Siasa za Zanzibar na Hatima ya Tanzania

MwanaDiwani

JF-Expert Member
Mar 22, 2013
5,536
2,264
Kwa mwananchi yoyote ambaye yuko nje ya uwanja wa siasa za Zanzibar anaweza akajidanganya kama anazifahamu na kuzielewa siasa za Zanzibar. Siasa za Zanzibar ni zaidi ya wengi wazijuavyo!.

Kuzifahamu siasa za Zanzibar ni lazima uijongee historia yake kwa mapana na marefu. Ndani ya mapana na marefu ya historia ya Zanzibar utapata mshangao kama siyo simanzi.

Kuna baadhi ya kikundi cha watu au vyama vya siasa wamezivamia siasa za Zanzibar wakitumia msingi wa adui wa adui yako ni rafiki yako bila kuelewa kuwa hata yeye anaweza akawa pia ni adui yako.

Kwa watu wanaotumia fikra pana wanaweza wakaelewa msingi wa hoja yangu hasa wakioanisha na tukio la Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Othman Masoud Othman lililotokea kwenye Bunge Maalum la Katiba ambapo ilibidi apate ulinzi ambao ni haki yake kikatiba kwa faida ya maisha yake na taifa kwa ujumla.

Itakumbukwa kuwa, kabla ya tukio hili kutokea, kulikuwa kuna ujumbe uliosambazwa kwa kasi katika mitandao ya kijamii, ili kuwagombanisha na kuwafitinisha wajumbe wa kundi la 201 kutoka Zanzibar.

Ujumbe huo uliwataka wajumbe wa kundi la 201 kutoka Zanzibar, kuondoka bungeni ili theluthi mbili ya Katiba inayopendekezwa isipatikane. Kwa habari zaidi unaweza kusoma hapa,
Ukijiuliza kwa nini haya yote yanatokea kwa upande wa Zanzibar, jibu utalipata kwa kuangalia historia ambayo ilizaa siasa ambayo ilizaa vyama vya siasa Zanzibar. Siasa za Zanzibar ni matokeo ya historia yake.

Huwezi kuifuta historia ya Zanzibar kwa kutumia Katiba ya zamani au katiba mpya bila kujali kama ni Katiba ya Tanzania au Zanzibar.

Ndani ya siasa za Zanzibar, ninawafananisha CHADEMA na msemo usemao, Kwenye kila msafara wa mamba na kenge wamo.

Siasa za Zanzibar hazibebi political opportunist kama CHADEMA.
 
Chadema la kuvunda wamshindwa kabla hata ya safari haijaanza.
 
MwanaDiwani hivi wajumbe wa ukawa mliowalazimisha kupiga kura ili kutimiza akidi mtawataja? Maana hata wajumbe waliopiga kura za siri wanajulikana....hivyo basi mtutajie ni wajumbe gani na aina ya kura watakazopiga....otherwise mnachakachua kama mlivyozoea kuchakachua kwenye chaguzi. Kuhusu AG wa Zanzibar amelinda kiapo chake cha kuilinda katiba ya Zanzibar na huyu ni shujaa....amemshinda hata Bosi wako kwa kushindwa kuilinda katiba ya JMT pale wazanzibar walipofanya mabadiliko ya katiba na kufanya tuwe na Serikali mbili na nchi mbili na sio Serikali moja nchi mbili tena. I know ur so conservative and I'm not expecting u to agree with the facts.
 
Last edited by a moderator:
Ukiwa CCM unajiona uko sahihi lakini Historia hiyohiyi inaonyesha kuwa MPAKA MZEE KARUME ANATUTOKA MWAKA 1972 TANU HAIKUWEZA KUJIPENYEZA KWENYE SIASA ZA ZANZIBAR MPAKA NYERERE ALIPOLAZIMISHI IJIUNGE NA ASP MWAKA 1977 BAADA YA KIFO CHA KARUME KAMA KARUME ANGEKWEPO CCM ISINGEKUWEPO.
LAKINI MUUNGANO WETU ULIKUWA WA VYAMA VIWILI.
KWA KULITAMBUA HILO KWA SIASA ZA ZANZIBAR KWA SASA AMBAPO TANU KWA UWINGI WAO HUWA WANAWACHAGULIA WAZANZIBAR RAIS PALE DODOMA HIVYO JAMAA WANAWEKA NGUMU CHINI KWA CHINI WAWEZE KUWA NA HADHI YA MWANZO.
TANU WAACHIENI ASP KAMA MLIVYOONA MTAIMEZA ZANZIBAR WAKAIACHIA MAMLAKA KIDOGO HIVYOHIVYO ASP ITOLEWE NDANI YA CCM MSIOGOPE KWA KUWA HAMNA WANACHAMA WA TANU KULE VISIWANI.
HUO NDIO UKWELI.
 
