Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,172
- 34,282
MISS TANZANIA
SEHEMU YA 1
MTUNZI : PATRICK.CK
“Patrick amka darling inakaribia saa nne sasa”Alisema Veronika kwa sauti laini ya kubembeleza.
“‘Mmmmhhh”Akaguna Patrick ,akajigeuza upande wa pili na kulivuta zaidi shuka.
“Amka ukaoge”Alizidi kubembeleza Veronika.Kwa uvivu Patrick akaamka na kuelekea bafuni kuoga.Dakika chache baadae alitoka akiwa amechangamka.
"Kweli maji ni dawa nzuri ya uchovu.Sasa najisikia safi kabisa.Nadhani kwa sasa itabidi nipunguze muda wa kufanya kazi .Nimekuwa nikifanya kazi kwa masaa mengi sana kwa siku kiasi kwamba nakosa hata muda wa kupumzika.Naogopa tukija kuoana nisije kushindwa kutimiza majukumu yangu kama mume kwa sababu ya uchovu” akasema Patrick na kumfanya Vero atabasamu halafu akatoa kicheko cha chini chini na kusema
“Kweli mpenzi jitahidi kwa sasa kupata muda wa kutosha wa kupumzika.”
“Nitajitahidi baby”
Baada ya kuhakikisha sasa yuko safi Vero akamshika mkono Patrick na kumpeleka sebuleni kupata stafstahi.
“Patrick dear nataka unisindikize Supermarket nikafanye manunuzi ya vitu vya ndani .Si unajua kesho Andrew na vicktoria wameahidi kututembelea”Akasema Veronika wakati wakiendelea kupata chai.
“Mhh ! Vero nenda mwenyewe mimi niache nipumzike ”Patrick akajibu
“jamani dear usifanye hivyo naomba unisindikize ,mimi naona uvivu kwenda peke yangu”
‘haya mama ,tumalize chai twende ili tuwahi kurudi”
“Nashukuru dear”
Katika vitu ambavyo Veronika alibarikiwa kuwa navyo ni uwezo wake mkubwa wa kushawishi.
* * * *
Veronika Rugi alikuwa ni msichana mrembo mwenye mvuto wa aina yake.Binti huyu licha ya kujaliwa kichwa kizuri chenye nywele laini ,nyingi na ndefu ,alikuwa na uso mpana wa mviringo ulionakshiwa na macho mapana yenye kurembua muda wote.Midomo mizuri ,laini ambayo akikupiga busu hutatamani abanduke mdomoni .Mtoto huyu alijaliwa shingo murua ambayo iliungana na kiwiliwili kilichokuwa na kifua chenye kupendeza kilichobeba chuchu changa zenye kusisimua,zenye kuwatoa udenda wakware.Kimwana huyu mwenye uzuri usiopimika alijaliwa umbo la utatanishi kuanzia kiunoni kushuka chini.Ni wasichana wachache sana waliopewa upendeleo wa namna hii na manani..
Pamoja na sifa hizo zote za nje lakini bado alikuwa na sifa lukuki za ndani.Kikubwa zaidi kinachomfanya apendwe na kila mtu ni uwezo wake mkubwa wa kuelewa mambo.Ni binti mwenye roho nzuri ya huruma na upendo asiyependa kujivuna wala kujikweza licha ya uwezo mkubwa familia yake ilionao.Ni binti mwenye heshima kwa watu wa rika zote ,mcheshi,asiyependa ubinafsi na zaidi ya yote ni mtu anayejua kupenda.
Veronika ambaye bado anaishi na mama yake mzazi baada ya baba yake kufariki miaka kadhaa iliyopita ,alikuwa ni mtoto wa tatu na wa mwisho katika familia ambayo haikubahatika kuwa na mtoto wa kiume.Dada mkubwa wa Veronika aliyeitwa Loniki hivi sasa anafanya kazi katika shirika la ndege la British airways ,ameolewa na anaishi nchini Uingereza.Mtoto wa pili kuzaliwa katika familia hii ni binti mrembo sana Sarah ambaye aliwahi kushika nafasi ya tatu katika kinyang’anyiro cha kumsaka mrembo wa taifa.naye amekwishaolewa na ni afisa mahusiano wa benki moja mpya kabisa nchini iitwayo African meckat bank.Mtoto wa tatu na wa mwisho ni Veronika ambaye bado hajaolewa ,ila alikuwa katika hatua za mwisho za kukamilisha maandalizi ya ndoa yake na mchumba wake Patrick.Ni hivi karibuni tu amehitimu shahada yake ya kwanza ya biashara katika chuo kikuu cha dar es salaam.Yeye ndiye msimamizi mkuu wa miradi yote ya familia kwa sasa.
* * *
“Patrick mpenzi nilisahau kukwambia toka mapema kuwa dada Loniki alifurahi sana kusikia tunataka tukafanye shopping ya harusi yetu nchini Uingrereza.Ameahidi kuwa yeye na mumewe watagharamia safari nzima ya kwenda na kurudi na gharama zote za manunuzi.Amesisitiza kuwa tusitumie hata shilingi yetu.Kwa maana hiyo wiki hii nataka niende tena kufuatilia yale maombi yetu ya viza pale ubalozini.Nadhani kama Mungu akijaalia basi ndani ya wiki mbili zijazo tutakuwa tumeshakamilisha taratibu zote zinazotakiwa.” Alisema Vero huku akijiegemeza karibu zaidi na kifua cha Patrick.Muda huo ilipata saa mbili za usiku , bado walikuwa wakipunga hewa safi baada ya mlo wa jioni.
“Wow! Hongera sana Vero kwa kuwa na ndugu wakarimu na wenye upendo wa hali ya juu sana kama ulivyo wewe.Tena umeongea kuhusu Loniki nimekumbuka zile CD alizonitumia wiki iliyopita.Unajua sijatazama hata moja.Hebu twende ndani nikaitazame ile filamu mpya ya Jack bauer.”
Akasema Patrick huku akijiinua toka pale walipokuwa wameketi na kuelekea sebuleni .Vero naye akakusanya vitu vyote vilivyokuwapo chini naye akaingia ndani.
