa njia ya kuchangamsha.

Miryam akaangalia chini kiasi kwa huzuni.

"Oya... ndiyo hivyo. Asante sana kwa hiyo therapy... si umeona nimefunguka daktari-mchizi wangu?" Tesha akasema hivyo.

Nikatabasamu na kusema, "Nimekuelewa. Umefanya vizuri. Kumbuka tu hili. Haijalishi uliyoyafanya, sawa? Ila yale ambayo unataka kuyafanya ndiyo ya muhimu."

"Amen," Tesha akasema hivyo kiutani.

Nikafarijika kuona namna ambavyo kijana huyu alikuwa ameweza kuufungua moyo wake na kuonyesha utambuzi, nami nikamtazama dada yake na kukuta anamwangalia mdogo wake kwa hisia.

"Ngoja nikakojoe Mimi... nakuja..." Tesha akasema hivyo.

Miryam akatikisa kichwa kukubali, naye Tesha akampita na kutoka ndani hapo.

Ni baada tu ya mdogo wake kutoka ndiyo Miryam akakisogelea kitanda na kukaa, nami nikamtazama na kuona jinsi uso wake ulivyokunjamana kwa njia ya kulia. Oh alikuwa analia, sana!

Lakini ni machozi tu ndiyo yaliyoonekana kutiririka na kwikwi zake kushtua mwili, ila huyu mwanamke hakutoa sauti. Kilikuwa kile kilio cha ndani sana kutoka kwenye moyo wake, nami kumwona akilia namna hiyo kiukweli kulinipa hisia mbaya sana. Alitia huruma.

Nikasogea mpaka hapo na kukaa pembeni yake, nami nikasema, "Miryam... jikaze tu. Mdogo wako atakuwa sawa."

"Ahh... nakosea wapi? Hhh... kwa nini najitahidi kujenga ila tu ndiyo mambo yanabomoka?" akaongea hivyo kwa sauti ya kunong'oneza, na kwa hisia sana.

"Siyo..."

"Mimi ni mpumbavu, eti?" akaniuliza hivyo na kunitazama.

Nikabaki kumwangalia kwa huruma.

"Mimi nina moyo wa kipumbavu sana. Najaribu... nafikiri kufanya hivi ndiyo inafaa, lakini kumbe ndiyo naharibu. Naangukia pua... mwisho wa siku ni mimi tu ndiyo naangukia pua. Hadi mdogo wangu nimeshindwa kumwongoza vizuri? Mpaka ana... hivi kweli jamani... ni nini kama siyo upumbavu? Ndiyo maana hata na wewe uliweza kunifanya nionekane mjinga mara ya kwanza tumekutana, siyo? Ni kwa sababu ya upumbavu wangu..." Miryam akasema hivyo kwa huzuni.

"Hapana... siyo hivyo Miryam..." nikajaribu kumtuliza.

Akaendelea kulia bila kutoa sauti sana, nami hadi nikalengwa na machozi kabisa!

Nikapitisha mkono wangu kwenye bega lake kwa njia ya kumvuta kiasi, naye akalaza kichwa chake begani kwangu. Nilipatwa na hisia ya uvuguvugu moyoni, kwa sababu hali ya huyu mwanamke ilinigusa sana, naye akawa anaendelea kulia kwa kwikwi huku mimi nikimbembeleza kwa kusugua mkono wake taratibu.

Mapigo yangu ya moyo yalikimbia kwa kasi sana na sikujua shida ni nini. Kuna kitu fulani kilichokuwa kikijijenga ndani yangu ambacho bado sikuwa nimeelewa ni nini, ila kiliweka msingi wa hisia tofauti ndani yangu ambayo ilikwenda kinyume kabisa na hali ya utu niliokuwa nimejipatia kwa kipindi hiki. Sikujua kwa sasa, lakini huenda ingekuja kueleweka baadaye.



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI

★★★★★★★★★★★★★★★★★


Nikiwa naendelea kumpa Miryam bembelezo kwa kusugua mkono na bega lake taratibu, mlango wa kuingilia hapo chumbani ukafunguka, nami nikatazama hapo na kumwona Ankia akiwa amesimama. Bila shaka ndiyo alikuwa amerudi, na inaonekana alikuja moja kwa moja mpaka humu chumbani kutuangalia mimi na Tesha, lakini akakuta niko na dada mtu.

Miryam akawa amemwona pia, naye akajitoa begani kwangu na kuanza kujifuta machozi kwa viganja vyake. Ankia alikuwa amesimama hapo mlangoni akitutazama kama vile anasubiri maelezo.

"Ndiyo umerudi?" nikamuuliza hivyo.

"Ee... ndiyo nimefika. Kila kitu kiko sawa jamani?" Ankia akauliza hivyo kwa kujali.

Miryam akasimama baada ya kujikausha machozi, nami nikasimama pia. Akasema, "Ndiyo, nimemwijia Tesha."

"Yuko wapi?" Ankia akamuuliza.

"Ameingia uani. Ngoja niende nikamsubiri hapo nje," Miryam akasema hivyo.

Nilikuwa namtazama tu kwa utulivu, naye akaanza kuelekea mlangoni lakini Ankia akamshika mkono kumzuia. Sote tukamtazama.

"Nime... nimeleta supu. Kaa basi tunywe pamoja na mdogo wako, eti?" Ankia akamwambia hivyo.

Miryam akasema, "Sitaweza Ankia. Naingia kazini, nataka nikajiandae. Ila Tesha anaweza kubaki, na...."

"Ankia umerudi?" Tesha akawa amefika na kusema hivyo.

"Eee. Namwambia dada yako tunywe supu, nimeleta nyingi, ila anataka kuwahi kazini..." Ankia akasema.

"Aaa, Mimi... kunywa tu hata bakuli moja. Sikumbuki mara ya mwisho tumekunywa supu pamoja..." Tesha akamwambia hivyo dada yake.

Ankia akatabasamu na kusema, "Ee bwana, hata bakuli moja tu. Ngoja nikaweke, sawa?"

Miryam akaonekana kutaka kumridhisha mdogo wake, hivyo akatikisa kichwa kukubali.

"Haya twendeni jamani. JC... njoo," Ankia akaniita.

Nikatikisa kichwa kukubali, nami nikafata nyuma yao wote mpaka hapo sebuleni.

Hakukuwa na ile hali changamfu sana iliyozoeleka kutokana na uwepo wa Tesha, kwa sababu wakati huu alikuwa chini ya mvurugo wa kihisia. Angalau Ankia angeongea kwa njia nyepesi ili kurudisha hali iliyosawazika zaidi kwa sehemu hiyo. Kulikuwa na hotpot mezani na mfuko wenye kitu kwa ndani, naye Ankia akawa ameleta sahani ya udongo na mabakuli manne pamoja na vijiko.

