mwanamichakato
JF-Expert Member
- Mar 20, 2015
- 897
- 715
Ni mfumo wa kiforodha unaohusisha mamlaka za kodi za nchi wanachama wa Afrika Mashariki katika usimamizi wa mizigo mbalimbali inayoingia na kutoka katika nchi wanachama ..Mfumo unahusisha waagizaji kufanya utaratibu wa utoaji mzigo ktk nchi zao na kulipia ushuru na kodi zote mzigo ukiwa bado haujatolewa ktk bandari .
Kongo DRC ni mteja mkubwa wa uagizaji na usafirishaji wa shehena kubwa za mizigo kupitia Bandari za Dar es salaam-Tanzania,Mombasa-Kenya,Beira-Msumbiji,Welvis Bay-Namibia na Durban -Afrika Kusini,Lobito-Angola kwa miaka nenda rudi ikichagizwa na mapana ya kijiografia na rasilimali
Kongo DRC amekaribishwa katika mfumo wa forodha wa SCT ili kuisaidia kusimamia mapato yake .Lakini mapana ya madhara ya kuikaribisha Kongo hayawaumizi Rwanda,Burundi,Uganda ama hata Kenya sababu ya strategic position Jimbo la Katanga lenye utajiri wa rasilimali madini na misitu.
Mamlaka ya usimamizi wa kodi na mapato ya Kongo {OFIDA} imefungua ofisi zake katika nchi wadau wa SCT ikiwamo Dar es salaam-Tanzania.Historia yaoshesha hakuna urafiki kati ya walipa kodi na wasimamia kodi hasa ktk nchi zinazoendelea sababu ya rushwa na ufisadi wa watumishi wa mamlaka za kodi na wafanyabiashara.
Madhara ya kuihusisha Kongo DRC ktk mfumo wa SCT yamepelekea ucheweleshaji wa utoaji wa mizigo ya wateja sababu ya mapungufu ya mfumo husika kiutekelezaji ,kiusimamiaji na maandalizi yenye mapungufu mtambuka hivyo kuongeza gharama maradufu katika uondoshaji wa mizigo kupitia bandari zetu hivyo kusababisha hasara kubwa kwa wateja na mawakala wao.Lakini pia wateja kulazimika kulipa ushuru mkubwa tofauti na awali kwa kuepuka malumbano kikodi yanayochukua muda mrefu huku gharama mtambuka za uhifadhi mizigo yao ikiongezeka ktk hifadhi za bandari.
Hili limekuwa msingi wa wateja wengi toka Congo DRC kuanza kuikimbia kutumia milango bahari inayofungamana na nchi za Afrika mashariki {SCT} hivyo kukimbilimbilia ktk nchi zisizofungamana kiforodha na Congo DRC.
Tayari idadi ya mizigo yakiwemo magari yanayopita bandari ya Dar es salaam imepungua kwa zaidi ya asilimia 15 ktk miezi michache iliopita na uthibitisho upo kupitia kuthibitishwa na utupu ktk bandari kuu na kavu kama Farion,TALL,Chikasa,Silver,Hesu n.k
Jitihada kubwa zinazofanywa na Serikari ya JPM ktk kurestructure na ku reform bandari yetu na mamlaka za kodi matunda yake yanaweza yasiwe na tija tarajiwa kwa manufaa ya taifa.Hatua stahiki zichukuliwe kwa kuifuta Congo DRC katika mfumo husika sababu ni kikwazo kwa jitihada za kuongeza mapato kwa nchi yetu kupitia fulsa malidhawa .
Kongo DRC ni mteja mkubwa wa uagizaji na usafirishaji wa shehena kubwa za mizigo kupitia Bandari za Dar es salaam-Tanzania,Mombasa-Kenya,Beira-Msumbiji,Welvis Bay-Namibia na Durban -Afrika Kusini,Lobito-Angola kwa miaka nenda rudi ikichagizwa na mapana ya kijiografia na rasilimali
Kongo DRC amekaribishwa katika mfumo wa forodha wa SCT ili kuisaidia kusimamia mapato yake .Lakini mapana ya madhara ya kuikaribisha Kongo hayawaumizi Rwanda,Burundi,Uganda ama hata Kenya sababu ya strategic position Jimbo la Katanga lenye utajiri wa rasilimali madini na misitu.
Mamlaka ya usimamizi wa kodi na mapato ya Kongo {OFIDA} imefungua ofisi zake katika nchi wadau wa SCT ikiwamo Dar es salaam-Tanzania.Historia yaoshesha hakuna urafiki kati ya walipa kodi na wasimamia kodi hasa ktk nchi zinazoendelea sababu ya rushwa na ufisadi wa watumishi wa mamlaka za kodi na wafanyabiashara.
Madhara ya kuihusisha Kongo DRC ktk mfumo wa SCT yamepelekea ucheweleshaji wa utoaji wa mizigo ya wateja sababu ya mapungufu ya mfumo husika kiutekelezaji ,kiusimamiaji na maandalizi yenye mapungufu mtambuka hivyo kuongeza gharama maradufu katika uondoshaji wa mizigo kupitia bandari zetu hivyo kusababisha hasara kubwa kwa wateja na mawakala wao.Lakini pia wateja kulazimika kulipa ushuru mkubwa tofauti na awali kwa kuepuka malumbano kikodi yanayochukua muda mrefu huku gharama mtambuka za uhifadhi mizigo yao ikiongezeka ktk hifadhi za bandari.
Hili limekuwa msingi wa wateja wengi toka Congo DRC kuanza kuikimbia kutumia milango bahari inayofungamana na nchi za Afrika mashariki {SCT} hivyo kukimbilimbilia ktk nchi zisizofungamana kiforodha na Congo DRC.
Tayari idadi ya mizigo yakiwemo magari yanayopita bandari ya Dar es salaam imepungua kwa zaidi ya asilimia 15 ktk miezi michache iliopita na uthibitisho upo kupitia kuthibitishwa na utupu ktk bandari kuu na kavu kama Farion,TALL,Chikasa,Silver,Hesu n.k
Jitihada kubwa zinazofanywa na Serikari ya JPM ktk kurestructure na ku reform bandari yetu na mamlaka za kodi matunda yake yanaweza yasiwe na tija tarajiwa kwa manufaa ya taifa.Hatua stahiki zichukuliwe kwa kuifuta Congo DRC katika mfumo husika sababu ni kikwazo kwa jitihada za kuongeza mapato kwa nchi yetu kupitia fulsa malidhawa .