Simulizi: "Angamizo"

Xav Emmanuel

JF-Expert Member
Jul 12, 2018
214
315
SIMULIZI: “ANGAMIZO” (01)
MTUNZI: XAVERY LUOGA (Starxav)
Email: xavemmanuel12@gmail.com
Namba: 0672493994
----------------------------------------------------- - -

SEHEMU YA KWANZA
Kelele za hapa na pale ziliendelea kusikika katika kila kona ya baa, hakukuwa na usikilizano kati ya sauti za binadamu na sauti za vifaa vya umeme vilivyoendelea kuburudisha mule ndani. Mwenye sauti nyembamba alisikika, nene ilisikika itaachaje sauti ya kukoroma sasa!. Hakukuwa na kiongozi yeyote mwenye kukeleekwa na kelele hizo, na hakuna aliyethubutu kuchukulia hatua suala hilo, kila mtu alikuwa huru na mambo yake.

Mimi nilikaa karibu na mlango wa kuingia na kutoka nje ili iwe rahisi kutoka pindi nimalizapo kinywaji changu.
Sikuwa mlevi wa kupindukia kuogopa kuchafua sare za kazi yangu. Nilipenda sana kazi yangu, kwani inahitaji mtu wa heshima, mtu ambaye hana chembe ya skendo.

Nilikuwa maridadi kuangaza kila kona ya upande kuona kama kuna tukio nzito naweza kulipata ili kesho liangukie katika vichwa vya habari vya magazeti. Niliambulia tu kuona watu wakiingia na kutoka wengine wakishikana mashati na kuachana, wengine wakikumbatiana na kuachana, wengine walitokomea nisikokujua. Kweli baa ni baani...

Zilinichukua takribani dakika saba kusikia vishindo vya wababe wakiingia ndani ya baa hiyo, niliwapokea na kuwasindikiza kwa macho hadi walipokaa. Hakuna alieagiza kitu chochote kile kati yao, zaidi walikuwa wakilaumiana sana, huku mmoja aliyejaa misuli iliyoshiba akikunja sura na kurusha mikono huku na kule kama mtu aliyechoshwa na tabia mbaya za wenzake.
Wanasema “kiburi ni mwanzo wa kifo” hivyo nikaona vyema kuondoka sehemu ile kabla mambo hayajawa mambo: niliogopa kwa ujio wao. Taratibu nikachukua kinywaji changu na kukimiminia mdomoni, nilivyoshusha tayari kilikuwa kimeisha, nikaangaza kopo kwa sekunde kama mbili hivi kwa kukagua kama kweli nilikuwa nimemaliza. Macho yangu yalithibitisha mwisho wa kimiminika kile, mara baada ya kukutana na maandishi tu ya lebo ya kinywaji kile “Fanta”. Nikasoma na kuliacha kopo ilo taratibu na kutoka ndani ya baa ile.

Nikatoka nje na kuangaza kila kona ya baa hiyo. Mikono ilikuwa kiunoni na mdomo ukiwa unaendelea kufuta tamu ya mwisho ya soda niliyotoka kuburudika nayo. Macho yangu yakapambana na bango kubwa la baa hiyo lililopo mbele kabisa jirani na mlango wa kutokea; “La Charz Bar” nilijisomea kimoyomoyo huku nikiangaza kuitafuta njia ya kwenda nyumbani. Nilikuwa sina mwendo wa haraka sababu ya kuwa bado ilikuwa ni mapema.

“Saa mbili kasoro! Aagh! Bado ni mapema mno. Daladala zipo chungu nzima”. Basi niliendelea na mwendo wangu wa maringo kama kinyonga katika mti aupendae.

Kichochoro nilichokuwa napita kilikuwa kimya kiasi na kupisha sauti za pikipiki na magari zikirindima mita chache katika eneo la barabara kuu. Nilisikia tu mihemo ya matairi ya magari hayo katika ngoma za masikio angali bado nipo vichochoroni kuitafuta njia kuu.

Kagiza ambako kanaanza kushonana tayari kalianza kuonesha udhaifu wa mji huu wa Songea, watu wanalala mapema sana. Nikazipiga hatua za haraka haraka kuhofu ukimya wa mtaa huo.
Toka nilipo na baa ilipo, ni umbali mchache sana kutoka eneo kuu la barabara. Nilikua napenda sana kuhudhuria baa hiyo kwani ni moja ya baa kubwa Songea Mjini, hakuna aina ya watu wanaokosekana sehemu hiyo. Kwa kazi yangu ya Mwanahabari ni pahali panapofaa kuchukua matukio ya siku, kwa maana ‘penye miti mingi hapakosi wajenzi’.

Wakati nafanya jitihada za kuchepukia katika barabara kuu, nilipokea onyo la mtetemeko wa kitu kama ndoo hivi likianguka!, “Alaah!!” nikagutuka mwenyewe na kusimama wima. Mlio niliousikia ni ule wa ndoo la takataka ambalo limeanguka. Woga wa mapema ukanikamata.

“Nani kaangusha?!!.., panya, paka..... anha panya.... No!!, mlio ni mkubwa, Mbwa!, Yes! Mbwa” nilianza kuhisi kwa kutaja kitu ambacho kinaweza kuwa na nguvu za kuangusha ndoo hilo lenye uchafu. Hayo yote yaliendelea kuongelewa moyoni.

Nikatoa hatua moja kuelekea mbele lakini nilisikia tena vishindo. Kwa sasa vilikuwa ni vishondo vya binadamu ambao walikuwa kasi kupita maelezo. Na walikuwa nyuma yangu kutokea upande ambao ipo baa niliotoka. Nikahofu kukumbana na vibaka muda ule takatifu, nikasogea pembeni kupata sehemu ya kujibanza. Nikajificha kuwaruhusu kwanza wao wapite.

“Deo! Umeona unavyozungua mwanangu?, Unazingua wewe, unazingua. Mi nakuambia ukweli. Wapi sasa?, wapi unadhani tunampata?” mmoja ya vijana wanne aliongea kwa uchungu kuwageukia wenzake.

Walipofika eneo ambalo nipo karibu nimejificha walisimama kwa mda kupisha malalamiko yachukue nafasi. Nilizikumbuka sura zile vizuri kwani ndizo nilizokutana nazo kule baa. Nikaendelea kujibanza sehemu wasije niunganisha bure katika harakati zao. Jambo jema kulikuwa na mwanga usiolidhisha eneo hilo. Ulikuwa unawaka kwa hafifu sana.

“Sikia mzee!, hana pa kwenda, Yule chapu tu yani paap!. Yule!, Yule haoni! Sema kuna sehemu kajificha tu. Hapa hatuna namna tuvamie kila kona bosi hawezi elewa mzee!.” Mwingine ambaye alikuwa hana mwili wa kutisha aliongea. Ilionekana wanamtafuta mtu ambaye kwa makosa yao amewatoroka. Walipewa kazi ya kumshikilia.

“Daaah! tumefanya kosa sana kutokuwa karibu nae, kwa sasa akiingia mikoni mwangu mimi, hakuna cha bosi, namaliza mchezo, kwa bosi napeleka macho tu kama ushaidi, yaani... alaaaah. Shit!” mwingine ambaye yeye alionekana kupagawa kabisa aliongea.

Huyu wa mwisho alikua na umbo la miraba minne ambalo alitosha kabisa kuingia katika masumbwi na kupigana kwa niaba ya taifa. Umbo lake ni kama huyu baunsa wa rahisi mmoja hivi nchi jirani hapa!.
Nani huyu! Aagh! Ni maharufu sana yani sema basi tu jina lake limenitoka. Jamaa huyo ulikuwa na ghadhabu zilizomfanya kuvua hadi shati na kuegeza begani. Niliendelea kushudia malumbano yao huku wakijongea taratibu sehemu niliyojificha. Wakasimama tena.