“Vero mbona ile CD ya Jack bauer siioni hapa au Andrew aliichukua?Akauliza Patrick baada ya kuitafuta CD ile bila kuiona.
“Yawezekana Andrew aliichukua kwa sababu siku ile aliing’ang'ania sana.Nakumbuka kuna CD alizichukua hapo nadhani na hiyo nayo ilikuwapo.”Akasema Vero
Patrick akalifunga kabati ,akaelekea katika friji akafungua na kujimimia Juice katika glasi .Vero alikuwa ameketi sofani akitazama Luninga.
“ Patrick ,Miss Tanzania mwaka huu itakuwa na ushindani mkubwa sana kwa sababu mabinti ni warembo kupita maelezo.Mhh………..”
Akasema Vero huku amekodoa macho yake katika Luninga kubwa iliyokuwamo humo sebuleni.
“kwani fainali za miss Tanzania ni lini?”Patrick akauliza
“Ni jumamosi ijayo na itafanyikia pale Diamond Jubilee.Kutapambwa na onyesho kali la Malaika band,vile vile wana Fm academia na wasanii wengine kibao watakuwepo.Nataka kesho nikakate tiketi zetu za V.I P ili tusikose nafasi siku hiyo”Alisema Vero
Akiwa na juice yake mkononi Patrick akajisogeza taratibu kuelekea mahali alipokaa Veronika .Kabla hajafika sofani alisimama akapiga funda la juice kisha akaelekeza macho yake katika luninga
“Naitwa Neema ni mrembo toka kanda ya kaskazini.Ni miss Arusha.Napendelea sana muziki wa dini,kusoma na michezo mbali mbali.Nategemea kuwa mwanamitindo wa kimataifa.Iwapo nitachaguliwa kuwa miss Tanzania nitajikita zaidi katika kuwasaidia watoto yatima kwani naelewa mateso na machungu wanayoyapata kwa kutokuwa na wazazi wao.Naombeni kura zenu namba yangu ya ushiriki ni ishirini.”Alikuwa ni mrembo wa Arusha akijinadi katika kipindi maalum cha kuwatambulisha washiriki wa kinyang’anyiro cha kumsaka mrembo wa Tanzania kilichorushwa moja kwa moja na televisheni ya Taifa.
“Du! Si mchezo”Aliguna Patrick huku akiisogelea zaidi Luninga
“nimekwambia Patrick warembo wa mwaka huu si mchezo .Hebu kaa uangalie jinsi watoto walivyo wazuri ”Akasema Vero
“Naitwa Happy kibaho.Ni mrembo wa wilaya ya Ilala .Napendelea sana muziki laini,kusoma hadithi ,magazeti,kutazama luninga,na wanyama.Nategemea kuwa mwanasheria.Iwapo nitachaguliwa kuwa miss Tanzania nitaelekeza nguvu zangu zote katika kuwasadia vijana wajasiria mali ikiwa ni pamoja na kuwatafutia wafadhili,nitaitumia kofia yangu kuiomba serikali ielekeze nguvu zake zaidi katika kuwasaidia vijana hawa katika kuwapatia mitaji na kuwatafutia masoko ya bidhaa zao wanazozizalisha ili kupambana na ongezeko la vijana wasiokuwa na ajira.Ninaomba kura zenu ili niweze kulitwaa taji hili la miss Tanzania kwani nina vigezo vyote vya kulitwaa taji hili .Namba yangu ya ushiriki ni 6.”
“Whaaaat!!!!!!!!!!!!!!........................”Patrick Akapiga ukelele mkubwa
“Nooooooooooo!!!!!!!!..I cant bel……………………”ghafla glasi aliyoishika ikamponyoka ikaanguka na kuvunjika .Taratibu nguvu zikaanza kumwishia akadondokea sofani kisha akapoteza fahamu.
“Patrick ,Patrick what’s wrong....!!!!!!!!!!!...”
Alihamaki Veronika huku akimsogelea Patrick pale sofani na kumtingisha.
“Patrick darling what’s wrong with you?
Alizidi kuuliza Vero huku akimtingisha.
“Ooh ! Nooo...!!!!...Wake up Patrick”Alipiga ukelele baada ya kugundua kuwa Patrick hakuwa na fahamu.Vero akataharuki asijue afanye nini.Hakukuwa na mtu yoyote wa karibu ambaye angeweza kumsaidia .Alitoka kutaka kwenda kuwaita majirani ,akafika mlangoni na kurudi tena ndani mpaka sofani alipolala Patrick.
“Patrick ! Patrick dear what’s wrong with you.Whats’s wrong Patrick!!!!!!!!!”Vero aliongea peke yake huku machozi yakimtiririka.Pale pale akapata wazo la kumpeleka Patrick hospitali.Kwa nguvu zake zote akamuinua Patrick na kumpakia garini ,akakimbia kufungua geti kisha akaingia garini na kuondoka kwa kasi ya ajabu pasi na kufunga mlango wowote wa nyumba.Kwa kasi ya ajabu Vero aliendesha gari hadi hospitali ya karibu maarufu kama Dr Heneriko hospital.Si mbali sana na makazi ya Patrick.Huku akilia akapaki gari na kuingia ndani ,akawaomba msaada wauguzi .Haraka haraka wauguzi wakamchukua Patrick na kumuwahisha katika chumba maalum kwa ajili ya kumpatia huduma ya haraka.
“Hurry up !.hurry up.! Ooh Patrick what’s wrong with you?”Alilalamika Vero huku akiwaomba manesi waharakishe.Muda wote huo machozi hayakumkauka.
Veronika alizuiliwa asiingie katika chumba cha huduma ya kwanza akaachwa hapo nje na mmoja kati ya manesi akiendelea kumfariji.
“Jipe moyo dada yangu Patrick atapona tu.Mtumaini Mungu.”Nesi yule alimbembeleza Vero kwa upole.
Dakika kama 20 hivi baadae dokta Heneriko alimwita Vero ofisini kwake na kumuomba awe mvumilivu wakati wakiendelea kuishughulikia hali ya Patrick.Dokta alitaka kufahamu nini hasa kilichopelekea Patrick kupoteza fahamu.