MwanaDiwani ndugu go straight acha kuzunguka zunguka!!This is a fact:

(1)AG Othman HAJAPIGA kura kama yy Othman bali kama msimamizi wa maslahi ya ZNZ ndani ya katiba hii

(2)AG Othman na Baraza lote la Mawaziri walikuwa na kikao wiki ya jana ZNZ wakakubaliana kuwa sababu baadhi ya vipengele vyao 17 havijakubaliwa na akina Sitta akakatae katiba hiyo

(3)Kipengele cha ZNZ kukopa kimataifa hadi "Tanzania"wakubali ndiyo kimewakasirisha zaidi ZNZ

(4)Kujiondoa kwa Waziri wa Sheria ZNZ Abubakr Khamis na baadae kujiuzuru kisha kurudi nyumbani kwake Tunguu kwa AG Othman ndiyo ilikuwa MWISHO wa katiba hii!Haya mengine ya Sitta ilikuwa mbwembwe zake tu
 
Last edited by a moderator:
Nape Nnauye unahangaika sana! Mwenyewe siasa hizo za zanzibar huzijui zaid ya kusoma historia ambayo pia huielewi! Hebu tueleze, waliomtishia AG mle ndani ya BMK walikua Chadema? Mwaka huu lazima mjinyee na Sitta wako, na lazima mkafufue chama chenu cha CCJ! Hamna pa kutokea walai! Na laana iwe juu yenu!
 
Last edited by a moderator:
Nape Nnauye unahangaika sana! Mwenyewe siasa hizo za zanzibar huzijui zaid ya kusoma historia ambayo pia huielewi! Hebu tueleze, waliomtishia AG mle ndani ya BMK walikua Chadema? Mwaka huu lazima mjinyee na Sitta wako, na lazima mkafufue chama chenu cha CCJ! Hamna pa kutokea walai! Na laana iwe juu yenu!
Ndugu,
Watu ambao hawana hoja mbadala huwa wanakimbilia kutaja taja majina ya waleta hoja ili kuwaaminisha wasomaji kama wanawafahamu, na kwa kufanya hivyo, wasomaji wazikubali hoja zao muflisi.

Nani amekuambia mimi ni Nape Nnauye?. Nape Nnauye ana Verified Id hapa Jf.

Usipende kuvunja kanuni na taratibu za Jf ukidhani hoja yako muflisi itakubaliwa. Hapa Jf kinachokubaliwa ni hoja mbadala.

Wewe hunifahamu kama mimi nisivyokufahamu.

Jikite kwenye hoja iliyoko mezani, na kama huwezi kujenga hoja mbadala, hata kusoma na kuondoka nayo pia inahesabiwa ni mchango kihoja.
 
MwanaDiwani ndugu go straight acha kuzunguka zunguka!!This is a fact:

(1)AG Othman HAJAPIGA kura kama yy Othman bali kama msimamizi wa maslahi ya ZNZ ndani ya katiba hii

(2)AG Othman na Baraza lote la Mawaziri walikuwa na kikao wiki ya jana ZNZ wakakubaliana kuwa sababu baadhi ya vipengele vyao 17 havijakubaliwa na akina Sitta akakatae katiba hiyo

(3)Kipengele cha ZNZ kukopa kimataifa hadi "Tanzania"wakubali ndiyo kimewakasirisha zaidi ZNZ

(4)Kujiondoa kwa Waziri wa Sheria ZNZ Abubakr Khamis na baadae kujiuzuru kisha kurudi nyumbani kwake Tunguu kwa AG Othman ndiyo ilikuwa MWISHO wa katiba hii!Haya mengine ya Sitta ilikuwa mbwembwe zake tu
Ndugu Malafyale ,
Wajumbe wa Bunge Maalum hawatambuliwi ndani ya Bunge Maalum kwa nyadhifa zao bali kwa Taasisi, Asasi na vyama vya siasa kama ilivyoainishwa kwenye Ibara ya 22 ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83.

