Sera ya Kuwawezesha watanzania weusi ni ya lazima?

Aisee wewe ni mtu hatari sana na natumaini haupo katika nafasi yoyote ya kuweza kutunga sheria ama sera unazozipigia debe hapa maana tutadumbukia katika shimo la chuki na ubaguzi usio na nafasi katika jamii yoyote ile iliyostaarabika!!

Nyani,
Hebu nikuulize na watu wote wa upande huo. Hivi ile sheria ya Marekani inayosema kuwa "Wahandisi wawili wakiomba kazi, wote wana pass karibu sawa, mmoja mweusi na mwingine mweupe, basi kazi apewe mweusi..." ni ya kibaguzi? Hata kwenye pass, weusi wanapendelewa. Tumesikia kuwa hata Tanzania kuna makabila kibao yamependelewa shuleni. Hii si kuleta ubaguzi. Hii kitu inatakiwa kufunguliwa na kulindwa kwa sheria kali. Wewe Nyani, Mwana kijiji, FM, Fundi Mchundo, Mkandara na wengine wengi haturuhusiwi kuwa kwenye listi ya watakaofaidika kwa kipesa, ila labda kimawazo.
Hivi usingelifanyika upendeleo KUTUSOMESHA sisi Lami, wengi humu tungelikuwamo? Mwaka Nyerere ametangaza shule zote bure, Mzee wangu aliyekuwa Mkulima, aliamua kuwachukua mabinti zake (dada zangu) warudi nyumbani waolewe. Hapo mmoja alikuwa aende form 5, mmoja form 1, mwingine darasa la tano. Kwa kuruhusiwa kusoma bure, dada yangu mkubwa alisoma hadi akawa Mhanidisi mwenye masters. Ilikuwa furaha kuona picha yake kwenye gazeti la Daily News akimuonyesha Nyerere (kama mfanyakazi wa Costech) matanki ya Biogas huko Dodoma.
Kumbe basi, kama serikali ikifanya sisi tunachokiita Upendeleo au wewe wakiita SERA ya kuwaendeleza Weusi katika biashara, kesho kutwa kuna vijana watamuonyesha Kikwete Biashara zao za kutisha, kama alivyofanya marehemu dada yangu. Halafu lazima mkumbuke ule msemo niliouona hapa kuwa "kwenye msafara wa Mamba na Kenge wamo". Hivyo katika kufaidisha weusi walio wengi, wahindi, Wazungu, Wachina, Waarabu, Wayahudi basi nao wao wata-tumbukiaMO.
 
Sikonge umetoa mfano mmoja mzuri sana.Nadhani fundi ano mchundo ama la anaufahamu mchundo ulivyo hadi kaamua kujiita jina hilo.Vijana wengi sana wa FTC wameweza kujiendeleza hadi kuwa na PhD kwa kupitia scholarship za russia ilihali UDSM iliwakataa.Lakini sasahivi UDSM imebadili muelekeo na inawasomba wengi kwelikweli.Na hayo ndio mabadiliko tunyoyahitaji ili kuwawezesha hawa wabongo ambao wameachwa nyuma kiuchumi.
Ukweli ni kwamba tunaposisitiza kuwezeshwa wazawa weusi tumejaribu kuona kuwa ndilo kundi ambalo kwa kiasi kikubwa limeachwa nyuma kiuchumi ukilinganisha na makundi mengine.Na hao wenzetu anaowazungumzia fundi kwa namna moja ama nyingine wana viji-connection na nchi nyingine kama india na pakistani.Na jambo la msingi hapa sio kuwazibia hao wenzetu ambao tayari wako vizuri, kinachotakiwa hapa ni kuwawezesha watanzania wazawa ambao wameonekana kuachwa nyuma kimaendeleo na kiuchumi ndani ya nchi yao.Hapo hakuna ubaguzi fundi ni suala la kuwavuta hawa walioachwa nyuma.

Hata kabla ya hili neno uzawa kuingia, sera za elimu ziliwapa nafasi watu weusi kuliko hao unaowazungumzia. Baada ya kunyang'anya shule zao, sehemu kubwa ya wanafunzi walikuwa weusi. Sehemu kubwa ya wanafunzi waliopatiwa nafasi ya kusoma nje walikuwa ni weusi bila kuwa na sera hii mnayoidai!