“Tusitembee kizembe sasa, tuwe tunaangalie hata huku ukutani, kwa jinsi nilivyo na hasira mwanangu.... Me ntaekutana nae tu mda hu, naosha dadeki!.” Kauli, kauli mzee, chunga kauli yako. Kijana wa kwanza Aliongea kauli mbavu ambayo ilinigusa hasa.

Kwani mimi ni mmoja kati watu ambao nipo maeneo hayo. Kwa vipi wangeniona?. Lakini nashukuru walipita salama. Walikagua eneo lililofuata baada ya nilipojificha mimi Walipita na kuenda zao nikawa nahakikisha tu kwa macho kama wamesongea mbali nami niokoze karoho kangu kepesi kuelekea makwangu..

Nikaanza kujikwamua toka pale nilipo huku mkono wangu ukiambaa kati ya moja ya mfuko wangu wa nyuma kuangalia kifaa chochote ninacho weza tumia kufutia jasho na kamasi. Pumzi ndefu ikafuata kukaribisha kuanza tena hatua mpya.

Nikajipanga kupiga hatua lakini wanasema ‘safari ya kifo haikosi maangaiko’. Pale pale nilipo zilisika pumzi za mtu mwingine, zilikuwa ndefu kipita za kwangu, kama ulishawai angalia kionjo chochote yeyote kile cha mchekeshaji maarufu wa kipindi hicho aitwae “Charles Champline” nadhani unajua kwa jinsi alivyo mwepesi wa mwili; usiombe atimue mbio, aisee mtapotezana.

Nilijisikia mtu ambaye napaswa kutoa kila aina ya haja sio ndogo tu, hadi kubwa. Nikahisi siku hiyo imekuwa mbaya kwangu. Mikosi imeniandama. Wepesi wa mwili wangu haukuwa tatizo kunifanya niweze kutimua mbio mahali pale, nilijikuta ganzi imenishika ghafla na mwili kusisimka. Nikaganda kusubiri hukumu na kuacha moyo uendelee tu kudunduliza mapigo ya mwisho mwisho.

ITENDELEA...
SIMULIZI: “ANGAMIZO” (02)
MTUNZI: XAVERY LUOGA (Starxav)
Email: Xavemmanuel12@gmail.com
Namba: 0672493994
Social Net: @star_xav

Nikaanza kujikwamua toka pale nilipo huku mkono wangu ukiambaa kati ya moja ya mfuko wangu wa nyuma kuangalia kifaa chochote ninacho weza tumia kufutia jasho na kamasi. Pumzi ndefu ikafuata kukaribisha kuanza tena hatua mpya.

Nikajipanga kupiga hatua lakini wanasema ‘safari ya kifo haikosi maangaiko’. Pale pale nilipo zilisika pumzi za mtu mwingine, zilikuwa ndefu kipita za kwangu, kama ulishawai angalia kionjo chochote yeyote kile cha mchekeshaji maarufu wa kipindi hicho aitwae “Charles Champline” nadhani unajua kwa jinsi alivyo mwepesi wa mwili; usiombe atimue mbio, aisee mtapotezana. Nilijisikia mtu ambaye napaswa kutoa kila aina ya haja sio ndogo tu, hadi kubwa. Nikahisi siku hiyo imekuwa mbaya kwangu. Mikosi imeniandama. Wepesi wa mwili wangu haukuwa tatizo kunifanya niweze kutimua mbio mahali pale, nilijikuta ganzi imenishika ghafla na mwili kusisimka. Nikaganda kusubiri hukumu na kuacha moyo uendelee tu kudunduliza mapigo ya mwisho mwisho.

ENDELEA SEHEMU YA PILI

“Kaka... Dada,... ewe mtu uliopo mbele yangu, tafadhali!!!. Tafadhali naomba msaada wako. Mimi mtu mwema tu. Wananitafuta!!, ndugu yangu naomba nitazame mara kwa mara kabla hujaniacha mwenyewe maeneo haya. Sijui hata nilipo ndugu. Nakuomba”. Maneno mageni ya mtu nisiye mfahamu yakagonga kwenye ngoma za masikio yangu. Nikawa tayari kama askari kanzu lindoni. Hofu ya kutambua nani anaongea na mimi ilinijia.

“Inamaana bado hajanijua e!” nilijisemea kwa moyo baada ya kusikia kwa masikio yangu mawili kuwa alikua anabashiri nani yupo karibu yake, maana alianza na dada akamaliza na kaka.

Likaja wazo lingine na kuongeza kwenye mawazo yangu mengine ya mwanzo, wazo hilo jipya ndiyo lilinikumbusha kuwa kweli kuna mtu anatafutwa. Tena anatafutwa haswa!, nimsaidie?, hmmm wakijua?. Nimwache! Afu nikimwacha hii dhambi itakuwa ya nani? Bila shaka ni yangu. Naogopa dhambi kuliko lawama. Nikaamua liwalo na liwe nikageuka.

“Ndugu yangu nipo hapa, nakuomba tafadhali, nakuomba wema wako wa leo tu unanisubiri mimi ili nisipotee. Nakuomba tafadhali....” sauti ya sasa ilikuwa ni ya machozi ambayo inakalibiana na kwikwi ili vitoke kwa pamoja, sikuthubutu kwenda mbele, nikageuka nyuma na kuangaza mtu huyo ambaye ni adimu kwa macho ya watu wanne waliotangulia wakimtafuta.

“We.. we ni nani?” nikahofu kwa kuuliza. Lakini mtu yule hakujubu zaidi ya kupapasa tu ukuta na kujitokeza kando ya giza alipojificha. Mtaa huo ulikuwa na taa chache sana kutokana na nyumba nyingi kutowasha au kutoweka taa kabisa za nje, kwani ukiweka usiku taa basi asubuhi huikuti. Imekwenda na maji.

“Ni mimi kaka!, mi..mi... nakuomba nisaidie nitoke hapa, nitakueleza zaidi huko mbele, nakuomba kaka angu. Usiniuze tena nakuomba?”. Aliongea kwa msisitizo. Inaonekana tulijificha sehemu moja lakini sikumuona. Nikabaki natafakari tu neno lake la usiniuze tena. Ina maana aliuzwa?. Maswali kedekede yakaandama kichwa changu.

“Kukuuza tena?” Nilihoji.

“Ah nisaidie kaka, watanikuta hapa” aliongea tena kwa hisia. Nikaamua kuchukua uamuzi wa kutoa msaada kwake, kwani hata katika sekta niliyopo niliona ni bora kutoa msaada na nisingeweza katu kumwacha mtu huyo akiangaika na kutokomezwa pasipo julikana.

“Aya njoo sogea!” nilitoa amri kuonesha ukali ili kama ulikuwa ni mpango wa kuniangamiza mimi basi apatwe na woga.

Kijana huyo alijitokeza kwa kupapasa tena ukuta kisha kusogea hatua chache na kusimama, aliinua mikono yake kama anamtafuta mtu hivi, dalili zote za kuonesha kwamba ni kipofu zikaonekana. Roho ya huruma ikanivaa na kunishinikiza kudondosha chozi. Lakini nilikomaa.

“Oh pole.. Kwa hapa, ah. Taratibu e!” nikamshika na kumsaidia kutoka pale. Roho iliniuma sana kuona mtu mwenye tatizo kama lile na bado anaangaika. Alikuwa kipofu mtu yule.

