Serikali yatangaza viwango vipya vya alama za ufaulu elimu ya sekondari

Hiyo ni movie inaendelea nimeangalia hizo data sikuamini kama kweli serikali inaweza kuamua kitu cha kuua elimu kiasi hicho!

Naunga mkono hoja. Nimeshindwa kumwelewa Mulugo anapotetea hivyo viwango eti hawajashusha lakini wameondoa tu mlundikano. Kama D ilikuwa inaanzia 35, je kuifanya ianzie 20 siyo kushusha viwango? Kama C ilikuwa inaanzia 50, je kuifanya ianzie 40 siyo kushusha viwango? Kama A ilikuwa inaanzia 81 kuifanya ianzie 75 siyo kushusha viwango? Kwa mujibu wa matokeo ya majaribio ya mfumo huo, kama yangetumika kwa matokeo ya K4 mwaka 2012 ufaulu ungekuwa 93%. Sasa kama bila kufanya mtihani mwingine wizara inaweza kucheza na viwango vya ufaulu na ukapanda toka asilimia 43 hadi 93, je huko siyo kushusha viwango vya ufaulu? Ona jedwali la majaribio
AINA YA WATAHINIWAMWAKADARAJAME%KE%WOTE% YA WOTE
S2012I6,1483.0128591.79,0072.42
S2012II17,6178.6379404.7325,5576.87
S2012III35,67817.481992011.8755,59814.95
S2012I - III59,44329.123071918.390,16224.24
S2012IV132,68765.0112578274.95258,46969.5
S2012I - IV192,13094.1315650193.25348,63193.74
S201211,9625.86113236.7523,2856.26
Analysis ya Wizara kuhusu matokeo ya majaribio ya mfumo mpya
Takwimu katika Jedwali la 3 zimeonesha kuwa kwa kutumia muundo mpya watahiniwa ambao wangefaulu kwa ufaulu
mzuri yaani wale walio kati ya Daraja la I-III ni asilimia 21.22 na wale watakaopata ufaulu hafifu yaani Daraja la IV ni asilimia 70.04. Wanafunzi ambao wangepata ufaulu usioridhisha kabisa ni asilimia 6.26. Kwa mantiki hii mfumo huu uliowazi kwa wote hauna athari ya kuwafanya hata wale ambao hawana uwezo wa kielimu waonekane wana ufaulu mzuri. Hii ina maana bado Taifa linawajibika kuwekeza nguvu zake katika kuimarisha elimu ya sekondari ili idadi kubwa ya wanafunzi iondoke kutoka ufaulu dhaifu na usioridhisha na kuingia kundi la wale wenye ufaulu mzuri na zaidi. Lakini pia ubora wa mfumo ni matokeo ya vitu vingi ikiwemo usimamizi mzuri, umakini na uadilifu ili mfumo uwe na tija
 
Hivi hii movie ya viwango vipya vya ufaulu ikoje? Watoto wetu wamefanya mitihani wakati ma Profesa waliopewa dhamana ya elimu wametangaza viwango viya vya ufaulu. Kila kukicha tunasikia kauli za wanasiasa na wasomi wakivipinga vikali. Sasa je hawa walishirikisha wadau gani? Nini haatma ya vijana wetu waliofanya mitihani 2013?
 
Continuous Assessment ama CA nani atakuwa anatunga mtihani huko Mashuleni? Wakiachiwa walimu watunge kuna uwezekano mkubwa mwanafunzi akawa ana maksi nzuri kwenye CA kutokana na mtihani hafify na zikamusha kwenda hatua nyingine ambako huko uwezekano wa kufeli ni mkubwa sana.

Wenzetu hapo kwenye shule za msingi hazitungi mitihani bali zinaenda kuchukuwa mtihani wilayani hivyo wanafunzi wa wilaya moja wanatahiniwa na mtihani unaofanana

Na waalimu wakware hawatabaki nyuma na hii Fursa ya CA kwa Vigori.
 


Screenshot_2023-08-16-23-57-56-1.jpg
 
Back
Top Bottom