BIREGU
Member
- Feb 10, 2013
- 31
- 8
Kaka yangu yupo masomoni ng'ambo Tangu mwaka jana,mwaka huu mwezi wa 10 atarudi likizo.Lakini mimi natamani arudi mapema nimwambie mambo ya mke wake.alipo kwenda huko aliniachia familia yake niwe namuangalia shemeji kwa maana ya kujua maendeleo yake pamoja na mtoto ( mwanae).Lakini siku moja shemeji yangu alinipigia simu akinitaka niende kwake usiku wa saa 5 na nusu kuna kitu anataka aniambie.nikatafuta usafiri nikafika kwake ,nilipofikatu na kugonga mlago alinifungulia na tukakaa sebureni lakini nikamuona kachangamuka sana,kama kalewa hivi!kisha akakaa kochi la mbele yangu yaani tukiwa tunatazamana.akaanza kwa kuniita shemeji kisha jina langu nimekuita nikwambie siri yangu,na sinabudi nikwambie tu vinginevyo nitazidi kuteseka,Unajua nakupenda sana alisema na natamani muda huu ambao kaka yako ayupo tujivinjari na itakuwa siri yetu,usidhani natania nimedhamilia na sikuwahi kuwa na nafasi ya kukueeleza haya.Nikapigwa butwaa na sikuamini maneno yake.Nikamsii sana anipe muda nilifikilie hilo.Ni mwezi sasa nahakikisha nikienda kwake nakuwa na marafiki zangu wawili au watatu,lakini ananisumbua sana kwenye simu akitaka nimpe jibu.Sasa wana janvi nifanyeje? kunawakati natamani nimwambie kaka akiwa huko huko,lakini najua anampenda sana mke wake nitamchanganya,na akirudi nitawezaje kumwambia wakati naogopa kuwa chanzo cha mwisho wa ndoa yao.najua aiwezekani kuanza mahusiano na mke wa kakaangu,ila kwangu nivigumu kumwambia kwani sijui atachukua hatua gani.Ushauri wenu jamani.