Wazo la mwanzo la kupanda daladala likayeyuka. kwani tungeweza kuonwa kwa haraka zaidi na wanao mtafuta. Tukajongea kwa haraka huku hisia na macho yangu zote zikiwa wazi kusikiliza nini kitatokea nikiwa bado barabarani. Uzuri hatukuwa katika sehemu ambayo inatisha sana, kwani kuchepuka tu tukakutana na dereva pikipiki akisubili pesa yake ya kukeshea kilabuni.

“Elfuu na mia tano, tupo wawili, Msamala”. Niliongea vile kwa kutotaka kupoteza muda, kwani nauli ni elfu moja kwa mtu mmoja kwa umbali niliotaja. Pesa niliyotaja haikuwa na mjadala kwa watu wawili kwenye chombo kimoja.
-----------
Nilifika nyumbani na kupokelewa na mke wangu ambaye toka naingia alikuwa ananiangalia tu kama mtu mwenye hasira. Hakujali sana uwepo wa mgeni niliye mbeba siku hiyo. Baada ya kumweka mgeni wangu kwenye kochi, mke wangu alipatwa na hekima ya kunivutia kando kunihoji.

“Mume wangu!, We si hata mwezi tu haujaisha toka tumalize kesi ya kupigana?!, Umepigana tena?”. Aliuliza mke wangu bila kusubiri hata dakika ipite.

“Hhahahahahahahaha..” baaada ya kujibu swali la huzuni kutoka kwa mke wangu nikajikuta nacheka kupita kipimo hadi nikajistukia na kuziba mdomo. Sikutegemea kabisa maneno kama yale. Huzuni yangu ikakimbia mbali na kuruhusu furaha kutoka kwa mke wangu.

“Ebu mwandalie chakula mgeni na maji ya kuoga. Tutaongea!!”, niliagiza huku nikitoa mkono wangu mdomoni baada ya kumaliza kucheka.

Mke wangu alijua nimefanya vurugu mara baada ya kuona shati langu jeupe limetapakaa tandu za buibui na uchafu kila pande. Na huo ulikuwa sio mwonekano wangu wa kila siku, hivyo akapata hofu na kutumia hekima ya kunitoa chemba kumaliza shauku yake. Nikapotezea swali lake na kuelekea nilikomwacha mgeni wangu. Alibaki kunishangaa tu kwa kutikisa kichwa huku mikono yake akishikilia kiuno.

“Pole sana!, unajisikiaje?” nilimuuliza mgeni yule huku nikimtazama kwa makini.

“Ndugu yangu najiskia tu ni katika dunia salama kabisa. Hisia zangu zinaniongoza kukuongezea thawabu zangu zote kwako. Sitaki kufa mimi, sitaki kufa kabisa, sitaki kufa nakuambia! hadi nilichonacho kifike sehemu husika. Baada ya kufika basi nitakufa lakini dunia lazima ijifunze..”. aliongea bila kupepesa maneno hadi nilianza kupagawa kwa kuzitazama hisia za mgeni wangu. Nikataka kujua kila kitu kilichomsibu. Kwa maneno yake hayo machache yalinijulisha kuwa anamengi ya kuhadithia dunia. Nikabaki kuduwaa.

“Kuwa huru! Upo sehemu salama. Kuna tatizo gani kwani? Wanakudai?”. Nilijikakamua kuhoji nipate mkanda kamili.

“Nani!!?, Nani anidai.. Mimi?!, na wananidai nini?, eeh! ndio labla! Labda kweli wananidai!. Nakuomba nisaidie haraka nitue huu mzigo nilionao. Unaniumiza. Unanitesa. Wananidai uhai. Uhai ni wangu lakini wananidai. Wanataka waniue!!” safari hii mgeni wangu alianza kulia kwa nguvu hadi mke wangu aliyekuwa mbali mda wote akitushangaa akasogea.

“Kwani kuna nini baba?” mke wangu akanigeukia na kunitwanga swali lingine ambalo nalo lilipita hewani kama lile la mwanzo bila kujibiwa. Ningejibu nini wakati hata mimi sifahamu chochote?.

“Loh! Pole sana. Tutaelekea polisi kesho kutoa taarifa kwa usalama zaidi!” nilimpa pole mgeni wangu kwa shida iliyompata. Sikuwa na habari na mke wangu, wala kuangaika kujibu swali lake.
“Polisi?, Ndugu yangu umesema Polisi e? Loh! Polisi!, polisi!, polisi!!... Hapana walewale tu. Nimeenda zaidi ya neno nimeenda. Lakini napelekwa kubaya kulekule nilikotoka. Wametapakaa kila sehemu wabaya wangu, hadi kwa viongozi wa dini” mgeni huyo bado aliendelea kunichanganya kwa vitu mbalimbali alivyokuwa anagusia.......

ITAENDELEA..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SIMULIZI: “ANGAMIZO” (02)
MTUNZI: XAVERY LUOGA (Starxav)
Email: Xavemmanuel12@gmail.com
Namba: 0672493994
Social Net: @star_xav

Nikaanza kujikwamua toka pale nilipo huku mkono wangu ukiambaa kati ya moja ya mfuko wangu wa nyuma kuangalia kifaa chochote ninacho weza tumia kufutia jasho na kamasi. Pumzi ndefu ikafuata kukaribisha kuanza tena hatua mpya.

Nikajipanga kupiga hatua lakini wanasema ‘safari ya kifo haikosi maangaiko’. Pale pale nilipo zilisika pumzi za mtu mwingine, zilikuwa ndefu kipita za kwangu, kama ulishawai angalia kionjo chochote yeyote kile cha mchekeshaji maarufu wa kipindi hicho aitwae “Charles Champline” nadhani unajua kwa jinsi alivyo mwepesi wa mwili; usiombe atimue mbio, aisee mtapotezana. Nilijisikia mtu ambaye napaswa kutoa kila aina ya haja sio ndogo tu, hadi kubwa. Nikahisi siku hiyo imekuwa mbaya kwangu. Mikosi imeniandama. Wepesi wa mwili wangu haukuwa tatizo kunifanya niweze kutimua mbio mahali pale, nilijikuta ganzi imenishika ghafla na mwili kusisimka. Nikaganda kusubiri hukumu na kuacha moyo uendelee tu kudunduliza mapigo ya mwisho mwisho.

ENDELEA SEHEMU YA PILI

“Kaka... Dada,... ewe mtu uliopo mbele yangu, tafadhali!!!. Tafadhali naomba msaada wako. Mimi mtu mwema tu. Wananitafuta!!, ndugu yangu naomba nitazame mara kwa mara kabla hujaniacha mwenyewe maeneo haya. Sijui hata nilipo ndugu. Nakuomba”. Maneno mageni ya mtu nisiye mfahamu yakagonga kwenye ngoma za masikio yangu. Nikawa tayari kama askari kanzu lindoni. Hofu ya kutambua nani anaongea na mimi ilinijia.

“Inamaana bado hajanijua e!” nilijisemea kwa moyo baada ya kusikia kwa masikio yangu mawili kuwa alikua anabashiri nani yupo karibu yake, maana alianza na dada akamaliza na kaka.

Likaja wazo lingine na kuongeza kwenye mawazo yangu mengine ya mwanzo, wazo hilo jipya ndiyo lilinikumbusha kuwa kweli kuna mtu anatafutwa. Tena anatafutwa haswa!, nimsaidie?, hmmm wakijua?. Nimwache! Afu nikimwacha hii dhambi itakuwa ya nani? Bila shaka ni yangu. Naogopa dhambi kuliko lawama. Nikaamua liwalo na liwe nikageuka.

