kimpe
JF-Expert Member
- Jan 26, 2012
- 911
- 861
Dar es Salaam. Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara nne za juu flyover katika jiji la Dar es Salaam ndani ya miaka mitatu na daraja la Kigamboni Juni mwakani, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli amesema.
Pia amesema Serikali imetenga Sh2 bilioni kununua kivuko cha mwendo kasi kitakachokuwa kikitoa huduma kati ya Dar es Salaam na Bagamoyo na kukamilika kwa ujenzi wa barabara za pembezoni katika jiji hili.
Waziri Magufuli alisema hayo jana katika ziara ya kukagua ujenzi wa barabara za jiji zinazojengwa kwa ufadhili wa Serikali ya Japan.
Tunajenga flyover nne katika makutano ya Tazara, Ubungo, Gerezani na DIT (Chuo cha Teknolojia Dar es Salaam) na ninaomba niwaahidi wakazi wa Jiji la Dar es Salaam kwamba ndani ya miaka mitatu foleni itabaki kuwa historia, alisema na kuongeza:
Tumetenga Sh28 bilioni kujenga kilomita 76.9 za barabara za pembezoni au pete ambazo zikikamilika zitawezesha kupunguza foleni.
Alisema daraja la Kigamboni limekamilika kwa asilimia 60 kwa gharama ya Sh214 bilioni, fedha kutoka Shirika la Hifadhi za Jamii (NSSF), Barabara ya Mwenge - Tegeta kwa Sh89 bilioni, Daraja la Tazara na Gerezani Sh100 bilioni.
Flyover Ubungo
Akizungumzia barabara hiyo ya juu ya Ubungo, Mkuu Idara ya Usanifu na Viwango wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Mhandisi Ebenezer Mollel alisema katika eneo la Ubungo kutakuwa na barabara za ngazi tatu ambazo zitakuwa katika mifumo isiyowezesha msongamano wa magari.
Mollel alisema barabara za mabasi yaendayo haraka (BRT) itaendelea kufanya kazi kama kawaida ikiongozwa na taa, huku magari yanayotoka barabara ya Sam Nujoma na Mandela, mfano Buguruni - Mwenge au Mwenge - Buguruni yatakuwa yakipita juu.
Katika barabara ya kwanza magari kutoka mjini (Barabara ya Morogoro) kwenda Buguruni (Mandela) na Kimara (Morogoro) kwenda Mwenge (Sam Nujoma) yataongozwa na taa. Magari yanayotoka Buguruni kwenda Mwenge na Kimara kwenda Buguruni nayo yatafuata mfumo wa taa, alisema Mollel.
Katika barabara ya pili magari yanayotoka mjini (Barabara ya Morogoro) kwenda Mwenge na Kimara kwenda Buguruni nayo yatatakiwa kuongozwa na taa na hii Flyover Interchange haitakuwa na msongamano kwani kila gari litakuwa na njia yake na hakutakuwa na msongamano wowote.
Alisema Serikali imekubaliana na Benki ya Dunia kufadhili mradi wa barabara hiyo itakayoondoa adha katika eneo la Ubungo Mataa.Meneja BRT, Barakael Mmari alisema barabara ya mradi huo awamu ya kwanza kutoka Kimara kwenda Kivukoni imekamilika lakini baadhi ya wananchi wameanza kuharibu miundombinu yake kama taa, alama na kuiba mifuniko ya majitaka.
Tulitakiwa kuikabidhi barabara hii leo (jana) ili tubaki kumalizia vituo tu, lakini Mheshimiwa Waziri (Dk Magufuli) wananchi wameiba taa za barabarani pindi zinapogongwa na madereva wasiozingatia sheria, alisema Mmari
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki aliwataka wananchi kulinda miundombinu ya barabara hizo ili iwanufaishe watu wengi zaidi.
Source:Mwananchi.
Pia amesema Serikali imetenga Sh2 bilioni kununua kivuko cha mwendo kasi kitakachokuwa kikitoa huduma kati ya Dar es Salaam na Bagamoyo na kukamilika kwa ujenzi wa barabara za pembezoni katika jiji hili.
Waziri Magufuli alisema hayo jana katika ziara ya kukagua ujenzi wa barabara za jiji zinazojengwa kwa ufadhili wa Serikali ya Japan.
Tunajenga flyover nne katika makutano ya Tazara, Ubungo, Gerezani na DIT (Chuo cha Teknolojia Dar es Salaam) na ninaomba niwaahidi wakazi wa Jiji la Dar es Salaam kwamba ndani ya miaka mitatu foleni itabaki kuwa historia, alisema na kuongeza:
Tumetenga Sh28 bilioni kujenga kilomita 76.9 za barabara za pembezoni au pete ambazo zikikamilika zitawezesha kupunguza foleni.
Alisema daraja la Kigamboni limekamilika kwa asilimia 60 kwa gharama ya Sh214 bilioni, fedha kutoka Shirika la Hifadhi za Jamii (NSSF), Barabara ya Mwenge - Tegeta kwa Sh89 bilioni, Daraja la Tazara na Gerezani Sh100 bilioni.
Flyover Ubungo
Akizungumzia barabara hiyo ya juu ya Ubungo, Mkuu Idara ya Usanifu na Viwango wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Mhandisi Ebenezer Mollel alisema katika eneo la Ubungo kutakuwa na barabara za ngazi tatu ambazo zitakuwa katika mifumo isiyowezesha msongamano wa magari.
Mollel alisema barabara za mabasi yaendayo haraka (BRT) itaendelea kufanya kazi kama kawaida ikiongozwa na taa, huku magari yanayotoka barabara ya Sam Nujoma na Mandela, mfano Buguruni - Mwenge au Mwenge - Buguruni yatakuwa yakipita juu.
Katika barabara ya kwanza magari kutoka mjini (Barabara ya Morogoro) kwenda Buguruni (Mandela) na Kimara (Morogoro) kwenda Mwenge (Sam Nujoma) yataongozwa na taa. Magari yanayotoka Buguruni kwenda Mwenge na Kimara kwenda Buguruni nayo yatafuata mfumo wa taa, alisema Mollel.
Katika barabara ya pili magari yanayotoka mjini (Barabara ya Morogoro) kwenda Mwenge na Kimara kwenda Buguruni nayo yatatakiwa kuongozwa na taa na hii Flyover Interchange haitakuwa na msongamano kwani kila gari litakuwa na njia yake na hakutakuwa na msongamano wowote.
Alisema Serikali imekubaliana na Benki ya Dunia kufadhili mradi wa barabara hiyo itakayoondoa adha katika eneo la Ubungo Mataa.Meneja BRT, Barakael Mmari alisema barabara ya mradi huo awamu ya kwanza kutoka Kimara kwenda Kivukoni imekamilika lakini baadhi ya wananchi wameanza kuharibu miundombinu yake kama taa, alama na kuiba mifuniko ya majitaka.
Tulitakiwa kuikabidhi barabara hii leo (jana) ili tubaki kumalizia vituo tu, lakini Mheshimiwa Waziri (Dk Magufuli) wananchi wameiba taa za barabarani pindi zinapogongwa na madereva wasiozingatia sheria, alisema Mmari
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki aliwataka wananchi kulinda miundombinu ya barabara hizo ili iwanufaishe watu wengi zaidi.
Source:Mwananchi.