Kwenye ule mfuko akatoa chapati sita za kusukumwa na kuziweka kwenye sahani, akisema ndizo zilizofanya akakawia kiasi kwa sababu ya kuhitaji kusubiri. Akaweka na supu kwenye mabakuli, nyama zikiwa zile zifananazo na maini (wanaita mapupu), naye akatusogezea kila mtu sehemu yake na kumsisitizia Miryam anywe na kula chapati.

Nilikuwa namwangalia mwanamke huyo na kuona namna alivyojitahidi kusitiri hisia zake. Kuna kitu kilichokuwa kinaisumbua nafsi yangu kutokana na kushindwa kumwambia maneno yenye kufariji alipokuwa anajilaumu kwa sababu ya matatizo yaliyokuwa yanatokea kwenye familia yake.

Hii ndiyo iliyokuwa mara ya pili kwangu kuweka ukaribu wa namna hiyo kwa huyu mwanamke, yaani vile nilivyombembeleza kidogo akiwa amenilalia begani, nikiwa nakumbukia mara ya kwanza aliponikumbatia kwa kutoa shukrani ya moyoni nilipomsaidia mdogo wake. Nilihisi kama ningeweza kujiweka karibu naye zaidi ili tushirikishane katika mambo yenye kujenga zaidi, lakini tatizo alikuwa wa kivyake mno.

Tukawa tunakunywa thupu, taratibu tu, naye Tesha akawa anasimulia kwa wanawake jinsi alivyojikuta anakabwa na vibaka na kuibiwa simu; bila kuongelea masuala ya wanawake aliokutana nao bar lakini. Akatania kwa kusema alitaka kurudi huko leo na kisu ili akawatafute hao vibaka, nasi tukamwambia awe mwangalifu kisije kikageuziwa kwake.

Kwa hiyo maongezi hapo yalikuwa mepesi tu mpaka tulipomaliza supu, Miryam na mimi tu ndiyo tukiwa tumekula chapati moja moja, kisha yeye na mdogo wake wakatuaga na kuelekea kwao. Tesha alikuwa anataka kwenda kuuweka mwili wake sawa zaidi ili baadaye nimsindikize kwenda kituo cha polisi kuangalia suala lake la simu, nami nilikuwa nimemwambia haina tatizo.

Bila shaka, wawili hao wangeenda kujaribu kuweka hali vizuri zaidi pale kwao, lakini bado nilikuwa na hofu kuelekea suala la huyo Joshua. Sikutaka kuwachanganyia habari kwa kuwaambia mambo niliyosikia huyo mjinga akisema, maana najua ningeizidisha tu hofu ya Miryam kutokana na vitu ambavyo mdogo wake angeweza kufanya.

Kwa sasa ingekuwa busara kutulia tu, lakini ningehakikisha nakuwa makini ili kuiepusha familia hiyo kutoka kwenye matatizo ambayo Joshua alitaka kuyaendeleza; hasa kumlinda Mariam.

★★

Muda mfupi baada ya Miryam na Tesha kuwa wameondoka hapa kwa Ankia, nikawa nimefanya usafi wa chumba na mwili, kisha nikavaa vizuri ili niweze kwenda pale kwao kushughulika na binti Mariam.

Ni leo ndiyo nilitaka kumpa Ankia hela ya kodi kwa ajili ya mwezi uliofuata, basi tu yaani ili wiki ambazo zingefuata nisiwaze kabisa kuhusu hilo suala. Nilipotazama matumizi yangu ya pesa za pembeni toka nimekuja mapumziko, nikaona nilikuwa nimetafuna nyingi kiasi, lakini hakukuwa na shida sana juu ya hilo.

Baada ya kupangilia mambo vyema, nikamfata Ankia na kumpatia pesa. Kama kawaida yake, alianza kujishaua mara JC mbona hivi, mbona vile, nami nikalazimisha azichukue na kumwambia akate mashauzi yake. Nikamuaga baada ya hapo, nikisema ndiyo naenda kwenye wajibu wangu wa kidaktari, nami nikaelekea mpaka kwa jirani yetu.

Tesha akawa amekuja kunifungulia geti, naye akasema kitu ambacho hata Bi Zawadi aliwahi kuniambia mapema sana kuhusu geti hilo. Ni kwamba kama mlango mdogo wa geti ungekuwa unaweza kufungukia kwa nje basi ningekuwa naingia tu badala ya kusumbuka kupiga hodi, hivyo nikaona nisaidie kuirekebisha hali hiyo kidogo.

Nikamwomba Tesha atafute kamba nyembamba, msumari, na nyundo ikiwezekana ili tujigeuze mafundi hapo. Akatii na kufata kamba nyembamba iliyoendana na zile walizoweka hapo nje kwa ajili ya kuanikia nguo, msumari mrefu, lakini hakukuwa na nyundo. Akaleta tu jiwe.

Nikaikata kamba hiyo kwa urefu uliotoshea upana wa kimlango hicho, kisha nikaifunga kwenye kale kadude ka kuvuta kwenye kifungio cha geti na kuipitisha nje kupitia uwazi mdogo mwanzoni mwa ukuta ambapo geti lilianzia. Nikatoka nje na kuugonga msumari ukutani, mwanzoni kabisa karibu na geti, kisha nikaifunga kamba hapo.

Tukaanza kufanya majaribio kwa kufunga kimlamgo cha geti, kisha naivuta kamba kiasi nikiwa kwa nje ili ikikivuta kile kidude kwa ndani, kiachie, na huo mlango ukafunguka. Akili mtu wangu! Ilikuwa ni njia ndogo tu ya kurahisisha kazi kwa sisi tuliozoea kuja hapo, naye Tesha akasema ilikuwa ni njia nzuri sema aliona uvivu tu kushughulika na geti hilo.

Nikaingia tena, na wakati huu ndiyo nikatilia maanani kuwa gari la Miryam halikuwepo, kumaanisha alikuwa ameshakwenda kazini. Nikamuuliza Tesha hali kwa sasa ilikuwaje, naye akaniambia tu twende ndani ili tukaongelee huko.

Kweli tukaenda, nami nikakuta hali isivyo kawaida na nilivyokuwa nimezoea. Sikuwakuta Bi Jamila na Bi Zawadi wakiwa wamekaa kwenye sofa lao kama kawaida, na sikumwona Mariam pia. Nikadhani labda wapo chumbani maana kulikuwa na hali ya utupu hapo.

Tukakaa na Tesha sofani, nami nikamuuliza, "Mariam yuko poa?"

"Eeh, ila ndo' hayupo. Wote hawapo," akasema hivyo.

"Wapi tena?"

"Da' Mimi kawachukua kuwapeleka kwa Joshua. Wakaongee huko," akasema hivyo kwa njia ya kukerwa.