Tukisema kuwa tutatunga sera ya kuwapa upendeleo watanzania walio nyuma kimaendeleo bila shaka sehemu kubwa mno itakuwa ya watu weusi. Mimi ndiyo maana naona haya madai ya kutaka upendeleo kutokana na rangi unatokana na wivu na chuki dhidi ya wenzetu na si hali halisi iliyopo. Leo hii kuna watanzania wenye asili ya uhindini ( wakina Rakesh Rajani wa Haki Elimu, Issa Shivji na wengine wengi) wamesimama kidete kuwatetea watanzania wenzao walio wanyonge dhidi ya serikali yao lakini hapana kwenu nyie yote haya hamyaoni. Kwenu nyie wakina Mkono, Tenga, IMMA ni bora mara kumi ya Issa Shivji kwa sababu tu ni wazawa! Yaani kweli hamuoni aibu. Badala ya kushirikiana na kuwakumbatia wakina Rajani na Shivji mnataka kuwatenga katika nchi yao? Kwa mwendo huo hatutafika kweli.

Amandla.....
 
Nyani,
Hebu nikuulize na watu wote wa upande huo. Hivi ile sheria ya Marekani inayosema kuwa "Wahandisi wawili wakiomba kazi, wote wana pass karibu sawa, mmoja mweusi na mwingine mweupe, basi kazi apewe mweusi..." ni ya kibaguzi? Hata kwenye pass, weusi wanapendelewa. Tumesikia kuwa hata Tanzania kuna makabila kibao yamependelewa shuleni. Hii si kuleta ubaguzi. Hii kitu inatakiwa kufunguliwa na kulindwa kwa sheria kali. Wewe Nyani, Mwana kijiji, FM, Fundi Mchundo, Mkandara na wengine wengi haturuhusiwi kuwa kwenye listi ya watakaofaidika kwa kipesa, ila labda kimawazo.
Hivi usingelifanyika upendeleo KUTUSOMESHA sisi Lami, wengi humu tungelikuwamo? Mwaka Nyerere ametangaza shule zote bure, Mzee wangu aliyekuwa Mkulima, aliamua kuwachukua mabinti zake (dada zangu) warudi nyumbani waolewe. Hapo mmoja alikuwa aende form 5, mmoja form 1, mwingine darasa la tano. Kwa kuruhusiwa kusoma bure, dada yangu mkubwa alisoma hadi akawa Mhanidisi mwenye masters. Ilikuwa furaha kuona picha yake kwenye gazeti la Daily News akimuonyesha Nyerere (kama mfanyakazi wa Costech) matanki ya Biogas huko Dodoma.
Kumbe basi, kama serikali ikifanya sisi tunachokiita Upendeleo au wewe wakiita SERA ya kuwaendeleza Weusi katika biashara, kesho kutwa kuna vijana watamuonyesha Kikwete Biashara zao za kutisha, kama alivyofanya marehemu dada yangu. Halafu lazima mkumbuke ule msemo niliouona hapa kuwa "kwenye msafara wa Mamba na Kenge wamo". Hivyo katika kufaidisha weusi walio wengi, wahindi, Wazungu, Wachina, Waarabu, Wayahudi basi nao wao wata-tumbukiaMO.

Ndiyo, ni ya kibaguzi. Kuna watu wanauita huo utaratibu (affirmative action) kuwa ni ubaguzi chanya (positive discrimination). Ila mimi sielewi inawezekana vipi ubaguzi ukawa ni jambo chanya. Binafsi napinga hiyo affirmative action na naunga mkono na mguu equal opportunity na equal protection under the law.

Kwa hiyo, kwa sababu tu eti Wamarekani wana utaratibu huo haina maana ya kwamba ni sawa. Kwanza kuna Wamarekani wengi wanaoupinga huo utaratibu na kama sikosei kuna baadhi ya majimbo wameshapiga kura kuuondoa. So go figure!
 
