Mpaka kufikia mwaka 2005, shule ya TUSIIME iliyoko Dar es salaam maeneo ya Tabata Segerea ilikuwa inavutia sana wazazi kupeleka watoto wao kutokana na mambo kadhaa kama; Ada ilikuwa ya kawaida, Idadi ya watoto kwa kila mkondo kati ya 25 hadi 30, walimu kujituma na kufuatilia wanafunzi kimasomo (diary ilijazwa kila siku na kukaguliwa kesho yake), chakula kizuri kinachozingatia diet, usafi wa mazingira ulikuwa wa kuridhisha, usafi wa vyoo ulikuwa wa kuridhisha na idadi ya matundu ya choo ilitosheleza idadi ya watoto, n.k
Sasa hivi mambo ni tofauti sana, Ada haishikiki (mwanzoni mwa mwaka jana ilipandishwa kwa takribani asilimia 30 bila maelezo yoyote ya kina kwa wadau/Wazazi), chakula siku hizi ni ugali maharage j3 hadi Ijumaa (hata hivyo chakula chenyewe hakitoshi, ni scramble kwa kwenda mbele, wale watoto legelege mara nyingi hushinda njaa, Ufuatiliaji wa walimu kwa wanafunzi umepungua sana kiasi kwamba hata kwenye diary hawaandiki na hata kama mzazi utawaandikia hawakujibu, Vyoo vichafu pia watoto wanapanga foleni, hakuna tena eneo la watoto kuchezea japokuwa kila Ijumaa wanavaa nguo za michezo n.k
Kwa kuwa mimi ni mdau katika shule hii (watoto wangu wawili wanasoma pale), juzi juzi nilijaribu kudadisi pale shuleni ili kujua ni nini hasa chanzo yote haya. Kati ya walimu watatu nilioongea nao kwa nyakati tofauti walikuwa na mtazamo unaofanana, kwamba ni UBINAFSI WA MWENYE SHULE. Kwamba pamoja na wazazi kulipa Ada kubwa, bado walimu wameendelea kupewa maslahi duni ikiwa ni pamoja na mishahara, na hivyo wengi wao wamekata tamaa na wengine wameanza kuikimbia shule.
Vile vile nikaelezwa kwamba shule haina hata BODI YA WAKURUNGENZI, kila kitu kinaamuliwa na mwenye shule akisaidiana na mke wake, hivyo hawana hata mahali pa kulalamikia.
Binafsi nafikiria kuwahamisha watoto wangu kuanzia mwakani, lakini kabla ya hapo nimeona ni vyema nilete hii kero hapa jamvini huenda mmiliki wa shule hii ni member hapa na anaweza kutupatia majibu. Vinginevyo naomba wadau tuijadili shule hii pamoja na zingine zinazofanana na hii.
Nawakilsha.
Sasa hivi mambo ni tofauti sana, Ada haishikiki (mwanzoni mwa mwaka jana ilipandishwa kwa takribani asilimia 30 bila maelezo yoyote ya kina kwa wadau/Wazazi), chakula siku hizi ni ugali maharage j3 hadi Ijumaa (hata hivyo chakula chenyewe hakitoshi, ni scramble kwa kwenda mbele, wale watoto legelege mara nyingi hushinda njaa, Ufuatiliaji wa walimu kwa wanafunzi umepungua sana kiasi kwamba hata kwenye diary hawaandiki na hata kama mzazi utawaandikia hawakujibu, Vyoo vichafu pia watoto wanapanga foleni, hakuna tena eneo la watoto kuchezea japokuwa kila Ijumaa wanavaa nguo za michezo n.k
Kwa kuwa mimi ni mdau katika shule hii (watoto wangu wawili wanasoma pale), juzi juzi nilijaribu kudadisi pale shuleni ili kujua ni nini hasa chanzo yote haya. Kati ya walimu watatu nilioongea nao kwa nyakati tofauti walikuwa na mtazamo unaofanana, kwamba ni UBINAFSI WA MWENYE SHULE. Kwamba pamoja na wazazi kulipa Ada kubwa, bado walimu wameendelea kupewa maslahi duni ikiwa ni pamoja na mishahara, na hivyo wengi wao wamekata tamaa na wengine wameanza kuikimbia shule.
Vile vile nikaelezwa kwamba shule haina hata BODI YA WAKURUNGENZI, kila kitu kinaamuliwa na mwenye shule akisaidiana na mke wake, hivyo hawana hata mahali pa kulalamikia.
Binafsi nafikiria kuwahamisha watoto wangu kuanzia mwakani, lakini kabla ya hapo nimeona ni vyema nilete hii kero hapa jamvini huenda mmiliki wa shule hii ni member hapa na anaweza kutupatia majibu. Vinginevyo naomba wadau tuijadili shule hii pamoja na zingine zinazofanana na hii.
Nawakilsha.