Serikali yamuumbua RC Mbeya

Mimi natoka Kyela na niko tired na hizi tuhuma za kila siku ambazo nyingi hazina maana kabisa.

Kwenye hili la maafa kuna watu wengi sana ambao wanasaidia, wengi wao hata hawahitaji kujitangaza. Kwa mfano hadi leo kuna kikosi cha JWTZ kiko kule kimejichimbia kikijenga madaraja na barabara ambayo imebomolewa. Sijasikia Mwamunyange akitamba sehemu jinsi alivyosaidia. Tunataka watu kama hao, chapa kazi, sifa itakuja baadaye.

Umesomeka MKUU....

Lakini jambo la msingi ni kwamba, mara nyingi tunakwamishwa na fikra hasi. Hata kama unafanya kazi na adui yako, ukiwa chanya, atakwama na kubadilika kuwa upande wako, lakini ukiwa hasi kwa kila mtu, hata rafikiyo atabadilika na kuwa adui yako, ama atakusaliti
 
viongozi wa tanzania wanapenda kufanya kazi kwa kujionyesha au niseme kwa malengo ya kupata sifa na sio kwa moyo wa kusaidia taifa.

mtu wa namna hiyo ndiye siku zote anaepewa kuongoza kwa vile kwa zile sifa zake alipofanya jambo dogo tu alionekana bingwa, lakini kiongozi mchapa kazi ni mara chache sana kusikia angalau kapanda cheo licha ya kusifiwa na wengine.

hao wa chache waliopo tunawapa hongera, lakini si mkuu wa mkoa huyu pekee, nusu na robo ya viongozi serikalini ni wa mfano wake.

suali kwako, tutawakomeshaje?
 
Nikirudi kwenye mada, Ukiondoa migongano ya kisiasa baina ya M'kyembe na M'kipesile, nini nafasi ya Uchifu huko Kyela katika koo hizi mbili?

Kibunango,

Mmmmm!!! kwa kweli sijui maana kwa mimi hata wala sikujua kama Mwakyembe
alikuwa chifu mpaka baada ya kuwauliza Kyela kwa wale watu wa zamani zaidi yangu. Maana yake ni kwamba huo uchifu hauna nguvu kabisa.

Hata nilikuwa sijui Mwakipesile ni chief.

Watu Kyela walichoka na Mwakipesile ukiachia wale wafuasi wake na wale aliokuwa anakula nao. Kujitokeza kwa Mwakyembe ilikuwa furaha kwa wana Kyela wengi. Ndio na yeye alitumia rafu nyingi kupata huo ubunge lakini wapenda maendeleo wengi tuliona bado ni nafuu hata kama hatukufurahia hizi njia za rafu.

Kwahiyo siamini kama uchifu ni issue, naweza kuwa wrong lakini sidhani kama ni issue kabisa kwa Kyela. Mimi hata machifu wa Kyela siwezi kuwataja, siwajui, ukiachia wachache wenye majina makubwa.

Nafikiri tatizo ni ulaji, ubunge unaenda na ulaji na kuwa na wapambe wengi. Wale wa Mwakipesile baada ya mtu wao kukosa ina maana na wao wamekosa ulaji. Ilitakiwa Mwakipesile aseme hapana na kuwakataza ili wasiendelee na mambo ya kampeni hata baada ya uchaguzi. Naamini yeye hajafanya hivyo na bado analitegemea hilo kundi. Mwakyembe naye alitakiwa awe inclusive na kuacha vijembe vya chini chini juu ya wapambe wa Mwakipesile, binafsi siamini kama alifanya hivyo. Matokeo yake makundi mawili ya walaji, moja linakula kwa Mwakipesile na lingine linakula kwa Mwakyembe. Hapo mgogoro hauwezi kuisha.

Ukiniuliza mimi nitasema hilo ndilo tatizo.
 
Umesomeka MKUU....

Lakini jambo la msingi ni kwamba, mara nyingi tunakwamishwa na fikra hasi. Hata kama unafanya kazi na adui yako, ukiwa chanya, atakwama na kubadilika kuwa upande wako, lakini ukiwa hasi kwa kila mtu, hata rafikiyo atabadilika na kuwa adui yako, ama atakusaliti

Mkuu,

Hapo uko sahihi hasa. Ningelikuwa mimi ni Mwakipesile au Mwakyembe, ninge behave tofauti kabisa kwenye huo mgogoro bahati mbaya kila mtu ana njia tofauti ya kushughulikia tatizo.