Nikamwangalia kwa umakini na kuuliza, "Kampeleka Mariam kwa Joshua?"

"Ndo' maana yake."

"Lakini si Miryam amesema anaenda kazini?"

"Ndiyo, kawapeleka huko wote na mama wakubwa, halafu ataenda kazini... labda na baadaye ataenda tena huko... kuwafata."

"Mbona we' hujaenda?"

"Kwani haiko wazi? Sitaki tu. Lakini nimesingizia kwa dada kwamba sijisikii fresh bado. Hapo wanaenda kudanganywa-danganywa tu na huyo fala."

"Aisee! Yaani akimgusa Mamu, atanitambua," nikajikuta nimesema hivyo kwa hasira.

"Nini? Nani, Joshua? Anataka kumuumiza Mamu?" Tesha akaniuliza hivyo kwa mkazo.

Nikamwangalia na kusema, "Aa... hapana, yaani namaanisha... hali ya Mariam siyo nzuri kivile bado, ikiwa ataogopeshwa sana na kaka yako itakuwa kurudi nyuma tena. Nimeongea tu vibaya."

"Siyo vibaya, me mwenyewe nitamuua huyo mjinga ikiwa Mamu atarudi hapa bila unywele hata mmoja. Sema ndiyo nimemwahidi dada kuwa mpole, kwa hiyo natulia tu."

"Ila ungeenda nao Tesha, huwezi kujua," nikasisitiza.

"Usiogope bro. Me najua Joshua anachokifanya hapa mwanzoni ni kuigiza tu, kwa hiyo lazima na mimi niigize pia. Hawezi kumgusa mtu yeyote sa'hivi, utaona," akanihakikishia.

Nikaangalia pembeni nikiwa nimeudhika kiasi. Sikujua nifanye nini maana hali hii ilikuwa ya kushtukiza, na hii ikanipa somo kuhusu kuwa chonjo zaidi na hii familia ili Joshua asije kufanikiwa kwenye mipango yake, mimi nikabaki tu mdomo wazi.

"Wanarudi saa ngapi?" nikamuuliza hivyo.

"Jioni. Hapa doro tu kaka. Nataka nikazurure wee mpaka hiyo jioni," akaniambia hivyo.

Nikatulia tu na kushusha pumzi.

"Oy... kama vipi tuoshe, ama nini?" akaniuliza.

"Kuelekea wapi?"

"Nataka nikazunguke Kigamboni leo. Halafu baadaye tutazamia kwa mshkaji fulani hivi, nina siku sijamwona. Unasemaje?" akasema hivyo.

Lengo la kuja hapa ilikuwa kuendelea na mazoezi yangu pamoja na Mariam, lakini hakuwepo. Sikuwa na jambo lingine muhimu la kufanya kwa hiyo nikaona nimkubalie tu rafiki yangu. Labda na matembezi yangeleta jambo jipya mbali na yale niliyokuwa natazamia yafike.

Alikuwa ameshaoga kwa hiyo nikakaa kumsubiri alipokwenda kuvaa. Alivalia kawaida tu kama mimi, na kofia yake kama kibandiko kichwani ikanifanya na mimi nitake kwenda kuichukua ya kwangu, lakini nikaahirisha.

Tukatoka pamoja, akafunga milango na geti, nasi tukaenda kwa Ankia ili Tesha amwachie funguo za kwao ili endapo kama ndugu zake wangewahi kurudi kabla yake basi wazikute hapo. Ankia akatutakia matembezi mema huku akisema tukirudi tumletee zawadi, nasi tukaingia barabarani baada ya hayo.

★★

Basi, tukawa tunatembea mdogo mdogo kuelekea Mzinga. Baada ya kufika Mzinga, kibishoo tu yaani, tukaamua kuifata Kongowe kwa kutembea pia. Mwendo wa taratibu tu, huku tukipeana story nyingi za mambo yetu wanaume ukatufikisha mpaka hapo Kongowe, na hii ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika eneo hilo tokea nimepajua Mzinga; na hata Mbagala pia.

Mwanzoni mwa eneo hilo kunakuwa na sehemu nyingi zenye biashara ndogo na kubwa za wajasiriamali sanasana, nasi tukaelekea upande ambao daladala zingesimama kwa ajili ya kubeba abiria. Tukakuta moja ambayo ilikuwa ikielekea Kigamboni ndiyo, nasi tukaingia na kukaa siti za nyuma kabisa. Mwonekano wangu na Tesha ungefanya watu wafikiri sisi ni ndugu wa damu labda, maana kuna sehemu kubwa ya pigo zetu iliyokuwa inafanana sana.

Tukiwa tu ndiyo tumekaa, Tesha siti ya dirishani kabisa na mimi pembeni yake, nikapokea ujumbe kutoka kwa mtu ambaye sikuwa nimetarajia kabisa kwa muda huu. Ilikuwa ni Adelina, dada mkubwa wa Joy; ama niseme marehemu Joy.

Yaani tokea tumebadilishana namba pale msibani sikuwahi kumtumia salamu hata mara moja, ijapokuwa nilikuwa kwenye harakati za kumtafutia mdogo wake haki kwa mauaji yaliyomsibu. Alikuwa ametuma salamu fupi, 'habari yako,' nami nikatuma jibu kuwa 'niko salama' na kuuliza yeye aliendeleaje.

Nikaanza kumsikia konda kutokea nje akisema kwa abiria fulani waingie kukaa, kwamba siti hazikuwa zimeisha. Yaani alikuwa anawashawishi kwa kusema tena kuna waarabu ma-handsome wamekaa huko mwishoni, na ndiyo Tesha akanishtua nitazame nje.

Nikaangalia kupitia kioo na kuona wanawake wawili pamoja na mwanaume kijana mmoja, wote wakiwa ni waislamu, na mwanamke mmoja alivalia yale manguo meusi yanayoficha mpaka uso kasoro macho, lakini kale kengine uso ulikuwa wazi tu na kuzungukiwa kwa hijab kichwani. Kalikuwa kembamba, keupe, kenye macho mazuri kweli, na nahisi wao walikuwa waarabu kasoro huyo mwanaume kijana aliyekuwa mweusi kabisa; akionekana kuwa mwandamani wao.

Huyo mwanamke aliyeficha uso alikuwa kama hataki kuingia kwa kuwa labda hakupenda kukaa mwishoni, naye Tesha akawa ananishurutisha tufanye jambo ili hako kadada kaingie maana alikuwa amekaelewa tayari. Adelina akawa amenitumia ujumbe akisema yuko poa na kuuliza kama bado nilikuwa Mbagala, naye Tesha akaendelea kunibonyeza-bonyeza mpaka nikahisi kero.

Agh, nikasogea kufikia uwazi wa kioo na kuwaangalia wanawake hao, nami nikasema, "Dada, ingieni tu. Nafasi ziko tatu, yaani kama vile zimebaki kwa ajili yenu tu."