Nyani,
Hebu nikuulize na watu wote wa upande huo. Hivi ile sheria ya Marekani inayosema kuwa "Wahandisi wawili wakiomba kazi, wote wana pass karibu sawa, mmoja mweusi na mwingine mweupe, basi kazi apewe mweusi..." ni ya kibaguzi? Hata kwenye pass, weusi wanapendelewa. Tumesikia kuwa hata Tanzania kuna makabila kibao yamependelewa shuleni. Hii si kuleta ubaguzi. Hii kitu inatakiwa kufunguliwa na kulindwa kwa sheria kali. Wewe Nyani, Mwana kijiji, FM, Fundi Mchundo, Mkandara na wengine wengi haturuhusiwi kuwa kwenye listi ya watakaofaidika kwa kipesa, ila labda kimawazo.
Hivi usingelifanyika upendeleo KUTUSOMESHA sisi Lami, wengi humu tungelikuwamo? Mwaka Nyerere ametangaza shule zote bure, Mzee wangu aliyekuwa Mkulima, aliamua kuwachukua mabinti zake (dada zangu) warudi nyumbani waolewe. Hapo mmoja alikuwa aende form 5, mmoja form 1, mwingine darasa la tano. Kwa kuruhusiwa kusoma bure, dada yangu mkubwa alisoma hadi akawa Mhanidisi mwenye masters. Ilikuwa furaha kuona picha yake kwenye gazeti la Daily News akimuonyesha Nyerere (kama mfanyakazi wa Costech) matanki ya Biogas huko Dodoma.
Kumbe basi, kama serikali ikifanya sisi tunachokiita Upendeleo au wewe wakiita SERA ya kuwaendeleza Weusi katika biashara, kesho kutwa kuna vijana watamuonyesha Kikwete Biashara zao za kutisha, kama alivyofanya marehemu dada yangu. Halafu lazima mkumbuke ule msemo niliouona hapa kuwa "kwenye msafara wa Mamba na Kenge wamo". Hivyo katika kufaidisha weusi walio wengi, wahindi, Wazungu, Wachina, Waarabu, Wayahudi basi nao wao wata-tumbukiaMO.

Affirmative action ya Marekani ni sera ya kibaguzi inayotumika kupunguza mzigo na barriers zinazotokana na ubaguzi usio wazi. Hii ililetwa kutokana na ukweli kuwa walioshika utamu marekani walikuwa ni wanaume wenye rangi nyeupe. Hawa walikuwa na nguvu ya utawala pamoja na wingi wa kura. Sera hii iliwekwa kumpa nafasi yule asiye na rangi au jinsia hizi kuweza kuingiwa katika sehemu ambazo kabla ya hapo asingeweza hata afanye vipi. Miaka zaidi ya 40 baada ya Equal Rights Amendments, matokeo yake bado ni debatable. Kweli watu wa jinsia na rangi tofauti wameanza kuonekana katika nyanja za juu ya utawala lakini umaskini wa sehemu kubwa ya watu hao bado uko palepale kama siyo kuzidi. Ndiyo maana sera ya upendeleo uliokuwa based kwenye rangi tu unazidi kupingwa hata na watu weusi ambao ungetegemea wangefurahia. Inadaiwa na baadhi kuwa kwa kuwadekeza na kuwabembeleza watu weusi, jamii imewaondolea self-confidence ambayo ni muhimu kwa mafanikio ya mtu yeyote. Hiki ndicho, ndugu zangu mnataka kutufanyia hapa nyumbani. Kwa kudai huu upendeleo, mnazidi kujenga imani kuwa sisi watu weusi hatuko sawa na hao wa rangi nyingine. Kwa bahati mbaya, wengi wenu hamlioni hili. Hii ndiyo inayonisikitisha.

Nyerere hakusema elimu bure kwa wazawa bali kwa watanzania. Si dada zako tu bali mabinti kibao wa kiarabu na kihindi nao walipata nafasi ya kusoma ambayo kabla ya hapo walikuwa wakizuiwa na jamii zao. Ni waswahili wangapi ambao hata pamoja na elimu kuwa bure waliamua kuwaozesha binti zao? Wengi tu walifanya hivyo na wanaendelea kufanya hivyo. Hii ndiyo tofauti kubwa kati ya sera zake na hizi zenu za kibaguzi.

Amandla.....
 