Mimi nikifanya na adui yangu naamini inaweza kuwa motivating factor, ili mradi yeye sio mwamuzi wa kunipa resources. Sasa kama Mbunge, naamini ana uwezo wa kuchapa kazi zake bila hata kumwangalia wala kumsikiliza mkuu wa mkoa.

Hivyo hivyo kwa mkuu wa mkoa, ana uwezo wa kuchapa kazi na kuendeleza Kyela bila hata kusikiliza Mwakyembe anasema nini.

Itakapofika 2010, sisi wananchi tutajua nani anatufaa zaidi.

Kwa ninavyojua mimi hawa waheshimiwa wote wanafanya kampeni za chini chini na kupakana matope. Sasa wanawaingiza na watu nje ya Kyela na vyombo vya habari kwenye hivyo vita vyao. Tatizo ni kwamba mwandishi wa habari hawezi kujua undani wote kuhusu Kyela na hivyo kuandika habari ambayo inaweza kuwa na upande mmoja zaidi.
 
....heee.....wapambe NUKSI...jamani!!......nuksi kweli kweli wa maendeleo
 
Kibunango,

Mmmmm!!! kwa kweli sijui maana kwa mimi hata wala sikujua kama Mwakyembe
alikuwa chifu mpaka baada ya kuwauliza Kyela kwa wale watu wa zamani zaidi yangu. Maana yake ni kwamba huo uchifu hauna nguvu kabisa.

Hata nilikuwa sijui Mwakipesile ni chief.
Kamanda Mtanzania;
Sina lengo la kupindisha wala kubadili mwelekeo mzima wa bandiko hili. Ila ningependa kukufahamisha kuwa Uchifu huko Kyela bado una nguvu na hasa katika koo za kichifu. Nguvu hizo zimebakia ndani ya koo husika na zile koo ambazo zinatambua kuwa koo fulani imetoka katika uchifu. Zaidi ya ushindani wa madaraka, ulaji na ujiko bado koo hizo za kichifu zinapenda kutukuzwa kichifu, na ukiongezea na mafanikio yao katika Tanzania ya leo.

Mafanikio yao katika siasa za Tanzania ya leo ni muendelezo wa uchifu bora wa enzi zile. Hivyo basi pamoja na upambe, wenyewe wanajua ni nini wanachogombea... Kwa ufupi ni koo gani ya kichifu iliyofanikiwa zaidi katika dunia na Tanzania ya leo isiokuwa na uchifu
 
mkuu Mtanzania Kushiriki Na Kutangaza Kwamba Hakuna Maafa Wala Njaa Huku Watu Wakitaanika Vitu Viwili Tofauti ,,,kibaya Watu Wanaendelea Kufa Na Kibaya Zaidi Cha Tatu Ni Kuidanganya Serikali Ya Jamhuri Ya Muungano Ili Isiwatumikie Wananchi Wake.......
kumbuka Unaweza Kuingia Sehemu Hifadhi(ghse) Na Fotball Yako Mfukoni Na Kuwaonyesha Watu Unaenda Kuitumia Barabara Lakini Ukiingia Ndani Baada Ya Muda Ukatoka Unalia Watu Wasijue Nini Kimetokea Kumbe Mifukoni Zipo Kama Zilivyonunuliwa ...uwe Makini Na Hawa Watu Mtanzania Watatumaliza
ahsante
 
Mtanzania/Halisi
Sijasoma post zenu zote lakini niwape tu angalizo,mimi nimeingia Mbeya saa 4 asubuhi kutoka kyela.Tatizo ni ukiritimba wa Mwakipesile kutokubali yaishe.Kama ni ulaji mbona amepewa cheo RC ambacho maslahi ni sawasawa na ubunge?Amesahau nini ambacho asingeweza kufanya kwa mda wote wa miaka 10(kuanzia 1995-2005).Sisi huku kyela tunamuona kama king'ang'anizi lakini sio kwa maslahi yake bali wanaomtumia.Hilo daraja liliombewa fedha bungeni,lakini kwa sababu lazima kikao cha mkoa(Regional Consultantive Council) kipitishe inakuwa vigumu kutekelezwa kwa sababu RC ni Chairman wa kikao hicho.Amekaririwa akisema watu wa kyela watamkoma,hawezi kupitisha mradi ambao utamnufaisha Mwakyembe kisiasa.Hizi ndio siasa za mbeya ni kukomoana na wananchi kuumia.

