Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo...

Ta Ruta,


Binafsi nilishasema kuwa JK na serikali yake hawana nia njema kwenye suala la katiba mpya. Toka mwanzo, Waziri Kombani na AG walikuwa wanajikanyaga kwani hawakujua kitu gani wananchi wanataka. Hata JK mwenyewe hakujua pia na alikiri hayo mbele ya vingozi wa CHADEMA.

Hata Wabunge walipoptisha mswada wa hii sheria kwa mara ya kwanza, nilionga na baadhi yao na kuwaeleza kuwa wangetumia busara kidogo kujielimisha ni kitu gani hasa wananchi wanahitaji. Badala yake, viongozi wetu wameendekeza ushabiki.

Kwa hapa tulipofika, tunahitaji akina Mtikila kuchukua hatua ili kutuepusha na huu usanii ambao unaweza kutuletea matatizo makubwa huko mbele ya safari.

mtikila ni sawa lakini nasi tuanze kujenga utamaduni wa kukataa kuburuzwa na hawa mafisadi........
 
kwa sheria ya mabadiliko ya katiba kukataza wananchi wasijadili kuhusu kuwepo kwa muungano au la ila kwa nia ya kuuboresha tu huko ni kuminya uhuru wa kutoa maoni, na sheria hii inalazimisha kuwepo kwa muungano na kuwepo kwa serikali ya mapinduzi zanzibar, kwa hiyo hapo mwananchi anabakia na maoni ya serikali tatu au mbili kama zilivyo sasa, maana yake ni kuyaweka jela mawazo ya watu kwa kuwachagulia mambo ya kusema badala ya kuwaacha waseme wanavyotaka! serikali inaogopa nini kuwapa watu uhuru wa kutoa mawazo yao bila kuwapangia cha kusema? je kweli katiba hii itakuwa na haki ya kuitwa imeandikwa na wananchi wenyewe? tatizo ni nini iwapo mwisho wa siku watu watapiga kura ya maoni, mchakato huu ni sawa na mwalimu kuwachagulia wanafunzi topics 4 kutoka kwenye syllabus yenye topics 10 baadae anawapa mtihani kutokana na hizo topics 4 alizowafundisha halafu wakifaulu huo mtihani aseme wamefuzu kumbe si kweli kwa sababu ili wafuzu walitakiwa wawe na uelewa wa topics zote kumi za kwenye mtaala huo.
Katiba mpya inaweza ikaja lakini naamini haitotatua sintofahamu ya muungano ndo maana mimi naungana na wazanzibari wanaotaka kwanza kura ya maoni kuhusu muungano halafu ndo tujadili katiba kwa maana matokeo ya kura ya maoni ndo yatakayoamua kama tunahitaji katiba ya muungano au vinginevyo.
NB: KASHESHE ZA MUUNGANO ZITAENDELEA KUWEPO

tatizo tulilonalo ni kuwa hatuna utaratibu ambao ni shirikishi wa kunuia mtanzania wa kawaida ashiriki katika zoezi hili na ndiyo maana viongozi huweka watu wao wafanye kile ambacho kitagusa matakwa yao tu......
 
kupanga si kuuza jk na washauri wake wamekaa ofisini na kuzuru nchi za wenzetu kila kukicha wakati hajui hata waliomchangua wanahitaji nini.2015 kijani kitabadilika rangi na kuwa chekunduuu khaki ya nani tena....
 
kupanga si kuuza jk na washauri wake wamekaa ofisini na kuzuru nchi za wenzetu kila kukicha wakati hajui hata waliomchangua wanahitaji nini.2015 kijani kitabadilika rangi na kuwa chekunduuu khaki ya nani tena....

yote machoni pa Mungu yawezekana...................ingaaje kwa mwanadamu ni kitendawili.....
 
Mkuu, yote uliyosema ni sahihi kabisa lakini kuna mambo kadhaa madogo madogo lakini ya msingi yunapaswa kuyaangalia.
Jana baada ya kupata wazo kutoka chombo kimoja cha habari cha nje, niliingia kwenye Google search, nikaandika Tanzanians are....
Kipengele cha mwanzo kilichokuja kilikua Tanzanians are....lazy ndio mengine yakafuata

Hii ni qualification mpya aliyoiweka PM Pinda katika kikao hiki cha bunge. Huko nyuma kuna watu waliambiwa "wanafikiri kwa masaburi, wana wivu wa kike, ni waoga, wanapenda kulalamika ovyo n.k., yote haya na mengine yanaweza kuwa matusi dhidi yetu lakini ndani yake yana ukweli usiopingika.

Hivi Tanzania, Watanzania, tuko vilaza kiasi gani wa kutoyaona hayo uliyotaja juu ya uvunjwaji wa katiba? Hivi nchi hii haina wanasheria huru (acha wale walafi wanaonunuliwa kwa "kitu kidogo), ambao wangelisimamia kidete suala la marekebisho ya katiba kisheria, mahakamani, kuanzia ya ndani Mahakama ya Katiba hadi mahakama za kimataifa ikibidi?

Kinyume chake tumefumba macho, masikio na midomo, hata tukisema tunaishia kulalamika tu. Tunasubiri mpaka katiba mpya ipitishwe kwa wanavyotaka wao, tunasubiri 2015 ili "tuwaondoe madarakani".

Watanzania, maslahi ya Tanzania haifikii kikomo 2015, ni ya daima. Katiba inayotakikana sio ya kumuondoa nani madarakani bali kwa ajili ya maslahi ya kudumu ya Tanzania, bila ya kujali nani anatawala. Tungekuwa na katiba inayotamka wazi kuwa hakuna aliye juu ya sheria (mfano, tafauti na kipengele cha sasa "Tume ikishatangaza matokeo ya raisi hakuna mahakama ya kupinga matokeo hayo.... Raisi hawezi kushitakiwa akiwa madarakani",...haya si matusi Watanzania?), kiongozi yeyote angefikiri kwanza kabla ya kufanya utumbo kwani "Katiba" ya kumhukumu ipo.

Leo tunakwenda kujadili "KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO" lakini tunalazimishwa na tunatishwa tujadili KATIBA tu bila ya kuujadili MUUNGANO, na atakayefanya hivyo tayari kuna adhabu imeshaandaliwa. Hiki ni kichekesho Watanzania, ni matusi. Na kama tukikubali kwenda na upuuzi huu, PM Pinda atakuwa yuko sahihi kuwa "[We]Tanzanians are lazy"
 
THE HYPOCRISY OF ENACTING A NEW CONSTITUTION.



For ccm and president kikwete, it is easier to expose their hypocrisy but with the opposition it is all a different gameplan altogether to do it! Neither did the ccm manifesto of 2010 nor did Kikwete campaign trail of the same year hinted of a political will to rewrite a new constitutional order and panning out of this both CCM and Kikwete are turncoats as far as this constitutional process is concerned. Both CCM and Kikwete embraced a new constitutional process just to stay relevant in our political terrain but have neither the determination nor the political will to bequeath to us a well meaning constitution.

But the opposition ranks can easily deceive many if you have been keen at following the ear deafening decibels generated by them. To their credit some opposition parties had garnished a quest for a new constitutional order into their manifesto and made that an election issue, too. After a bungled 2010 election where the real winner of presidential race was flashed out by unjust electoral system well oiled by the government in power through NEC (a national electoral body carefully handpicked by an incumbent president to do him a favour and announce him as a president –elect) and TISS ( an intelligence national body that is notorious at rigging all our post-one party elections since 1995), the opposition went berserk demanding a new constitutional order that will assure them people's power that was perceived stolen from them by the treacherous electoral terrain.


On their part, ccm through ministerial outbursts the impression we were getting was that the effort to rewrite the constitution was too costly and an exercise in futility. But ccm; seeing that it was getting the scissors whether from the streets or from the vociferous media waves, decided to cave in a manner that will protect the interests of the status quo ante. First ccm avoided to follow the law where in the hitherto constitution only the house has the power to effect the changes it deems fit. The problem for ccm were multifarious in many fronts: First almost one third of members of the House belong to the opposition bench and a number of young ccm MPs who refuse to kowtow the established party position is growing in line with the public opinion. Under this new political complexion, ccm mandarins felt insecure to follow the constitution in enacting the law that will guide the whole constitutional changing process.


According to Rev. Mtikila v. Attorney General Case urging for independent candidates, the full bench of the Appeals court made it clear that it is only the House that has the legal power to change the constitution and if the process clearly laid down in the constitution was not followed the courts could be called to interfere and rectify the illegalities. But now ccm led constitutional process has defied the highest court of the land when it embarked to enact an act of parliament that has vitiated the constitutional onus of the House to rewrite the constitution! Out of this, unconstitutional creatures such as the presidential commission empowered to collate constitutional views, two Houses of Isles and of the United Republic of Tanzania let alone referendum leeway were enacted to confuse the electorate that we are on the right track to deliver a new order while the concomitant order was only receiving a cosmetic facelift.


Parliament has no powers to incorporate or delegate her constitutional authority in the existing constitution and by extension cannot seek solace via a simple majority voting process to revoke what the House has enacted in the constitution through a two third majority. The solution to this archaic encroachment to the existing constitution under frivolous excuses that the ends can justify the means is out right wrong and we ought to ask the constitutional court to rectify these colossal anomalies via court injunctions pending a final determination of the main constitutional dispute.
 
Mkuu, yote uliyosema ni sahihi kabisa lakini kuna mambo kadhaa madogo madogo lakini ya msingi yunapaswa kuyaangalia.
Jana baada ya kupata wazo kutoka chombo kimoja cha habari cha nje, niliingia kwenye Google search, nikaandika Tanzanians are....
Kipengele cha mwanzo kilichokuja kilikua Tanzanians are....lazy ndio mengine yakafuata

Hii ni qualification mpya aliyoiweka PM Pinda katika kikao hiki cha bunge. Huko nyuma kuna watu waliambiwa "wanafikiri kwa masaburi, wana wivu wa kike, ni waoga, wanapenda kulalamika ovyo n.k., yote haya na mengine yanaweza kuwa matusi dhidi yetu lakini ndani yake yana ukweli usiopingika.

Hivi Tanzania, Watanzania, tuko vilaza kiasi gani wa kutoyaona hayo uliyotaja juu ya uvunjwaji wa katiba? Hivi nchi hii haina wanasheria huru (acha wale walafi wanaonunuliwa kwa "kitu kidogo), ambao wangelisimamia kidete suala la marekebisho ya katiba kisheria, mahakamani, kuanzia ya ndani Mahakama ya Katiba hadi mahakama za kimataifa ikibidi?

Kinyume chake tumefumba macho, masikio na midomo, hata tukisema tunaishia kulalamika tu. Tunasubiri mpaka katiba mpya ipitishwe kwa wanavyotaka wao, tunasubiri 2015 ili "tuwaondoe madarakani".

Watanzania, maslahi ya Tanzania haifikii kikomo 2015, ni ya daima. Katiba inayotakikana sio ya kumuondoa nani madarakani bali kwa ajili ya maslahi ya kudumu ya Tanzania, bila ya kujali nani anatawala. Tungekuwa na katiba inayotamka wazi kuwa hakuna aliye juu ya sheria (mfano, tafauti na kipengele cha sasa "Tume ikishatangaza matokeo ya raisi hakuna mahakama ya kupinga matokeo hayo.... Raisi hawezi kushitakiwa akiwa madarakani",...haya si matusi Watanzania?), kiongozi yeyote angefikiri kwanza kabla ya kufanya utumbo kwani "Katiba" ya kumhukumu ipo.

Leo tunakwenda kujadili "Katiba ya Jamhuri ya Muungano", lakini tunalazimishwa na tunatishwa tujadili KATIBA tu bila ya kuujadili MUUNGANO, na atakayefanya hivyo tayari kuna adhabu imeshaandaliwa. Hiki ni kichekesho Watanzania, ni matusi. Na kama tukikubali kwenda na upuuzi huu, PM Pinda atakuwa yuko sahihi kuwa "[We]Tanzanians are lazy"

MAMAMMIA..................ninaamini ugumu wa misha utatuzindua kwenye huu usingizi wa pono........
 
Pia wanasheria wasaidie kupinga Mahakamani yale marekebisho ya Katiba ya Zanzibar. Kwa jinsi yalivyopitishwa yamevunja sheria na katiba ya Muungano.
 
..You would expect JK to do this the right way, as it appears this is his only chance of remaining in the good books of Tanzanians. But there are morons around him who will spoil everything.
 
kusema la kweli hilo n tatizo la african yote ,serikali zina kuwa hazijui haki za wananchi wanafanya vitu kwa faida yao ,kusema la kweli changes ya tanzania haiwezi kutokea bcz ukosefu wa human right,, na kujadiliwa kwa katiba ktk bunge ,wanajua kua kila wanacho kifanya n kinyume na sheria bcz wanatakiwa washirikishe wananchi na visiwani pia ili wapate makubaliano na wananchi wafanidike but humo muna mslahi yao wao ,sio ya wananchi,so hawatofikisha popote na maamuzi watatoa ,watafanya wanavyoona wao.
 
Nadhani zaidi ya "ugumu wa maisha" kutuzindua toka usingizi wa pono, pia tunahitaji pia "mapinduzi ya kiakili na kimwamko".

MAMMAMIA mwanadamu ni mvivu wa kuchakarika hadi aone kitanzi kipo shingoni................na kitanzi sasa kimezama shingoni na ubongo lazima uchangamke kutafuta suluhu au vinginevyo kaburi halipo mbali sana.......
 
kusema la kweli hilo n tatizo la african yote ,serikali zina kuwa hazijui haki za wananchi wanafanya vitu kwa faida yao ,kusema la kweli changes ya tanzania haiwezi kutokea bcz ukosefu wa human right,, na kujadiliwa kwa katiba ktk bunge ,wanajua kua kila wanacho kifanya n kinyume na sheria bcz wanatakiwa washirikishe wananchi na visiwani pia ili wapate makubaliano na wananchi wafanidike but humo muna mslahi yao wao ,sio ya wananchi,so hawatofikisha popote na maamuzi watatoa ,watafanya wanavyoona wao.

Wahida usemavyo ni kweli lakini swali langu kwako ni umejiandaa vipi kupambana na hii dhuluma?
 
..You would expect JK to do this the right way, as it appears this is his only chance of remaining in the good books of Tanzanians. But there are morons around him who will spoil everything.

Sooth! Why are soothing and shushing JK out of his real image that he is the political criminal in-chief...................look at his cabinet how it is milking the country dry.................do you want to tell me he is unaware and he is not a collaborator?
 
Back
Top Bottom