“Unajua dokta ,Patrick ni mpenzi wangu na tuko katika maandalizi ya harusi yetu.Mimi siishi naye kwa sasa ila huja kwake kila mwisho wa wiki .Leo hii toka asubuhi alikuwa akilalamika kuwa alihisi uchovu mwingi .Tulitoka kidogo kisha tukarudi na akaendelea kupumzika.Usiku tukiwa sebuleni tukiangalia Tv nikaona mwenzangu akipiga ukelele akaishiwa nguvu na kuangukia sofani akapoteza fahamu.kwa kweli sina hakika mpaka sasa ni kitu gani hasa kilichopelekea hali ile kutokea.Naomba Dokta ufanye kila linalowezekana ili Patrick apone.Niko tayari kutoa kiasi chochote cha pesa ili mradi apone.”
Vero alishindwa kujizuia akaangua kilio.
“Nyamaza Vero,Hali ya Patrick inaendelea vizuri. nina hakika muda si mrefu atazinduka.Kwa hiyo yawezekana kuwa kuna habari yoyote aliyoitazama ambayo ilimpelekea Patrick kupata mstuko ?
“Sidhani dokta kwa sababu wakati tunaangalia Tv hakukuwa na taarifa yoyote ya kutisha au kustusha inayoweza kupelekea mtu kupata mstuko hadi kupoteza fahamu.Tulikuwa tukiangalia washiriki wa miss Tanzania wakijinadi.Ni hilo tu”Vero akajibu
Dokta Heneriko akanyamaza kimya kwa sekunde kadhaa kisha akasema
“Kwa kumbukumbu zako toka umekuwa naye kuna siku yoyote tukio kama hili limewahi kumtokea zaidi ya leo?
“Hapana dokta tangu mimi nimekuwa naye halijawahi tokea tukio kama hili Patrick kupoteza fahamu.”
“Ok Vero hivi sasa waweza kwenda kupumzika na kutuacha sisi tuendelee kumuhudumia mgonjwa wako.Iwapo kutakuwa na mabadiliko yoyote tutakupigia simu kukutaarifu.Na kama itahijika kumuhamisha kumpeleka katika hospitali kubwa zaidi tutakutaarifu pia.Lakini kwa sasa hali yake inaendelea vizuri,mapigo ya moyo wake yako sawa na kila kitu kinaonekana kufanya kazi vizuri.Huu ulikuwa ni mstuko wa kawaida tu ambao unaweza kumtokea mtu yeyote na hasa akiwa na msongo wa mawazo.”Akasema Doctor Henry.
“No Dokta ,siwezi kwenda nyumbani bila kujua hali ya mpenzi wangu iko vipi.Nitalala hapa hapa .Nataka niwe wa kwanza kuniona pindi atakapofumbua macho.Samahani dokta naweza kuitumia simu yako kuongea na mama yangu na kumtaarifu juu ya ugonjwa wa Patrick”
Dokta Heneriko hakuwa na kipingamizi akamruhusu Vero aitumie simu yake.
Vero akampigia simu mama yake na kumtaarifu juu ya tukio lile ,halafu akawapigia simu ndugu zake wote bila kumsahau Andrew rafiki mkubwa wa Patrick pamoja na Alois kaka yake Patrick.Wazazi wa Patrick walikuwa safarini nje ya nchi.
* * * *
Ilimchukua kama nusu saa toka Andrew apate taarifa ya ugonjwa wa patrick,kuwasili pale hospitali.Akiwa na mpenzi wake Vick walishuka garini na kukimbia kuelekea mapokezi.Mara tu baada ya kuingia hapo mapokezi walilakiwa na sura yenye kusawajika ya Vero.Alipowaona Andrew na Vick wakiingia humo hospitali Vero aliangua kilio ambacho kiliwachanganya zaidi Andrew na Vick.
“Where is Patrick??”Andrew akauliza huku akijikaza lakini ni wazi alikuwa akitetemeka
“Calm down Vero tuambie Patrick yuko wapi?”Aliuliza tena Andrew .Vick akamkumbatia Vero huku naye machozi yakimtoka.
Andrew alimfuata muuguzi aliyekuwa mapokezi na kumuuliza juu ya hali ya Patrick.Hakuridhika na jibu alilolipata ,kwa kasi akakimbia hadi katika ofisi ya Dokta Heneriko lakini hakumkuta.Taratibu akatoka humo ofisini jasho likimtiririka na kurudi mapokezi.Tayari Alois kaka yake Patrick alikwisha wasili hapo hospitali akiwa ameongozana na mke wake nao wote waliungana na Vick katika kumbembeleza Vero.
Andrew akawasalimia kisha akamvuta mkono alois wakasogea pembeni kidogo.
“Hebu niambie Andrew kitu gani kinachoendelea hapa na Patrick yuko wapi ?Aliuliza Alois huku naye jasho likimtiririka
“Brother Aloia hata mimi mpaka muda huu sielewe chochote kwani toka nimefika hapa muda mfupi uliopita sijaweza kuongea lolote na Vero.Ila kwa maelezo niliyoyapata toka kwa muuguzi ni kwamba Patrick yuko katika chumba cha huduma ya kwanza akipatiwa matibabu.Nasikia ni mstuko ndio uliopelekea akapoteza fahamu”
Mara dokta Heneriko akatokea.Muuguzi aliyekuwapo mapokezi akamtambulisha kwa akina Andrew.
“Dokta hawa ni ndugu zake Patrick wamefika sasa hivi na walitaka kupata taarifa juu ya maendeleo ya mgonjwa wao’
Dr henry akawasalimu wote halafu akawaomba Alois na Andrew wamfuate ofisini kwake..