Hilo daraja ambalo wamejenga jeshi pale kivuko cha Lusungo,ni busara za Gen.Mwamyange kutumia TPDF kuepuka malumbano yasoisha ya wanasiasa na kujenga taswira nzuri ya jeshi kwa wananchi.Na juzi wananchi waliandaa sherehe kubwa kushukuru kikosi hicho ja jeshi na wananchi wametoa shukrani za dhati za kikosi hicho.RC alikuja kukagua shughuri hizo akiambatana na M?kiti wa CCM(M) Nawab Mullah,lakini wananchi hawakuwatilia maanani.
 
Mtanzania/Halisi
Sijasoma post zenu zote lakini niwape tu angalizo,mimi nimeingia Mbeya saa 4 asubuhi kutoka kyela.Tatizo ni ukiritimba wa Mwakipesile kutokubali yaishe.Kama ni ulaji mbona amepewa cheo RC ambacho maslahi ni sawasawa na ubunge?Amesahau nini ambacho asingeweza kufanya kwa mda wote wa miaka 10(kuanzia 1995-2005).Sisi huku kyela tunamuona kama king'ang'anizi lakini sio kwa maslahi yake bali wanaomtumia.Hilo daraja liliombewa fedha bungeni,lakini kwa sababu lazima kikao cha mkoa(Regional Consultantive Council) kipitishe inakuwa vigumu kutekelezwa kwa sababu RC ni Chairman wa kikao hicho.Amekaririwa akisema watu wa kyela watamkoma,hawezi kupitisha mradi ambao utamnufaisha Mwakyembe kisiasa.Hizi ndio siasa za mbeya ni kukomoana na wananchi kuumia.

Hilo daraja ambalo wamejenga jeshi pale kivuko cha Lusungo,ni busara za Gen.Mwamyange kutumia TPDF kuepuka malumbano yasoisha ya wanasiasa na kujenga taswira nzuri ya jeshi kwa wananchi.Na juzi wananchi waliandaa sherehe kubwa kushukuru kikosi hicho ja jeshi na wananchi wametoa shukrani za dhati za kikosi hicho.RC alikuja kukagua shughuri hizo akiambatana na M?kiti wa CCM(M) Nawab Mullah,lakini wananchi hawakuwatilia maanani.

Mpoki,

Nakubalikana na mengi uliyoyaandika hapo juu ila hilo la kwamba bunge lilipitisha pesa za daraja na imeshindwa kutekelezwa kwasababu mkuu wa mkoa anakwamisha, nafikiri wanaojua sheria za bunge na miradi wanaweza kutuelemisha zaidi hapa.

Mimi nilipokuwa Kyela kulikuwa na uvumi huo huo kwamba bunge limetenga pesa za kujenga barabara moja mkoani Mbeya, na kwamba eti Mwakyembe alimfuata Mwakipesile kumwomba hiyo barabara iwe ni ya Kyela mpaka Ipinda na kwamba Mwakipesile alikwamisha.

Je ni kweli? Mimi sijui ila nina wasiwasi mkubwa mno na statements kama hizo. Sasa naona unaongelea daraja ingawaje mtililiko ni kama ule ule.

Naamini kuna watu wanavumisha hayo maneno hata kama huenda hayana ukweli. Ndio siasa za Kyela ambazo wengine tunazipinga.

Hivi mnaojua mambo ya miradi ya maendeleo mkoani na wilayani, tusaidieni juu
ya nafasi ya mkuu wa mkoa kukwamisha mradi fulani.

Nafikiri mwaka 2010, mmoja atakuwa anasema mnaona mbunge wenu hajafanya chochote, mwingine nilikuwa na mipango mikubwa ila nilikwamishwa na Mwakipesile. Naona kila mchezaji anajipanga kwa scenario hiyo.

Ndio maana Tanzania ni maskini, mabingwa wa kukwamishana na kutafuta sababu.
 