Mwanamke aliyekuwa amefunika mpaka uso akawa ananiangalia sana, naye konda akaongeza spidi ya kuwashawishi.

Nikakaa sawa tena na kumwambia Tesha, "Nimeweka jitihada hiyo kama ulivyotaka. Umefurahi?"

Akacheka kidogo na kusema, "We' ni chizi! Ndo' mpaka utuchoreshe? Ona washamba wanavyotuangalia."

"Unasumbua mno," nikamwambia hivyo nikiwa makini na simu.

Nikamjibu Adelina kwamba bado niko Mbagala ndiyo, na kumuuliza kama alisharudi Mbezi. Tesha akanibonyeza kidogo, nami nikaangalia mbele na kuona wale wanawake wameshapanda na kuja upande wa nyuma. Yule mwanaume kijana hakupanda, inawezekana labda alikuwa anawasindikiza tu, nao wakaja kukaa pamoja nasi; nafasi iliyobaki ikiwa imetutenganisha katikati.

Kale kadada kenyewe kakawa dirishani kabisa, huyo mficha uso akiwa pembeni yangu, nami nikamtazama Tesha na jamaa akajikausha tu kama vile siyo yeye aliyenisisitiza kuwashawishi waingie. Inaonekana kwa muda huu abiria waliokuwa wanataka kuelekea huko mbele walikuwa wachache, kwa sababu hakukuwa hata na mtu aliyesimama na safari ikaanza.

★★

Vuuu, mwendo ukaendelea huku na mimi nikiendelea kuchat na Adelina. Ilianza kidogo kidogo tu lakini mpaka ikafika hatua tukaanza kutaniana, kirafiki yaani. Akawa ameniambia kuwa kwa sasa hivi alikuwa amekwenda pale Mbagala kwa rafiki yake mmoja kumsalimia na ndiyo alifikiria uwezekano wa kupata nafasi ya kuja kunitembelea mimi na Ankia pale nyumbani.

Unajua, mpaka leo Adelina alikuwa anafikiri mimi ni mume wake Ankia, ndiyo ikabidi nimwambie kwamba ile ilikuwa danganya toto tu niliyofanya pamoja na Ankia; wala hata hakuwa mke wangu, na ndiyo matani baina yangu na Adelina yalianzia hapo.

Mwendo ulikuwa mrefu kiasi kuelekea Kigamboni, mara kwa mara watu wakiongezeka kwenye gari na kupungua, na uvumilivu ulikuwa unamshinda Tesha. Alitaka sana kuipata namba ya kale kadada keupe pembeni yetu, lakini alihofia kwamba huenda huyo mwanamke mwingine alikuwa mama yake kwa hiyo kungekuwa na utata.

Lakini akawa ananishawishi kwa kunitumia sms nijaribu kumsemesha maana alikuwa na uhakika kwamba mwanamke huyo aliingia tu kwenye gari kwa sababu yangu, nami nikamwambia Tesha aache umalaya la sivyo ungekuja kumuua siku moja.

Kama ninavyosemaga, mimi siyo mtu wa kuogopa mtu kabisa, na kama ningekuwa nataka kupata namba za mwanamke yeyote niliyekutana naye, ningezipata. Ila kuanza kumwelezea Tesha kwamba nilikuwa sitaki tu najua ingegonga mwamba, na hata hivyo nilikuwa nataka rafiki yangu huyu ajisikie vizuri tu baada ya mambo yote aliyokuwa amepitia jana, kwa hiyo nikamwambia atulie ili nimrekebishie mitambo.

Adelina bado nilikuwa nachat naye, akiwa amesema kwamba anaweza hata akaja leo kunitembelea mimi na Ankia pale nyumbani, nami nikaona nimjibu kwanza. Nikamwandikia kuwa kwa sasa nilielekea Kigamboni kwa hiyo endapo kama alikuwa na mpango wa kwenda kwa Ankia muda huu, asingenikuta, lakini labda kama ni jioni ndiyo tungeweza kuonana.

Ilishangaza kiasi kwamba hakuwa hata amemtafuta Ankia bado kuongelea suala la kwenda kumtembelea ilhali walikuwa ni marafiki, lakini labda ni kwa sababu tu hakuwa amewahi kuwasiliana nami kabisa, na kule kudhani mimi ndiyo kichwa sasa pale kwa Ankia.

Nilipomaliza kumweleza, nikamtazama mwanamke yule mwislamu. Hilo baibui jeusi alilovaa lilificha uzuri wa ngozi nyeupe aliokuwa nao, maana nilitazama vidole vyake vyenye kucha ndefu kidogo na nyekundu, vilivyoshikilia simu ya macho matatu, na kiuhakika nikaona kwamba havikuwa na hata chembe ndogo ya sugu nyeusi. Sijui walikuwa waarabu kweli?

Tesha akanibonyeza tena na kunipa ishara kwamba eti nichangamke, nami nikatabasamu kiasi na kufungua simu yangu tena upande wa sms.

Nikaandika pale patupu hivi, 'Habari? Naomba namb yako kam hutojal'

Nikanyoosha simu kwa chini kumwelekea mwanamke huyo, naye akaitazama. Sikuwa hata nikimwangalia lakini nikamwona akinyanyua uso wake kuniangalia, hivyo na mimi nikamwangalia. Huwa naweza kuweka macho fulani hivi ya kumvuta mwanamke aamshe upendezi kunielekea, macho ya ushawishi yaani, nami nikawa namtazama kwa hiyo njia.

Akaangalia mbele tu kama vile hataki, kisha akaichukua simu yangu kichinichini na kuiunganisha na yake. Nilikuwa nimeweka uso makini, nikiona wazi jinsi Tesha alivyojikausha kwa kujifanya anatazama nje tu, na kwa jicho la mbali nikaweza kuona mwanamke huyo anaandika kitu fulani kwenye simu yangu.

Kisha, akaitelezesha simu kwenye hiyo siti kuelekea upande wangu bila kuitazama, kukiwa na pete nene zenye kuonekana kuwa kama za dhahabu kwenye vidole vyake viwili, nami nikaipokea nikiwa nimeweka mwonekano makini bado. Mambo ya siri hayo, na Tesha ndiyo akawa ameniingiza majaribuni!

Wanawake wa hivi nawaelewa sana, yaani wanapoamuaga kujitafutia vitulizo vya nje huwa wanapenda mno usiri wa hali ya juu, na huyu inaonekana alikuwa amenielewa sana ndiyo maana akakubali kufanya hivyo akiwa pembeni ya binti yake, sijui mdogo wake, sikujua.