“Ndugu yangu nipo hapa, nakuomba tafadhali, nakuomba wema wako wa leo tu unanisubiri mimi ili nisipotee. Nakuomba tafadhali....” sauti ya sasa ilikuwa ni ya machozi ambayo inakalibiana na kwikwi ili vitoke kwa pamoja, sikuthubutu kwenda mbele, nikageuka nyuma na kuangaza mtu huyo ambaye ni adimu kwa macho ya watu wanne waliotangulia wakimtafuta.

“We.. we ni nani?” nikahofu kwa kuuliza. Lakini mtu yule hakujubu zaidi ya kupapasa tu ukuta na kujitokeza kando ya giza alipojificha. Mtaa huo ulikuwa na taa chache sana kutokana na nyumba nyingi kutowasha au kutoweka taa kabisa za nje, kwani ukiweka usiku taa basi asubuhi huikuti. Imekwenda na maji.

“Ni mimi kaka!, mi..mi... nakuomba nisaidie nitoke hapa, nitakueleza zaidi huko mbele, nakuomba kaka angu. Usiniuze tena nakuomba?”. Aliongea kwa msisitizo. Inaonekana tulijificha sehemu moja lakini sikumuona. Nikabaki natafakari tu neno lake la usiniuze tena. Ina maana aliuzwa?. Maswali kedekede yakaandama kichwa changu.

“Kukuuza tena?” Nilihoji.

“Ah nisaidie kaka, watanikuta hapa” aliongea tena kwa hisia. Nikaamua kuchukua uamuzi wa kutoa msaada kwake, kwani hata katika sekta niliyopo niliona ni bora kutoa msaada na nisingeweza katu kumwacha mtu huyo akiangaika na kutokomezwa pasipo julikana.

“Aya njoo sogea!” nilitoa amri kuonesha ukali ili kama ulikuwa ni mpango wa kuniangamiza mimi basi apatwe na woga.

Kijana huyo alijitokeza kwa kupapasa tena ukuta kisha kusogea hatua chache na kusimama, aliinua mikono yake kama anamtafuta mtu hivi, dalili zote za kuonesha kwamba ni kipofu zikaonekana. Roho ya huruma ikanivaa na kunishinikiza kudondosha chozi. Lakini nilikomaa.

“Oh pole.. Kwa hapa, ah. Taratibu e!” nikamshika na kumsaidia kutoka pale. Roho iliniuma sana kuona mtu mwenye tatizo kama lile na bado anaangaika. Alikuwa kipofu mtu yule.

Wazo la mwanzo la kupanda daladala likayeyuka. kwani tungeweza kuonwa kwa haraka zaidi na wanao mtafuta. Tukajongea kwa haraka huku hisia na macho yangu zote zikiwa wazi kusikiliza nini kitatokea nikiwa bado barabarani. Uzuri hatukuwa katika sehemu ambayo inatisha sana, kwani kuchepuka tu tukakutana na dereva pikipiki akisubili pesa yake ya kukeshea kilabuni.

“Elfuu na mia tano, tupo wawili, Msamala”. Niliongea vile kwa kutotaka kupoteza muda, kwani nauli ni elfu moja kwa mtu mmoja kwa umbali niliotaja. Pesa niliyotaja haikuwa na mjadala kwa watu wawili kwenye chombo kimoja.
-----------
Nilifika nyumbani na kupokelewa na mke wangu ambaye toka naingia alikuwa ananiangalia tu kama mtu mwenye hasira. Hakujali sana uwepo wa mgeni niliye mbeba siku hiyo. Baada ya kumweka mgeni wangu kwenye kochi, mke wangu alipatwa na hekima ya kunivutia kando kunihoji.

“Mume wangu!, We si hata mwezi tu haujaisha toka tumalize kesi ya kupigana?!, Umepigana tena?”. Aliuliza mke wangu bila kusubiri hata dakika ipite.

“Hhahahahahahahaha..” baaada ya kujibu swali la huzuni kutoka kwa mke wangu nikajikuta nacheka kupita kipimo hadi nikajistukia na kuziba mdomo. Sikutegemea kabisa maneno kama yale. Huzuni yangu ikakimbia mbali na kuruhusu furaha kutoka kwa mke wangu.

“Ebu mwandalie chakula mgeni na maji ya kuoga. Tutaongea!!”, niliagiza huku nikitoa mkono wangu mdomoni baada ya kumaliza kucheka.

Mke wangu alijua nimefanya vurugu mara baada ya kuona shati langu jeupe limetapakaa tandu za buibui na uchafu kila pande. Na huo ulikuwa sio mwonekano wangu wa kila siku, hivyo akapata hofu na kutumia hekima ya kunitoa chemba kumaliza shauku yake. Nikapotezea swali lake na kuelekea nilikomwacha mgeni wangu. Alibaki kunishangaa tu kwa kutikisa kichwa huku mikono yake akishikilia kiuno.

“Pole sana!, unajisikiaje?” nilimuuliza mgeni yule huku nikimtazama kwa makini.

“Ndugu yangu najiskia tu ni katika dunia salama kabisa. Hisia zangu zinaniongoza kukuongezea thawabu zangu zote kwako. Sitaki kufa mimi, sitaki kufa kabisa, sitaki kufa nakuambia! hadi nilichonacho kifike sehemu husika. Baada ya kufika basi nitakufa lakini dunia lazima ijifunze..”. aliongea bila kupepesa maneno hadi nilianza kupagawa kwa kuzitazama hisia za mgeni wangu. Nikataka kujua kila kitu kilichomsibu. Kwa maneno yake hayo machache yalinijulisha kuwa anamengi ya kuhadithia dunia. Nikabaki kuduwaa.

“Kuwa huru! Upo sehemu salama. Kuna tatizo gani kwani? Wanakudai?”. Nilijikakamua kuhoji nipate mkanda kamili.

“Nani!!?, Nani anidai.. Mimi?!, na wananidai nini?, eeh! ndio labla! Labda kweli wananidai!. Nakuomba nisaidie haraka nitue huu mzigo nilionao. Unaniumiza. Unanitesa. Wananidai uhai. Uhai ni wangu lakini wananidai. Wanataka waniue!!” safari hii mgeni wangu alianza kulia kwa nguvu hadi mke wangu aliyekuwa mbali mda wote akitushangaa akasogea.

“Kwani kuna nini baba?” mke wangu akanigeukia na kunitwanga swali lingine ambalo nalo lilipita hewani kama lile la mwanzo bila kujibiwa. Ningejibu nini wakati hata mimi sifahamu chochote?.

“Loh! Pole sana. Tutaelekea polisi kesho kutoa taarifa kwa usalama zaidi!” nilimpa pole mgeni wangu kwa shida iliyompata. Sikuwa na habari na mke wangu, wala kuangaika kujibu swali lake.
“Polisi?, Ndugu yangu umesema Polisi e? Loh! Polisi!, polisi!, polisi!!... Hapana walewale tu. Nimeenda zaidi ya neno nimeenda. Lakini napelekwa kubaya kulekule nilikotoka. Wametapakaa kila sehemu wabaya wangu, hadi kwa viongozi wa dini” mgeni huyo bado aliendelea kunichanganya kwa vitu mbalimbali alivyokuwa anagusia.......

ITAENDELEA..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SIMULIZI: “ANGAMIZO” (03)
MTUNZI: XAVERY EMMANUEL (Starxav)
Email: Xavemmanuel12@gmail.com
Namba: 0672493994
Social Net: @star_xav

“Polisi?, Ndugu yangu umesema Polisi e? Loh! Polisi!, polisi!, polisi!!... Hapana walewale tu. Nimeenda zaidi ya neno nimeenda. Lakini napelekwa kubaya kulekule nilikotoka. Wametapakaa kila sehemu, hadi kwa viongozi wa dini” mgeni huyo bado aliendelea kunichanganya kwa vitu mbalimbali alivyokuwa anagusia.......