Kamanda Mtanzania;
Sina lengo la kupindisha wala kubadili mwelekeo mzima wa bandiko hili. Ila ningependa kukufahamisha kuwa Uchifu huko Kyela bado una nguvu na hasa katika koo za kichifu. Nguvu hizo zimebakia ndani ya koo husika na zile koo ambazo zinatambua kuwa koo fulani imetoka katika uchifu. Zaidi ya ushindani wa madaraka, ulaji na ujiko bado koo hizo za kichifu zinapenda kutukuzwa kichifu, na ukiongezea na mafanikio yao katika Tanzania ya leo.

Mafanikio yao katika siasa za Tanzania ya leo ni muendelezo wa uchifu bora wa enzi zile. Hivyo basi pamoja na upambe, wenyewe wanajua ni nini wanachogombea... Kwa ufupi ni koo gani ya kichifu iliyofanikiwa zaidi katika dunia na Tanzania ya leo isiokuwa na uchifu

Kibunango,

Huenda una habari ambazo wengine hatuna. Uchifu Kyela? Wabunge wa Kyela toka inakuwa wilaya ni Mwakalukwa, Mwakipesile, Kasupya, Mwakipesile (ni tofauti na Mwakipesile wa mwanzo) na sasa Mwakyembe. Je machifu hapo ni akina nani?

Niko tayari kusahihishwa lakini sioni uchifu kama issue Kyela.
 
Kibunango,

Huenda una habari ambazo wengine hatuna. Uchifu Kyela? Wabunge wa Kyela toka inakuwa wilaya ni Mwakalukwa, Mwakipesile, Kasupya, Mwakipesile (ni tofauti na Mwakipesile wa mwanzo) na sasa Mwakyembe. Je machifu hapo ni akina nani?

Niko tayari kusahihishwa lakini sioni uchifu kama issue Kyela.
Kwa hakika uchifu Kyela bado upo, tofauti kidogo na Rungwe ingawa hawa ni wapinzani wa jadi licha ya kuzungumza lugha moja.

Katika hao uliowataja nimewahi kukuta na Mwakalukwa, Kasupya na Mwakyembe, katika wakati tofauti wa uongozi wao hapo Kyela. Jinsi mazungumzo yao yalivyokuwa ni wazi kuwa wana lengo la kusimamia uchifu japo sio rasmi. Hata wakati wa kifo cha marehemu Mwakalukwa yalizungumzwa hayo kutokana na utata uliojitokeza wakati wa maziko yake.

Kama nilivyosema hapo awali lengo sio kupindisha muelekeo wa mada, ambapo umesimamia kidete kuzungumzia hali halisi ya mafuriko na usambazaji wa misaada kwa waathirika wa mafuriko hayo. Mwakyembe ni koo nyingine ya kichifu ambayo imepanuka hadi Tz Visiwani na kwa muda mrefu imekuwa ikitafuta nafasi ya kusimamia uchifu wa koo hiyo katika Kyela. Nashukuru Mungu Mbunge wa sasa wa Kyela ana muelekeo mzuri wa koo hiyo na iwapo atapatiwa nafasi zaidi kuna uwezekano mkubwa wa kuwepo na mabadiliko ya mfumo wa sasa wa kiutawala.Hili limeonekana na litaendelea kuonekana kadiri atakapoendelea kuwa mbunge wa jimbo hilo.
 
Nimepekua makabrasha yangu na kupata ujumbe huu ambao ndio yalikuwa malengo ya Dr. Mwakyembe kuhusu Kyela.

My dear brother XXXXX,
Nimerejea Dar kwa mapumziko ya muda mfupi baada ya uchaguzi kuahirishwa hadi Disemba 14.. Kazi niliyoifanya Kyela katika miezi miwili niliyokuwa huko ni kubwa. Nimejieleza vizuri kwa wananchi na kuwaandaa kisaikolojia kuwa miaka mitano ijayo ni ya kazi ngumu na mabadiliko makubwa kijamii na kiuchumi. Nina uhakika kuwa nimeng'oa mizizi yote ya Mwakipesile for a fresh start.

Nimefurahi sana kuona barua pepe ya kwako, ya XXX, XXX na XXX, zote zikiitakia Kyela na mimi mwenyewe mambo mema. Sikuweza kuzisoma mapema kutokana na hali halisi ya Kyela ya kutokuwa na reliable internet services. All the same, thanks a million times for your encouraging remarks.

