Serikali kupitia IGP yataka Mahabusu wanaoshikiliwa bila Sababu za Msingi na wanaostahili haki ya Dhamana waachiwe

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,814
11,991
Fuatilia yanayojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 11, Kikao cha 19 leo Mei 5, 2023.



Wizara ya Mambo ya Ndani kupitia IGP imewataka ma RPC, OCD na wakuu wa vituo vya Polisi kukagua mara kwa mara mahubusu ili kuona watu waliopo ndani sababu gani zinafanya waendelee kukaa ndani ili waachiwe kama hakuna sababu za msingi za kuwashililia.

Aidha, Serikali imebaini pia kuwa baadhi ya watu wanaowekwa ndani hata ndugu zao hugoma kuwawekea dhamana sababu ya matukio ya kujiridua wanayofanya ambayo hufedhehesha jamii.

"Niwaombe pia ndugu wawe wepesi pia kuwadhamini kwa wale ambao dhamana zinakuwa wazi, lakini tumewasisitiza wakuu wa vituo, pale inapowezekana kwa makosa yanayodhaminiwa waweze kutoa dhamana" amesema Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Jumanne Sagini.

DKT. TULIA: MBEYA JIJI HAKUNA GARI LA ZIMA MOTO, PELEKENI GARI
Spika Dkt. Tulia Ackson amesema “Mbeya Jiji hakuna gari la Zimamoto na majanga ya moto yanatokea mara kwa mara, hivyo pelekeni gari.”

Awali, Mbunge Stella Simon Fiyao alisema ni Halmashauri 2 (Mbozi na Tunduma) kati ya 5 Mkoani Songwe hazina huduma ya magari ya Zimamoto, huku Halmashauri za Ileje, Momba na Songwe zikiwa hazina huduma na hata zile zenye huduma hizo zina magari madogo.

Akijibu, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Jumanne Sagini amesema “Tunawasiliana na Mkuu wa Zimamoto ili kupata gari moja wakati mpango wa Serikali wa kununua magari ukiwa njiani, pia kwenye Wilaya ambazo hazina magari hakuna matukio ya majanga ya moto ya mara kwa mara."

BULAYA AHOJI KILICHOPO NYUMA YA PAZIA SAKATA LA TANGA CEMENT NA TWIGA CEMENT
Mbunge Ester Bulaya amehoji kinachokwamisha mchakato wa kibiashara unaoendelea kati ya Kampuni ya Twiga Cement na ile ya Tanga Cement, akitaka Waziri wa Uwekezaji Viwanda na Biashara kuelezea kwa undani kilichopo nyuma ya pazia na kuhusu maslahi ya Taifa katika skata hilo.

MBUNGE: KWA NINI WAKIMBIZA MWENGE WALIMWAGA POMBE ZA KIENYEJI MTWARA?
Mbunge wa Momba, Condester Michael Sichalwe amehoji sababu za mamlaka kuzuia uuzwaji wa Pombe za kienyeji Nchini na kudai unachangia kuminya ubunifu wa wazawa wakati vinywaji kutoka nje ya Nchi vinaruhusiwa kuingizwa na vinauzwa kwa bei kubwa.
 
Rubber stamp. Bunge la chama kimoja lililotengenezwa na mtu mmoja kwq malengo ya kutaka kututawala milele. Sasa yanataka kugawanya majimbo ili yazidi kuongeza gharama pasi na tija!
Weee utaacha lini upumbavu wako?!, swala la haki toka lini likawa na muegamo kisiasa?
 
Rubber stamp. Bunge la chama kimoja lililotengenezwa na mtu mmoja kwq malengo ya kutaka kututawala milele. Sasa yanataka kugawanya majimbo ili yazidi kuongeza gharama pasi na tija!
Wakati Tulia anaaza harakati zake za kugombea ubunge Mbeya alileta gari linalo daiwa la maji taka na kudai la zimamoto.
 
BAJETI iliyopita ilitangazwa kwamba zilitolewa Bilioni 15 kwaajili ya kununua Magari ya Polisi hivi yaliletwa mangapi? au bado yapo njiani hapa tatizo SIYO wanaotoa pesa tatizo ni waagizaji inakuwaje Magari kuchukua mwaka mzima KUFIKA? Au walinunua Magari machache yenye thamani kubwa kwaajili ya viongozi
 
Fuatilia yanayojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 11, Kikao cha 19 leo Mei 5, 2023.



Wizara ya Mambo ya Ndani kupitia IGP imewataka ma RPC, OCD na wakuu wa vituo vya Polisi kukagua mara kwa mara mahubusu ili kuona watu waliopo ndani sababu gani zinafanya waendelee kukaa ndani ili waachiwe kama hakuna sababu za msingi za kuwashililia.

Aidha, Serikali imebaini pia kuwa baadhi ya watu wanaowekwa ndani hata ndugu zao hugoma kuwawekea dhamana sababu ya matukio ya kujiridua wanayofanya ambayo hufedhehesha jamii.

"Niwaombe pia ndugu wawe wepesi pia kuwadhamini kwa wale ambao dhamana zinakuwa wazi, lakini tumewasisitiza wakuu wa vituo, pale inapowezekana kwa makosa yanayodhaminiwa waweze kutoa dhamana" amesema Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Jumanne Sagini.