“Vijana wangu kwanza poleni sana kwa matatizo ‘
“Ahsante sana dokta tumeshapoa”Wakajibu kwa pamoja
“sasa vijana wangu nimewaiteni hapa ili tuongelee zaidi suala la ndugu yenu..Patrick aliletwa hapa kwangu usiku huu akiwa amepoteza fahamu.Kwa haraka nikisaidiana na madokta wenzangu tumejitahidi kumpatia huduma ya kwanza na mpaka sasa maendeleo yake ni mazuri.Tumejitahidi kuyashusha mapigo ya moyo yaliyokuwa juu sana na kwa sasa yako kawaida.Taratibu anaanza kurejewa na fahamu zake ingawa bado anahitaji kupumzika zaidi kwani bado fahamu hazijarejea vizuri.Maendeleo yake ni mazuri na baada ya muda mfupi ujao basi atarejea na fahamu zake zote.”
Alois akashusha pumzi nzito kwa kusikia taarifa ile ya dokta.Akatoa leso na kujifuta jasho lililokuwa likimtirirka kwa kasi muda huo.
“Thanks God”Alisema Alois huku ameinua mikono juu ishara ya kumshukuru Mungu
“kwa hivi sasa bado ataendelea kuwapo katika uangalizi maalum mpaka hapo hali yake itakapokuwa nzuri kabisa.Tatizo lililompata ni mstuko wa moyo.Ni tatizo la kawaida kutokea.Ila hali yake itakapokuwa nzuri tutamshauri aonane na daktari bingwa wa magonjwa ya moyo ili aweze kumfanyia uchunguzi zaidi katika moyo wake ”
Baada ya kupata maelezo ya kutosha toka kwa dokta,Alois na andrew waliridhika kabisa na dokta akawashauri waende kupumzika mpaka kesho .Alois alikubaliana na wazo hilo lakini akashauri andrew awarudishe kwanza Vero na Vick nyumbani wakapumzike.Yeye atabaki pale kuangalia hali ya Patrick inavyokwenda.
Wakati wakiendelea kujadili mama yake Vero akatokea.Akawasalimu wote aliowakuta hapo kisha kwa wasiwasi akataka kujua juu ya hali ya Patrick.Alipewa maelezo mafupi ya hali ya mgonjwa halafu akaomba aonane na dokta Heneriko,akaongea naye na kupewa kwa muhtasari juu ya hali ya Patrick na maendeleo yake na akahakikishiwa uangalizi wa hali ya juu.
“Ok . sasa utaratibu gani unaoendelea hapa? Aliuliza Bi stella Rugi mama yake na Vero.
“Tumepanga kuwa Andrew awarudishe nyumbani Vero na vick wakapumzike ,mimi nitaendelea kubaki hapa hapa na kufuatilia hali ya mgonjwa”Akasema alois
“Vizuri ,basi msipate shida ,Vero na Vick nitaondoka nao mimi na kwenda nao nyumbani kwangu , Andrew nenda nyumbani kwa Patrick ukahakikishe kuko salama .Alois utaendelea kubaki hapa kumwangalia mgonjwa .Nitakuwa nakupigia simu mara kwa mara ili kujua maendeleo ya mgonjwa ." akasema mama yake Vero
“sawa mama tumekuelewa .”Andrew na alois waliitika kisha wote wakatawanyika na kumwacha Alois hapo hospitali
Saa saba usiku Patrick akarejewa na fahamu zake kamili.Kitu cha kwanza kuhisi ni harufu kali ya dawa akageuza shingo kutazama pande zote akatambua kuwa pale alikuwa hospitali.Taratibu akavuta kumbukumbu za nyuma na mara akakumbuka kitu kilichopelekea yeye kuwepo pale.
“I saw her. I real saw her. she’s alive” Alijikuta akitamka maneno haya huku jasho likikimtiririka na mapigo yake ya moyo kwenda kasi .
Muuguzi aliyekuwa akimuangalia aliingia ndani na kumkuta tayari Patrick amerejewa na fahamu na amekaa kitandani.Haraka akaenda kumwita daktari.Dk heneriko alikuja kwa kasi na kumpima akagundua kuwa bado mapigo ya moyo wa Patrick yalikuwa juu sana.
“‘Lazima kuna kitu kinamsumbua huyu si bure”Akawaza dokta Heneriko.
“Patrick “Dokta akamwita baada ya kumaliza kumfanyia vipimo.
“naam dokta”Aliitika Patrick kwa sauti yenye kukwaruza.
“Pole sana “
“Ahsante sana dokta”
“Patrick kijana wangu usijali utapona tu hali yako inaendelea vizuri .Unahitaji kupumzika sasa mpaka asubuhi tutakapochukua tena vipimo vingine”
“Sawa dokta.” akajibu Patrick
“Endelea pumzika Patrick na iwapo utahitaji kitu chochote muuguzi yuko hapo nje na atakuwa akija hapa mara kwa mara kukuangalia.Tena nimekumbuka kaka yako yuko nje muda sijui kama ungependa kumwona?”Akasema dokta heneriko.
“Ndiyo dokta naomba uniitie..”
Dokta Heneriko akafungua mlango na kutoka.
Alois alikuwa amesinzia katika sofa lililoko mapokezi Mara akastuliwa na sauti ya Dokta Heneriko.
“Alois ,Patrick amekwisha rejewa na fahamu zake kamili kwa hiyo unaweza kwenda kumwona.Ila tafadhali usijaribu kumuuliza chochote kuhusiana na kilichopelekea yeye kupoteza fahamu.Ongea naye maongezi mengine ya kawaida.sawa?”
“sawa dokta”Alijibu Patrick huku akifikicha macho yaliyojaa usingizi.Muuguzi aliyekuwepo mapokezi akampeleka hadi katika chumba alimolazwa Patrick.
“Vipi Patrick unajisikiaje kwa sasa?Akasema Alois
“Sasa hivi sijambo brother najisikia vizuri.nashukuru kwa kuja kuniona”
“Usijali Patrick kwa sasa endelea kupumzika.bado unahitaji mapumziko ya kutosha.Mimi niko hapo nje.i”
“Vero yuko wapi?” Akauliza Patrick
" Vero amechukuliwa na mama yake.Andrew amekwenda nyumbani kwako kuhakikisha kuko salama" akasema Alois.
" Naomba umpigie simu na umwambie kwamba niko salama,asiwe na mawazo" akasema Patrick
" Sawa Patrick ngoja nimfahamishe" akasema Alois
TUKUTANE SEHEMU IJAYO..........................