Tesha akakunja ngumi yake karibu na paja langu, akiwa anataka tugonge tano ya ushindi, nami nikaweka kiganja changu hapo huku nikimnyanyulia kidole cha kati. Nikatazama simu yangu na kukuta namba za simu zikiwa zimeandikwa hapo, nami nikazitumia ujumbe.

'Jina lako mremb?'

Nikajikausha kama simwangalii, nami nikaona anaandika kitu fulani kwenye simu yake kisha akatazama pembeni.

Ujumbe ukaingia kwenye simu yangu, namba hiyo hiyo, ukisomeka, 'niambie lako na wew.'

Nikajibu, 'JC'

'Ndiyo nn'

'Ndiyo my name'

'Me naitw Ibtisam'

'Ooh saw. Jina lako zur kam wew mremb'

'Uremb wang umeon wp'

Nikiwa bado sijajibu ujumbe wake huo ndiyo tukawa tumeingia maegesho ya daladala kwenye eneo la Kigamboni, na watu wakawa wanasimama ili washuke.

Nikamwandikia hivi, 'Ngj tushuke nikwambie'

Kweli tukaanza kushuka mpaka nje, nami pamoja na Tesha tukaenda upande wa nyuma wa gari na kuwaangalia wanawake hao waislamu. Wenyewe wakaelekea upande mwingine kwa pamoja, huku kale kembamba kakigeuka kututazama mara moja.

Nikaangalia simu na kukuta ujumbe wa huyo mwanamke akiwa amejibu, 'Saw, lkn ntakuchek badae. Kun shm naend sahiv'

Tesha akaniuliza, "Oy, umemwambiaje? Anasemaje?"

"Kaka utakuja kuniweka matatizoni siku moja!" nikamwambia hivyo.

Tukaanza kutembea kuelekea sehemu iliyoturuhusu kuiona vyema Bahari ya Hindi.

"Kwani vipi?" akaniuliza.

"We' kila demu unataka tu, wengine ni majini."

"Ahahahah... me kwani nilikwambia namtaka huyo jini wako? Mimi nilikuwa nakataka kale kengine, we' si umechukua namba ya huyo maza'ake kwa upendo wako?"

"Nimeomba namba yake ili uje kuipata ya hako unakokataka. Halafu Tesha!"

"Hahahah... JC bana! Kwo' jini linasemaje?"

"Atanicheki baadaye, na linaonekana limeolewa. Ah, sijui hata kwa nini nimemwomba namba!"

"Si kwa ajili yangu? We' ukishamzuzua utanifanyia unyama na mimi nipate ya hako kengine. We' utakula mazeli, mimi kimweli. Tena tutafanyia kwenye double deka kabisa."

Nikacheka kidogo tu na kusema, "Tesha tunaingia Kigamboni, wanawake wazuri kama wote, utawasahau hao uliowaona. Tulia mdogo wangu."

"Ah, kwenda huko! Huu ndiyo wakati wangu, we' ushazeeka ndo' maana. Twende tukapande meli huko."

Nikacheka na kutikisa kichwa, nami kweli nikaanza kumfata.

Tukapita sehemu nyingi zenye biashara, watu wengi, wadada wazuri ndiyo usiseme, nasi tukaelekea sehemu ya kununulia kadi za tiketi kwa ajili ya kuvuka bahari kwenda upande wa pili wa Kigamboni; ule wenye majengo ya ukweli. Tesha akapata kadi, nasi tukaenda kuvuka kwa kupanda meli ndogo ya uvukishaji abiria na magari. Watu walikuwa wengi kufikia kiasi kilichohitajika, na wakati tukiwa tumeanza kuvuka mvua ikaanza kunyesha.

Mpango ulikuwa kwenda kuzurura sehemu kadha wa kadha kwa eneo hilo, lakini mvua ikaongezeka mno kiasi kwamba jambo hilo likaingiwa na utata. Yaani ile tumeshuka tu, ikatubidi tuingie kwenye daladala ambazo zilielekea Kariakoo, na safari ikaanza tena. Hii haikuwa mara ya kwanza kutembelea Kigamboni na hata niliwahi kutoka na mwanamke fulani aliyekuwa wa pande hizi, ila hiyo ni hadithi nyingine, ya kusimuliwa kwa wakati mwingine.

★★

Mwendo wa dakika kadhaa ukatufikisha mpaka Kariakoo, na kwa huku mvua ilikuwa ishakatika. Tukashuka, Tesha akiwa bado anawashwa kutembea, hivyo tukachukua mwendokasi na kwenda pande za Ubungo. Tukazurura wee, Tesha hata akanipitisha kule alikokuwa anaenda kufata wanawake wa kulipwa, chimboni yaani, naye akawa akisema hizo mishe siku hizi hafanyi.

Tukatoka huko na kuzunguka mpaka Uhasibu, nasi tukashukia hapo. Tesha alikuwa na rafiki yake mwanachuo aliyekaa eneo la Uwanja wa Benjamin Mkapa, hivyo tukatembea mdogo mdogo kuelekea huko. Alikuwa ameshawasiliana naye. Yaani safari hii yote leo ilikuwa ni kwa udhamini wa Tesha, mimi ndiyo nilikuwa kama mtalii wake, nasi tulipokuwa tu ndiyo tumeyapita malango ya uwanja nikaanza kuona mdada fulani akija upande wetu taratibu.

Tesha alikuwa ameniambia kwamba tunaenda kumsalimia tu mshkaji wake, kwa hiyo sikuwa nimetarajia kwamba ingekuwa ni mwanamke mpaka mdada huyo alipotukaribia na kukumbatiana na Tesha kirafiki. Alikuwa mfupi kiasi, mweusi, mwili wa kawaida tu, na tabasamu lake lilionyesha mwanya mdogo katikati ya meno yake ya mbele.

Wakawa wanasemeshana kirafiki sana, naye akaniangalia na kunisalimu pia. Alikuwa mchangamfu sana, jina lake ikiwa ni Dina, naye akatuongoza kuelekea pale alipoishi. Ilikuwa ni kwenye zile nyumba za wapangaji zilizojaa hasa wanafunzi wa chuo, nasi tukaingia kwenye chumba chake.

Kilikuwa simple tu, safi, godoro chini kwenye sakafu ya vigae, friji ndogo, begi la nguo pembeni ya shehena ndogo ya vyombo, vifaa vya mapodozi na manukato, viti vitatu vya plastiki. Jiko dogo la gesi lilibeba sufuria lenye chakula kwa ndani bila shaka, nasi tukakaa na kuanza kupiga story.

Mimi nilikaa kwenye kiti, Tesha na Dina wakakaa kwenye godoro, na ni wao sanasana ndiyo walioongea huku mimi nikichangia mada mara moja moja kukoleza ucheshi. Dina akaniuliza natumia soda gani, nami nikamwambia Pepsi. Tesha vilevile akasema Pepsi ingawa alitania kutaka bia.

