Siku Nilipoiona Simu Kwa Mara ya Kwanza Odeon Cinema 1955 au 1956 au Nyuma ya Hapo Kidogo Sijavuka Miaka 4

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,921
30,265
SIKU NILIYOIONA SIMU KWA MARA YA KWANZA ODEON CINEMA 1955 AU 56 AU NYUMA YA HAPO KIDOGO SIJAVUKA UMRI WA MIAKA MINNE

Nakumbuka kama jana vile.

Nilikuwa mgonjwa na baba yangu mdogo Mzee Issa akanichukua kunipeleka hospitali.

Ilikuwa usiku lakini si usiku mkubwa kiasi cha saa moja hivi.

Nina hakika na hili kwa kuwa Mzee Issa kanibeba tunatoka nyumbani Mtaa wa Kipata (Sasa Kleist Sykes Street) kwa miguu na nawaona watu mtaani njia nzima hadi tunafika New Street tunavuka Mnazi Mmoja tunapita kushoto tunaelekea Sultan Street (Libya Street).

Hapa Mnazi Mmoja palikuja kujengwa Mnara wa Uhuru. Siku zile Mnazi MMoja ile ilikuwa uwanja mtupu hauina chochote ni mchanga mtupu.

Tunaingia Ring Street (Sasa Jamhuri Street) tunapita pembeni ya Odeon Cinema tunaingia mitaa ya Uhindini jirani na Msikiti wa Sunni kulikuwa na hospitali maarufu sana ya daktari wa Kihindi nakumbuka ingawa sina hakika jina lake lilikuwa kama Dr. Koya.

Mama zetu wakimsifia sana kwa kutibu watoto.

Hii hospital imedumu hapo kwa miaka mingi hadi mimi nimekuwa mtu mzima nikipita pale nikiiona.

Baada ya kutibiwa baba yangu mdogo Mzee Issa miaka ile alikuwa kijana akawa ananirudisha nyumbani.

Ndipo tulipopita tena Odeon Cinema tukaingia ndani kwenye call box (kibanda cha simu) kilichokuwa pale ndani.

Baba yangu alikuwa kazini akifanyakazi Telephone Exchange.
Jumba hili hadi leo lipo.

Mzee Issa akatia pesa kisha akapiga simu kuzungumza na baba yangu kumfahamisha kuwa kanipeleka hospitali na nimetibiwa.

Mzee Issa akanipa simu nimwamkie baba yangu.
Sikuweza kuzungumza.

Miaka mingi ikapita.

Siku moja nikamhadithia Mzee Issa habari hii.
Alishtuka.

Akawa kashangaa kisha akaniuliza, ''Mohamed unakumbuka habari hii?''

326990267_3458502591073338_625044799509994387_n.jpg

327556309_1913726512302146_4804005542629042379_n.jpg

327246206_488592410128550_2450343156164433652_n.jpg


 
Mzee Mohamed ndio anapaswa kujiita Born Town
Cvez,
Aaah bwana kwani ni jambo kubwa hilo?
Tusingeweza sote tuzaliwe Dar es Salaam.

Nikushangaze.
Mama yangu kazaliwa Musoma.

Baba yake Sheikh Mohamed Mvamila kazaliwa Mkamba akaenda Musoma katika ujana wake kusomesha dini.

Amekufa Musoma na kazikwa Musoma.

Alitoka Mkamba na mkewe bibi yangu Mwatum bint Rajabu Mgeni kabila Mluguru hawajapata mtoto huko Musoma ndiyo wakamzaa mama yangu na ndugu zake wanne.

Baba yangu kazaliwa Tabora lakini kakulia Dar es Salaam.
Baba yake kazaliwa Shirati Musoma.

Babu yake kazaliwa Bukavu Belgian Congo kaingia Germany Ostafrika mwishoni 1800 kama askari katika jeshi la Wajerumani na akafikia Shirati na hapo ndipo babu yangu Salum Abdallah alipozaliwa.
 
Kipindi hiko Saigon ilikuwepo mkuu...?
Niache....
Saigoon ilikuja 1967 baada ya mgawinyoko wa club yetu ya kwanza Everton.
Sote tulikuwa shule ya msingi.

Mimi nilikuwa na umri wa miaka 15 wastani wa umri wetu sote ulikuwa katika hapo yaani miaka 15, 16, 17.

Wala hatukujua kama hii club itakuwa maarufu kiasi hiki.

Picha hiyo hapo chini ni Saigon Club 1980s Mtaa wa Sikukuu na Narung'ombe.