SEHEMU YA 1
MTUNZI : PATRICK.CK
“Patrick amka darling inakaribia saa nne sasa”Alisema Veronika kwa sauti laini ya kubembeleza.
“‘Mmmmhhh”Akaguna Patrick ,akajigeuza upande wa pili na kulivuta zaidi shuka.
“Amka ukaoge”Alizidi kubembeleza Veronika.Kwa uvivu Patrick akaamka na kuelekea bafuni kuoga.Dakika chache baadae alitoka akiwa amechangamka.
"Kweli maji ni dawa nzuri ya uchovu.Sasa najisikia safi kabisa.Nadhani kwa sasa itabidi nipunguze muda wa kufanya kazi .Nimekuwa nikifanya kazi kwa masaa mengi sana kwa siku kiasi kwamba nakosa hata muda wa kupumzika.Naogopa tukija kuoana nisije kushindwa kutimiza majukumu yangu kama mume kwa sababu ya uchovu” akasema Patrick na kumfanya Vero atabasamu halafu akatoa kicheko cha chini chini na kusema
“Kweli mpenzi jitahidi kwa sasa kupata muda wa kutosha wa kupumzika.”
“Nitajitahidi baby”
Baada ya kuhakikisha sasa yuko safi Vero akamshika mkono Patrick na kumpeleka sebuleni kupata stafstahi.
“Patrick dear nataka unisindikize Supermarket nikafanye manunuzi ya vitu vya ndani .Si unajua kesho Andrew na vicktoria wameahidi kututembelea”Akasema Veronika wakati wakiendelea kupata chai.
“Mhh ! Vero nenda mwenyewe mimi niache nipumzike ”Patrick akajibu
“jamani dear usifanye hivyo naomba unisindikize ,mimi naona uvivu kwenda peke yangu”
‘haya mama ,tumalize chai twende ili tuwahi kurudi”
“Nashukuru dear”
Katika vitu ambavyo Veronika alibarikiwa kuwa navyo ni uwezo wake mkubwa wa kushawishi.
* * * *
Veronika Rugi alikuwa ni msichana mrembo mwenye mvuto wa aina yake.Binti huyu licha ya kujaliwa kichwa kizuri chenye nywele laini ,nyingi na ndefu ,alikuwa na uso mpana wa mviringo ulionakshiwa na macho mapana yenye kurembua muda wote.Midomo mizuri ,laini ambayo akikupiga busu hutatamani abanduke mdomoni .Mtoto huyu alijaliwa shingo murua ambayo iliungana na kiwiliwili kilichokuwa na kifua chenye kupendeza kilichobeba chuchu changa zenye kusisimua,zenye kuwatoa udenda wakware.Kimwana huyu mwenye uzuri usiopimika alijaliwa umbo la utatanishi kuanzia kiunoni kushuka chini.Ni wasichana wachache sana waliopewa upendeleo wa namna hii na manani..
Pamoja na sifa hizo zote za nje lakini bado alikuwa na sifa lukuki za ndani.Kikubwa zaidi kinachomfanya apendwe na kila mtu ni uwezo wake mkubwa wa kuelewa mambo.Ni binti mwenye roho nzuri ya huruma na upendo asiyependa kujivuna wala kujikweza licha ya uwezo mkubwa familia yake ilionao.Ni binti mwenye heshima kwa watu wa rika zote ,mcheshi,asiyependa ubinafsi na zaidi ya yote ni mtu anayejua kupenda.
Veronika ambaye bado anaishi na mama yake mzazi baada ya baba yake kufariki miaka kadhaa iliyopita ,alikuwa ni mtoto wa tatu na wa mwisho katika familia ambayo haikubahatika kuwa na mtoto wa kiume.Dada mkubwa wa Veronika aliyeitwa Loniki hivi sasa anafanya kazi katika shirika la ndege la British airways ,ameolewa na anaishi nchini Uingereza.Mtoto wa pili kuzaliwa katika familia hii ni binti mrembo sana Sarah ambaye aliwahi kushika nafasi ya tatu katika kinyang’anyiro cha kumsaka mrembo wa taifa.naye amekwishaolewa na ni afisa mahusiano wa benki moja mpya kabisa nchini iitwayo African meckat bank.Mtoto wa tatu na wa mwisho ni Veronika ambaye bado hajaolewa ,ila alikuwa katika hatua za mwisho za kukamilisha maandalizi ya ndoa yake na mchumba wake Patrick.Ni hivi karibuni tu amehitimu shahada yake ya kwanza ya biashara katika chuo kikuu cha dar es salaam.Yeye ndiye msimamizi mkuu wa miradi yote ya familia kwa sasa.
* * *
“Patrick mpenzi nilisahau kukwambia toka mapema kuwa dada Loniki alifurahi sana kusikia tunataka tukafanye shopping ya harusi yetu nchini Uingrereza.Ameahidi kuwa yeye na mumewe watagharamia safari nzima ya kwenda na kurudi na gharama zote za manunuzi.Amesisitiza kuwa tusitumie hata shilingi yetu.Kwa maana hiyo wiki hii nataka niende tena kufuatilia yale maombi yetu ya viza pale ubalozini.Nadhani kama Mungu akijaalia basi ndani ya wiki mbili zijazo tutakuwa tumeshakamilisha taratibu zote zinazotakiwa.” Alisema Vero huku akijiegemeza karibu zaidi na kifua cha Patrick.Muda huo ilipata saa mbili za usiku , bado walikuwa wakipunga hewa safi baada ya mlo wa jioni.
“Wow! Hongera sana Vero kwa kuwa na ndugu wakarimu na wenye upendo wa hali ya juu sana kama ulivyo wewe.Tena umeongea kuhusu Loniki nimekumbuka zile CD alizonitumia wiki iliyopita.Unajua sijatazama hata moja.Hebu twende ndani nikaitazame ile filamu mpya ya Jack bauer.”
Akasema Patrick huku akijiinua toka pale walipokuwa wameketi na kuelekea sebuleni .Vero naye akakusanya vitu vyote vilivyokuwapo chini naye akaingia ndani.