Sikonge Mkuu. Unachanganya vitu. Hapa tunazungumzia ubaguzi wa rangi. Huyo Ogondieki angesema ni mafundi mchundo wanaotoka sehemu fulani au wa rangi fulani ndiyo pekee wangepewa nafasi ya kwenda kusoma nje, ningemwita mbaguzi. Nyinyi mngesema wawezeshwe watanzania wote wasio na uwezo bila kujali rangi, dini au jinsia, ningewaunga mkono. Kutanguliza kwenu uzawa au weusi kama kigezo ndiko ninakopinga. Kwa nini mtoto wa Mengi apendelewe kwa sababu tu ni mweusi wakati mtoto wa mvuvi wa kishihiri anyimwe upendeleo kwa sababu tu babu wa babu yake alitokea Yemen?

Halafu unamhukumu kijana wa kiarabu kwa upumbavu wetu wa kuenzi vilivyo vyeupe? Mbona hata katika makabila fulani, mahari inapimwa kutokana na rangi ya binti? Haya ni mapungufu yetu na kamwe hatuwezi kuwalaumu wengine kwa hili. Ndiyo, ni wao ndiyo waliotufundisha kuwa kilicho cheupe ni bora lakini miaka zaidi ya 40 baada ya kuondoka kwao ni lazima tujiulize kwa nini bad tunaona hivyo! Hata hii sera yenu ina muelekeo huo huo. Tunajiona hatuwezi kushindana na walio weupe zaidi bila kupewa upendeleo. Mimi hiki nakipinga kwa nguvu zote. Nimeshindana nao na wengi nimewashinda. Sihitaji nipendelewe ili nijijue kuwa hatupishani kitu. Sihitaji kukubalika na mhindi, methiopia, mwarabu ili nijione kamili kama vile yeye asivyo nihitaji mimi ili kulegitimise uutu wake.

Amandla......

Fundi mchundo,
Naona tupo pamoja ila tumekosana kipengele kidogo sana. Ni kidogo mno hadi kinachekesha kiasi unaweza kusema kuwa HAKIPO. Nikianzia kwa Mwarabu, sijui kama ulisoma habari nzima. Nimesema "sikuhukumu kwa kuwa sikufahamu ulivyo...." Sasa bado wewe wasema mie nimemhukumu? Niliandika hivyo mapema maana nilijua watu watajibu hivi. Pia nimesema Ngozi Nyeupe kwa sisi Wanyamwezi ni deal sana. Hiyo ilikuwa na iko hivyo. Sasa je, tukitaka kuibadili na tuweke somo kwa Mipingo, itakuwa tumefanya ubaguzi?
Nafurahi kuwa unawazidi hao watu darasani. Mungu bariki hata mie wengine nilishawahi wazidi ingawa walikuwa weupe sana au kidogo. Nikafika hatua nikawa nawaona ni wa kawaida. Ila hiyo ilitaka miaka mingi ipite. Tunachotaka ni hawa Mipingo wafungue macho. Ndiyo maana nasema kuwapendelea zaidi ni KIMAWAZO na si kipesa. Ukiwapa pesa kweli watanunua TV za LCD na watundike ukutani.
Kabla ya pesa hazijatoka, wapate kwanza shule. Mmoja kasema hapa kuwa huko misikiti ya Jamatini, hawasali tu, ila misheni zao zote hufanyika hapo. Sisi hatuna Mikisikiti yetu. Wayahudi wana yao, Wazungu wana namna yao. Ili muradi somo linafika. Kuna vitu kama serikali inataka, inaweza kuwa inafanya ingawa havijaandikwa. Kama alivyofanya Ogondieki, hakukuwa na sehemu imeandikwa kuwa hii ni SERA maana form six wangelimshika shati.
Ukimalizia hii ya WEUSI na Wasio a uwezo. Tannzania nafikiri asilimia 95 ya watu masikini saana ni Watz weusi. Hao wengine nafikiri wako kama asilimia 5. Sasa FM, ukifanya aproximation, hao si 100%??? Uandike Watz masikini au uandike Mipingo, watakaokuja hapo ni almost watu walewale. Sema tu Internation wise, ina-sound vizuri WATZ masikini sanaa. Hapa ndipo nasema tunapishana kipoint kidogo sana, ila mengine yote tuko sawa. Hiyo itakuwa kazi ya serikali kujua hiyo SERA waiite ya Weusi au Masikini sana.
 