Ibara hiyo inasema hivi,
22.-(1) Kutakuwa na Bunge Maalum litakalokuwa na wajumbe wafuatao:
(a) wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano;
(b) wajumbe wote wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar;
(c) wajumbe mia mbili na moja watakaoteuliwa kutoka:
(i) asasi zisizokuwa za kiserikali;
(ii) asasi za kidini;
(iii) vyama vya siasa vilivyo na usajili wa
kudumu;
(iv) taasisi za elimu ya juu;
(v) makundi yenye mahitaji maalum katika jamii;
(vi) vyama vya wafanyakazi;
(vii) jumuiya ya wakulima;
(viii) jumuiya ya wafugaji; na
(ix) kikundi kingine chochote cha watu wenye malengo yanayofanana
Hakuna neno Waziri au binadamu inayeitwa Waziri ndani ya Bunge Maalum.

Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Othman Masoud Othman amepiga kura kama mjumbe na siyo kama Waziri.
 
Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Othman Masoud Othman amepiga kura kama mjumbe na siyo kama Waziri.

Mkuu una uelewa ukweli sema hapa unatafuta relief tu!Rais wa ZNZ na Baraza lake walikutana na AG huyu kabla ya kura hizi!AG anabeba maslahi mapana ya nchi na AG wa ZNZ alizingatia hayo!

Sitta anahitaji kura 6 ili hawa jumla waliosema hapana 76 wateremke hadi wawe 70 ili 2/3 iweze patikana!Tatizo hao 6 nani atabadili msimamo ikiwa wengine wamewasili tayari ZNZ

Sita anaweza pitisha katiba "kijela jela" anyway!
 
Ndugu,
Watu ambao hawana hoja mbadala huwa wanakimbilia kutaja taja majina ya waleta hoja ili kuwaaminisha wasomaji kama wanawafahamu, na kwa kufanya hivyo, wasomaji wazikubali hoja zao muflisi.

Nani amekuambia mimi ni Nape Nnauye?. Nape Nnauye ana Verified Id hapa Jf.

Usipende kuvunja kanuni na taratibu za Jf ukidhani hoja yako muflisi itakubaliwa. Hapa Jf kinachokubaliwa ni hoja mbadala.

Wewe hunifahamu kama mimi nisivyokufahamu.

Jikite kwenye hoja iliyoko mezani, na kama huwezi kujenga hoja mbadala, hata kusoma na kuondoka nayo pia inahesabiwa ni mchango kihoja.

Sasa hapa una hoja gani? mavi matupu.

Ndio maana Moses Nnauye amekufa hana hata kibanda yeye naye alidhani ni sifa kumpigia kinanda Nyerere. Unaijuwa historia hii? Acha kurukia ya Zanzibar usiyoyajuwa.
 
Kwa mwananchi yoyote ambaye yuko nje ya uwanja wa siasa za Zanzibar anaweza akajidanganya kama anazifahamu na kuzielewa siasa za Zanzibar. Siasa za Zanzibar ni zaidi ya wengi wazijuavyo!.

Kuzifahamu siasa za Zanzibar ni lazima uijongee historia yake kwa mapana na marefu. Ndani ya mapana na marefu ya historia ya Zanzibar utapata mshangao kama siyo simanzi.

Kuna baadhi ya kikundi cha watu au vyama vya siasa wamezivamia siasa za Zanzibar wakitumia msingi wa adui wa adui yako ni rafiki yako bila kuelewa kuwa hata yeye anaweza akawa pia ni adui yako.

Kwa watu wanaotumia fikra pana wanaweza wakaelewa msingi wa hoja yangu hasa wakioanisha na tukio la Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Othman Masoud Othman lililotokea kwenye Bunge Maalum la Katiba ambapo ilibidi apate ulinzi ambao ni haki yake kikatiba kwa faida ya maisha yake na taifa kwa ujumla.