“Vero mbona ile CD ya Jack bauer siioni hapa au Andrew aliichukua?Akauliza Patrick baada ya kuitafuta CD ile bila kuiona.
“Yawezekana Andrew aliichukua kwa sababu siku ile aliing’ang'ania sana.Nakumbuka kuna CD alizichukua hapo nadhani na hiyo nayo ilikuwapo.”Akasema Vero
Patrick akalifunga kabati ,akaelekea katika friji akafungua na kujimimia Juice katika glasi .Vero alikuwa ameketi sofani akitazama Luninga.
“ Patrick ,Miss Tanzania mwaka huu itakuwa na ushindani mkubwa sana kwa sababu mabinti ni warembo kupita maelezo.Mhh………..”
Akasema Vero huku amekodoa macho yake katika Luninga kubwa iliyokuwamo humo sebuleni.
“kwani fainali za miss Tanzania ni lini?”Patrick akauliza
“Ni jumamosi ijayo na itafanyikia pale Diamond Jubilee.Kutapambwa na onyesho kali la Malaika band,vile vile wana Fm academia na wasanii wengine kibao watakuwepo.Nataka kesho nikakate tiketi zetu za V.I P ili tusikose nafasi siku hiyo”Alisema Vero
Akiwa na juice yake mkononi Patrick akajisogeza taratibu kuelekea mahali alipokaa Veronika .Kabla hajafika sofani alisimama akapiga funda la juice kisha akaelekeza macho yake katika luninga
“Naitwa Neema ni mrembo toka kanda ya kaskazini.Ni miss Arusha.Napendelea sana muziki wa dini,kusoma na michezo mbali mbali.Nategemea kuwa mwanamitindo wa kimataifa.Iwapo nitachaguliwa kuwa miss Tanzania nitajikita zaidi katika kuwasaidia watoto yatima kwani naelewa mateso na machungu wanayoyapata kwa kutokuwa na wazazi wao.Naombeni kura zenu namba yangu ya ushiriki ni ishirini.”Alikuwa ni mrembo wa Arusha akijinadi katika kipindi maalum cha kuwatambulisha washiriki wa kinyang’anyiro cha kumsaka mrembo wa Tanzania kilichorushwa moja kwa moja na televisheni ya Taifa.
“Du! Si mchezo”Aliguna Patrick huku akiisogelea zaidi Luninga
“nimekwambia Patrick warembo wa mwaka huu si mchezo .Hebu kaa uangalie jinsi watoto walivyo wazuri ”Akasema Vero
“Naitwa Happy kibaho.Ni mrembo wa wilaya ya Ilala .Napendelea sana muziki laini,kusoma hadithi ,magazeti,kutazama luninga,na wanyama.Nategemea kuwa mwanasheria.Iwapo nitachaguliwa kuwa miss Tanzania nitaelekeza nguvu zangu zote katika kuwasadia vijana wajasiria mali ikiwa ni pamoja na kuwatafutia wafadhili,nitaitumia kofia yangu kuiomba serikali ielekeze nguvu zake zaidi katika kuwasaidia vijana hawa katika kuwapatia mitaji na kuwatafutia masoko ya bidhaa zao wanazozizalisha ili kupambana na ongezeko la vijana wasiokuwa na ajira.Ninaomba kura zenu ili niweze kulitwaa taji hili la miss Tanzania kwani nina vigezo vyote vya kulitwaa taji hili .Namba yangu ya ushiriki ni 6.”
“Whaaaat!!!!!!!!!!!!!!........................”Patrick Akapiga ukelele mkubwa
“Nooooooooooo!!!!!!!!..I cant bel……………………”ghafla glasi aliyoishika ikamponyoka ikaanguka na kuvunjika .Taratibu nguvu zikaanza kumwishia akadondokea sofani kisha akapoteza fahamu.
“Patrick ,Patrick what’s wrong....!!!!!!!!!!!...”
Alihamaki Veronika huku akimsogelea Patrick pale sofani na kumtingisha.
“Patrick darling what’s wrong with you?
Alizidi kuuliza Vero huku akimtingisha.
“Ooh ! Nooo...!!!!...Wake up Patrick”Alipiga ukelele baada ya kugundua kuwa Patrick hakuwa na fahamu.Vero akataharuki asijue afanye nini.Hakukuwa na mtu yoyote wa karibu ambaye angeweza kumsaidia .Alitoka kutaka kwenda kuwaita majirani ,akafika mlangoni na kurudi tena ndani mpaka sofani alipolala Patrick.
“Patrick ! Patrick dear what’s wrong with you.Whats’s wrong Patrick!!!!!!!!!”Vero aliongea peke yake huku machozi yakimtiririka.Pale pale akapata wazo la kumpeleka Patrick hospitali.Kwa nguvu zake zote akamuinua Patrick na kumpakia garini ,akakimbia kufungua geti kisha akaingia garini na kuondoka kwa kasi ya ajabu pasi na kufunga mlango wowote wa nyumba.Kwa kasi ya ajabu Vero aliendesha gari hadi hospitali ya karibu maarufu kama Dr Heneriko hospital.Si mbali sana na makazi ya Patrick.Huku akilia akapaki gari na kuingia ndani ,akawaomba msaada wauguzi .Haraka haraka wauguzi wakamchukua Patrick na kumuwahisha katika chumba maalum kwa ajili ya kumpatia huduma ya haraka.
“Hurry up !.hurry up.! Ooh Patrick what’s wrong with you?”Alilalamika Vero huku akiwaomba manesi waharakishe.Muda wote huo machozi hayakumkauka.
Veronika alizuiliwa asiingie katika chumba cha huduma ya kwanza akaachwa hapo nje na mmoja kati ya manesi akiendelea kumfariji.
“Jipe moyo dada yangu Patrick atapona tu.Mtumaini Mungu.”Nesi yule alimbembeleza Vero kwa upole.
Dakika kama 20 hivi baadae dokta Heneriko alimwita Vero ofisini kwake na kumuomba awe mvumilivu wakati wakiendelea kuishughulikia hali ya Patrick.Dokta alitaka kufahamu nini hasa kilichopelekea Patrick kupoteza fahamu.
