Kiby
JF-Expert Member
- Nov 16, 2009
- 6,899
- 4,623
Ama ndani ya biblia katika kitabu cha methali 3:5 kuna onyo hili. 'mtumaini BWANA kwa moyo wako wote, wala usizitumainie akili zako mwenyewe.
Kwa wale wanaozitumainia akili zao wanapaswa kukumbuka kuwa, elimu ya dunia hii itakusaidia katika fedha, riziki lakini kumbuka jambo moja huna budi kufa. Sasa hiyo haidhuru una elimu kiasi gani. Mkristo hawi mkristo kwa kujiunga na dhehebu fulani au elimu fulani ya kundi fulani, mkristo ni mkristo kwa kuzaliwa upya katika ufalme wa Mungu. Maana isipokuwa umeteulowa kuzaliwa upya hauwezi, kwani Bwana Yesu alisema hakuna awezae kuja kwangu asipokuwa amevutwa na baba, na wote aliyonipa baba watakuja.
Hakuna mahali hata pamoja katika biblia, panapotaka watu kulielewa neno la Mungu zaidi ya kutakiwa kuliamini. Kwani kama unalifahamu(elewa basi unabatilisha imani. Kama ningelikuwa namfahamu Mungu isingenibidi kumwamini. Vivyo hivyo silifahamu neno la Mungu ila naliamini kwa kulikubali.
Katika ayub 38:2-4 kuna maneno haya 'Ni nani huyu atiae mashauri giza kwa maneno yasiyo maarifa? Basi jifunge viuno kama mwanamume, maana nitakuuliza neno nawe niambie. Ulikuwa wapi nilipoiweka misingi ya nchi? Haya! Sema kama ukiwa na ufahamu.
BWANA MUNGU WA MANABII WATAKATIFU NA ATUJALIE KULITAFAKARI NENO LAKE KWA KULIAMINI.
Kwa wale wanaozitumainia akili zao wanapaswa kukumbuka kuwa, elimu ya dunia hii itakusaidia katika fedha, riziki lakini kumbuka jambo moja huna budi kufa. Sasa hiyo haidhuru una elimu kiasi gani. Mkristo hawi mkristo kwa kujiunga na dhehebu fulani au elimu fulani ya kundi fulani, mkristo ni mkristo kwa kuzaliwa upya katika ufalme wa Mungu. Maana isipokuwa umeteulowa kuzaliwa upya hauwezi, kwani Bwana Yesu alisema hakuna awezae kuja kwangu asipokuwa amevutwa na baba, na wote aliyonipa baba watakuja.
Hakuna mahali hata pamoja katika biblia, panapotaka watu kulielewa neno la Mungu zaidi ya kutakiwa kuliamini. Kwani kama unalifahamu(elewa basi unabatilisha imani. Kama ningelikuwa namfahamu Mungu isingenibidi kumwamini. Vivyo hivyo silifahamu neno la Mungu ila naliamini kwa kulikubali.
Katika ayub 38:2-4 kuna maneno haya 'Ni nani huyu atiae mashauri giza kwa maneno yasiyo maarifa? Basi jifunge viuno kama mwanamume, maana nitakuuliza neno nawe niambie. Ulikuwa wapi nilipoiweka misingi ya nchi? Haya! Sema kama ukiwa na ufahamu.
BWANA MUNGU WA MANABII WATAKATIFU NA ATUJALIE KULITAFAKARI NENO LAKE KWA KULIAMINI.