Affirmative action ya Marekani ni sera ya kibaguzi inayotumika kupunguza mzigo na barriers zinazotokana na ubaguzi usio wazi. Hii ililetwa kutokana na ukweli kuwa walioshika utamu marekani walikuwa ni wanaume wenye rangi nyeupe. Hawa walikuwa na nguvu ya utawala pamoja na wingi wa kura. Sera hii iliwekwa kumpa nafasi yule asiye na rangi au jinsia hizi kuweza kuingiwa katika sehemu ambazo kabla ya hapo asingeweza hata afanye vipi.
Nyerere hakusema elimu bure kwa wazawa bali kwa watanzania. Si dada zako tu bali mabinti kibao wa kiarabu na kihindi nao walipata nafasi ya kusoma ambayo kabla ya hapo walikuwa wakizuiwa na jamii zao. Ni waswahili wangapi ambao hata pamoja na elimu kuwa bure waliamua kuwaozesha binti zao? Wengi tu walifanya hivyo na wanaendelea kufanya hivyo. Hii ndiyo tofauti kubwa kati ya sera zake na hizi zenu za kibaguzi.

Amandla.....

FM,
Hii sera hata mie kwa USA naona imepitwa na Wakati. Tumemuona Powel, Rice na sasa Obama. Ila siyo siri, imeinua wengi sana USA. Unaweza kukataa au kukubali ila huo ndiyo ukweli kama ulivyoandika hapo nimeweka rangi. Hata Tanzania inaweza kuwekwa kwa miaka kadhaa na baadaye ife. Kuna vitu vingine huwa vya mpito na lazima kifanyike kwa muda, na baadaye wakishaamka kundi la matajiri wafanya biashara, mpango unakufa. Hata Tanzania leo shule unalipia. Shida kubwa kwa Watz kwa sasa ni kutokujua kufanya biashara. Wenzetu Wahindi na Waarabu uongo mbaya, hawajambo. Jamani kuwaamsha Weusi kadhaa hiyo ni UBAGUZI? Wacheni hiyo.
Kwanza mwajua ubaguzi ninini? Mmeshauona ubaguzi lakini au mwasikia? Mnafikiri sisi tunasema Mhindi apigwe na Black skinhead? Akae nyuma ya basi, asiruhusiwe kusoma na sisi, tumtenge hadi AKOME!!!! Mhhh, mwaenda mbali nyie watu? Ukitaka kukamua jipu, huu ndiyo ubaguzi positive.
 
Baada ya sera ya kuwawezesha Watanzania weusi...tutalilia sera ya kuwawezesha watanzania maji ya kunde na maalbino. Then sera ya kuwawezesha wanawake weusi...then wazee weusi...then na wanawake na wazee maji ya kunde na maalbino nao watataka kuwezeshwa.

...dhambi ya ubaguzi huwa haifutiki.
 
Mama,
Yesu alisema (samahani kama wee Muislam au ....) kuwa ukiwa na Kondoo mia moja, akapotea mmoja, utawaacha hao 99 na kwenda kumtafuta humo mmoja. Huo nao ni ubaguzi ehh. Hakuna aliyesema kuwa watu wasio weusi wasifanye biashara. Hata kama zitaanzishwa shule za biashara, unaweza kukuta hawa Wahindi hawaendi kwani kwao zitakuwa ni kupoteza muda. Wao wana zao huko Jamatikana na mimi na wewe haturuhusiwi kuingia. Lakini wenzetu hamlioni. Ningependa kwa mfano kuwa kwenye dini yao, je wataniruhusu? Hata kama wanapanga kupindua nchi wala hatutajua. Heri ya Waarabu, utaingia msikitini.
Jifunzeni na nyie kuuma na kupuliza. Siyo kupokea kila kitu kizimakizima. Fumbeni macho tuombee ubaguzi usije Tanzania ........ Amen. Ukifumbua macho, mali zote na biashara zote za Tanzania zimeshikwa na Wageni weupe. Hapo hata Shivji wao hatakusaidia.

Napenda msemo wa MSAFARA WA MAMBA NA KENGE WAMO.
 
US offers GM, Chrysler $13.4-B lifeline

Agence France-Presse
First Posted 05:44:00 12/20/2008

Filed Under: Economy and Business and Finance, Automotive Equipment, World Financial Crisis

WASHINGTON - US officials Friday announced a $13.4-billion rescue loan for two of the Big Three automakers, requiring tough reforms, in a move aimed at staving off an economic calamity.