“Unajua dokta ,Patrick ni mpenzi wangu na tuko katika maandalizi ya harusi yetu.Mimi siishi naye kwa sasa ila huja kwake kila mwisho wa wiki .Leo hii toka asubuhi alikuwa akilalamika kuwa alihisi uchovu mwingi .Tulitoka kidogo kisha tukarudi na akaendelea kupumzika.Usiku tukiwa sebuleni tukiangalia Tv nikaona mwenzangu akipiga ukelele akaishiwa nguvu na kuangukia sofani akapoteza fahamu.kwa kweli sina hakika mpaka sasa ni kitu gani hasa kilichopelekea hali ile kutokea.Naomba Dokta ufanye kila linalowezekana ili Patrick apone.Niko tayari kutoa kiasi chochote cha pesa ili mradi apone.”
Vero alishindwa kujizuia akaangua kilio.
“Nyamaza Vero,Hali ya Patrick inaendelea vizuri. nina hakika muda si mrefu atazinduka.Kwa hiyo yawezekana kuwa kuna habari yoyote aliyoitazama ambayo ilimpelekea Patrick kupata mstuko ?
“Sidhani dokta kwa sababu wakati tunaangalia Tv hakukuwa na taarifa yoyote ya kutisha au kustusha inayoweza kupelekea mtu kupata mstuko hadi kupoteza fahamu.Tulikuwa tukiangalia washiriki wa miss Tanzania wakijinadi.Ni hilo tu”Vero akajibu
Dokta Heneriko akanyamaza kimya kwa sekunde kadhaa kisha akasema
“Kwa kumbukumbu zako toka umekuwa naye kuna siku yoyote tukio kama hili limewahi kumtokea zaidi ya leo?
“Hapana dokta tangu mimi nimekuwa naye halijawahi tokea tukio kama hili Patrick kupoteza fahamu.”
“Ok Vero hivi sasa waweza kwenda kupumzika na kutuacha sisi tuendelee kumuhudumia mgonjwa wako.Iwapo kutakuwa na mabadiliko yoyote tutakupigia simu kukutaarifu.Na kama itahijika kumuhamisha kumpeleka katika hospitali kubwa zaidi tutakutaarifu pia.Lakini kwa sasa hali yake inaendelea vizuri,mapigo ya moyo wake yako sawa na kila kitu kinaonekana kufanya kazi vizuri.Huu ulikuwa ni mstuko wa kawaida tu ambao unaweza kumtokea mtu yeyote na hasa akiwa na msongo wa mawazo.”Akasema Doctor Henry.
“No Dokta ,siwezi kwenda nyumbani bila kujua hali ya mpenzi wangu iko vipi.Nitalala hapa hapa .Nataka niwe wa kwanza kuniona pindi atakapofumbua macho.Samahani dokta naweza kuitumia simu yako kuongea na mama yangu na kumtaarifu juu ya ugonjwa wa Patrick”
Dokta Heneriko hakuwa na kipingamizi akamruhusu Vero aitumie simu yake.
Vero akampigia simu mama yake na kumtaarifu juu ya tukio lile ,halafu akawapigia simu ndugu zake wote bila kumsahau Andrew rafiki mkubwa wa Patrick pamoja na Alois kaka yake Patrick.Wazazi wa Patrick walikuwa safarini nje ya nchi.
* * * *
Ilimchukua kama nusu saa toka Andrew apate taarifa ya ugonjwa wa patrick,kuwasili pale hospitali.Akiwa na mpenzi wake Vick walishuka garini na kukimbia kuelekea mapokezi.Mara tu baada ya kuingia hapo mapokezi walilakiwa na sura yenye kusawajika ya Vero.Alipowaona Andrew na Vick wakiingia humo hospitali Vero aliangua kilio ambacho kiliwachanganya zaidi Andrew na Vick.
“Where is Patrick??”Andrew akauliza huku akijikaza lakini ni wazi alikuwa akitetemeka
“Calm down Vero tuambie Patrick yuko wapi?”Aliuliza tena Andrew .Vick akamkumbatia Vero huku naye machozi yakimtoka.
Andrew alimfuata muuguzi aliyekuwa mapokezi na kumuuliza juu ya hali ya Patrick.Hakuridhika na jibu alilolipata ,kwa kasi akakimbia hadi katika ofisi ya Dokta Heneriko lakini hakumkuta.Taratibu akatoka humo ofisini jasho likimtiririka na kurudi mapokezi.Tayari Alois kaka yake Patrick alikwisha wasili hapo hospitali akiwa ameongozana na mke wake nao wote waliungana na Vick katika kumbembeleza Vero.
Andrew akawasalimia kisha akamvuta mkono alois wakasogea pembeni kidogo.
“Hebu niambie Andrew kitu gani kinachoendelea hapa na Patrick yuko wapi ?Aliuliza Alois huku naye jasho likimtiririka
“Brother Aloia hata mimi mpaka muda huu sielewe chochote kwani toka nimefika hapa muda mfupi uliopita sijaweza kuongea lolote na Vero.Ila kwa maelezo niliyoyapata toka kwa muuguzi ni kwamba Patrick yuko katika chumba cha huduma ya kwanza akipatiwa matibabu.Nasikia ni mstuko ndio uliopelekea akapoteza fahamu”
Mara dokta Heneriko akatokea.Muuguzi aliyekuwapo mapokezi akamtambulisha kwa akina Andrew.
“Dokta hawa ni ndugu zake Patrick wamefika sasa hivi na walitaka kupata taarifa juu ya maendeleo ya mgonjwa wao’
Dr henry akawasalimu wote halafu akawaomba Alois na Andrew wamfuate ofisini kwake..
