Serikali imepiga marufuku wanafunzi wa shule binafsi ambao hawajamaliza ada kusimamishwa au kufukuzwa shule

GRAMAA

JF-Expert Member
Nov 1, 2014
1,155
3,399
Akiwa katika kipindi leo katika T.V ya taifa TBC naibu waziri wa TAMISEMI Mwita Waitara ambaye pia ni mbuge wa Ukonga kupitia chama cha mapinduzi( ccm) amewapa onyo na tahadhali wamiliki wote wa shule za binafsi ambayo hawafuati utaratibu uliowekwa na serikali na kuanzisha sheria zao binafsi.

Akifafanua zaidi kiongozi huyo ametoa onyo kali kwa mmiliki yoyote wa shule binafsi atayepanga wastani wake kwa wanafunzi tofauti na ule wa serikali.

Nikimnukuu alisema " serikali peke yake ndiyo yenye mamlaka ya kuwapangia watoto wastani wa kutoka darasa moja kwenda darasa lingine sasa wewe mmiliki wa shule mamlaka hayo umeyapata wapi mpaka umfukuze mtoto shule eti kisa kashindwa kufikia wastani wako wa ajabu ajabu"

Mwita alienda mbali zaidi kiasi kwamba alitoa namba zake hadharani ili kama kuna mzazi yoyote atasumbuliwa na shule binafsi basi ampigie haraka iwezekanavyo ili aende kuwaonesha cha mtema kuni.

Pia mwita amepiga marufuku wamiliki wa shule binafsi kupandisha ada hovyo hovyo na kumrudisha mtoto nyumbani eti kisa ada.

Mwita amewataka wamiliki wote wasipandishe ada zao kipindi hiki mpaka hapo serikali itakapotoa ada elekezi kwa shule binafsi na ole wake mmiliki yoyote wa shule binafsi atakayekiuka agizo hili la serikali kwani hato sita kuifungia shule hiyo Mara moja bila kujali shule hiyo inamilikiwa na nani.

Akifafanua kuhusu kutatua uhaba wa madarasa kiongozi huyo ameeleza kwamba serikali imeamua kuanzisha utaratibu wa wanafunzi kuingia kwa zamu mashuleni kwa mtindo wa kupokezana madarasa yaani kuna wale watakaoingia asubuhi na wengine wataingia mchana. Na ili kuweza suala hili serikali imetenga zaidi ya bilioni 400 ili kusaidia utaratibu huo.

Ndugu mtanzania kama mwanao atarudishwa darasa au kufukuzwa shule kwa ajili ya ada. Au kama utapata usumbufu wowote kutoka kwenye shule binafsi na uliiokosa namba ya Naibu waziri ambaye ameitoa hadharani Leo asubuhi basi chukua namba hii 0767221344.

Kweli serikali hii ni sikivu sana na ipo kwa ajili ya wanyonge. Hongera Mwita waitara

=====

UPDATES; 10 Jan 2019

Dar es Salaam. Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mwita Waitara amepiga marufuku wanafunzi wa shule binafsi ambao hawajamaliza ada kusimamishwa au kufukuzwa shule.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Alhamisi Januari 10, 2019, jijini Dar es Salaam, Waitara amesema kuanzia kesho Ijumaa ataanza kupokea taarifa kutoka kwa katibu tawala wa mikoa, wakurugenzi wa halmashauri na wadhibiti ubora wa shule ambazo zimewafukuza au kuwarudisha wanafunzi.

Amesema ni marufuku mwanafunzi kusimamishwa au kufukuzwa shule kwa sababu ya kutolipa ada bila kujali anasoma shule ya umma au binafsi.

Waitara amesema jambo jingine ambalo Serikali haikubaliani nalo ni la wazazi kulazimishwa kulipa ada kwa mkupuo na iwapo hawajafanya hivyo wanafunzi hawataendelea na masomo hata kama mwaka uliopita walifanya hivyo.

"Nina sms (ujumbe mfupi wa maandishi) nilizotumiwa na wazazi wa shule ambazo zimerudisha wanafunzi nyumbani kwa kukosa ada na malipo mengine ya kiholela kama vile kulazimishwa kununua sare za shule shuleni, for figer, rim na madaftari ya ganda gumu (counter book),” amesema Waitara.

“Nataka maofisa elimu, wakurugenzi na makatibu tarafa kwenda kwenye hizi shule (anazitaja shule) hadi kufikia kesho niwe na majibu yanayoonyesha kupatikana ufumbuzi."

Waitara pia amewataka wazazi ambao watoto wao wamerudishwa kwa ajili ya kutolipa au kukamilisha ada wafike kwenye ofisi alizozitaja au Tamisemi kwa ajili ya kupatiwa ufumbuzi.

Naibu waziri huyo amesema kuna haja ya kurudisha mjadala wa ada elekezi.