General Motors and Chrysler, facing a threat of imminent bankruptcy, agreed to the loan terms and will get the funds starting Dec. 29. GM would get $9.4 billion in two tranches through mid-January and Chrysler up to $4 billion on Dec. 29, officials said.

Ford said it would not be part of the loan program, which could include $4 billion more for GM pending congressional action.

"These are not ordinary circumstances," President George W. Bush said in announcing the aid. "In the midst of a crisis and a recession allowing the US auto industry to collapse is not a responsible course of action."

NB: FMes, naona Wamarekani wameamua kusaidia watoto wao wasife. Mcheza kwao hutuzwa. Ila siye hatujui tu hilo. Hapa unafanyika ni Upendeleo tunaosema Tanzania tunauhitaji sana. Tafadhali msiuite UBAGUZI. Heri muuite UAMSHO wa MTU MWEUSI.
 
msilinganishe Affirmative action ya Marekani na sera ya Uzawa ya Iddi Simba.
tofauti yake ni hii, Umasikini wa mtu mweusi Marekani umesababishwa na institutionalized injustice, kwa maana kwamba kabla ya hii affirmative action Taasisi na sheria za Nchi ile zilikuwa zinawapendelea na kuwainua weupe kuliko Weusi, mathalani,kuna wakati katika historia ya Marekani ilikuwa ni kinyume cha sheria kumfundisha mtu mweusi kusoma na kuandika. hata Martin Luther King miaka zaidi ya arobaini iliyopita alisema "we refuse to accept that the bank of justice is bankrupt",hii inaonyesha ni kwa kiasi gani hawa ndugu zetu weusi walikandamizwa na serikali yao.
sasa katika kutibu madhara ya muda mrefu, serikali ya Marekani ikaja na mpango wa affirmative action ili angalau kuwainua weusi ambao mfumo wa ubaguzi uliwakandamiza kwa miaka tele. kwanza hawa weusi walipaswa walipwe fidia kubwa sana kutokana na kutendewa kinyama kipindi kile cha biashara ya watumwa, na pia fidia kubwa kutokana na sheria kandamizi za kuwanyima haki zao za binadamu kama vile elimu.
hivi unafikiri injustice ya miaka 300 inaweza kutibika kwa miaka 40 ya affirmative action?. kiufupi ni kwamba affirmative action kule marekani inabidi iendelee tena kwa muda mrefu.

sasa tukija kwa sera hii ya uzawa ya Iddi Simba,Watanzania weusi hawajawahi kutungiwa sheria ya kubaguliwa na serikali yao, Serikali yao haijawahi kuruhusu Wananchi wake kuuzwa mnadani, Watanzania wasio weusi hawajawahi kushika madaraka na hivyo kuweka mfumo wa kuwakandamiza Watanzania wenzao ambao ni weusi. kwa hiyo kama ni umasikini Watanzania wengi ni masikini bila kujali rangi zao, hivi nyinyi mnadhani kwa sababu wahindi wengi wanakaa kwenye maghorofa pale city Centre kwa hiyo ndo matajiri?. wapo wahindi na waarabu masikini kweli kweli pale Tanzania, sasa hao sera ya "uweusi" itawasaidia vipi?
 
Wengi wetu hatumtetei Idd Simba, na inawezekana sera ya uzawa kama ilivyopendekezwa naye ni tofauti na tunachuunga mkono hapa.

Kuwawezesha wazawa sio lazima kuambatane na kuwabagua Watanzania ambao sio wazawa. Kwani tunapowawezesha kina mama kwa kuhakikisha wanaingia bungeni (kwa kura na kwa kuteuliwa) imebidi tuwabague wakina baba?

Kuwawezesha waliobaki nyuma ni kujenga usawa. Sio kubagua. It is to lend a hand so that they can catch up. Then we can walk together.

Swali basi linakuja: Ziko njia za kuwawezesha wazawa ambazo si za kibaguzi? Zipo. Mfano mmoja niliojadili tayari ni wa kuwarasilimisha mali zao. Wapewe hati miliki za mali walizokalia. (Nikumbushe aliyosema Kawawa miaka ya sabini kwamba "Watanzania utajiri mnao lakini mmeukalia"). Hakuna ubaguzi hapo kwani mali zenyewe ni zao. Wapewe tu kitambulisho cha kisheria cha kuwa na mali hizo.

