Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,898
Hoja ya Katiba imeibuliwa na wanasiasa kipindi cha Kampeni Mwakajana. Hatimaye hoja ikaungwa mkono na wananchi baada ya kuelimishwa umuhimu wake. Faulo iliyofanywa na serikali kufinyanga matokeao ya uchachuzi kupitia tume ya uchaguzi imehamasisha zaidi wasomi, wanavyuo, wanachi na wanasiasa kudai mabadiliko ya Katiba.
Waangalizi wa kimataifa hasa wa kutoka Jumuiya ya Ulaya waliweka bayana jinsi uchakachuaji wa uchaguzi ulivyofanywa na serikali kupendelea waliopo madarakani, na hivyo kupendekeza mabadiliko katika sheria za uchaguzi maana yake mabadiliko ya katiba inayotendea haki wananchi wote bila kujali chama cha kisiasa ili kila raia awe na uhuru wa kugombea na haki katika kulinda na kutangaza matokeo ya uchaguzi.
Viongozi wa kisiasa ndio weledi wa kuelimisha wananchi na ndio wanaoeleweka kwa kutafsiri vizuri kuliko kutumia vyombo vya serikali ambavyo hutumia nguvu bila weledi wa kuelimisha umma. Kutumia watumishi wa serikali tu maana yake watakuwa na jukumu la kulinda maslahi ya wakubwa wao waliowaweka madarakani. Wanasiasa ndio wanaofahamu zaidi matatizo yanayojilia nchini na ndio wanaosikiliza matatizo ya wananchi, sasa iweje wawekwe kando maana yake kuna kiinimacho kinachokusudiwa kufanywa ili kuendelea kulinda himaya ya watawala waliopo.
Mswada wa Katiba mpya utafsiriwe katika lugha ya kitaifa, lugha ambayo Watanzania wanaijua, na hivyo wananchi watakuwa na fursa ya kuisoma na kuelewa kilichomo ndani ya mswada, na hii itajenga uelewa wa yaliyomo, wananchi kuchangia maoni yao baada ya kusoma, kuujadili na kuuelewa.
Katu wananchi tusikubali kudangwanywa tena safari hii, na hakuna sababu ya kukimbiza mswada wa katiba hadi wananchi waelewe.
Rais, Wabunge, wawakilishi wengine pamoja na watumishi wa serikali ni waajiriwa na wawajibikaji kwa wananchi waliowapa udhamini wa kuwatumikia, kwa msingi huo wasitumie nafasi walizopewa na wananchi kunyang'anya haki yao ya msingi ya kuchangia uundwaji wa katiba ya nchi.
Hakuna mtu atakayepinga kwa namna ye yote hata kupeleka pingamizi mahakamani kama kila mtu ameshirikishwa ipasavyo, la sivyo ni usanii tu unaokusudiwa kurudiwa katika uundwaji wa Katiba kama ilivyozoeleka kuundwa tume mbalimbali huko nyuma na kisha kuishia ikulu tu.
Vitisho vya kupelekwa jeja kwenye mswada uliopelekwa Dodoma viondolewe mara moja bila masharti kwa kuwa kufanya hivyo ni kukandamiza demokrasi nchini na inaweza sababisha machafuko ambayo yanaepukika.
Waangalizi wa kimataifa hasa wa kutoka Jumuiya ya Ulaya waliweka bayana jinsi uchakachuaji wa uchaguzi ulivyofanywa na serikali kupendelea waliopo madarakani, na hivyo kupendekeza mabadiliko katika sheria za uchaguzi maana yake mabadiliko ya katiba inayotendea haki wananchi wote bila kujali chama cha kisiasa ili kila raia awe na uhuru wa kugombea na haki katika kulinda na kutangaza matokeo ya uchaguzi.
Viongozi wa kisiasa ndio weledi wa kuelimisha wananchi na ndio wanaoeleweka kwa kutafsiri vizuri kuliko kutumia vyombo vya serikali ambavyo hutumia nguvu bila weledi wa kuelimisha umma. Kutumia watumishi wa serikali tu maana yake watakuwa na jukumu la kulinda maslahi ya wakubwa wao waliowaweka madarakani. Wanasiasa ndio wanaofahamu zaidi matatizo yanayojilia nchini na ndio wanaosikiliza matatizo ya wananchi, sasa iweje wawekwe kando maana yake kuna kiinimacho kinachokusudiwa kufanywa ili kuendelea kulinda himaya ya watawala waliopo.
Mswada wa Katiba mpya utafsiriwe katika lugha ya kitaifa, lugha ambayo Watanzania wanaijua, na hivyo wananchi watakuwa na fursa ya kuisoma na kuelewa kilichomo ndani ya mswada, na hii itajenga uelewa wa yaliyomo, wananchi kuchangia maoni yao baada ya kusoma, kuujadili na kuuelewa.
Katu wananchi tusikubali kudangwanywa tena safari hii, na hakuna sababu ya kukimbiza mswada wa katiba hadi wananchi waelewe.
Rais, Wabunge, wawakilishi wengine pamoja na watumishi wa serikali ni waajiriwa na wawajibikaji kwa wananchi waliowapa udhamini wa kuwatumikia, kwa msingi huo wasitumie nafasi walizopewa na wananchi kunyang'anya haki yao ya msingi ya kuchangia uundwaji wa katiba ya nchi.
Hakuna mtu atakayepinga kwa namna ye yote hata kupeleka pingamizi mahakamani kama kila mtu ameshirikishwa ipasavyo, la sivyo ni usanii tu unaokusudiwa kurudiwa katika uundwaji wa Katiba kama ilivyozoeleka kuundwa tume mbalimbali huko nyuma na kisha kuishia ikulu tu.
Vitisho vya kupelekwa jeja kwenye mswada uliopelekwa Dodoma viondolewe mara moja bila masharti kwa kuwa kufanya hivyo ni kukandamiza demokrasi nchini na inaweza sababisha machafuko ambayo yanaepukika.