1674838324869.jpeg

Kulia: Marehemu Yunus, Mussa Shagow, Mohamed Said, Mkongo na Marehemu Ghalib Hamza(Guy).

Saigon katika 2020s:
1674838741271.jpeg

Kulia: Marehemu Nusura Faraj, Manzi, Marehemu Abdulkarim Shah (BuljiI) chini kulia Shariff Pazi na Mshike.
 
Niache....
Saigoon ilikuja 1967 baada ya mgawinyoko wa club yetu ya kwanza Everton.
Sote tulikuwa shule ya msingi.

Mimi nilikuwa na umri wa miaka 15 wastani wa umri wetu sote ulikuwa katika hapo yaani miaka 15, 16, 17.

Wala hatukujua kama hii club itakuwa maarufu kiasi hiki.

Picha hiyo hapo chini ni Saigon Club 1980s Mtaa wa Sikukuu na Narung'ombe.

View attachment 2497529
Kulia: Marehemu Yunus, Mussa Shagow, Mohamed Said, Mkongo na Marehemu Ghalib Hamza(Guy).

Safi sana kiongozi wewe ni mmoja kati ya Hazina nyingi zilizopotea MUNGU akulinde na akutunze zaidi na zaidi In Shaa Allah.
 
Cvez,
Aaah bwana kwani ni jambo kubwa hilo?
Tusingeweza sote tuzaliwe Dar es Salaam.

Nikushangaze.
Mama yangu kazaliwa Musoma.

Baba yake Sheikh Mohamed Mvamila kazaliwa Mkamba akaenda Musoma katika ujana wake kusomesha dini.

Amekufa Musoma na kazikwa Musoma.

Alitoka Mkamba na mkewe bibi yangu Mwatum bint Rajabu Mgeni kabila Mluguru hawajapata mtoto huko Musoma ndiyo wakamzaa mama yangu na ndugu zake wanne.

Baba yangu kazaliwa Tabora lakini kakulia Dar es Salaam.
Baba yake kazaliwa Shirati Musoma.

Babu yake kazaliwa Bukavu Belgian Congo kaingia Germany Ostafrika mwishoni 1800 kama askari katika jeshi la Wajerumani na akafikia Shirati na hapo ndipo babu yangu Salum Abdallah alipozaliwa.
Kiongozi Mungu azidi kukupa uhai ili tuendelee kufaidi historia unayotupatia

Naomba ufafanuzi kidogo hapo unaposema Shirati mkoa wa Musoma nachojua Mimi ni Mkoa wa Mara tena sasa ivi ni wilaya ya Rorya.... imenishangaza sana kusikia una viasili vya Wilaya ya Rorya nyumbani kwetu
 
SIKU NILIYOIONA SIMU KWA MARA YA KWANZA ODEON CINEMA 1955 AU 56 AU NYUMA YA HAPO KIDOGO SIJAVUKA UMRI WA MIAKA MINNE
Nakumbuka kama jana vile.

Nilikuwa mgonjwa na baba yangu mdogo Mzee Issa akanichukua kunipeleka hospitali.

Ilikuwa usiku lakini si usiku mkubwa kiasi cha saa moja hivi.

Nina hakika na hili kwa kuwa Mzee Issa kanibeba tunatoka nyumbani Mtaa wa Kipata (Sasa Kleist Sykes Street) kwa miguu na nawaona watu mtaani njia nzima hadi tunafika New Street tunavuka Mnazi Mmoja tunapita kushoto tunaelekea Sultan Street (Libya Street).

Hapa Mnazi Mmoja palikuja kujengwa Mnara wa Uhuru.

Siku zile Mnazi MMoja ile ilikuwa uwanja mtupu hauina chochote ni mchanga mtupu.

Tunaingia Ring Street (Sasa Jamhuri Street) tunapita pembeni ya Odeon Cinema tunaingia mitaa ya Uhindini jirani na Msikiti wa Sunni kulikuwa na hospitali maarufu sana ya daktari wa Kihindi nakumbuka ingawa sina hakika jina lake lilikuwa kama Dr. Koya.

Mama zetu wakimsifia sana kwa kutibu watoto.

Hii hospital imedumu hapo kwa miaka mingi hadi mimi nimekuwa mtu mzima nikipita pale nikiiona.

Baada ya kutibiwa baba yangu mdogo Mzee Issa miaka ile alikuwa kijana akawa ananirudisha nyumbani.

Ndipo tulipopita tena Odeon Cinema tukaingia ndani kwenye call box (kibanda cha simu) kilichokuwa pale ndani.