Ikumbukwe vile vile serikali sio baba wala mama wala mjomba. Kuwawezesha wazawa si kazi ya serikali peke yake. Wale wanaosubiri serikali ije iwashike mkono iwawezeshe watasubiri sana!

Nitoe mfano wa mradi wa kuwawezesha wazawa ambao unafanywa na Kanisa. Kanisa linawawezesha sana wazawa kwa kuwaelimisha. Angalia Bagamoyo. Kuna kampeni kali ya kuwawezesha wazawa Bagamoyo inayofanywa na Kanisa wakati huu. Wameanza kwa kujenga Marian College. Ilipoonekana wazawa wa pale hawapati marks za kutosha kuingia shule hiyo, Kanisa liliamua kujenga shule ya msingi ya kuwatayarisha.

Si vibaya mipango ya kuwawezesha wazawa inapowawezesha wengine vile vile. Tunaposema tuwe na sera kamili za kuwawezesha wazawa hatumaanishi kwamba hakuna mtu mwingine anaruhusiwa kufaidika. Affirmative action ni proper subset ya set ya mipango ya kuwawezesha wazawa. Kuwawezesha wazawa ni zaidi sana ya mfumo wa affirmative action.
 
Kumwezesha huyu haina maana kumbagua yule, huyu yuko pale tayari sasa yule ambaye hajafika awezeshwe ili afike pale. Kumwezesha inaweza ikawa hata kumfundisha namna ya ku"bargain" vizuri bei za mazo yake au mshahara wake, tusiogope hili sana nchi nyigi wanazo lakini hawaziweki "for public consumption" lakini zinafanya kazi.
 
Kila mahali hapakosekani "exceptions" ni wahindi wangapi wanatetea wazawa????????? bila shaka hujachunguza kule majamatini wanafanya nini, ndipo utaona wao wanawezeshana wenyewe, sisemi ni vibaya lakini inakuonyesha haja ya kufanya hivyo. Ndio maana ukimkuta mhindi -mtanzania anaomba leo, kesho utamkuta anafanya kazi fulani kapewa na mhindi mwenzake, kamwezesha tu - HAKUNA UBAYA WOWOTE
 
Je uko tayari kubadili mawazo yako????????????????????????? maana isije ikawa ni ubishi tu badala ya mjadala!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kila mahali hapakosekani "exceptions" ni wahindi wangapi wanatetea wazawa????????? bila shaka hujachunguza kule majamatini wanafanya nini, ndipo utaona wao wanawezeshana wenyewe, sisemi ni vibaya lakini inakuonyesha haja ya kufanya hivyo. Ndio maana ukimkuta mhindi -mtanzania anaomba leo, kesho utamkuta anafanya kazi fulani kapewa na mhindi mwenzake, kamwezesha tu - HAKUNA UBAYA WOWOTE
Kuna watu hapa wanasema itakuwa ni Ubaguzi kwa wa-Tanzania weusi kuwezeshwa ninataka kuwauliza je wa-Hindi watanzania sio wabaguzi? Yaani kwenye mambo yao hawajichanganyi kabisaa, tena afadhali hata waarabu kuliko Wahindi. Ni wanafiki na huwa sizimii watu wanafiki period! (Will that make me a racist? sijui, lakini mtu yeyeto mnafiki huwa simzimii period!.
 
Wajameni wajameni, ingawa mimi sio mtoa mada ila mjadala unaenda halijojo. Unaelekea kule kusiko. Unageuka wabaguzi na wapinga ubaguzi.
Jamani issue ya msingi sio kutunga sheria ya ubaguzi ama utetezi wa wazawa bali sheria imlinde native awe part and parcel ya utajiri wa maliasili iliyomzunguka. Kwanini umfukuze mzawa pale Mwadui/Buzwagi/Mererani n.k eneo hili la asili la mzawa umpe mzungu eti kwa sababu eneo hilo -lina Alimasi/Dhahabu/Tanzanite nk. Kisa eti mzawa hawezi kuchimba hiyo Almasi/Dhahabu/Tanzanite nk. Kwa nini huyo mzawa asingekuwa sehemu ya umiliki na huyo mwekezaji ili na yeye afaidi matokeo ya uwekezaji huo?.

kwa waliofika Afrika Kusini pale Santon Town, utakuta tangazo la The Bigest Tanzanite Shop in the World!. Ndilo duka kubwa kabisa la vito vya Tanzanite duniani and there is no mention ya Tanzania. How do you feel?.