DKT. TULIA: MBEYA JIJI HAKUNA GARI LA ZIMA MOTO, PELEKENI GARI
Spika Dkt. Tulia Ackson amesema “Mbeya Jiji hakuna gari la Zimamoto na majanga ya moto yanatokea mara kwa mara, hivyo pelekeni gari.”

Awali, Mbunge Stella Simon Fiyao alisema ni Halmashauri 2 (Mbozi na Tunduma) kati ya 5 Mkoani Songwe hazina huduma ya magari ya Zimamoto, huku Halmashauri za Ileje, Momba na Songwe zikiwa hazina huduma na hata zile zenye huduma hizo zina magari madogo.

Akijibu, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Jumanne Sagini amesema “Tunawasiliana na Mkuu wa Zimamoto ili kupata gari moja wakati mpango wa Serikali wa kununua magari ukiwa njiani, pia kwenye Wilaya ambazo hazina magari hakuna matukio ya majanga ya moto ya mara kwa mara."

Hakuna bunge hapo bali kikao cha machawa
 
HAWATOAACHIWA KWA SABABU HIZO HIZO ZA MSINGI...

NI SIASA TU HII KAULI IMETOKA KUWADANGANYA WASIOFIKIRI...UKWELI HAKUNA EFFECT YA HII KAULI...I HATE POLITICIANS.
 
Nachofahamu huwa kuna mawakili wanapita vituo vya polisi kuangalia kama wapo mahabusu wanaostahili kupelekwa mahakamani, na kama hawajapelekwa shida yao ni nini.

Sasa hii kauli iliyotolewa na Wizara ya mambo ya Ndani inaonesha kuna tatizo mahali, ina maana wizara haijui kama wapo maafisa wenye kushughulika na hilo suala?
 
Vituo vidogo vingi hutumika kuonea watu.

Vituo vikubwa ni nadra kukuta mtu kawekwa bila kosa la msingi.

Dhamana mtu aruhusiwe jidhamini kama ana vigezo i.e kulipa pesa kwa control number ambayo atarudishiwa kesi ikiisha
 
BAJETI iliyopita ilitangazwa kwamba zilitolewa Bilioni 15 kwaajili ya kununua Magari ya Polisi hivi yaliletwa mangapi? au bado yapo njiani hapa tatizo SIYO wanaotoa pesa tatizo ni waagizaji inakuwaje Magari kuchukua mwaka mzima KUFIKA? Au walinunua Magari machache yenye thamani kubwa kwaajili ya viongozi
Fedha zenyewe zinatolewa na mtu (Rais) badala ya kufuata bajeti iliyopitishwa na bunge, huoni kuna tatizo hapo?
 
Hivi wewe umemlalamikia mtu kwa kosa alilokufanyia, kisha Polisi akamuachia mtuhumuwa wako @ kwa kigezo sio kosa la msingi. Utamuelewaje Polisi?
Wao ndio waliotunga hiyo sheria ya hilo kosa ambalo mtu awe mahabusu, kwanini wasiyafute na kusema kosa fulani na fulani liondoke kwenye mtiririko wa kuwekwa mtuhumiwa mahabusu.
Polisi imepewa mamlaka makubwa nchi zote duniani na ndio maana kila lawama anatupiwa imuhusu au haimuhusu lazima atapewa Polisi.
Kaja majuzi kuna clip imesambaa Mh: makamu wa raisi ktk ziara yake kanda ya ziwa akiwalaumu Polisi wa Mwanza kwa kuzuia magari yasitembee maasa manne kisa yeye mtoto wa masikini anapi, wakati alitoka Dodoma hadi Mwanza hajapishana na gari wala pikipiki hata moja njiani, tuseme hajui kua hiyo barabara sio ya kwake pekeyake, au siku hio watu hawasafiri kutumia hiyo barabara. Ila lawama kwa Polisi kisa Polisi kafanya kazi yake nzuri ya kuhakikisha kiongozi kapita salama. Ingekuwaje kwa Polisi endapo angeruhusu gari kutembea na msafara wake ungepata ajali?
Mitaani watu wakiibwa wananchi wanawauwa kwa kuwachoma moto, ila Morogoro Mungu mwenyewe aliwachoma moto kwa wizi wa mafuta ktk gari la mafuta, lawama zikaenda kwa Polisi walichelewa kufika. Polisi nao ni binaadamu na ni ndugu zetu ktk familia zetu.
 
Vituo vidogo vingi hutumika kuonea watu.
Askari ukimuona kituo kidogo jua katokea kituo kikubwa.
Vituo vikubwa ni nadra kukuta mtu kawekwa bila kosa la msingi.
Kosa ambalo sio la msingi ni lipi?
Dhamana mtu aruhusiwe jidhamini kama ana vigezo
Hili lipo wazi na linafanyika Polisi na Mahakamani
i.e kulipa pesa kwa control number ambayo atarudishiwa kesi ikiisha
Ufafanuzi wa hili. Polisi au Mahakama.

Eg. Polisi utalipa kwa Control No. Akwa makosa ya usalama barabarani. Labda cosa hauna leseni, siku ukipata leseni urudishiwe pesa yako uliolipa wakati haukuwa na leseni?
Eg. Mahakama, Uko na ndugu yako unataka kumzamini, masharti ya dhamani ni watu wa 2 kwa dhamana ya Tsh, milioni 2 kila mmoja, wewe utakuwanazo? Nielewavyo mimi ni za maandishi, utazilipa endapo mtuhumiwa hatofika mahakamani.
 
Back
Top Bottom