Dina akatoka kwenda kufata soda, nasi tukabaki hapo, nikisikiliza maneno ya kipuuzi ya Tesha kuhusu jinsi nilivyotakiwa kubaki hapa leo ili nifanye jambo fulani na Dina. Ni hapa ndiyo nikawa nimepokea ujumbe kutoka kwa yule mwanamke mwislamu tuliyekutana kwenye daladala, akiwa ametuma tu 'mambo,' nami kabla hata sijamjibu, simu yangu ikaanza kuita. Mpigaji? Bertha. Hatimaye!

Sikutaka Tesha asikie jambo lolote ambalo lingemfanya atambue nani naongea naye, hivyo nikapokea nikiwa nimejihakikishia kutosema lolote litakalomshtua jamaa.

"Hallo?" sauti yake Bertha ikasikika.

"Hello, vipi?" nikasema hivyo.

"Poa. Uko wapi?"

"Niko kwa Mkapa hapa."

"Unafanyeje huko?"

"Nimekuja kwa mshkaji wangu, niambie..."

Tesha akaniuliza kwa ishara, "nani?" nami nikamwonyesha ishara pia kuwa atulie.

"Nataka uje. Au biashara uliyonayo sasa hivi huko ni muhimu sana?"

"Hakuna chochote muhimu zaidi yako dear."

"Usiniite dear, mazoea ya hivyo sitaki."

"Sawa dear," nikasema hivyo makusudi.

"Halafu wewe!" akasikika kwa ukali.

Nikajikaza nisicheke na kumwambia, "Pole, nimejikwaa tu. Ulimi hauna mfupa."

"Na nitakuja kuuwekea mfupa usipoangalia."

"Sorry."

"Toka huko sasa hivi. Niko Masai," akaniambia hivyo.

Ni muda huu ndiyo Dina akawa ameingia ndani tena, lakini wakati huu alikuwa pamoja na mwanadada mwingine mweupe, mwembamba, mrefu kiasi, aliyekuwa amevalia T-shirt nyeusi na suruali ya jeans ya samawati iliyobana. Nywele zake zilisukwa kwa mtindo wa dread nyeusi na fupi, naye akaenda kukaa godoroni baada ya Tesha kunyanyuka na kukaa kwenye kiti.

"Umeelewa?" Bertha akasikika kwenye simu.

Nikasema, "Eeh, nimeelewa. Ila... niko mbali kama hivi, naweza kuchelewa kidogo."

Dina akawa ametufungulia soda zetu na kutupatia, na ukimya mfupi uliofuata kwenye simu ukanifanya nitambue kwamba Bertha alikuwa amekasirishwa na maneno yangu.

Nikamwambia, "Ila nakuja. Nitakuwa nimeshafika muda siyo mrefu."

Likakata simu!

Kazi nilikuwa nayo. Nikashusha pumzi na kumwangalia Tesha, aliyekuwa akinitazama kama anasubiri nijielezee.

"Kuna dharura bro. Natakiwa nifike location mara moja," nikamwambia hivyo.

"Tumekuja wote, unataka kuondokaje mwenyewe bana?" Tesha akaniuliza kwa uthabiti.

"Iih, unataka kutukimbia?" Dina akaniuliza hivyo.

"Kuna dharura imetokea, nahitajika sehemu haraka ndo' maana..."

"Acha bangi! Hautoki hapa. Keki tamu kama hizi unakimbia kweli?" Tesha akasema hivyo kiutani.

Tukacheka kidogo, na Dina akamsonta huku akisema, "Afu' wewe!"

"Inanibidi tu kaka," nikamwambia Tesha.

"Jamani, mbona ghafla? Chakula hiki napakua," akasema Dina.

"Oh usijali Dina, niko poa. Labda umpakulie huyu mbwa," nikamwambia hivyo.

Akacheka kidogo, naye Tesha akasema, "Em' pakua mama, tule."

"Basi kunywa hata soda, imeshafunguliwa," akaniambia hivyo yule mdada mwingine.

"Ee, kunywa soda ndiyo uende kaka," Dina akaniambia.

"Poa," nikajibu.

Ingenibidi nipige hii soda fasta maana huyo Bertha hakuwa mtu wa subira hata kidogo, na hiki ni kitu ambacho nilikuwa nimekisubiria sana kwa hiyo wiki nzima kwa hiyo nisingeweza kuchezea nafasi hata kama ningepewa ofa ya utatu na hawa wadada!

Nikawa napiga fundo ndefu ndefu, huku nikiwa nimeanza kuchat na yule mwanamke mwislamu pia. Alikuwa mmoja kati ya wale wanawake ambao walipenda mtu aende moja kwa moja kwenye pointi ya kitu ambacho alitaka kutoka kwake, nami nikamwambia ndiyo, nilimkubali sana kutokana na kupenda macho yake na ngozi yake.

Akaniambia ooh nimeshaolewa, kwa hiyo ukinitaka lazima upande ngazi, nami nikamwambia hakuna ngazi za kupanda; ikiwa alinikubali pia basi tuje kucheza, lakini asipotaka basi sitalazimisha. Kwa kauli hiyo akawa ametulia kwanza, nami nikawa nimemaliza soda.

Nikamshukuru Dina na kusimama, Tesha bado akiwa analalama kuhusu mimi kuondoka, hivyo ikanibidi nitoe ahadi ya kuja naye tena kesho ikiwezekana kumtembelea rafiki yetu. Dina alipenda sana hilo wazo na kusisitiza nisije kuacha kuja, nami nikamwambia aondoe shaka. Huyo rafiki yake mwingine alikuwa akiniangalia sana kwa sura yake ya kiupole, nami nikamuaga pia nikiwa hata simjui jina.

Nikawaacha marafiki hao hapo na kuanza kuelekea barabarani, nikiwa natumaini kuwahi, na Tesha asijue kwamba sehemu niliyokwenda ilikuwa ni Masai. Angeshangaa sana!

★★

Nilifanikiwa kupata usafiri wa daladala zilizoelekea Mbagala, na mpaka kufikia huko tayari ilikuwa inaelekea kuingia saa moja. Nilikuwa nikijiuliza ni kwa nini madam Bertha alikuwa ameamua kuja Masai mapema sana leo, lakini hayo yote ningeyajua nikishafika pale.

Badala ya kuchukua daladala tena kutokea Rangi Tatu, nikaamua kupanda bodaboda ili niwahi zaidi, brrrr mpaka Mzinga, nami nikaunganisha moja kwa moja kufikia Masai, lakini nikaona nielekee kwa Ankia kwanza.

Nikafika hapo dukani kwa Fatuma na kumkuta huyo dada pamoja na wanawake wengine wengine wakiwa wamekaa kama kikundi cha kupiga umbeya, nami nikamwambia bodaboda anisubirie nikachukue mzigo ndani kisha anirudishe Masai upesi. Nikawapita hao wavaa dera kama siwaoni, nami nikaelekea mpaka ndani na kuingia.