Issue sio ubaguzi ni uwezeshaji.
 
msilinganishe Affirmative action ya Marekani na sera ya Uzawa ya Iddi Simba.
..........!!!!!!!!
......... tukija kwa sera hii ya uzawa ya Iddi Simba,Watanzania weusi hawajawahi kutungiwa sheria ya kubaguliwa na serikali yao, Serikali yao haijawahi kuruhusu Wananchi wake kuuzwa mnadani, Watanzania wasio weusi hawajawahi kushika madaraka na hivyo kuweka mfumo wa kuwakandamiza Watanzania wenzao ambao ni weusi. kwa hiyo kama ni umasikini Watanzania wengi ni masikini bila kujali rangi zao, hivi nyinyi mnadhani kwa sababu wahindi wengi wanakaa kwenye maghorofa pale city Centre kwa hiyo ndo matajiri?. wapo wahindi na waarabu masikini kweli kweli pale Tanzania, sasa hao sera ya "uweusi" itawasaidia vipi?

Si sawa kulinganisha sera za Marekani na za Tanzania kwa sababu hakuna common ground hapo.Marekani si sawa kijamii, kiuchumi au kimaaendelea na Tanzania.
Ni Jambo la kusikitisha kuwa si watu wengi wanaomwelewa Iddi Simba kwa sera za uzawa.Hakuna nchi duniani ambsyo iko wazi kabisa(open) kwa foreighners.
Tofauti ni kuwa hapa kwetu Tanzania mtu (wenzetu walioko Serikalini)anaona fahari kubwa kumwezesha Mzungu , Mhindi wa India , au Pakistan au hata Mwingereza. Ukifuatilia sana utakuta 10% imetembea.
Mimi kwa macho yangu nimeona mtu wa nje akimtukana ofisa mmoja wa umma kwa kumletea kazi ndogo ili afanye.Huyo mtu wa nje akamwabia ofisa huyo kuwa nchini kwetu mtu anaweza kufungwa kwa kuto wapa kipaumbele wananchi wa nchi yake.Kwa aibu afisa wa umma ikabidi akitoe-lakini yeye moyoni akaona amekosa 10%!!!
 
Kuna watu hapa wanasema itakuwa ni Ubaguzi kwa wa-Tanzania weusi kuwezeshwa ninataka kuwauliza je wa-Hindi watanzania sio wabaguzi? Yaani kwenye mambo yao hawajichanganyi kabisaa, tena afadhali hata waarabu kuliko Wahindi. Ni wanafiki na huwa sizimii watu wanafiki period! (Will that make me a racist? sijui, lakini mtu yeyeto mnafiki huwa simzimii period!.

Hakuna mtu anayepinga kuwa kuna wahindi wabaguzi. Kama ilivyo kuna waarabu wabaguzi, wachina wabaguzi, wahaya wabaguzi, wazaramo, wabaguzi, wazungu wabaguzi, watu weusi wabaguzi n.k. Lakini hii haihalashi kuwa na sheria ya kibaguzi kwa vile tuu baadhi yetu ni wabaguzi. Nchi yeyote yenye kuthamini uhuru wa wananchi wake inawapa uhuru wa kuamua nani wachanganyike nae. Uko huru kutompenda mhindi kama vile yeye alivyo huru kutokukupenda! Kinachopingwa ni kumnyima haki yeyote kwa vile tu ni mhindi au mwarabu. Sheria kamwe haiwezi kuondoa wabaguzi lakini inaweza kuzuia ubaguzi.

Wewe kama unawachukia wahindi WOTE kwa kuamini kuwa ni wanafik basi ni mbaguzi. Hauna tofauti na mzungu wa Mississippi anaechukia watu weusi WOTE kwa kuamini kuwa ni hawana akili, majambazi na kucha wanatamani kubaka wanawake zake. Wote ni wabaguzi (racists), period.

Amandla.....
 
Back
Top Bottom