Itakumbukwa kuwa, kabla ya tukio hili kutokea, kulikuwa kuna ujumbe uliosambazwa kwa kasi katika mitandao ya kijamii, ili kuwagombanisha na kuwafitinisha wajumbe wa kundi la 201 kutoka Zanzibar.

Ujumbe huo uliwataka wajumbe wa kundi la 201 kutoka Zanzibar, kuondoka bungeni ili theluthi mbili ya Katiba inayopendekezwa isipatikane. Kwa habari zaidi unaweza kusoma hapa,

Ukijiuliza kwa nini haya yote yanatokea kwa upande wa Zanzibar, jibu utalipata kwa kuangalia historia ambayo ilizaa siasa ambayo ilizaa vyama vya siasa Zanzibar. Siasa za Zanzibar ni matokeo ya historia yake.

Huwezi kuifuta historia ya Zanzibar kwa kutumia Katiba ya zamani au katiba mpya bila kujali kama ni Katiba ya Tanzania au Zanzibar.

Ndani ya siasa za Zanzibar, ninawafananisha CHADEMA na msemo usemao, Kwenye kila msafara wa mamba na kenge wamo.

Siasa za Zanzibar hazibebi political opportunist kama CHADEMA.

Kwa hiyo wewe Kikaragosi cha MAFISEM ndio unaijua Siasa ya Zanzibar hadi kuja kuhara hapa JF asubuhi asubuhi??
 
Kwenye siasa hakuna rafiki au adui wa kudumu. Nakushangaa unaishi kwa kutegemea siasa, bila siasa wanao hawaendi chooni, lakini unashindwa kuelewa simple facts za kwenye siasa. Mbona JK na EL hawakukutana barabarani lakini JK huyu huyu kawaita Dodoma ma RC, DC, DED, RSO, DSO kwa ajili ya kuweka msimamo Pinda ndio mgombea wa CCM bila kujali kuwa hakukutana na Lowasa barabarani. Urafika au uadui kwenye siasa Ni kwa ajili ya maslahi Tu, maslahi yakiisha kila kitu kinaisha. Simple fact
 
Sasa hapa una hoja gani? mavi matupu.

Ndio maana Moses Nnauye amekufa hana hata kibanda yeye naye alidhani ni sifa kumpigia kinanda Nyerere. Unaijuwa historia hii? Acha kurukia ya Zanzibar usiyoyajuwa.
Mark Twain once said, Never argue with stupid people, they will drag you down to their level and then beat you with experience.

Jog on.

Thanks.
 
Ndugu Malafyale ,
Wajumbe wa Bunge Maalum hawatambuliwi ndani ya Bunge Maalum kwa nyadhifa zao bali kwa Taasisi, Asasi na vyama vya siasa kama ilivyoainishwa kwenye Ibara ya 22 ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83.

Ibara hiyo inasema hivi,

Hakuna neno Waziri au binadamu inayeitwa Waziri ndani ya Bunge Maalum.

Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Othman Masoud Othman amepiga kura kama mjumbe na siyo kama Waziri.

We jamaa elewa kitu kimoja..kura ya HAPANA ya Pinda inabeba maana kubwa sana kuliko kura ya HAPANA ya MajiMarefu...sikulazimishi ukubali lakini huo ndio ukweli..kuna watu wengi wasio na ufahamu wa sheria are looking up to AG kwenye mambo ya kisheria na katiba..so him saying HAPANA inabeba maana kubwa sana kwa wazanzibar
 
Mark Twain once said, Never argue with stupid people, they will drag you down to their level and then beat you with experience.

Jog on.

Thanks.

Ni aibu sana mtu kama Mzee Nnauye kufa akiwa anaishi National housing mpaka Makamba akaona aibu akaubeba msiba akauweka nyumbani kwake.
 
Ni aibu sana mtu kama Mzee Nnauye kufa akiwa anaishi National housing mpaka Makamba akaona aibu akaubeba msiba akauweka nyumbani kwake.
Great minds are more likely to enjoy discussing ideas. Average minds are more likely to enjoy discussing events. Small minds are more likely to enjoy discussing people.

Enjoy the moment!.
 
Back
Top Bottom