UMUGHAKA
JF-Expert Member
- Sep 1, 2021
- 2,157
- 10,756
Nisikuchoshe na usinichoshe, tusichoshane!.
Miaka ya nyuma hawa watu walioitwa wachambuzi wa kandanda akiwemo Shaffih Dauda na wenzie wametupiga sana ndoige kuhusu Kandanda na historia yake ni kwasababu miaka hiyo watanzania wengi walikuwa wavivu kusoma na kutafuta maarifa zaidi yanayohusu soka, kitu kingine pia ilikuwa ni ufinyu wa teknolojia ikiwemo ukosefu wa luninga,ukosefu wa simu janja pamoja na ukosefu wa kimtandao(Internet).
Watanzania wa leo si wa miaka 15 iliyopita kwasababu sasa hivi kuna kila aina ya miundombinu(Facilities)za kupata taarifa kwa urahisi na kurahisisha usomaji.
Sasa wachambuzi wengi wanadhani watanzania wa leo ni mazumbukuku kama wa miaka 15 - 20 iliyopita.
Hii imepelekea wachambuzi wengi wa kandanda walio sahihi na wasio sahihi kupewa jina linalosadifu uhalisia wao "WACHAMBUZI WA MICHONGO".
Kitendo cha Shaffih Dauda kusema ya kwamba "Emiliano Martinez ndiye goli kipa wa kwanza kutoka America kusini kushinda tuzo ya goli kipa bora wa kombe la dunia" kimenisikitisha sana na kuwaza mambo mengi sana kuhusu huyu jamaa na wachambuzi wengine niliyowaamini na bila shaka watanzania wengi wapenda soka watakuwa walishangaa sana na kutoamini kama kweli ni yeye ndiye aliyetoa ile posti.
Shaffih Dauda kama mchambuzi nguli wa kabumbu hapa nchini alijizolea umaarufu hadi kuaminiwa na makampuni makubwa na kuwa balozi wao,ukiachana na mambo ya ubalozi pia aliweza kuwashawishi wadau mbalimbali kudhamini michuano ya ndondo cup ambako huko amejipatia mipesa ya kutosha.
Sasa nilichogundua ni kwamba,hawa wachambuzi wa miaka hiyo akiwemo Shaffih Dauda mwenyewe, walitudanganya sana kwasababu watanzania wengi tulikuwa si wafuatilia mambo na kujikuta tunavutiwa nao tukiamini wanalifahamu soka kumbe ilikuwa sivyo!.
Kitendo cha Shaffih Dauda kukosolewa hadharani na mpigania haki Malisa kinaonyesha namna ambavyo jamaa halijui soka bali ni kanjanja,hivi ni kweli kabisa Shaffih hili halikuwa halifahamu mpaka kufahamishwa na mtu ambaye uchambuzi wa soka si kazi yake?,hivi kweli kwa teknolojia ya leo alishindwa hata ku-google ili kuhalalisha uchambuzi wake?,au ni mapenzi na mahaba ya Emiliano Martnez ndiyo yalifanya aposti ule ujinga.
Hiki kitendo kimefichua mambo mengi sana kwa jamaa na tafsiri yake ni kwamba,hata hapo Clouds ashukuru miaka hiyo anapata ajira bado wabongo wengi walikuwa vilaza kwenye masuala ya soka, kupitia uongo wake jamaa leo amejipatia maisha mazuri sana.
Kibaya zaidi bado anataka kuendeleza uongo kwenye dunia ambayo imejaa wasomi,wafuatilia mambo na watu makini katika soka,akiendelea na ujinga huu katika dunia ya watu wanaojua zaidi yake ataumbuka kwa ukanjanja wake.
Ni hayo tu.
Miaka ya nyuma hawa watu walioitwa wachambuzi wa kandanda akiwemo Shaffih Dauda na wenzie wametupiga sana ndoige kuhusu Kandanda na historia yake ni kwasababu miaka hiyo watanzania wengi walikuwa wavivu kusoma na kutafuta maarifa zaidi yanayohusu soka, kitu kingine pia ilikuwa ni ufinyu wa teknolojia ikiwemo ukosefu wa luninga,ukosefu wa simu janja pamoja na ukosefu wa kimtandao(Internet).
Watanzania wa leo si wa miaka 15 iliyopita kwasababu sasa hivi kuna kila aina ya miundombinu(Facilities)za kupata taarifa kwa urahisi na kurahisisha usomaji.
Sasa wachambuzi wengi wanadhani watanzania wa leo ni mazumbukuku kama wa miaka 15 - 20 iliyopita.
Hii imepelekea wachambuzi wengi wa kandanda walio sahihi na wasio sahihi kupewa jina linalosadifu uhalisia wao "WACHAMBUZI WA MICHONGO".
Kitendo cha Shaffih Dauda kusema ya kwamba "Emiliano Martinez ndiye goli kipa wa kwanza kutoka America kusini kushinda tuzo ya goli kipa bora wa kombe la dunia" kimenisikitisha sana na kuwaza mambo mengi sana kuhusu huyu jamaa na wachambuzi wengine niliyowaamini na bila shaka watanzania wengi wapenda soka watakuwa walishangaa sana na kutoamini kama kweli ni yeye ndiye aliyetoa ile posti.
Shaffih Dauda kama mchambuzi nguli wa kabumbu hapa nchini alijizolea umaarufu hadi kuaminiwa na makampuni makubwa na kuwa balozi wao,ukiachana na mambo ya ubalozi pia aliweza kuwashawishi wadau mbalimbali kudhamini michuano ya ndondo cup ambako huko amejipatia mipesa ya kutosha.
Sasa nilichogundua ni kwamba,hawa wachambuzi wa miaka hiyo akiwemo Shaffih Dauda mwenyewe, walitudanganya sana kwasababu watanzania wengi tulikuwa si wafuatilia mambo na kujikuta tunavutiwa nao tukiamini wanalifahamu soka kumbe ilikuwa sivyo!.
Kitendo cha Shaffih Dauda kukosolewa hadharani na mpigania haki Malisa kinaonyesha namna ambavyo jamaa halijui soka bali ni kanjanja,hivi ni kweli kabisa Shaffih hili halikuwa halifahamu mpaka kufahamishwa na mtu ambaye uchambuzi wa soka si kazi yake?,hivi kweli kwa teknolojia ya leo alishindwa hata ku-google ili kuhalalisha uchambuzi wake?,au ni mapenzi na mahaba ya Emiliano Martnez ndiyo yalifanya aposti ule ujinga.
Hiki kitendo kimefichua mambo mengi sana kwa jamaa na tafsiri yake ni kwamba,hata hapo Clouds ashukuru miaka hiyo anapata ajira bado wabongo wengi walikuwa vilaza kwenye masuala ya soka, kupitia uongo wake jamaa leo amejipatia maisha mazuri sana.
Kibaya zaidi bado anataka kuendeleza uongo kwenye dunia ambayo imejaa wasomi,wafuatilia mambo na watu makini katika soka,akiendelea na ujinga huu katika dunia ya watu wanaojua zaidi yake ataumbuka kwa ukanjanja wake.
Ni hayo tu.