Baba yangu alikuwa kazini akifanyakazi Telephone Exchange.
Jumba hili hadi leo lipo.

Mzee Issa akatia pesa kisha akapiga simu kuzungumza na baba yangu kumfahamisha kuwa kanipeleka hospitali na nimetibiwa.

Mzee Issa akanipa simu nimwamkie baba yangu.
Sikuweza kuzungumza.

Miaka mingi ikapita.

Siku moja nikamhadithia Mzee Issa habari hii.
Alishtuka.

Akawa kashangaa kisha akaniuliza, ''Mohamed unakumbuka habari hii?''

326990267_3458502591073338_625044799509994387_n.jpg

327556309_1913726512302146_4804005542629042379_n.jpg

327246206_488592410128550_2450343156164433652_n.jpg


Mzee Mud ungeandika kitabu cha historia ya mitaa mbalimbali ya Dar es Salaam ya leo ilivyokuwa wakati huo ingenoga sana
 
Mzee wangu, inaonesha dhahiri wew ni mtu mzima sana, babu yangu alipokua na umri kama wako (marehemu kwa sasa) alikua amechoka sana kimwili hata kiakili. Wew umewezaje katika umri huo kua mtu "active" sana kiakili, nina uhakika hata kimwili pia bado upo na nguvu za kutosha hata kuupanda mlima kilimanjaro. Umeishi katika namna ipi mpaka kuvilinda mwili na ubongo wako mpaka umri huo?
 
Hivi saigon ni maarufu kwà draft
Niache....
Saigoon ilikuja 1967 baada ya mgawinyoko wa club yetu ya kwanza Everton.
Sote tulikuwa shule ya msingi.

Mimi nilikuwa na umri wa miaka 15 wastani wa umri wetu sote ulikuwa katika hapo yaani miaka 15, 16, 17.

Wala hatukujua kama hii club itakuwa maarufu kiasi hiki.

Picha hiyo hapo chini ni Saigon Club 1980s Mtaa wa Sikukuu na Narung'ombe.

View attachment 2497529
Kulia: Marehemu Yunus, Mussa Shagow, Mohamed Said, Mkongo na Marehemu Ghalib Hamza(Guy).

Saigon katika 2020s:
View attachment 2497531
Kulia: Marehemu Nusura Faraj, Manzi, Marehemu Abdulkarim Shah (BuljiI) chini kulia Shariff Pazi na Mshike.
Hivi saigon ni maarufu kwà draft kahawa na story za simba na nyanga au tiss waliingiaje hapo?
 
Hivi saigon ni maarufu kwà draft
Niache....
Saigoon ilikuja 1967 baada ya mgawinyoko wa club yetu ya kwanza Everton.
Sote tulikuwa shule ya msingi.

Mimi nilikuwa na umri wa miaka 15 wastani wa umri wetu sote ulikuwa katika hapo yaani miaka 15, 16, 17.

Wala hatukujua kama hii club itakuwa maarufu kiasi hiki.

Picha hiyo hapo chini ni Saigon Club 1980s Mtaa wa Sikukuu na Narung'ombe.

View attachment 2497529
Kulia: Marehemu Yunus, Mussa Shagow, Mohamed Said, Mkongo na Marehemu Ghalib Hamza(Guy).

Saigon katika 2020s:
View attachment 2497531
Kulia: Marehemu Nusura Faraj, Manzi, Marehemu Abdulkarim Shah (BuljiI) chini kulia Shariff Pazi na Mshike.
Hivi saigon ni maarufu kwà draft kahawa na story za simba na nyanga au tiss waliingiaje hapo?
 
Mzee wangu, inaonesha dhahiri wew ni mtu mzima sana, babu yangu alipokua na umri kama wako (marehemu kwa sasa) alikua amechoka sana kimwili hata kiakili. Wew umewezaje katika umri huo kua mtu "active" sana kiakili, nina uhakika hata kimwili pia bado upo na nguvu za kutosha hata kuupanda mlima kilimanjaro. Umeishi katika namna ipi mpaka kuvilinda mwili na ubongo wako mpaka umri huo?
Maso...
Mimi nina miaka 70 Alhamdulilah.

Kuwa niko "active kiakili," labda maana sina hakika nikipenda kusoma na kuandika toka udogoni.

Nguvu ya kuukwea Kilimanjaro sina.

Labda kitu kimoja ni kuwa sijatumia tumbaku wala ulevi wa aina yeyote toka kuzaliwa.
 
Back
Top Bottom