“Vijana wangu kwanza poleni sana kwa matatizo ‘
“Ahsante sana dokta tumeshapoa”Wakajibu kwa pamoja
“sasa vijana wangu nimewaiteni hapa ili tuongelee zaidi suala la ndugu yenu..Patrick aliletwa hapa kwangu usiku huu akiwa amepoteza fahamu.Kwa haraka nikisaidiana na madokta wenzangu tumejitahidi kumpatia huduma ya kwanza na mpaka sasa maendeleo yake ni mazuri.Tumejitahidi kuyashusha mapigo ya moyo yaliyokuwa juu sana na kwa sasa yako kawaida.Taratibu anaanza kurejewa na fahamu zake ingawa bado anahitaji kupumzika zaidi kwani bado fahamu hazijarejea vizuri.Maendeleo yake ni mazuri na baada ya muda mfupi ujao basi atarejea na fahamu zake zote.”
Alois akashusha pumzi nzito kwa kusikia taarifa ile ya dokta.Akatoa leso na kujifuta jasho lililokuwa likimtirirka kwa kasi muda huo.
“Thanks God”Alisema Alois huku ameinua mikono juu ishara ya kumshukuru Mungu
“kwa hivi sasa bado ataendelea kuwapo katika uangalizi maalum mpaka hapo hali yake itakapokuwa nzuri kabisa.Tatizo lililompata ni mstuko wa moyo.Ni tatizo la kawaida kutokea.Ila hali yake itakapokuwa nzuri tutamshauri aonane na daktari bingwa wa magonjwa ya moyo ili aweze kumfanyia uchunguzi zaidi katika moyo wake ”
Baada ya kupata maelezo ya kutosha toka kwa dokta,Alois na andrew waliridhika kabisa na dokta akawashauri waende kupumzika mpaka kesho .Alois alikubaliana na wazo hilo lakini akashauri andrew awarudishe kwanza Vero na Vick nyumbani wakapumzike.Yeye atabaki pale kuangalia hali ya Patrick inavyokwenda.
Wakati wakiendelea kujadili mama yake Vero akatokea.Akawasalimu wote aliowakuta hapo kisha kwa wasiwasi akataka kujua juu ya hali ya Patrick.Alipewa maelezo mafupi ya hali ya mgonjwa halafu akaomba aonane na dokta Heneriko,akaongea naye na kupewa kwa muhtasari juu ya hali ya Patrick na maendeleo yake na akahakikishiwa uangalizi wa hali ya juu.
“Ok . sasa utaratibu gani unaoendelea hapa? Aliuliza Bi stella Rugi mama yake na Vero.
“Tumepanga kuwa Andrew awarudishe nyumbani Vero na vick wakapumzike ,mimi nitaendelea kubaki hapa hapa na kufuatilia hali ya mgonjwa”Akasema alois
“Vizuri ,basi msipate shida ,Vero na Vick nitaondoka nao mimi na kwenda nao nyumbani kwangu , Andrew nenda nyumbani kwa Patrick ukahakikishe kuko salama .Alois utaendelea kubaki hapa kumwangalia mgonjwa .Nitakuwa nakupigia simu mara kwa mara ili kujua maendeleo ya mgonjwa ." akasema mama yake Vero
“sawa mama tumekuelewa .”Andrew na alois waliitika kisha wote wakatawanyika na kumwacha Alois hapo hospitali
Saa saba usiku Patrick akarejewa na fahamu zake kamili.Kitu cha kwanza kuhisi ni harufu kali ya dawa akageuza shingo kutazama pande zote akatambua kuwa pale alikuwa hospitali.Taratibu akavuta kumbukumbu za nyuma na mara akakumbuka kitu kilichopelekea yeye kuwepo pale.
“I saw her. I real saw her. she’s alive” Alijikuta akitamka maneno haya huku jasho likikimtiririka na mapigo yake ya moyo kwenda kasi .
Muuguzi aliyekuwa akimuangalia aliingia ndani na kumkuta tayari Patrick amerejewa na fahamu na amekaa kitandani.Haraka akaenda kumwita daktari.Dk heneriko alikuja kwa kasi na kumpima akagundua kuwa bado mapigo ya moyo wa Patrick yalikuwa juu sana.
“‘Lazima kuna kitu kinamsumbua huyu si bure”Akawaza dokta Heneriko.
“Patrick “Dokta akamwita baada ya kumaliza kumfanyia vipimo.
“naam dokta”Aliitika Patrick kwa sauti yenye kukwaruza.
“Pole sana “
“Ahsante sana dokta”
“Patrick kijana wangu usijali utapona tu hali yako inaendelea vizuri .Unahitaji kupumzika sasa mpaka asubuhi tutakapochukua tena vipimo vingine”
“Sawa dokta.” akajibu Patrick
“Endelea pumzika Patrick na iwapo utahitaji kitu chochote muuguzi yuko hapo nje na atakuwa akija hapa mara kwa mara kukuangalia.Tena nimekumbuka kaka yako yuko nje muda sijui kama ungependa kumwona?”Akasema dokta heneriko.
“Ndiyo dokta naomba uniitie..”
Dokta Heneriko akafungua mlango na kutoka.
Alois alikuwa amesinzia katika sofa lililoko mapokezi Mara akastuliwa na sauti ya Dokta Heneriko.
“Alois ,Patrick amekwisha rejewa na fahamu zake kamili kwa hiyo unaweza kwenda kumwona.Ila tafadhali usijaribu kumuuliza chochote kuhusiana na kilichopelekea yeye kupoteza fahamu.Ongea naye maongezi mengine ya kawaida.sawa?”
“sawa dokta”Alijibu Patrick huku akifikicha macho yaliyojaa usingizi.Muuguzi aliyekuwepo mapokezi akampeleka hadi katika chumba alimolazwa Patrick.
“Vipi Patrick unajisikiaje kwa sasa?Akasema Alois
“Sasa hivi sijambo brother najisikia vizuri.nashukuru kwa kuja kuniona”
“Usijali Patrick kwa sasa endelea kupumzika.bado unahitaji mapumziko ya kutosha.Mimi niko hapo nje.i”
“Vero yuko wapi?” Akauliza Patrick
" Vero amechukuliwa na mama yake.Andrew amekwenda nyumbani kwako kuhakikisha kuko salama" akasema Alois.
" Naomba umpigie simu na umwambie kwamba niko salama,asiwe na mawazo" akasema Patrick
" Sawa Patrick ngoja nimfahamishe" akasema Alois
TUKUTANE SEHEMU IJAYO..........................