My two-month long campaign trail in Kyela has been hectic, rough, nerve-racking but also rewarding in the sense that I can now confidently claim to know Kyela"s economic and social landscape thoroughly well. Kyela is, to say the least, a complete shamble and may rank one of the least developed and ill-provided for districts in the country. Whenever it rains, most of the key roads linking Kyela town with the district's productive areas and commercial centres like Ipinda, Matema, Makwale and Ipande, are rendered impassable. A large majority of Kyela residents has no access to clean water, hence the recurrent outbreak of cholera, dysentery and other water borne diseases in the district. Coupled with the rising HIV/Aids infection in the district which places Kyela at the top of the most affected districts in the country by the pandemic, and the abject poverty of most residents in the district, Kyela looks distressing.

Kielimu Kyela imeachwa mbali sana na Rungwe. Wakati miaka ya 80 Rungwe ilikuwa na shule za sekondari tatu tu na Kyela moja, leo hii Rungwe ina shule za sekondari 34 na high schools 7. Kyela ina secondary schools 7 na haina high school hata moja (44 years after independence!) Tena shule mbili kati ya hizo 7 ni mpya tu, zina madarasa machache tu na ujenzi unaendelea! Kutokana na hali hii, idadi kubwa ya vijana wa Kyela wanaishia darasa la saba. Mwaka jana tu, watoto 2,120 wa Kyela walifanya mtihani wa darasa la saba. Waliofaulu walikuwa zaidi ya asilimia 75 (75%) lakini waliochaguliwa kuingia secondary schools walikuwa asilimia 22 (22%) tu! Hivyo, Kyela ina idadi kubwa ya vijana walioishia darasa la saba ambao hawawezi kufua dafu kwenye soko la kisasa la ajira.

Kiuchumi, Kyela imekwisha bila kubadilisha mindset ya watu wake. Watu, hasa vijana, wamekuwa wavivu sana. Wanapenda maisha ya starehe na anasa na wanapenda sana fedha lakini hawataki kufanya kazi. Ukifika Kyela utagundua hilo kwa haraka kutokana na kila kijana, kila mtoto na sasa kila mzee kukuomba pesa. Kyela inakaribia kuipiku Dodoma kwa tabia ya ombaomba. Tatizo la msingi ni kwamba vijana hawapendi kufanyakazi. Pombe imewatawala. Wanakunywa pombe za kienyezi toka ahsubuhi hadi jioni. It is pathetic!

Hakuna kijana anayejishughulisha na bustani za mbogaboga licha ya kwamba Mungu ameipendelea sana Kyela kuwa na mito mingi inayo crisscross the district. Matokeo yake ni kuwa kila siku ya Mungu, wafanyabiashara wa Mbeya wanaleta kila asubuhi mboga za majani kutoka Uyole na Tukuyu ili kuilisha Kyela! Leo hii, Rungwe inailisha Kyela kila siku kwa ndizi na kwa maziwa! Paradoxically, wafugaji wa Rungwe hawana nyasi za kutosha kulishia ng'ombe wao wa maziwa. Nyasi nyingi wanazitoa Kyela!

A lot has gone astray in Kyela but the way forward is to stop mourning and stem the tide of degeneration. Kyela which enjoys several comparative advantages in Mbeya region must, in the coming five years, take up its rightful position as pace-setter in the agribusiness sector. We are producers of the finest organic cocoa in Africa if not the world; producers of a high quality, aromatic type of rice; producers of palm oil,cashewnuts etc. Tulichokosa Kyela for all the 44 years of indepence ni committed and focussed leadership.

