Sh. milioni 300 kununua magari mawili ya serikali

EMT

Platinum Member
Jan 13, 2010
14,483
15,308
Bunge limeidhinisha Sh. milioni 300 kwa ajili ya kununua magari mawili ya serikali. Uidhinishwaji huo umefanywa muda mfupi baada ya serikali kudai kuwa imesitisha kununua magari ya starehe na gharama kubwa ili kupunguza matumizi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mh.Celina Kombani, amesema kuwa fedha hizo zimetengwa kwa ajili ya kununua magari mawili kwa sababu kuna uhaba wa magari.

Hata hivyo, Bunge limeishinisha fedha hizo bila kuhoji madai ya serikali kupunguza matumizi ya anasa. Juhudi za wabunge wa upinzani kupinga matumizi hayo ziligonga mwamba kutokana wingi wa wabunge wa chama tawala walioidhinisha matumizi ya fedha hizo.

Inadaiwa kuwa Sh. milioni 300 zilizoidhinishwa na Bunge kununulia magari hayo mawili zinaweza kununua matrekta sita kwa ajili ya kuwasaidia wakulima na pia kujenga madarasa matano ya shule za msingi.
 
Mshangao zaidi ni pale utakapoambiwa hayo magari ni kwa ajili ya kuwabeba wakuu wa miradi ya malaria kutoka nyumbani hadi ofisini na kuwarudisha nyumbani. Wote hawa wanaishi sehemu moja na wanafanyakazi sehemu moja lakini kila mmoja anahitaji kuwa na gari lake.

Magari waliyokuwa wanatumia awali yamechakaa kwa sababu ni miaka miwili sasa tangu yanunuliwe.
 
Tatizo watu wemekuwa walalamikaji kwa serikali tu wakati vyama vya siasa vinafanya ufisadi mkubwa watu mpo kimya.

Chadema wametumia milioni 400 kununua Fuso 2 hakuna aliyelalamika, Chadema wamenunua pikipiki za M4C China kila moja milioni 3 zipo pikipiki 100.

Lema alikwenda Uingereza kununua Chopa akapiga na picha mpaka leo kimya hakuna wa kuhoji.

Cc.. Chris Lukosi, chama
 
Last edited by a moderator:
Tatizo watu wemekuwa walalamikaji kwa serikali tu wakati vyama vya siasa vinafanya ufisadi mkubwa watu mpo kimya.

Chadema wametumia milioni 400 kununua Fuso 2 hakuna aliyelalamika, Chadema wamenunua pikipiki za M4C China kila moja milioni 3 zipo pikipiki 100.

Lema alikwenda Uingereza kununua Chopa akapiga na picha mpaka leo kimya hakuna wa kuhoji.

Cc.. Chris Lukosi, chama

Hii tabia ya kulinganisha kila ovu la serikali na chadema, inapotosha maana ya serikali! Acheni kulinganisha chama cha siasa na serikali iliyopo madarakani!
 
Last edited by a moderator:
Tatizo watu wemekuwa walalamikaji kwa serikali tu wakati vyama vya siasa vinafanya ufisadi mkubwa watu mpo kimya.

Chadema wametumia milioni 400 kununua Fuso 2 hakuna aliyelalamika, Chadema wamenunua pikipiki za M4C China kila moja milioni 3 zipo pikipiki 100.

Lema alikwenda Uingereza kununua Chopa akapiga na picha mpaka leo kimya hakuna wa kuhoji.

Cc.. Chris Lukosi, chama, @ZeMacaporo,
Hivi kwanini hunaga utaratubu wa kujibu hoja iliyopo mbele yako na badala yake huwa unarefer to other kind of theft??? Kwani wizi wa huko ndio unaufuta wizi huu wa serikali??? Wewe jadili ni haki hii kweli kunnua gari kwa kumtoa nyumbani na kumrudisha afu ucku analiacha nje anakwenda kulala chumbani kwake wakati watu wanakosa mahitaji muhimu hukovijijin??

Uonavyo wewe unaweza ukajustify haya kwa mtoto wako akakuelewa??? Hivi huwa unajiskilizaga mwenyewe before you talk to other people???Usiwe unapinga kila kitu vingine uwe unatumia kichwa yako kufikiri, kazi ya kichwa sio kufugia nywele na kukuvusha barabara. Tumia kichwa chako kuanalyse mambo critically, some issues hazikuhutaji kusoma degree ya Political Science kuzielewa.
 
Tatizo watu wemekuwa walalamikaji kwa serikali tu wakati vyama vya siasa vinafanya ufisadi mkubwa watu mpo kimya.

Chadema wametumia milioni 400 kununua Fuso 2 hakuna aliyelalamika, Chadema wamenunua pikipiki za M4C China kila moja milioni 3 zipo pikipiki 100.

Lema alikwenda Uingereza kununua Chopa akapiga na picha mpaka leo kimya hakuna wa kuhoji.

Cc.. Chris Lukosi, chama
Hiyo chopa aliyokwenda kununua Lema ililipiwa shi ngapi?
 
Hii tabia ya kulinganisha kila ovu la serikali na chadema, inapotosha maana ya serikali! Acheni kulinganisha chama cha siasa na serikali iliyopo madarakani!

CHADEMA ndio wanaoendesha serikali kwa sasa. 95% ya hotuba ya bajeti ya Pinda ilikuwa ni kuijibu CHADEMA, which means CDM ndio wanaorun the show. Walizoea vyama vya msimu hawa maCCM sasa wamebanwa kweli hadi akina Kinana wanaamua kuzunguka nchi kupima upepo wakati zamani walikuwa wananunua kura na kurudi uchaguzi mwingine, hakuna tena vyama vya msimu mbele ya Chadema
 
Ubinafsi Serikali inachukua kodi kutoka kwa Watanzania wanaoingizi magari ya bei nafuu kusaidia familia zao na kununua magari ya milioni 150 kwa gari.
 
Tatizo watu wemekuwa walalamikaji kwa serikali tu wakati vyama vya siasa vinafanya ufisadi mkubwa watu mpo kimya.

Chadema wametumia milioni 400 kununua Fuso 2 hakuna aliyelalamika, Chadema wamenunua pikipiki za M4C China kila moja milioni 3 zipo pikipiki 100.

Lema alikwenda Uingereza kununua Chopa akapiga na picha mpaka leo kimya hakuna wa kuhoji.

Cc.. Chris Lukosi, chama

Kwa hiyo hata chadema ni wezi.....msikaripiwe nyie peke yenu..
 
Last edited by a moderator:
Siju maf. Ritz ni mgonjwa zaidi Lukosi! unalinganisha Chadema na serikali!
Wonders will never end in Serukambaland!
 
Tatizo watu wemekuwa walalamikaji kwa serikali tu wakati vyama vya siasa vinafanya ufisadi mkubwa watu mpo kimya.

Chadema wametumia milioni 400 kununua Fuso 2 hakuna aliyelalamika, Chadema wamenunua pikipiki za M4C China kila moja milioni 3 zipo pikipiki 100.

Lema alikwenda Uingereza kununua Chopa akapiga na picha mpaka leo kimya hakuna wa kuhoji.

Cc.. Chris Lukosi, chama

Kwanini una wa CC Chris Lukosi na Chama? Wao ndio the SOURCE???
 
Mleta thread nae hajaweka wazi hayo magari ni ya nini, na yatatumika kwa ajili gani. labda ni magari kwa ajili ya Ambulances huko vijijini,
 
Wizi ni wizi tu wafanye Chadema wafanye serikali kama wananchi tuna haki ya kuhoji kodi zetu.
 
For a woman to do such a thing it hurts Celina Kombani historia itakuhukumu. Ni watoto wangapi wangepata fursa ya kufikia ndoto zao kwa hiyo hela? Na zile posho za payroll ulizoziweka za kufanya kazi usiku one on these days Celina Kombani you will pay for not defending the poor especially women and children hear me!
 
haijalishi ni chadema au ccm .......kununua magari la mil 300 wakati kina mama hawana vitanda mwananyamala hospitali....watu wanakufa njaa nchii hiii inaonyesha jinsi gani viongozi wetu hawaelewi hali halisi ya watanzania......hauitaji N.G.O au research ya REPOA kueleza hivi vitu ......pesa nyingi zinaenda kwenye kuandika vitu ambavyo havitekelezwi aibu sana ....ni kweli hata mi sitashangaa haya magari ni kwa ajili ya mradi wa kupunguza umaskini ....
 
Tatizo watu wemekuwa walalamikaji kwa serikali tu wakati vyama vya siasa vinafanya ufisadi mkubwa watu mpo kimya.

Chadema wametumia milioni 400 kununua Fuso 2 hakuna aliyelalamika, Chadema wamenunua pikipiki za M4C China kila moja milioni 3 zipo pikipiki 100.

Lema alikwenda Uingereza kununua Chopa akapiga na picha mpaka leo kimya hakuna wa kuhoji.

Cc.. Chris Lukosi, chama

there you go!......you missed the point.....broda!
 
Tatizo watu wemekuwa walalamikaji kwa serikali tu wakati vyama vya siasa vinafanya ufisadi mkubwa watu mpo kimya.

Chadema wametumia milioni 400 kununua Fuso 2 hakuna aliyelalamika, Chadema wamenunua pikipiki za M4C China kila moja milioni 3 zipo pikipiki 100.

Lema alikwenda Uingereza kununua Chopa akapiga na picha mpaka leo kimya hakuna wa kuhoji.

Cc.. Chris Lukosi, chama

Hivi ndugu unataka kusema kwa kuwa CDM wamenunu magari kwa sh.400m ndio halali serikali kununua magari 2 kwa mil 300?nyie watu msioishi tz mnakera sana.unajua hali ilivyo kwenye hospt zetu? Unajua hali ya shule zetu? kama cdm wamefanya hivyo si sahihi ila kwa serikali ni mbaya zaidi.wacha kuonesha uwezo wako mdogo wa kufikiri unakuwa kama Serukamba bwana
 
Last edited by a moderator:
Serikali taahira, Serikali dhalimu na Serikali a,mbayo haistahili kuendelea kuwepo madarakani ndio inaweza kufanya maamuzi kama haya. Sasa hivi kuna deni kubwa sana, shule zetu ziko katika hali ya kusikitisha sana, hospitali nazo hazitamaniki lakini bado wanatanua kwa matumizi ambayo hayaingii kabisa akilini kila kukicha bila ya huruma kwa walipa kodi. Hakukosea kabisa Mnyika alipmuita Kikwete DHAIFU. Tungekuwa na kiongozi anayewajali Watanzania na kuitakia mema nchi yetu matumizi ya kipumbavu kama haya ambayo hayana tija yoyote kwa Watanzania yasingekuwepo.


 
Back
Top Bottom