"Nafanya utaratibu kurudisha mjadala wa kuangalia namna ambavyo Serikali itatoa msimamo wa ada elekezi kwa sababu kuna shule zinatoza kuanzia Sh1.5 milioni hadi Sh6 milioni na zinasema zinatoa huduma," amesema Waitara.

Waitara amefafanua kama mazazi anaweza kulipa fedha yote hiyo kuna haja gani ya kupata mkopo chuo kikuu.

"Hili limekuwa changamoto kwa wanafunzi wengine wanaishi kwa ndugu wanaporudishwa inazua taharuki kwa wanafunzi na wazazi" amesema.

"Mtoto amesoma shule kwa miaka mitatu na kukamilisha michango yote, anaposhindwa haongezewi hata wiki moja badala yake anafukuzwa shule na mzazi hataki kukanyaga kabisa shule bila kuwa na risiti ya malipo," amesema

"Hili halivumiliki hata kidogo, wakibainika wanaofanya hivyo tutawachukulia hatua kwa sababu wao wanatoa huduma na hawalipi kodi na ninawakumbusha elimu inasimamiwa na Serikali" amesema Waitara
 
Akiwa katika kipindi leo katika T.V ya taifa TBC naibu waziri wa TAMISEMI Mwita Waitara ambaye pia ni mbuge wa Ukonga kupitia chama cha mapinduzi( ccm) amewapa onyo na tahadhali wamiliki wote wa shule za binafsi ambayo hawafuati utaratibu uliowekwa na serikali na kuanzisha sheria zao binafsi.

Akifafanua zaidi kiongozi huyo ametoa onyo kali kwa mmiliki yoyote wa shule binafsi atayepanga wastani wake kwa wanafunzi tofauti na ule wa serikali.

Nikimnukuu alisema " serikali peke yake ndiyo yenye mamlaka ya kuwapangia watoto wastani wa kutoka darasa moja kwenda darasa lingine sasa wewe mmiliki wa shule mamlaka hayo umeyapata wapi mpaka umfukuze mtoto shule eti kisa kashindwa kufikia wastani wako wa ajabu ajabu"

Mwita alienda mbali zaidi kiasi kwamba alitoa namba zake hadharani ili kama kuna mzazi yoyote atasumbuliwa na shule binafsi basi ampigie haraka iwezekanavyo ili aende kuwaonesha cha mtema kuni.

Pia mwita amepiga marufuku wamiliki wa shule binafsi kupandisha ada hovyo hovyo na kumrudisha mtoto nyumbani eti kisa ada.

Mwita amewataka wamiliki wote wasipandishe ada zao kipindi hiki mpaka hapo serikali itakapotoa ada elekezi kwa shule binafsi na ole wake mmiliki yoyote wa shule binafsi atakayekiuka agizo hili la serikali kwani hato sita kuifungia shule hiyo Mara moja bila kujali shule hiyo inamilikiwa na nani.

Akifafanua kuhusu kutatua uhaba wa madarasa kiongozi huyo ameeleza kwamba serikali imeamua kuanzisha utaratibu wa wanafunzi kuingia kwa zamu mashuleni kwa mtindo wa kupokezana madarasa yaani kuna wale watakaoingia asubuhi na wengine wataingia mchana. Na ili kuweza suala hili serikali imetenga zaidi ya bilioni 400 ili kusaidia utaratibu huo.

Ndugu mtanzania kama mwanao atarudishwa darasa au kufukuzwa shule kwa ajili ya ada. Au kama utapata usumbufu wowote kutoka kwenye shule binafsi na uliiokosa namba ya Naibu waziri ambaye ameitoa hadharani Leo asubuhi basi chukua namba hii 0767221344.

Kweli serikali hii ni sikivu sana na ipo kwa ajili ya wanyonge. Hongera Mwita waitara
Shule binafsi zinajiendesha kwa ada ,kama mtu hana uwezo kwanini umpeleke shule binafsi wakati st. Kanumba zipo.acha vitisho visivyo na msingi. Nakuunga mkono uzuwiaji upandaji holela ada ila kila waziri ajae hapo anazungumza tu huo mwongozo unatoka lini au ni domo tu ili tujuwe kuwa wewe si CDM sasa?
Mchujo muhimu sana unasukuma hamasa kwa watoto.atashindwa utampokea serikalini ataongoza darasani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanataka kuingilia maisha yetu kuliko hata dini.nikiwa mzazi kama mtoto wangu hawezi ushindani wamrudishe kuliko kulipa milions mwishoni anafeli.nitampeleka shule nafuu zisizo na mchujo aendelee kukua.kama wamiliki wa shule binafsi wangekuwa walafi wa fedha wasingeweka mchujo,basi tuwapongeze badala ya vitisho.Imarisha shule za umma zifanye vizuri hatutapeleka private.
Wanawapangia utafikiri wanawapa ruzuku

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo mie nimefurahia kupata namba zake. Kuna shule fulani hivi ya Serikali tena ni kongwe hapa Tanzania huwa waalimu wake wana mambo ya "hovyo hovyo", lazima niwachome kwa Mwita Waitara. Ahsante kwa kutoa namba yake ya simu.
hayo mengine hayanihusu ya shule za binafsi
 
Siasa bwana....
Hao watoto wao wanasoma hizo shule za serikali? Hayo matamko ya kutoa mwongozo kwa shule za private hayajaanza kutoka leo ila hatujawahi kusikia utekelezaji wake

Boresheni huduma za shule za serikali ndipo muongee hayo...
Vyuo vyenu vya serikali vinataka wanafunzi walioufaulu wakati huohuo shule za kata zinaongoza kwa four na zero... vyuo gani vitawadahili???


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuwa mpinzani kwani ni kupinga kila cha serikali acheni mambo yenu ya vyama na bifu za kipuuzi , hata kama private wanapaswa kufuata taratibu zilizopo kisheria, je kama wataamua kufundisha ushoga waruhusiwe sbb private?
Mda mwengine haya ndio mambo yanayotufanya tuone vyama ni ubabaishaji tu yaani mtu anadiriki kuvaa miwani ya mbao kisa tu kasema mtu wa chama fulani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kawaida ya Mlevi akipata cheo na Nyongeza ya Mshahara kinachofuata ni kutoa namba hadharani, kisingizio kimepatikana, Malaya wote wa Mjini washaijua namba..
 
Hili jambo siyo dogo hata kidogo maana sasa ni vitisho kutoka kwa serikali wakati bado serikali haiwezi kuwahudumia wanafunzi wote ,sasa kama shule za private zikifungwa au kufungiwa watoto wataenda wapi wakati tayari mmezidiwa mpaka watoto wanasoma kwa zamu.Ukijiuliza swali kama watoto wanasoma kwa zamu je masaa ambayo anatakiwa kuwa darasani kwa muhula yatafikaje?Je walimu wameomgezewa malipo kuhusu kufundisha kwa muda wa zaida kutokana na ongezeko la wanafunzi ?
Tunaomba usikurupuke na matamko bali angalia jinsi ya kutatua matatizo yaliopo lukuku kwenye elimu yetu kuanzia darasa la kwanza mpaka vyuo na angalia pia mazingira rafiki ya kuweka ili wenye uwezo waweze kuwekeza kwenye shule maana serikali inalemewa na idadi ya wanafunzi na rais amesema tuangalie jinsi ya kuweka mazingira rafiki ili kuvutia uwekezaji

Usiwe na mawazo ya kufungia bali kuwa na mawazo ya jinsi gani kuendeleza ikiwa ni private au Government

Kumbuka kuna ambao waliwatisha wafanyi biashara mwanzoni na wafanyi biashara wakahamisha biashara zao kwenda Zambia na kwingineko na sasa wanaomba usuluhisho maana mapato yanapungua so kuwa makini maana hizo private school zinasaidia sana serikali na wanalipa pia kodi

Ukisumbua shule binafsi watu wanapeleka watoto kenya na Uganda kama zamani na utakosa kodi eneo hilo

Kumbuka Rais mstaafu Benjamini W Mkapa ndiy aliomba watu kuwekeza kwenye Elimu maana serikali ilielemewa na wengi wa wanafunzi na kutoa mazingira rafiki sasa ukiyaondoa watu watatafuta njia mbadala
 
Sasa what is the meaning of Private school????
As long as ni private acheni watu waendeshe shule zao nyie serikali si mnazo zenu aisee
Private haina maana ujiamulie mambo yako kinyume na taratibu za nchi.

Private school maana yake unasaidiana na serikali katika kutoa elimu ila kwa gharama ya juu kidogo kuliko inayotolewa serikalini ila haina maana kua uwe na sheria zako, kama ndio hivyo basi kua na mtaala na mitihani na vyeti vyako.

Shule binafsi zilitoka kwenye madhumuni makuu ya kutoa elimu zikajikita kwenye biashara. Hakuna kitu kama hicho kwenye huduma za kijamii.

Ni sawa na uwe na hospitali binafsi alafu hutaki wagonjwa waliozidiwa sana, unataka wenye nafuu ambao wanaweza kurudi nyumbani, wagonjwa mahututi hutaki, hiyo sio huduma ya afya ni utaahira.
 
Kawaida ya Mlevi akipata cheo na Nyongeza ya Mshahara kinachofuata ni kutoa namba hadharani, kisingizio kimepatikana, Malaya wote wa Mjini washaijua namba..
Namba ni kwa ajili ya kudil na wamiliki wa shule binafsi watakaokiuka utaratibu uliowekwa na serikali na si vinginevyo mkuu
 
Back
Top Bottom