ENDELEA SEHEMU YA TATU
“Hhmmm!! Mume wangu me sielewi eti, kuna tatizo gani?” kama ilivyo tamaduni ya jinsia ya kike katika kuorodhesha viwango vya woga wao hadharani. Mke wangu alionyesha hofu ya juu kabisa kuonja kiu ya majibu kwa maswali anayouliza. Nilimtazama na kumwomba atulie chini.

“Mama eh!! Huyu ni mgeni humu ndani kama unavyojua, nimemsaidia huko mtaani kutokana na kutafutwa na watu wabaya. Hapa alipo sijui kama anaona sawasawa. Mke wangu si unajua kazi yangu inahitaji ushuhuda mkubwa? Naachaje kumsaidia wakatika mimi pia ni sehemu maridhawa na kufanikisha nia yake!” nikajitapa kwa Mama watoto wangu kwa kile ninacho jivunia. Nilikuwa namaanisha nina uwezo wa kufikisha taarifa za mgeni wangu sehemu husika.

“Nisiwatie shaka! Mimi nahitaji tu vyombo vya habari!! Basi. Ukinipa msaada huo utakuwa umeokoa hadhi yangu na kizazi changu kilicho teseka duniani.. naomba msaada wako tafadhari” Mgeni aliendelea kuongea kwa kututia mashaka na sasa alihitaji vyombo vya habari.

“Vyombo vya habari!!!” tukajikuta tunasema wote mimi na mke wangu kwa pamoja.

“Ndio! Nataka mwandishi mahiri na shupavu wa kutumia karama yake ya uandishi kuandika maneno yanayouma haswa kwa wahusika, nahitaji mtangazaji mahiri wa kutoweza kukosea majina yangu hadi mwisho wa habari, nahitaji vifaa imara vya kurekodi saiti yangu ili palipo na machozi yasikike kisawasawa.... naitaji tafadhali!, roho yangu ipo katika nungwe za mwisho katika kuutafuna uhai wa dunia. Wamenifuata hadi nimechoka. Wameniwinda hadi wamechoka. Wamenichezea hadi tumechoka. Sasa ni muda wangu wa kufungua kinywa na kueleza kile nilichoficha kwa muda mrefu...”

Tulivuta pumzi ndefu kwa pamoja mimi na mke wangu bila kutegeana, nikamwangalia mke wangu na yeye akatikisa kichwa kuashilia niseme kila nilichonacho: Nikasema.

“Pole sana!, dah! Pole kaka. Kama msaada huo, wa vyombo vya habari basi umeupata, hakuna tatizo kabisa nakuambia!. Labda nikuulize swali moja, ushawai kusikia tetesi za mwandishi bora wa magazeti Tanzania? Na ambaye anawika kwa sasa?” nilimtupia swali ambalo lilikuwa katika utani lakini likiwa na maana kubwa.

“Wanasema ‘mchagua jembe sio mkulima’ siwezi kuchagua nani asimamie kazi yangu, sipendi nikae hapa mda mrefu nitawasababishia matatizo. Nawaomba nipate huduma hiyo mapema kabla sijatokomezwa tena!, waandishi wengi nawajua, nawajua kwa majina na sauti ila kwa waandishi magazeti Mmmh!..... yah! yupo huyu Xavery Luoga. Nadhani ni bora kwa sasa, nafuatilia sana maandiko yake!”. Hapo aligusia pale ambapo mimi nililenga. Nilishukuru mungu kwa kurahisishiwa kazi yangu maana ingekuwa ngumu mno kuaminika.

“Sasa bila shaka umefika sehemu sahihi! Huyo mwandishi ambaye maneno yake yanatembea katika maandishi ndio mimi ninayeongea na wewe hapa. Ni vigumu kuamini ila ndio ualisia. Nafanya kazi na kampuni changa ya StarXav Entertainment ambayo makazi yake yapo hapo hapa Songea Mjini, ina wafanyakazi wachache sana na mahiri nikiwemo mimi. Tumejizolea umaharufu mkubwa sana hasa katika sekta ya fahisi ya Kiswahili. Nakuomba nikusaidie tafadhari!!, mimi ndiye mtu sahihi na nilijitokeza kukusaidia hadi sasa.”

Baada ya utambulisho huo kwake hakuongea lolote kwa mda. Tukabaki kumsikiliza nini ataongea maana ukiona ‘kobe kainama ujue anatunga sheria’. Mgeni huyo hakuonyesha ishara yeyote ile kama amekubali au amekataa, aliinua kichwa na kukirudisha chini, akatikisika kidogo kwenye kochi kama mtu anayetaka kunyoosha misuli ili apambane na mshindani wake. Mwishowe akakaa sawa na kutoa neno.

“whwwwwww!, nilihisi ilo mda mrefu uliopita, ni sahihi kuwa ni wewe, sijawai kudanganywa toka nijitambue kuwa mimi ni mkubwa. Hizi ndizo hekima ambazo Mama yangu alinishushia. Na wewe ni miongoni mwa wahusika mwa mkasa huu…” Mgeni huyo alipoendelea kuongea, akaanza tena kulia. Ila alinishangaza pale aliposema mimi pia ni mhusika wa mkasa wake!, kivipi?.

“Ni kweli nipo sehemu sahihi lakini.., bado, bado nahitaji kutoka hapa. Nimekumbuka mtu ambaye anaratiba nzima ya siku yangu. Maisha yangu ni robo tu yapo hapa. Robo tatu kilo yapo kwa mpenzi wangu!, Mwandishi tafadhali mpenzi wangu hajui nipo wapi hadi mda hu. Nataka nikamuone jamani. nimemkumbuka” Kilio kilizidi ndani mule huku tusijue nini cha kufanya. Kumbe pia anampenzi kwa hali ile?.

“Hapana baba, mda umekwenda sasa, nje ni hatari sana si kwema kama mlivyotoka. Nakuomba vumilia pumzika, kesho atafuatwa huyo mpenzi wako asubuhi, utamuona!, ukitoka tu nje tumepoteza kila kitu” mke wangu alidakia, na hakusubiri neno kutoka kwa mtu yoyote mke wangu akaendelea kuongea.

“Kwani hana simu?” akauliza,

“Ndio! Ndio!!, ipo ipo simu mwandishi, naomba uwasiliane nae. Hatakuwa yupo katika hali mbaya, sio kuto kula tu hata kujifungia ndani bila kutoka!, ongea naye tafadhali!”. Haraka nikatoa simu yangu mfukoni na kuanza kutafuta uwanja wa kuandikia namba ngeni.

“Namba yake tafadhari!” nilimuamuru huku nikiwa nipo makini kuandika bila kukosea.

“0769765........” nikapiga.. iliita kwa sekunde nne tu ikapokelewa. Nikampa simu ili aongee mwenyewe.

“Rose!, Mimi mume wako mpenzi, nipo salama, eh! mikono salama kabisa..... nahakika, eeh! kesho Mama. Nashukuru eh!. Ondoa hofu bhasi. Kumbuka kusali unapolala... Amina.” Simu ilikuwa fupi kisha ikakata. Tulishajua jina la mpenzi wake kuwa ni Rose. Lakini hadi wakati hule bado mgeni wetu hakujitambulisha.

“Sasa kaka jisikie hupo huru kabisa, hapa ni sehemu salama. Hawawezi jua kama hupo humu, mtaa wetu pia hupo na ulinzi wa kutosha, lakini bado hatujakufahamu hata kwa majina, mimi kama nilivyojitambulisha, huyu ni mke wangu anaitwa Marry. Tupo wawili tu hatujabahatika kupata mototo bado.” Nikamaliza na kusubiri mpenzi wa Rose azungumze.

