Sijui huwa kinatokea nini!!

Kigarama

JF-Expert Member
Apr 23, 2007
2,492
1,230
Afrika iliwahi huko nyuma kupata wanasiasa mahiri na weledi na wazalendo kweli kweli kwa Bara lao na watu wake.

Wanasiasa wa aina ya Kwame Nkurumah na Mwalimu Nyerere ambao mabishano yao ya jinsi gani ya kuiunganisha Afrika yameacha athari kubwa sana mpaka sasa. Kulikuwa na wanamapinduzi kama kina Samora Macel na Mzee Jomo Kenyata ambao nusu ya maisha yao waliyatumia msituni kupigania haki na uhuru wa nchi zao na watu wake. Wanasiasa wa aina hii hawakuishi sana hadi kuonekana kubadilika tabia zao walipokuwa madarakani ukiondoa Nyerere.

Lakini katika Afrika jambo moja linaloshangaza ni pale baadhi ya wanamapinduzi au wanasiasa hao hao ambao wakiwa nje ya madaraka wanakuwa ni wanamapinduzi wa kweli kweli, wakiingia madarakani wanageuka ving'ang'anizi na wakandamizaji wakubwa wa wananchi wao ambao kabla ya kuingia madarakani walidai wanapigana kwa ajili yao.

Yoweri Museveni kimemtokea nini mpaka anaamini kwamba bila ya yeye kuwa Rais hakuna Uganda. Kwa nini Raila Odinga anaamini yeye pekee ndiye anayefaa kuwa mgombea Urais wa kupitia chama cha ODM. Nini kimembadilisha Mugabe mpigania uhuru aliyeheshimika sana kwenye miaka ya themanini kuwa vile alivyo leo? CCM hii ya leo lengo lake la kuundwa kwake lilikuwa ni kuwatetea wakulima na wafanya kazi. Lakini leo hii ndani ya chama hicho kumetamalaki ufisadi wa kutisha hadi ile hali ya kuamini kama kinaweza kujisafisa ni sawa sawa na Sifuri.

Hali hii inanifanya nijiulize, ni kitu gani huwa kinawatokea wanasiasa wengi wa Afrika wanaposhika madaraka?

Wewe unajua kinachotokea?
 
usisahau kamwe wanamapinduzi wakiafrika kuwa wana uchu wa madaraka, na wanapenda kujilimbikizia mali na heshima mfano unao nafikiri. lakini kikubwa tunachotakiwa kukipinga kama wana afrika ni unyanyasaji unaotokana na ukandamizwaji na unyonyaji. Wengi wa viongozi wetu hawataki mabadiliko hasa ya haki pasi kwa mtutu. nafikiri nchi zote za africa zenye asili ya kiarabu zimeshatuthibitishia hayo.

kazi ipo kwetu wa tanzania, unajua kuna siku mimi nilikuwa nasema hapa bongo bila mtut heshima na haki havitapatikana, najua wengi watapoteza maisha ila watakao pona wataishi peponi. Nnaumia sana kuona midege inaondoka na dhahabu na alimasi pamoja na tanzanite na sisi tunabaki maskini wa kutupwa ilihali wenye navyo wanaendesha ma v8 na misafara mikubwa.
 
lakini labda niwaulize wana jamvi weli tunasababu ya kusubiri hadi tuingie msituni ili haki yetu ipatikane? na je inamaana hao wenye nchi yao hawaoni japo huruma kwa vizazi vilivyobaki? nijuavyo mimi resourses ambazo ni non renewable zitaisha tutabakiwa na mapango tu huku kansa inayosababishwa na cyanide pamoja na mercury ikitumaliza na wao wakiendesha mashangingi yao na kuish kwenye makasri ya kifahari.
 
wapenzi wana jf huwa naumia sana nikianza kutafakari habari za Tz. na nina umia zaidi pale unapopita maeneo unakutana na big investment unaskia hii ni mali ya rizi1, sasa huwa najiuliza rizi huyu niliyesoma naye juzi mwaka 2005 leo hii ni tajiri kuliko hata baba yake? jamani inauma sana
 
Afrika iliwahi huko nyuma kupata wanasiasa mahiri na weledi na wazalendo kweli kweli kwa Bara lao na watu wake.

Wanasiasa wa aina ya Kwame Nkurumah na Mwalimu Nyerere ambao mabishano yao ya jinsi gani ya kuiunganisha Afrika yameacha athari kubwa sana mpaka sasa. Kulikuwa na wanamapinduzi kama kina Samora Macel na Mzee Jomo Kenyata ambao nusu ya maisha yao waliyatumia msituni kupigania haki na uhuru wa nchi zao na watu wake. Wanasiasa wa aina hii hawakuishi sana hadi kuonekana kubadilika tabia zao walipokuwa madarakani ukiondoa Nyerere.

Lakini katika Afrika jambo moja linaloshangaza ni pale baadhi ya wanamapinduzi au wanasiasa hao hao ambao wakiwa nje ya madaraka wanakuwa ni wanamapinduzi wa kweli kweli, wakiingia madarakani wanageuka ving'ang'anizi na wakandamizaji wakubwa wa wananchi wao ambao kabla ya kuingia madarakani walidai wanapigana kwa ajili yao.

Yoweri Museveni kimemtokea nini mpaka anaamini kwamba bila ya yeye kuwa Rais hakuna Uganda. Kwa nini Raila Odinga anaamini yeye pekee ndiye anayefaa kuwa mgombea Urais wa kupitia chama cha ODM. Nini kimembadilisha Mugabe mpigania uhuru aliyeheshimika sana kwenye miaka ya themanini kuwa vile alivyo leo? CCM hii ya leo lengo lake la kuundwa kwake lilikuwa ni kuwatetea wakulima na wafanya kazi. Lakini leo hii ndani ya chama hicho kumetamalaki ufisadi wa kutisha hadi ile hali ya kuamini kama kinaweza kujisafisa ni sawa sawa na Sifuri.

Hali hii inanifanya nijiulize, ni kitu gani huwa kinawatokea wanasiasa wengi wa Afrika wanaposhika madaraka?

Wewe unajua kinachotokea?
Tafuta hotuba ya P.W Botha, google botha's popular appathaid speech utajua nini kinawatokea
 
uchu na tamaa ya madaraka ukiongezea kujilimbikizia mali
Kila mtu duniani ana uchu wa vitu hivi viwili, lakini imekuwaje kwa wenzetu wa Ulaya wameweza kujizuia au inakuwaje jamii za huko zinawezaje kuwadhibiti wanasiasa wao waroho na wenye uchu wa madaraka.
 
Back
Top Bottom