Shule za selikali za bweni zaanza kufungwa

jonas amos

JF-Expert Member
Jul 4, 2016
3,621
4,401
Salamu wapendwa wana jf
Naomba kuweka wazi kabisa katika hili sipo kwa maslai ya ccm chama tawala au ukawa/chadema kwa wapinzani naomba nisimame kama mtanzania


Siku chache baada ya Mh. Rais wa JAmhuri ya muungano Tanzania Dr. John pombe Magufuli kukataza michango ya aina yoyote ile katika shule zote za serikali. Ikumbukwe tu baada ya kauli hiyo ambayo kisheria tamko la Rais ni sheria na inayofuta ni utekelezaji tu


Baada ya kauli hiyo wadau na wananchi mbalimbali walizungumza wengi wao wakionesha wazi kutokufurahishwa na hilo.


Sasa hapa naomba nielekee kama kichwa cha habari kinavyojieleza

Kutokana na katazo hilo shule mbali mbali za serikali za bweni zimeanza kuwaondoa wanafunzi wake

Ikiwemo mkoa wa katavi
Naomba niistaje kwa majina shule hizo kwa sasa
Wanafunzi wametakiwa kurudi nyumbani mapema iwezekanavyo huku kikao cha wazazi na bodi ya shule vikisubiliwa. Hali hii inatokana na wingi wa wanafunzi hao na shule ikijikuta haina uwezo wa kuwahudumia wanafunzi hak kwa chakula na baadhi ya shule ambazo zilikuwa zikiharakisha ujenzi wa mabweni zikijikuta kusitisha kwa muda huku wakisubir miongozo Kutoka kwa waajiri wao ya mkurugenzi wa halmashauri


Ikumbukwe maeneo ya vijijini wanafunzi wengi wanatoka mbali na mashule ya secondary kwani unakuta kata nzima sekondari ni zaidi ya tatu zinategemea sekondari moja. Aidha kwa wazazi waliowengi wamepokea hili kwa masikitiko makubwa na baadhi niliojaribu kuongea nao bado hawajajua nini wafanye kunusuru elimu kwa vijana wao hasa kulingana na gharama na changamoto za usafiri

Inawezekana kabisa watafiti au washauri wa mh Rais walifanyia Dar pekee ambapo wanafunzi wengi wanatokea nyumbani kwani usafiri wa uhakika unapatikana na pengine kwa gharama nafuu kuliko
Huku kwetu kwanza niseme hakuna ruti za daladala bei ya chini ya usafir ambayo nitatoa hapa mchanganuo wake ni sh. 2000 kwa safari ya kwenda tu hakuna nafasi za wanafunzi kwani safari hizo hufanywa na mabasi makubwa ya mikoani

Mzazi moja

"Nauli ya kutoka nyumban hadi stendi kwa bodaboda ni sh3000
Stand kwenda shule ililo ni sh. 2000
Hivyo kwa asubuhi tu itakuwa ni sh. 5000 manake kwa siku atatumia sh 10000

Uwezo huo mzazi anase sina mie ni bora nilipe chakula na mlizi ambapo huwa ni gunia moja na sh. 5000 thaman ya gunia ni elfu 30000 hivyo ni afadhar alipe hata laki moja kwa mwaka kuliko kulipa tsh. 260, 000/=kwa mwezi


Lakini pia kwa watoto wa kike itakuwa ni Changamoto nyingine kubwa mno hasa kutoka vijana wa kiume wasio wastaarabu hasa bodaboda usishangae baada ya miezi kadhaa wanafunz wakashindwa kumaliza shule kwa sababu za mimba

Ikumbukwe malengo ya kujenga mabweni ilikuwa ni kumpatia mazingira mazuri mwanafunzi ikiwemo muda wa kujisomea kwa uturivu awapo shuleni

Hivyo kama watoto hao watatokea nyumba kuna uwezekano mkubwa ufaulu ukashuka kwa kasi kama ya uchumi

Kwa mikoa kama dar wataathirika nao manake wanafunzi sina uhakika kama watapewa vitambulisho wa shule ili wakapandie kwenye mabasi kwa gharama ya tsh. 200
Manake makonda mmmmmmm nao hawana dogo
Hii ni kwa sekondari tu msingi
Watashindwa kufanya majaribio ya kutosha kwa madarasa ya mtihani hasa darasa la 7


Mh. Naomba ungeruhusu ila kuwe na ukomo selikali bado haina uwezo wa kumuhudumia mwanafunzi hadi kukidhi mahitaji

Bado mzazi anajua uchungu na umuhimu wa elimu ila kwa wenye pesa watoto wao watasoma fedha na baobab sasa kwa wazazi wengi hiku kwetu uwezo huo hakuna ndo mana watoto wanarundikana darasa moja tena wengine wakikaa chini
Mawazir fanyeni kazi ya kushaur kama ilivyokatiba yetu

Najua watoto wa viongozi wengi hawapo shule za kata
Natafta namna ya kwenda ikulu

Sorry nina mwandiko mbaya lakini najua naweza kueleweka wazo langu

Tuseme ni nini sisi

Naomba kuwasilisha
Mods naomba msifute na naomba msiunganishe na uzi mwingine tafadhar wakuu
 
Mleta mada huna lolote!Inaelekea wewe ni kati ya walimu mliokuwa mnanufaika na michango ya wanafunzi.
Mmepewa ushauri wazazi ndio wenye wajibu wa kuji organise na kukusanya michango huku wakiisimamia wenyewe.Ninyi walimu mnataka nini?
Kaka samahani ni vyema ukajibu kistaarabu mimi sio mwalimu na sijasomea uwakimu mbaya zaidi sio mwajiliwa wa selikali wala sekta binafsi nimejiajir na ndo mana natumia jina langu kamili la kwenge chet
 
Mkuu, umeeleza vyema lakini kuna point ya msingi umeikosa..

Michango iliyokatazwa ni Ile ya upande mmoja, yaani kutoka shule kwenda kwa wazazi, ile ambayo imetamkwa Na waalimu tu.

Lakini michango ya pamoja, ambayo inatokaa Na majadiliano baina ya waalimu wa wazazi hiyo haijakatazwa..

Wazazi wanatakiwa wachangie kwa hiari kama vile wanavyo changia kwenye maharusi Na sherehe mbali mbali.

Kumbuka, makubaliano baina ya pande mbili yakifikia hitimisho zuri huwa Sheria ambayo imewekwa Na pande hizo mbili.
 
Ulianza vizuri mada lkn umeimalizia kisiasa. Ushauri wako ni mzuri, pengine utafanyiwa kazi na wakubwa. Kosa moja la kitaalam ambalo pengine hufanywa na watu wengi ni kudhani kuwa kauli ya Rais ni sheria. Rais akitamka jambo, aidha anatoa maagizo au maelekezo. Bado ipo nafasi ya kumshauri naye akapima na kuamua vinginevyo. Kauli ya Rais inaweza tu kuwa sheria pale ambapo kauli hiyo inafuatiwa na presidential decree. Katika hali ya kawaida chombo rasmi kilichokasimiwa mamlaka ya Kutunga sheria, ni Bunge. Tusimtafsiri vibaya Mhe. Rais hasa anapotoa maagizo na maelekezo.
 
Ulianza vizuri mada lkn umeimalizia kisiasa. Ushauri wako ni mzuri, pengine utafanyiwa kazi na wakubwa. Kosa moja la kitaalam ambalo pengine hufanywa na watu wengi ni kudhani kuwa kauli ya Rais ni sheria. Rais akitamka jambo, aidha anatoa maagizo au maelekezo. Bado ipo nafasi ya kumshauri naye akapima na kuamua vinginevyo. Kauli ya Rais inaweza tu kuwa sheria pale ambapo kauli hiyo inafuatiwa na presidential decree. Katika hali ya kawaida chombo rasmi kilichokasimiwa mamlaka ya Kutunga sheria, ni Bunge. Tusimtafsiri vibaya Mhe. Rais hasa anapotoa maagizo na maelekezo.
magagagigikoko kwa suala hili la michango unalizungumziaje/? nani wa kumshauri bwana mkubwa?
 
Mkuu umechanganya kitu hapa
Kuna shule za bweni na za kutwa

Zile za bweni serikali inapeleka chakula yenyewe kwa mfano ttabora boys,kilakala iyunga n.k hizi ni chache tu kati ya shule za bweni za serikali,ambazo hupelekewa chakula hakuna shule inatambulika kama ni ya bweni mzazi akachangia chakula

Kuna shule za kutwa nyingi zinamilikiwa na kata hizi shule kulingana baadhi ya maeneo zilipo na umbali wa vijiji husika vinavyopeleka wanafunzi hapo,waliona pawepo hosteli wanafunzi wanaotoka mbali wawe wanakaa hosteli na wanajichangia chakula,kumlipa mpishi,mlinzi n.k hizi shule hazikusajiliwa kama za bweni bali ni za kutwa
Sasa usichanganye mada kwamba shule za bweni zimeanza kurudisha wanafunzi kitu ambacho si kweli kwa maana shule za bweni chakula upelekewa na serikali

By the way habari yako ni nzuri
Serikali inabidi iliangalie jambo hili kwa ukaribu zaidi
Maana ata mm Nina kijana wangu anasoma shule ya kata na utaratibu wetu tulikuwa tunachangia debe la mahindi na maharage kg 2 ,ikiisha basi unapeleka tena maana walikuwa wanaishi hapo hapo hosteli na ambao.

Wanarudi bado walikuwa wanatakiwa kula chakula cha mchana hapo hapo shuleni ili kumfanya mwanafunzi hajitume kwenye masomo na matunda tumeyaona kwenye matokeo ya mithani ya taifa ya kidato cha pili na NNE yako vizuri,sasa hii kauli ya mkuu Ina madhara makubwa sana na inawachanganya sana wazazi mno
 
Nadhani hadi sasa kuna waraka huu hapa ambao umeelezea vizuri michango inayotakiwa kutozwa, ikiwemo wajibu wa kuanzia Mkuu wa mkoa hadi bodi za shule kuhusu michango muhimu kama vile chakula kwa wanafunzi wa kutwa na chakula pamoja na mahitaji mengine muhimu kwa wanafunzi wa hostel. Unaweza kuusoma Zaidi hapa. Sijui kama kuna waraka mwingine, au kauli ya mheshimiwa rais inafuta waraka huo?
 

Attachments

  • waraka_wa_elimu_namba_3_wa_mwaka_2016_utekelezaji_elimu_bure.pdf
    1.9 MB · Views: 203
Kausheni basi wadau, binafsi nimenufaika sana sana na hii kauli, wanafunz kwenye twition center niliyopo wanafunz wameongezeka kutoka 72 mpk 216 ndan ya nusu wiki, hk ni kiwanda tosha, mapato yamesababisha mshahara kuongezeka mara tatu zaidi. Kutesa kwa zamu mkuu ngoja na wengne wafaid. Sio kila sehem utampinga mkulu, hapa nipo nae 100%
 
Back
Top Bottom