“Kama mnavyoniona sio nyinyi tu ambao mumekosea umri wangu. Wengi huko nje wananiita babu, kutokana na udhoofu wa mwili wangu, lakini katu nawaambia hata mwaka harobaini na kenda bado sijafika, mikunjo na hadaa za uso pamoja na mwili wangu ni kutokana tu na maangaiko mbalimbali ambayo nimepitia kwa takribani miaka na ushee sasa!, kwa jina Naitwa..” akasita kidogo kisha kuendelea,

“Abdul”. Akataja huku akiinamisha uso chini na kilio cha chinichini kikaanza tena, tulisikia tu jina hilo likitajwa tena kwa marudio katika kilio. Kulitaja tena alimaanisha hajakosea “Ab...dulii”. aliinama kuzuia machozi yake yasimchafue mbele ya mwanamke. Tukamtia moyo na kumbembeleza ili apunguze japo theruthi ya maumivu yake.

“Abdul, Shida nini?” mke wangu hakuridhika, akaendelea kudadisi. Lakini cha ajabu Abdul sasa aliinua uso wake juu na kufuta machozi kwa mkono wake wa kushoto, baada ya hapo akatabasamu.

“Ndugu! Nitaeleza ayo yote hadi mpenzi wangu awepo hapa. Kwa maana miaka yote niliyokaa na msichana huyo sijawai mwambia sababu ya mimi kutafutwa kwa namna hii, kila siku nampiga chenga tu kwa maana ilifikia hatua hata kumwamini mtu ilikuwa ni sumu. Siri hii naijua mimi tu peke yangu, labda kwa uchache ni hao wanaonitafuta kwa sababu wanaogopa kutolewa kwa siri yao. Mwenyezi mungu wa rehma kesho mapema pindi afikapo mpenzi wangu basi nitaweka kila kitu hadharani...... aaaagh! Ndio samahani kwa hilo mama!” alimaliza kwa kumtaka mke wangu radhi kwa kuto jibu alichomuuliza..

ITAENDELEA...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SIMULIZI: “ANGAMIZO” (04)
MTUNZI: XAVERY EMMANUEL (Starxav)
Email: Xavemmanuel12@gmail.com
Namba: 0672493994
Social Net: @star_xav

“Ndugu! Nitaeleza ayo yote hadi mpenzi wangu awepo hapa. Kwa maana miaka yote niliyokaa na msichana huyo sijawai mwambia sababu ya mimi kutafutwa kwa namna hii, kila siku nampiga chenga tu kwa maana ilifikia hatua hata kumwamini mtu ilikuwa ni sumu. Siri hii naijua mimi tu peke yangu, labda kwa uchache ni hao wanaonitafuta kwa sababu wanaogopa kutolewa kwa siri yao. Mwenyezi mungu wa rehma kesho mapema pindi afikapo mpenzi wangu basi nitaweka kila kitu hadharani...... aaaagh! Ndio samahani kwa hilo mama!” alimaliza kwa kumtaka mke wangu radhi..

NA HII NI SEHEMU YA NNE.
Hatukuwa na lingine zaidi ya kumwandalia sehemu ya kulala pamoja na chakula, kila mda sikusita kumpa pole kwa magumu aliyopitia, ingawa sikuyafahamu bado.

Kwa kweli ukimwangalia Abdul kwa sura ya karibu unapata kila aina ya majibu ya shida duniani, sura na umbo lake limebeba maswaibu yote ya ulimwengu kabla hujaupata mkasa wake. Kwa kumwangalia tu utajua kuwa kweli Abdul ni mwamba na shupavu kwani mifupa yake imegangamaa kwa michosho na maangaiko ya dunia.

Alikuwa ni mrefu kiasi, urefu uliomtosha mwenyewe kujiingizia kipato, alikuwa ni mweusi ambae rangi yake alipatikana baada ya vita kati ya rangi nyeusi na maji ya kunde, nani awe mtawala rasmi wa uso, na hatimaye weusi ulizidi shapavu kwa kunde na kutawala mwili mzima, yaani alikuwa mweusi wa matatizo mwili mzima.

Alikua mwembamba kwa kukosa lishe ya mwili kwa mda mrefu takribani milongo tisa na ushee. Hiyo tisa, kumi alikuwa ni kipofu, lakini uzuri wa hapa; kipofu chake kilikuwa ni cha macho tu lakini sio kuona. Kweli alikuwa hana uwezo wa kuona kabisa, lakini alikuwa na uwezo wa kufanya vitu vikubwa vinavyoonekena kumshinda hata alievalia miwani maarufu kama macho manne.

Kosa kumpeleka au kumwelekeza kitu kwa mara moja, mara ya pili anafanya mwenyewe. Hivyo hatukupata shida kumwelekeza mazingira ya chumba kilivyo, sehemu ya maliwato na pembe nyingine za chumba. Kila kitu kilichofuata kuhusu chumba hicho alijua yeye jinsi ya kupanga na kuweka kwa ustadi asipate shida kukitafuta. Kilikuwa ni chumba kwaajili ya wageni.

Basi tuliagana baada ya chakula na kumtaka alale salama huku mimi na mke wangu tukiliendeleza valangati la kutatua mgogoro wa mawazo kuhusu mgeni wetu mpya na wapi pa kuanzia kuhusu kumpata Rose ambaye ni mpenzi wa Abdul.

“Baba eh!! kama unavyojua bhana... ‘Abilia chunga mzigo wako’, unakoenda kesho unaenda kumchukua Rose na kurudi, marafuku tamaa!” hicho kilikuwa ni kijembe cha mke wangu kilichotokana na wivu,

Mke wangu amabaye tulizoea kuishi kwa matani kila kinapokutana, lakini jambo jema la kumshukuru Mungu ni kwamba hakuwai kunivunjia heshima hata siku moja, toka nimtoe kwao undendeuleni. Heshima kwake ilikuwa muhimu kama kula tu.

Tuliongea kidogo na mpango wa kuwahi kwenda kumchukua Rose kwani siku iliyofuata ilikuwa sio siku ya kazi; ni jumamosi. Na hatimaye tukalala kwani kila upande ulikuwa bize kuwaza historia kali ya maisha ya kijana ambaye yupo hatihani kutolewa roho kwa sababu ambazo hakuna anayejua zaidi ya msimuliaji mwenyewe, ambaye kwa wakati huo tayari neno Fofofofo Liliendelea katika chumba chake.
-------------

“Kokolikooooo!, kokokoko kokoli…” kama ilivyo majogoo ya kila siku, siku pendwa katika historia nyingine ya maisha ikaanza. Tukajuliana hali kila mmoja, na kwa mara ya kwanza jua la asubuhi liliniwezesha kuona kabisa uso wa Abduli ukiwa na tabasamu.

Baada ya kifungua kinywa nikaaga kwenda sehemu ambayo kila mtu aliifahamu, Abdul alinipa maelezo sehemu ambayo wanaishi kwa siri na mpenzi wake Rose, niliwasiliana na Rose kujua sehemu gani tunakutana, na kwa vile nilikuwa na namba yake ya simu haikunipa shida.

Nilianza safari kwa kuchukua daladala moja kwa moja hadi Bombambili stendi, sehemu ambayo tuliahidiana kupatana. Nilishuka stendi ya Bombambili na kuanza kutafuta namba ya mwanamke ambaye Abdul alimjaa kinywani, kila kichwao yeye ni Rose, Rose, Rose hadi kero! sijui ndio mzimu wake alaaah!.