Akili yangu ilikuwa imekazia fikira jambo moja tu kiasi kwamba mpaka nikashtuka kiasi moyoni baada ya kuingia na kumkuta Ankia akiwa amekaa pamoja na Adelina! Ile hali ya kutotegemea kumkuta mwanamke huyu hapa ingawa tulikuwa tumewasiliana ilikuwepo yaani, halafu nilikuwa kwenye kasi kwelikweli.

Wawili hao, baada ya kuniona, wakatabasamu kwa pamoja, nami nikatabasamu pia na kusogea karibu zaidi na walipokaa.

"Mume amerudi," Adelina akasema hivyo.

"Ee, baba mwenye nyumba ndiyo kafika," Ankia akasema hivyo pia.

Nikajikuta tu natenda bila kufikiri sana kwa kuinama na kumkumbatia Adelina, nami nikamwambia, "Karibu."

Nafikiri alikuwa ameshangaa kiasi lakini akaweza kucheka kidogo kwa pumzi, naye akasema, "Asante."

Nikamwachia na kusema tena, "Karibu sana."

Kisha nikaelekea chumbani, bila shaka nikiwaacha wanawake hao wanatazama haraka yangu.

Nikaingia chumbani na kutoa yale madawa niliyotengeneza, nami nikachukua kiasi kidogo na kukiweka kwenye karatasi tu baada ya kuwa nimekosa pa kuwekea, kwa kuwa sehemu niliyohifadhia dawa yote ilikuwa ndani ya mifuko minene; madawa yakionekana kama glucose. Nikachomeka hicho kikaratasi mfukoni, kisha nikaelekea sebuleni tena.

"Unatoka?" Ankia akauliza hivyo.

"Ndiyo, kuna sehemu nafika mara moja lakini... sikawii, nakuja. Sawa?" nikaongea hivyo nikiwa nimeelekeza fikira zangu kwa Adelina.

Akatikisa kichwa kukubali, naye Ankia akasema, "Unawahi nini kinachokutoa kijasho hivyo? Tuambiane..."

"Utajua tu, ngoja nirudi," nikasema hivyo na kuelekea mlango.

Nikawaacha wanawake hao wakicheka kidogo, nami nikaenda mpaka nje tena. Nikapanda bodaboda na kugeuza kuirudia Masai, nasi tukafika hapo huku sasa giza likiwa limeshaingia. Nikamlipa jamaa na kumwambia atokomee, kisha nikaelekea pale ndani.

Wanywaji walikuwepo na nafikiri kuna wahudumu wapya waliokuwa wameongezwa hapa na wachache niliowajua kuondoka, nami nikawa nimemwona Bobo pamoja na DJ fulani hivi wa hapo Masai. Nikamfata.

"Oyo, mchina..." akaniambia hivyo tukiwa tunagonganisha mabega yetu kirafiki.

Nikagongesha tano kwa yule DJ pia, kisha nikamwambia Bobo, "Oya umepotea kweli."

"Ah, mimi, wewe? Yaani hutokei Masai siku hizi mwanangu. Check watu wanavyokuangalia kama vile hujawahi kuonwa hapa," akasema hivyo.

Nikatabasamu na kusema, "Na mimi nimetingwa kaka, ila mdogo mdogo narudi. Ishu zinakwendaje?"

"Kama kawa budha. Oy... mtu wako yupo huko ndani," akaniambia hivyo kwa kuninong'onezea sikioni.

"Eeh, nimeona gari nje," nikamwambia.

"Yuko VIP, kamchangamkie..."

"Ndo' mpango mzima," nikasema hivyo.

Tukacheka tena pamoja, kisha nikamwacha hapo na kuelekea pande ya VIP. Na Bobo alikuwa sahihi kabisa, watu walikuwa wananiangalia kweli, lakini umakini wangu wote ulikuwa kumfikia huyo madam.

Nilipofika mlangoni, nikajiwekea hali ya utulivu, kisha nikaingia ndani hapo. Nikamkuta madam Bertha akiwa amekaa sofani, glasi yenye wine kiganjani, na kwenye sofa la pembeni alikaa yule baunsa wake; a.k.a shemeji.

Kama kawaida ya mwanamke huyo, alikuwa amependeza kwa kuvaa kigauni kifupi chekundu, kilichoyaacha mapaja yake meupe wazi kutokana na namna alivyokuwa amepiga nne, na inaonekana kilikuwa cha mgongo wazi. Wakati huu alishonea wigi la nywele za kizungu kichwani, na baunsa wake alikuwa amevaa kaushi tu na suruali nyeusi, akionyesha misuli yake imara.

Nikasogea usawa wa meza moja hapo, nami nikamtikisia kichwa jamaa kama salamu, naye akairudisha. Nikamwangalia Bertha, ambaye alikuwa akinitazama tu kwa utulivu, nami nikamwambia, "Nimefika madam."

"Umechelewa," akaniambia hivyo.

"Kweli? Mbona naona kama bado party haijaanza?" nikamuuliza hivyo.

Baunsa wake akamwangalia na kucheka kidogo, naye Bertha akawa amenikazia macho yake.

"Tupishe," Bertha akamwambia hivyo jamaa.

Baunsa akasimama na kuja upande wangu, naye akaniuliza, "Una ule unyama jembe?"

"Nakosaje labda?" nikamuuliza hivyo.

Akatabasamu huku akitikisa kichwa taratibu, nami nikaitoa ile dawa na kumfungulia.

"Si iko kama ile?" akaniuliza hivyo.

"Kwa asilimia zote," nikamwambia.

Akachovya kwa kidole na kulamba, kisha akatikisa kichwa kwa nguvu kiasi na kunishika begani. "We' dogo ni nyoko!" akaniambia hivyo.

Nikatabasamu kidogo, naye akanipita na kutoka ndani humo.

Nikabaki na madam. Alikuwa ananitazama kwa yale macho ya kuhukumu bado, naye akasema, "Njoo."

Nikatii na kumfata. Sikuwa na hofu kumwelekea huyu mwanamke, ila kujifanya mnyenyekevu sana ilikuwa lazima. Nikasimama usawa wa sofa alilokalia na kubaki mtulivu.

"We' vipi, si ukae?" akaniambia hivyo.

Nikasogea na kukaa kwenye sofa karibu yake.

Akawa ananitazama sana, naye akasema, "Yaani hiyo sura! Kama mwanamke!"

Dah! Kashfa hizo.

Nikatabasamu kwa kujilazimisha na kusema, "Asante. Moja kati ya silaha zinazonisaidia kupita huku na kule ni hii sura."