I strongly believe that with your support (XXX, XXX, XXX, XXX and our brothers and sisters residing in Dar, Arusha, Mwanza, Nairobi etc.), we shall turn Kyela round and never again let our people down. I have the following rough ideas in mind which I'd like to think loudly with you with a view to implementing them in my five-year term of office. Baadhi ya mawazo nimeyapata kwenye e-mail yenu:
(1) Kuhakikisha kuwa katika miaka mitano ijayo kila kata iwe angalau na shule moja ya sekondari. Wilaya ya Kyela ina kata 15, nusu yake hazina shule za sekondari. Vilevile katika miaka mitano ijayo baadhi ya shule za sekondari zilizopo ambazo hazijakamilika au zina majengo machakavu, zitakamilishwa, zingine kupanuliwa na kukarabatiwa ili ziwe kwenye viwango vinavyokubalika. Ikiwa Prof. Mwakyusa (Rungwe Magharibi) ameweza kujenga shule mpya za sekondari 13 katika miaka mitano tu na Prof. Mwandosya (Rungwe Mashariki) amejenga shule mpya 9 za sekondari katika miaka hiyohiyo mitano, tutashindwaje Kyela kujenga shule mpya 8 za sekondari na zingine kuzimalizia au kuzikarabati katika miaka mitano ijayo?
(2) Kuhakikisha kuwa Kyela inajenga High School moja au mbili katika miaka mitano ijayo. Ili kufanikisha malengo (1) na (2), tutatumia nguvu ya wananchi, pesa za serikali za miradi (TASAF, MES, nk), michango ya wana Kyela wote waishio ndani na nje ya wilaya na vilevile, tutahamasisha taasisi zisizo za kiserikali na watu wenye pesa waanzishe private schools.
(3) Kuchimba visima kadhaa katika kila kijiji ili kuhamasisha uanzishwaji na uendeshaji wa bustani za nyanya, vitunguu na mboga mbalimbali za majani. Baadhi ya visima hivyo vitasaidia kilimo cha umwagiliaji wa mazao ya chakula kama mahindi, maharage, njegere, viazi vitamu n.k. wakati wa kiangazi. What we badly need ni mtambo wa kuchimbia visima.
Gharama za kukodisha mitambo hiyo ni kubwa mno kwa wananchi kuzimudu. Kisima kimoja kinagharimu (pamoja na mabomba yake) kiasi cha sh. milioni tatu hadi nne.
(4) Kuanzisha na kusimamia mpango wa ku-add value ya mazao makuu tunayozalisha Kyela. Kwa maneno mengine, badala ya kuyasafirisha au kuyatoa nje ya wilaya mazao yetu makuu k.m. mpunga, cocoa, mawese, korosho n.k. yakiwa raw au unprocessed, Halmashauri ya Wilaya ianzishe mpango wa kuwahamasisha watu wenye mitaji ili wawekeze Kyela kwa kujenga processing plants za mazao hayo. Mkakati huo utasaidia kuongeza thamani ya mazao yetu katika soko, utaongeza kipato cha mkulima wa Kyela na kuongeza nafasi za ajira kwa vijana wanaozagaa hovyo hovyo mitaani. Nimeomba appointment na mabalozi wa Ghana na Indonesia ili wanipe uzoefu wao katika kuongeza thamani ya cocoa na mawese. Tayari nimeongea na Ministry of Trade and Industries kuhusu uwezekano wa kuupa mchele wa Kyela a distinct Trade Mark ambayo itaulinda mchele wa Kyela usichanganywe na michele mingine mibovu, itaongeza thamani ya mchele wa Kyela katika soko la ndani na nje na kutoa incentive kwa wakulima kuongeza zaidi mavuno yao kwa mwaka. (Proposed Trade Mark itakuwa na maneno yafuatayo: "KYELA RICE – Tasty, Aromatic & 100% Organic". Tutalazimika kuteua kampuni chache zenye sifa na uwezo stahili, kujenga viwanda vya kukoboa na ku-pack kwenye mifuko ya ujazo na uzito mbalimbali wilayani Kyela na kuajiri extension officers wa kuhakikisha ubora wa mpunga mashambani
(5) Kuihimiza serikali kujenga chuo cha ufundi Kyela (vocational training college) ili kutatua tatizo kubwa linaloikabili Kyela la kuwa na kundi kubwa la class seven leavers ambao hawana ujuzi wowote kuweza kujiajiri. Tayari nimeongea na Southern Highlands Zonal Director wa VETA, amekielewa kilio cha Kyela. Nasubiri iundwe serikali mpya tupeleke kilio chetu moja kwa moja kwa waziri mhusika.
(6) Kuongeza juhudi za kuwaelimisha wananchi kuhusu janga la ukimwi, maambukizi ya ukimwi na hali mbaya inayoikabili Kyela. Kwa sasa Kyela ni ya pili baada ya wilaya ya Kinondoni kitaifa katika kuathirika na ukimwi. Licha ya hali hiyo mbaya sana, bado wananchi wanaendeleza mila hatari za kurithi wake wa ndugu zao, wanaendekeza promiscuity, wanaendelea na tabia ya kuchangia unywaji pombe kwenye bakuli moja! Tatizo ni lack of awareness. Kyela haijafaidika na vipindi vingi vya televisheni na redio juu ya ukimwi kutokana na umbali wa Kyela na vituo vya kurushia habari. Hivyo upo umuhimu mkubwa wa kuanzisha an FM Radio station hapa Kyela. It is not a bad investment at all for you people there to think about! Radio Kyela FM itasikilizwa Malawi, Ileje na Rungwe na haitakosa small adverts to keep it afloat.
(7) We hardly have effective charity programmes to assist HIV/AIDS orphans. Most orphans in Kyela are of tender age and cannot fend for themselves. Many of them are out of school for obvious reasons. We need to put our heads together to tackle the matter.
(8) I wholeheartedly endorse XXX idea of creating a marketing profile of Kyela. Kyela's interesting crop and fish varieties, beautiful beaches at Matema and Ikombe along Lake Nyasa, Kyela's traditional handicrafts and pottery as well as its rich cultural heritage embodied in the people's language, songs and dances, won't contribute anything meaningful to the district without s marketing/publicity profile as suggested by Dr. Lennard. Dr. Lennard, your help in this regard is badly needed.
(9) Kuunda chombo cha kuratibu maendeleo wilayani Kyela kitakachojulikana kama Kyela Development Fund (KDF). KDF itasajiliwa as an NGO na office bearers wake watatoka kwenye kanda tatu: kanda ya Kyela, kanda ya Dar es Salaam (itakayojumuisha wilaya zingine zote mbali na Kyela) na kanda ya nje ya Tanzania. Tunategemea wawakilishi wawili kutoka kwenu huko (Marekani/Uingereza) watakaokuwa alternate committee members. Tunaandaa draft constitution ya NGO hiyo ambayo tutahakikisha kuwa ina mfumo imara wa kuwajibika kwa uwazi kwa wadau wote wa Kyela.

Kwa leo niishie hapo. Once again, mnisamehe sana kwa kushindwa kuwaandikia mapema. Nafikiria namna ya kuanzisha an internet cafe in Kyela. Nawategemea sana. Kwa ushirikiano wetu sote, tutaipa Kyela sura mpya kabisa katika miaka michache ijayo.

N.B. Dhamira yetu njema ya kuipa Kyela sura mpya inaungwa mkono na viongozi wengi wa serikali. Hata kabla sijatawazwa kuwa mbunge wa Kyela, nimepata taarifa nzuri kutoka wizara mbili nyeti kuwa: (1) town centre ya Kyela inawekwa lami kuanzia mwenzi huu kuashiria a fresh promising start; (2) barabara kuu ya Kyela inamaliziwa kuwekwa lami hadi Itungi Port kuanzia mwezi huu. Wahusika wote nimewashukuru kwa niaba ya wananchi wa Kyela.


Cheers,
Dr. Harrison Mwakyembe (Mbunge Mtarajiwa, Kyela)
 
Kamanda Mtanzania:
Nimeona, na baadhi ya hayo ndani ya barua pepe hiyo niliwahi kumsikia mwenyewe Mwakyembe akiyasema alipokuwa nje ya Nchi
 
Mtanzania,

....nilidhani utaanza kwa kusema.........mmeshafanya (wewe inclusive) mambo kadha wa kadha.......hivi Mbunge peke yake ataweza?
 
Sasa JK Kwanini hakumpa u-RC kwenye mkoa mwingine? kuliko hivi kumuwekwa kwenye mkoa ambao alinyimwa kura? Naona anawagombanisha makusudi wananchi na viongozi wao na hata vongozi kwa viongozi ana maana gani?
 
Sasa JK Kwanini hakumpa u-RC kwenye mkoa mwingine? kuliko hivi kumuwekwa kwenye mkoa ambao alinyimwa kura? Naona anawagombanisha makusudi wananchi na viongozi wao na hata vongozi kwa viongozi ana maana gani?

Kwanini amepewe Ukuu wa Mkoa? anapotentials gani zinazomfanya awe Mkuu wa Mkoa?

Hata hivyo sioni sababu ya kuwa na Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya. Mkoani kuna Regional Administrative Secretary na wilayani Kuna District Administrative Secretary kwani hawa hawawezi? kwanini wasijengewe uwezo ili watimize hata majukumu ya DC au RC? Kwanini tusijifunze mfumo Mzuri wa wenzetu Kenya? wao wanamtu mmjo tu ofisini, yaani DC ni Mtaalam (anapewa uDC kutokana na taaluma) na ndiye Administrative Officer wa Wilaya.

Tutaokoa pesa nyingi sana.

At all kazi za DC au RC ni zipi na ni ngumu kiasi gani mpaka zitumie gharama kubwa za walipa kodi?
 
Mtanzania,

....nilidhani utaanza kwa kusema.........mmeshafanya (wewe inclusive) mambo kadha wa kadha.......hivi Mbunge peke yake ataweza?

Ogah,

Wapi hapo ningeanza kwa kusema tumefanya nini?

Mimi sitaki kuelezea ya kwamba ninafanya nini maana sio lengo la mjadala
huu. Wanayofanya akina Mtanzania ni kuwaachia wengine wayaseme.

Kwenye huu mjadala ninayoyasema mimi labda ni chini ya 10% ya ninayoyajua. Sitaki kuchochea moto kwa kumwaga mafuta zaidi. Badala yake ningependa hawa waheshimiwa wachape kazi na kuacha malumbano ya kisiasa. Anayechapa kazi zaidi ndio tutampa kura zetu.

Wale wa mbali mnaotumia Kyela kwa ajili ya kukuza mgogoro, acheni, tuachieni wenyewe maana waarabu wa pemba hujuana kwa viremba.

Si mmeona wenyewe wakati wa maafa jinsi Kyela ilivyo? Inahitaji maendeleo makubwa na maendeleo yatakuja tu kama wananchi wake wataungana na kuchapa kazi badala ya kushinda kwenye majungu na kugeuka wapambe wa watu wawili.
 
mzee hiyo barua ya Mwakyembe imenikatisha tamaa... naona kweli hili ni la kuwaachia wana Kyela wenyewe.

Sasa katika mipango yake hadi hivi sasa amefikia wapi? Ni kitu gani kinazuia maendeleo ya Kyela ukiondoa siasa hizi maana miaka karibu hamsini tangu Uhuru hatuwezi kulaumu kina Mwakyembe, Mwakipesile n.k kuna tatizo mahali.
 
mzee hiyo barua ya Mwakyembe imenikatisha tamaa... naona kweli hili ni la kuwaachia wana Kyela wenyewe.

Sasa katika mipango yake hadi hivi sasa amefikia wapi? Ni kitu gani kinazuia maendeleo ya Kyela ukiondoa siasa hizi maana miaka karibu hamsini tangu Uhuru hatuwezi kulaumu kina Mwakyembe, Mwakipesile n.k kuna tatizo mahali.

Mwanakijiji,

Wewe ni mwana Kyela tu kwahiyo unaruhusiwa kujadili kwi kwi kwi!!!

Tanzania maendeleo yatakuwa mbali sana, mpaka tutakapoacha haya mambo
ya kutaka ukubwa, upambe, majungu, visingizio na badala yake kuamua kuchapa kazi.

Ukitaka kufanikiwa Kyela lazima uamue kwamba huo ubunge huutaki tena, badala yake ama zao au zako. Naamini baada ya miaka mitano watatambua juhudi zako na kukuchagua tena.

Ya Dr. bado miaka mitano haijaisha kwahiyo tumpe the benefits of doubt kama ambavyo bado tunamsubiri JK atengeneze one million jobs
 
Ogah,

.................Wale wa mbali mnaotumia Kyela kwa ajili ya kukuza mgogoro, acheni, tuachieni wenyewe maana waarabu wa pemba hujuana kwa viremba..........

Mtanzania,

...........sio madhumuni yangu HATA SIKU MOJA kukuza/kuchochea migogoro.....kwa jumbe ninazoandika hapa.......sijui huo ujumbe wangu ni kwa vipi unakuza mgogoro!!......

well....siku hizi Tanzania ni mwendo wa kujuana kwa vilemba eeehh......anyhow......nilifikiri kuchangia kwangu hoja hapa, kwa namna moja au nyingine ni kusaidiana kimawazo...........i'm deeply sorry kama nimekukwaza.
 
Back
Top Bottom