Shida za ndoa ( maoni ya wanaume)

bahati mbaya

JF-Expert Member
Oct 23, 2012
578
192
Mimi ni mwanamke, nina miaka 36. Tumejaliwa kupata watoto 2 katika ndoa yetu. Kipato cha mme wangu ni cha kawaida maana siyo kwamba anakaa nyumbani naye ni mtafutaji. Kwa lugha nyingine yeye kajiajiri. Mimi ni mwajiriwa wa Serikali ila kipato changu ni cha hali ya chini.

Jambo la kushangaza yeye haudumii familia kwa chakula, mavazi wala Elimu ya watoto. Pamoja na kutonunua chakula bado anapata huduma zote hapa nyumbani bila kujali nani anauhudumia familia yake. Mwanzoni mwa mahusiano yetu alikuwa walao anachangia mahitaji ya familia ingawa siyo kwa kukidhi. Miezi sita iliyopita kachukua mkopo ambao sikujua aliutumia kufanya nini maana nimegundua hivyo baada ya kufuatilia sana. Naelemewa na majukumu ya familia.

Je wanaume wote ndivyo mnavyoishi katika familia zenu?
 
Mod hamishia huu uzi MMU sio mahala pake hapa..na mtoa mada jaribu kupitia majukwaa mbalimbali yaliyomo humu ili ujue wapi pa kupost nini.Pole ila endelea kumlea mumeo umeshamzoesha.
 
Poleeeee! Ndo maana wenzio tunawajengea utamaduni wa kutuhudumia na kuzoea kuchunika tangu stage za awali, ukimzoesha kumuhudmia ndo inakuwa kama hivo tena majukumu yanakuzidi. Hapo tiba ni kuwaambia washauri wenu wa ndoa waongee nae ama na wewe unaanza kujiakausha!
 
Kaa nae mlizungumzie hili lasivyo mtimue nyumbani usimlee kama mtoto mdogo naona yeye kazi yake kwako nikumega baaaasi
 
Aisee kumbe kuna wanaume mashujaa kweli kweli, jamani na sisi tunaumizwa na wanawake hawasupport chochote na wanatuzidi kipato ila tunakufa kiume tu na maumivu yetu. kwahiyo likipatikana dume moja kama hilo si mbaya sana anafidia maimuvu ya wanaume tuliowengi.
 
Kaa nae mlizungumzie hili lasivyo mtimue nyumbani usimlee kama mtoto mdogo naona yeye kazi yake kwako nikumega baaaasi

Je kama hataki mkae mjadiliane? utakuta mwanaume wa hv kila siku hakosi sababu! hao wanaume siku hizi ni wengi sana. pole my dia Mazoea hayo. wanaume wengi siku hizi hawana mshipa wa aibu kabisa.
 
wanawake tumeumbwa kuwawasaidizi sio vichwa vya familia
kama mtu sio kichwa inatisha
 
Mh na wewe embu tukuulize kama kakipato chako ni kadogo unawezaje kuhudumia hiyo familia kwa kila kitu,,, au kaka yetu kuna mtu anamsaidia na yeye kashtukuia kaamua kuwaachia muendelee kumsaidia na yeye aendelee kula bata zake???????
 
Mwanaume daima ni kichwa cha familia. je yeye yupo upande gani? vunja ukimya zungumza na mmeo, ukiona hataki kuzungumza washirikishe washenga, mchungaji/padre/ watu wa karibu kama wazazi
 
Mh na wewe embu tukuulize kama kakipato chako ni kadogo unawezaje kuhudumia hiyo familia kwa kila kitu,,, au kaka yetu kuna mtu anamsaidia na yeye kashtukuia kaamua kuwaachia muendelee kumsaidia na yeye aendelee kula bata zake???????

hili nalo neno
 
Lol! Yaani umenichekesha hadi nimesahau stress zangu. Hivi unajua kuwa mazahausi kama Natalia nao ni ushujaa? Unaomba hela ya saluni (ya kucha, nywele na facial), shopping zisizo na idadi, eating out, mmmh!
Aisee kumbe kuna wanaume mashujaa kweli kweli, jamani na sisi tunaumizwa na wanawake hawasupport chochote na wanatuzidi kipato ila tunakufa kiume tu na maumivu yetu. kwahiyo likipatikana dume moja kama hilo si mbaya sana anafidia maimuvu ya wanaume tuliowengi.
 
Last edited by a moderator:
wanawake tumeumbwa kuwawasaidizi sio vichwa vya familia
kama mtu sio kichwa inatisha
Hapa ndipo ninapounaga unafki wa wanawake karibu wote, likija swala la mkwanja ndio utasikia eti mwanaume kichwa cha familia, tukitoka hapo utawasikia wanapinga mfumo dume na wanataka 50 kwa 50. huu ni ujinga, naunga mkono system ya waraabu kiasi fulani ila siungi mkono kuwakataza wanawake wasiende shule.
 
Lol! Yaani umenichekesha hadi nimesahau stress zangu. Hivi unajua kuwa mazahausi kama Natalia nao ni ushujaa? Unaomba hela ya saluni (ya kucha, nywele na facial), shopping zisizo na idadi, eating out, mmmh!
Na inakela zaidi unakuta pesa yake anakuja kununuwa kigari wakati wewe unaandamwa na madeni kila SACCOS lakini yeye hajui ili mradi watoto waende shule, yeye kazi yake kujisifu tu na kuwashauri ujinga wenzake kwamba mwanangu anasoma shule nzuri English Academia!! mwambie mumeo mumuamishe mtoto wenu shule ya serikali kule hawafundishi. Nyambafu.
 
Hapa ndipo ninapounaga unafki wa wanawake karibu wote, likija swala la mkwanja ndio utasikia eti mwanaume kichwa cha familia, tukitoka hapo utawasikia wanapinga mfumo dume na wanataka 50 kwa 50. huu ni ujinga, naunga mkono system ya waraabu kiasi fulani ila siungi mkono kuwakataza wanawake wasiende shule.
mwanamke kulisha familia 100% noo sio fair aisee!
 
Poleeeee! Ndo maana wenzio tunawajengea utamaduni wa kutuhudumia na kuzoea kuchunika tangu stage za awali, ukimzoesha kumuhudmia ndo inakuwa kama hivo tena majukumu yanakuzidi. Hapo tiba ni kuwaambia washauri wenu wa ndoa waongee nae ama na wewe unaanza kujiakausha!

inaelekea wewe umekaa kibiashara sana. Kwani haki mnazozidai sio hizo? Simtetei ila msipende kukwepa majukumu sana kama mtu wewe. Maisha ni kusaidiana na sio kuchunana. Huo sio utu!
 
Back
Top Bottom