Niliendelea kuongea mwenyewe kimoyomoyo kwa muda kabla maada haijabadilika kichwani mwangu na kuanza kuwaza ni aina gani ya mwanamke ambaye bwana Abdul ametunikiwa, mke mjasiri ambaye amekubali kuishi na Kipofu kwa umaskini na maangamizo kadha wa kadha, hakika nilipata msisimko sana na kupongeza baadhi ya jitihada wafanyazo wanawake katika kupigania mapendo yao.

Nilipofika nikafungua simu yangu kwa kutoa nenosiri, nikatafuta namba za Rose kupitia missed call na kuipiga.

“Hallo!, hallo,... eh wapi, wapi!!, ehh hallo!” bila maelewano simu hiyo ilikata, nikaipiga tena lakini nikajibiwa na muhudumu ambaye alikuwa zamu siku hiyo,

“Namba unayopiga haipatikani, Jaribu tena baadae”, nikakata na kupiga tena lakini mchezo ukawa vilevile, uso wangu ukaanza kuchukia na kuendelea kuangaza uku na uko kumtafuta mtu nisie mfahamu, niliangaza sana lakini sikufanikiwa kupata nilichokitaka.

Mshituko wa mayo ukanipata palepale nilipokuwepo mara baada ya macho yangu kuona mwanamke ambaye kwa mbali rangi yake ya maji ya kunde ilimulika mboni ya macho yangu. Picha ya mke wangu ikafutika kichwani kwa kuanza kutoa sifa sisizostaiki kwa mwanamke ambaye sio mke wangu.

“Jamani Mungu fundi... Lo!” nikapaza ukuu wa Mungu na nikajikuta namsogelea msichana huyo, kama tujuavyo wanaume sifa zetu pindi tumuonapo mwanamke ambaye maumbile yake ni mfano tosha wa kuamsha sehemu ambazo zimelala kwa mda.

Alikuwa ni mchana mwenye rangi yake, sikumbuki kama kipodozi cha kemikali kishawahi pita katika uso wake; hakika anavutia. Alikuwa na nyele ndefu nyeusi ambazo alizifunga tu kwa kamba kichwani mwake upande wa juu, utadhani anazitumia kama ngata katika kubebea mizigo mizito.

Nilimsogelea kuendelea kufahidi japo mapozi tu, alikuwa anakata kucha za mkono wake kwa kutumia meno huku mkono mwingine ukiangaika na simu ndogo kabisa ambaye ilikuwa haiendani na umbo lake. Nilipoganda kuendelea kumchora ghafla alinishtua na swali.

“Kaka naweza azima simu yako mara moja?” Swali hilo halikuwa na majibu kichwani kwangu, kwani aliendelea kunichanganya kabisa kwa kutumia sauti yake iyo ambayo kama wataalamu wa utengenezaji wa simu wangeigundua basi wangeinyunyiza katika teknologia ya mlio wa kuitia katika moja ya kampuni zinazofanya poa duniani.

Kweli niliongeleshwa ila nilibaki nimeduwaa kwa kukosa jibu, kwani hata kilichosemwa nilikikumbuka?, nikabaki kuishia tu aah!, Ah!... na kabla sijaangaika sana kijigonga gonga akarudia kile alichosema.

“Samahani lakini.... simu! Naazima!” Hapo kilichozungumzwa kilikaa kichwani, haraka nikatoa simu yangu na kumpa mrembo yule, macho yangu bado hayakuchomoka usoni mwake.

“Kaka mimi siwezi tumia hizi! Naomba niandikie namba....” aliongea na kunizidishia mawazo. Inakuaje kwa kizazi hiki mtu mrembo na mwenye miaka yake duniani anashindwa tumia smartphone. Nikabaki nashangaa tu. ‘Jamani kwa lika kama ya huyu dada halafu anasema eti hawezi kutumia “Smartphone” Laulaaa!’, nilipigwa na butwaa la moyomoyo ambalo hakula alieliona zaidi ya moyo wangu wenyewe.

“Mhhh namba!” nikajikwakwamua kutoa msaada.

“0757.. 9947....” kabla hajamalizia kuitaja namba hiyo, nikainua macho yangu na kumtazama kwa makini, nilikutana na uso wa tabasamu wa mrembo yule, kilichonishangaza ni kuwa namba hizo alizokuwa anazitoa kichwani.

Yaani bila kuangalia sehemu yoyote ile jambo ambalo lilinishangaza sana. Sikumbuki kama alimalizia kutaja namba za mwisho au la, lakini tukabaki tu kuangaliana, huku mimi nikimshangaa yeye na yeye akishangaa mimi kwa mshangaa yeye…….

“Unamtafuta nani?” Nikajikuta namtupia swali rahisi kwake.

“Abdul..... A....” likarudiwa mara mbili lile jina la Abdul, hapo nikastuka katika dimbwi la mawazo na kuanza kumkazia tena macho mrembo yule.

Nilikuwa kama sijaelewa alichozungumza kwa mara nyingine. Lakini alitaja bila kusita tena mara mbili!. Kitu ambacho kilinifanya niamini ni yeye Rose ni kuwa alipotaja namba alitaja namba zangu kabisa ambazo nilitumia kuwasiliana na yeye.

Nikataka kupingana na macho yangu kama yule ndio kweli mwanamke ambaye ametekwa na kijana kama Abdul. Kwa kweli baada ya jina hilo, kilichofuata ni maswali na majibu tu ambayo nilikuwa najiuliza mwenyewe bila kupata nafasi ya kujijibu.

“We ni rose?” na mimi nikamtwanga swali ambalo lilimwacha kinywa wazi!, niliuliza kutaka kuhakikisha tu. Akainamisha kichwa chini kwa hofu ya kujibu. Alikuwa anaogopa…..

ITAENDELEA…

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SIMULIZI: “ANGAMIZO” (05)
MTUNZI: XAVERY LUOGA (Starxav)
Email: Xavemmanuel12@gmail.com
Namba: 0672493994
Social Net: @star_xav

Nikataka kupingana na macho yangu kama yule ndio kweli mwanamke ambaye ametekwa na kijana kama Abdul. Kwa kweli baada ya jina hilo, kilichofuata ni maswali na majibu tu ambayo nilikuwa najiuliza mwenyewe bila kupata nafasi ya kujijibu.

“We ni rose?” na mimi nikamtwanga swali ambalo lilimwacha kinywa wazi!, niliuliza kutaka kuhakikisha tu. Akainamisha kichwa chini kwa hofu ya kujibu. Alikuwa anaogopa…..

ENDELEA SEHEMU YA TANO…

“Okey mimi ni Xavery!, Xav... kama unamtafuta Abdul basi hapa ndipo sehemu sahihi na muafaka kabisa, nipo nae kwangu!”. Nikamwaminisha.

“Kaka samahani, nilikuwa naitaji huduma ya simu tu basi, kama hapatikani naomba mimi niende” akainua kichwa chake chenye aibu na kuongea, hakuchukua sekunde akaanza kugeuka tayari kuondoka.

“Rose ni mimi bhana, nimeagizwa na Abdul, nimepatwa na mshangao mara baada ya kusikia namba iliyotaja ni yangu. Mwishoni ni 87! Si ndiyo?, Abdul yupo salama na anakuitaji, na mguu huu ulikuwa kwako. Sikufahamu na nisingeweza kukufahamu kwa mapema namna hii, utambulisho pekee ambao nilikuwea nao mkononi mwangu nilikuwa nao ni namba yako tu ya simu. Nimepiga sana lakini hupatikanai” nilijitahidi kutokwa na maneno ya ukweli kwa mfurulizo kwa kumwaminisha binti yule, akageuka tu na kutoa chozi jembamba lililotililika hadi mashavuni mwake, lakini hakuharibu kitu katika kung’aza uzuri wake, alipendeza hadi wakati analia. Alinisogelea na kunitaka radhi.

“Kaka angu, ni vigumu kumwamini kila mtu kwa sasa, tunatafutwa sana, sio mimi wanaoniitaji, ni Abdul, kwa maana hata tukiwa wawili mimi na yeye, basi wataanza na yeye. Nampenda sana mume wangu jamani, naomba nikamwone” alito ombi la mwisho kwa kilio, nilimwonea huruma kwa kweli, nikawaza shida anazopata kwa kuishi na kipofu angali yeye ni malaika namna ile, vipi kero za wanaume wanaomsumbua kumtaka kimapenzi?. Basi nikachukua nafasi ya kumbembeleza hadi kutulia.

Tukachukua usafiri wa pikipiki, Maana niliwaza sana tunapandaje pikipiki moja na hali ya nyuma ilivyo nzuri ya binti yule. Rose alibeba kila kitu sehemu zake za nyuma, alikuwa mwemabamba wa kukonda kwa maisha tu ila mwili ulimkaa vizuri sana, mbinuko wake wa nyuma na shepu yake ya uchanga ilionekana.

Sasa nawezaje kupanda nae pikipiki moja? Nani atakaa mbele na nani nyuma? Mwanaume nikae mbele, hapana, nikae nyuma! Lo! Na ilo sebene ya matuta njiani ikuru yangu itaweza vumilia kweli ikigusana na mlima Rose? Na akiniona mke wangu huo ni ugomvi mwingine, nikatabasamu na kuchukua pikipiki mbili, kila mmoja alipanda yake na mimi kuanza kuingoza njia kuelekea nyumbani.
------------

Hatukuchukua mda mrefu tayari tulishaingia mlangoni, sikuwa na mlinzi wala haouse girl nyumbani mwangu, nikafungua mlango mwenyewe na kuingizana ndani na Rose ambaye roho yake tayari ilianza kuweuka mara baada ya kuona amekaribia sehemu ambayo roho yake imefia mazima.

Ile kuingia tu.. tukakaribisha vilio vya furaha vilivyosindikizwa na machozi. Si kwa furaha ya Rose, vipi upande wa Abdul?, kwa mara ya kwanza nikaona nyuso ya tabasamu kwa Abdul. Huyu jamaa ukimwangalia kwa makini unaweza sema sio kipofu. Kwa maana hakuna anachokosea yaani kila kitu anafanya sahihi utadhani ana macho yote mawili!!!
Hakuchukua muda Abdul akaanza kutupa siri!, ile siri ambayo inajulikana na wachache tu. Si yeye Abdul pekee bali na wale ambao wanamtafuta. Hakika lilikuwa ni chozi la damu.
-------------

“Ndugu Mwandishi, labda nianze kwa kujitambulisha vyema kabisa ambapo kila mtu sasa anijue kwa mapana. Haikuwa kusudi langu kusema ukweli huu uliojificha kwangu kwa miaka zaidi therathini na mbili, hakuna yeyote yule mwenye dhamana ya kujua wapi natoka wala wapi naelekea,” akasita kidogo kuongea na kisha kuangalia upande ambao kipenzi chake Rose alikuwepo, utadhani walionana vile, macho yao yakagongana angali mmoja alikuwa haoni na mwingine alikuwa anaona vyema kabisa, macho yao yalifumuka kama ‘tai aliponyang’anywa kitinda mimba chake’. Kisha bwana Abdul akaendelea.

“Samahani sana kipenzi changu Rose, samahani sana dunia, hamkupasa kujua kweli hii, nimefumbuliwa lindo la matataizo ambayo yamenifanya kufungua kinywa changu kwa kueleza kila kitu.

Ndugu mwandishi mimi kwa majina halisi kabisa ambayo nilibatizwa na Baba yangu mzazi Mzee Yohana, ni Denis Ephrehem, jina ambalo nilipewa halali kabisa na Padre wa kizungu aliyekuja kutubatiza kipindi chake cha likizo fupi aliyokuwa akimalizia uko wilayani Ludewa, mkoa wa Njombe.

Familia yetu ilikuwa karibu sana na kanisa katoliki la Roma, hakuna siku ikaisha hatujataja jina la Yesu Kristo wa Nazareth. Familia yetu ya Mzee Yohana na Bi Naomi Alfred ambaye ndio mama, ilikuwa ya amani sana, tulikuwa watoto wawili tu, mimi Denis na dada yangu kipenzi Maria….” Hapo Adbul ambaye kwa muda huo alijitambulisha kwa jina la Denis alianza kutililisha chozi lake taratibu kwa kukumbuka kitu. Rose alionekana kukosa amani baada ya kujua kwa mara ya kwanza kuwa mpenzi wake jina lake halisi ni Denis na sio Abdul kama anavyojua. Aliongopewa.

“Mwandishi dada yangu! Dada yangu mpenzi anaitwa Maria!, Mimi na Maria tulipishana miaka Minne tu toka kuzaliwa kwangu, nakumbuka alizaliwa miaka minne ya mbele baada ya kuzaliwa mimi mwaka 1986. Ukiniangalia kwa sasa utadhani mimi ni kikongwe ambaye nina miaka kuanzia sitini na mbili hadi sabini na tano; umri ambao unatosha kabisa kustafu kero na shida za dunia.

Bado kijana mimi Mwandishi, ni maisha magumu niliyopitia hadi kufanya mwili wangu kuzeeka angali umri bado upo kijana kabisa.

Mwandishi baba yangu alibahatika kuwa na baadhi ya fedha za kujikimu katika maisha, wachache wenye upumbavu kichwani wanasema ni Mali. Alikuwa na makampuni kadhaa karibia kila mji, mengine ya kuchakata tumbaku, mengine ya alizeti, mengine kuchakata mkonge, mengine sijui nini. Kwa takwimu chache ambazo familia nzima tulikuwa tunaijua ni jumla ya makampuni si chini ya kumi. Achana na zile ambazo baba aliamua kutuficha, si mimi wala mdogo wangu aliyekuwa anazijuwa. Alikuwa na makampuni kedekede.

Siku zilienda na maisha yalikuwa mazuri, sikupata bahati ya kuwajuwa ndugu wote wa upande wa baba na wale wa upande wa mama. Maisha yetu yalikuwa ndani tu, hakuna misiba wala sherehe za jirani tulizohusika nazo. Tukitoka nje basi ni kwenda shule na kurudishwa na gari. Shule zenyewe ndo hizi za Yes, No, Ofcourse. Kila hatua kwetu ilinukia pesa tu...

Baba alikuwa mtu mkubwa amabaye, hata akiomba sehemu awe kiongozi basi wapinzani wote wanarudi nyuma kwa kuogopa ushindani; pesa zilitupa kiburi mno. Nadhani huu ndio mshahara wa dhambi zetu, umenitesa sana Baba!, umemtesa Mama, Umemtesa Maria, Umenitesa mimi na kizazi chako kijacho!, ziko wapi pesa zako Baba!!”. Abdul aliishia hapo na kuanza tena kulia, kilio chake hakikuwa cha sauti, nyumba yote ilikuwa kimya sana.

Mke wangu alikuwa ameduwaa kwa utamu na uchachu wa machungu wa maneno alikuwa anautoa Abdul, Abdul alikuwa fundi wa lugha kweli kweli, kwa hatua hii hakuna asiyeamini kuwa mtaa ulimfunza. Baada ya kufuta chozi mwanaume akaendelea…

ITAENDELEA…

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom