ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 43,060
- 49,748
Hayo yameelezwa na Waziri wa Tamisemi Hommed Mchengerwa wakati Akitoa taarifa ya Watoto Waliofaulu na kupangiwa shule za Sekondari mwaka 2024 tayari kuanza utekelezwaji wa Elimu Kwa mtaala Mpya.
===============
WANAFUNZI 1,092,984 ambao walifaulu mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi mwaka 2023 wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza Januari 2024 huku 1,410 wakipangwa kwenye baadhi ya Shule za Sekondari za mkondo wa Amali za kihandisi ikiwa ni kuanza utekelezaji wa mtaala mpya wa elimu.
Akizungumza leo Desemba 17,2023 na waandishi wa habari jijini Mwanza, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Mohamed Mchengerwa, amesema kati ya idadi hiyo wasichana ni 585,051 na wavulana 507,933 wamefaulu na kupangiwa katika Shule za Sekondari za Serikali ili waanze masomo ya Kidato cha Kwanza Januari, 2024.
Amesema idadi hiyo inajumuisha wanafunzi wenye mahitaji maalum 3,587 wakiwamo wasichana 1,590 na wavulana 1,997.
“Wanafunzi waliopangiwa katika shule 48 za bweni za Kitaifa ni 5,606 sawa na asilimia 0.5, katika Shule teule za mikoa ni 17,412 sawa na asilimia 1.6 na Shule 4,566 za Kutwa ni 1,069,966 sawa na asilimia 97.9,” amesema.
Amefafanua kuwa waliochaguliwa shule za wenye ufaulu wa alama za juu ni 942 na watakwenda Shule za sekondari saba ambazo ni Ilboru, Msalato, Kibaha, Kilakala, Mzumbe, Wavulana Tabora na Wasichana Tabora.
“Wanafunzi 1,410 wakiwemo wavulana 1,136 na wasichana 274 wamechaguliwa kujiunga katika Shule za Sekondari tisa za amali za Kihandisi ambazo ni Bwiru Boys, Ifunda, Mwadui, Iyunga, Moshi, Mtwara, Musoma, Tanga na Chato. Idadi hii ya wanafunzi inajumuisha wanafunzi wenye mahitaji maalum 274 wakiwemo wasichana 31 na wavulana 243,”amesema.
Mchengerwa amesema wanafunzi 3,254 wakiwamo wasichana 1,511 na wavulana 1,743 wamechaguliwa kujiunga katika Shule za Sekondari 32 za Bweni za Kitaifa za Kawaida. Idadi hii inajumuisha wanafunzi wenye Mahitaji Maalum 1,629 wakiwemo wasichana 836 na wavulana 793.
Amefafanua kuwa jumla ya Wanafunzi 17,412 wakiwemo Wasichana 7,816 na wavulana 9,596 wamechaguliwa kujiunga na shule za Bweni Teule na zile za wasichana za Mikoa. Shule za wasichana za mikoa saba zimepangiwa wanafunzi wasichana 897 wakijumuishwa wanafunzi wenye mahitaji maalum 116.
TAMISEMI
===============
WANAFUNZI 1,092,984 ambao walifaulu mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi mwaka 2023 wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza Januari 2024 huku 1,410 wakipangwa kwenye baadhi ya Shule za Sekondari za mkondo wa Amali za kihandisi ikiwa ni kuanza utekelezaji wa mtaala mpya wa elimu.
Akizungumza leo Desemba 17,2023 na waandishi wa habari jijini Mwanza, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Mohamed Mchengerwa, amesema kati ya idadi hiyo wasichana ni 585,051 na wavulana 507,933 wamefaulu na kupangiwa katika Shule za Sekondari za Serikali ili waanze masomo ya Kidato cha Kwanza Januari, 2024.
Amesema idadi hiyo inajumuisha wanafunzi wenye mahitaji maalum 3,587 wakiwamo wasichana 1,590 na wavulana 1,997.
“Wanafunzi waliopangiwa katika shule 48 za bweni za Kitaifa ni 5,606 sawa na asilimia 0.5, katika Shule teule za mikoa ni 17,412 sawa na asilimia 1.6 na Shule 4,566 za Kutwa ni 1,069,966 sawa na asilimia 97.9,” amesema.
Amefafanua kuwa waliochaguliwa shule za wenye ufaulu wa alama za juu ni 942 na watakwenda Shule za sekondari saba ambazo ni Ilboru, Msalato, Kibaha, Kilakala, Mzumbe, Wavulana Tabora na Wasichana Tabora.
“Wanafunzi 1,410 wakiwemo wavulana 1,136 na wasichana 274 wamechaguliwa kujiunga katika Shule za Sekondari tisa za amali za Kihandisi ambazo ni Bwiru Boys, Ifunda, Mwadui, Iyunga, Moshi, Mtwara, Musoma, Tanga na Chato. Idadi hii ya wanafunzi inajumuisha wanafunzi wenye mahitaji maalum 274 wakiwemo wasichana 31 na wavulana 243,”amesema.
Mchengerwa amesema wanafunzi 3,254 wakiwamo wasichana 1,511 na wavulana 1,743 wamechaguliwa kujiunga katika Shule za Sekondari 32 za Bweni za Kitaifa za Kawaida. Idadi hii inajumuisha wanafunzi wenye Mahitaji Maalum 1,629 wakiwemo wasichana 836 na wavulana 793.
Amefafanua kuwa jumla ya Wanafunzi 17,412 wakiwemo Wasichana 7,816 na wavulana 9,596 wamechaguliwa kujiunga na shule za Bweni Teule na zile za wasichana za Mikoa. Shule za wasichana za mikoa saba zimepangiwa wanafunzi wasichana 897 wakijumuishwa wanafunzi wenye mahitaji maalum 116.
TAMISEMI