Akacheka kwa mguno, kisha akaweka glasi yake pembeni.
"Nimekufatilia kwa hiyo wiki dogo, naona una maisha magumu sana mpaka ukaamua kutoka Goba Center kuja kuishi Mbagala," akaniambia hivyo.

Umeona sasa? Nilikuwa sahihi. Huyu mwanamke alikuwa amefanya uchunguzi kunihusu mpaka kujua kitu ambacho bado sijaelezea kujihusu. Nikataka kujua anaelewa mambo mengi kadiri gani kuhusu maisha yangu.

"Ahah... eeh... maisha magumu. Nimekaa sehemu nzuri lakini... hazijanifiti ndo' maana nimeangukia huku sasa hivi," nikaongea hivyo kiupole, ikiwa kimtego zaidi.

Akasema, "Me sijali ulikuwa unaishi vipi. Nataka tu ujue nikiamua kukuharibia maisha yako endapo kama utanigeuka basi sitosita kuanza hata na familia yako."

"Usiwe na hofu juu ya hilo madam. Siwezi kukusaliti. Kwanza... familia yangu iko Mwanza, mimi huku ni mtafutaji tu kwa hiyo niko mwenyewe," nikamdanganya.

"Una uhakika na kile ulichojiingiza kukifanya huku dogo?" akaniuliza.

"Ndiyo najua. Nina ujanja mwingi, usinichukulie poa. Sema mambo huko Goba hayakwenda fresh tu ndo' maana nikaja huku kujitafuta, na najua nimejipata tena kwa kuwa chini yako. Sitakuangusha madam. Najua nachokifanya, na nitafata utakachonielekeza kufanya," nikamwambia hivyo.

Akatulia kidogo, kisha akasema, "Sawa. Nipe hiyo kitu nionje."

Nikamfungulia kikaratasi chenye dawa ya cocaine, naye akachovya na kulamba kidole chake huku akinitazama kwa macho makini. Kidogo tu yakalegea naye akawa ananiangalia utadhani ananitaka kimapenzi. Ah mimi nilikuwa mtaalamu bwana!

Na angalau kufikia hapa nikawa nimetambua kwamba hakujua mengi zaidi kuhusu maisha yangu isipokuwa tu kuwa amefatilia na kujua nilikotokea kihalisi kabla ya kufika huku, kwa hiyo mchezo wangu kwake ungeendelea taratibu.

Vibe likiwa limemgonga, akaniambia, "Unyama mzuri huu."

Nikatabasamu kidogo.

"Kuna ishu nataka nikushirikishe," akasema hivyo.

Pasi ndefu hiyoo! Nikatikisa kichwa kuonyesha namsikiliza.

"Kesho utakuja pale pale ulipokuja siku ile, uje jioni," akasema hivyo.

"Sawa. Nije na unyama wetu?" nikamuuliza.

Akaweka macho ya udadisi, naye akauliza, "Unamaanisha kwamba unao mwingi?"

"Nimetengeneza kiasi fulani. Hakijazi mifuko mikubwa lakini si unajua ni tamu mno, kwa hiyo kidogo tu...."

"Ni nyingi," akamalizia maneno yangu.

Nikatikisa kichwa kukubali.

Akaninyooshea kidole chake na kunipiga kofi laini shavuni, naye akasema, "Safi sana. Kumbe we' kweli wa faida. Uje nao kesho. Nitakuelekeza mengine ukishafika."

"Imeisha hiyo," nikamwambia hivyo.

Akawa ananitazama kwa njia fulani utadhani alikuwa ananisoma, naye akasema, "Nataka kuona kama we' siyo mwanaume sura tu."

Nikamsogelea karibu zaidi na uso wake na kumuuliza, "Kivipi?"

"Kesho. Kesho ndiyo nitaona," akasema hivyo huku akipindisha shingo yake kiasi, midomo yetu ikiwa karibu sana.

Nikasema, "Ahaa... nilidhani unataka nikuonyeshe sasa hivi."

Akatabasamu na kuangalia chini, kisha akatoa tusi kunielekea bila kuniangalia.

Nikatabasamu pia baada ya kuona kwamba alikuwa ameanza kuonyesha roho ya kuniamini kiasi, na bila shaka ishu hiyo ya kesho ingehusiana na mengi ya vitu nilivyotaka kuhakikisha vinaporomoka kwa msaada wa askari Ramadhan. Ingebidi kusubiri kuona.

Akawa amekivuta kinywaji chake tena na kuikunjua miguu yake, naye akaniangalia usoni. "Kwa hiyo toka mpenzi wako amekufa, haujaingiza substitute?" akaniuliza hivyo.

Nikatazama chini kwa ufupi, nikielewa alimaanisha Joy.

"Oh, nimegusa pabaya? Mhm... inawezekana ulikuwa unampenda sana."

"Joy na mimi ilikuwa kama biashara tu. Wala hakukuwa na kitu tense kivile," nikamwambia.

"Mm? Unanidanganya mimi? Ahah... unajua bado natakiwa niwe mwangalifu sana juu yako maana inaweza ikawa unataka kumlipizia kisasi mpenzi wako," akasema hivyo.

Dah! Lina akili!

Nikatoa kicheko cha kujilazimisha na kusema, "Madam una vituko. Najua hauamini hilo kwa sababu tayari unaniamini mimi."

"Unajuaje?"

"Usingemwambia bodyguard wako atoke nje kama ungeamini naweza kukufanyia kitu kibaya. Hadi dawa nayotengeneza unakula, kama ingekuwa kukuua si ningewekea hata sumu?"

Akatulia kidogo akiniangalia kwa umakini, naye akasema, "Huwezi kuwa na uhakika sikuzote. Ndiyo maana bado nataka nikupime."

Nikaegamia sofa, huku nikimwangalia kizembe na kusema, "Fanya chochote madam... JC ni mali yako sasa hivi."

"Nhhaa... unanifurahisha. Bado akili yako ni ndogo sana."

Nikamshika kiunoni taratibu, naye akawa makini na kuniangalia machoni. "Ndiyo unifunze sasa. Mi' wa faida kweli," nikamwambia hivyo kwa sauti ya chini.

Akabaki kuniangalia tu huku akizungusha-zungusha kinywaji ndani ya glasi aliyoshika, na ni hapo ndiyo mlango wa kuingilia ndani humo ukasikika ukifunguka. Kwa sababu nilikuwa nimeupa mlango mgongo, nisingeweza kujua nani kaingia upesi, lakini nikaona macho yake Bertha yakimtazama aliyeingia kwa njia ya kukerwa.

Nikiwa nafikiri ni mhudumu labda au yule baunsa, nikageuka bila kuwa na utayari wa kumchukulia serious huyo mtu aliyeingia mpaka nilipojikuta nashangaa kiasi baada ya kuona ni Chalii Gonga mwenyewe!



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom