"Samia Bridge" Ndoto inayoishi na itakayokamilishwa na awamu hii ya 6.

Nsennah

JF-Expert Member
Jan 9, 2021
1,560
1,085
Ndoto iliyopitishwa!! Usiku ule nikiwa ndotoni ghafla nikaona madaraja matatu mazuri ambayo ni msaada mkubwa kwa wananchi wote; Nyerere bridge, Busisi bridge na Samia Bridge!! Daraja moja limeanzishwa na kujengwa na Mama mzaliwa wa visiwa vya Zanzibar hadi kukamilika hivyo kwa kuheshimu na kuuthamini mchango wake kwa sauti ya pamoja daraja hilo likaitwa Samia bridge ili akumbukwe kutoka kizazi hadi kizazi. Madaraja mengine yanafahamika lakini daraja la Samia ndiyo ndoto inayoishi. Daraja la Samia linaunganisha kisiwa na ni wilaya ya Ukerewe hadi wilaya ya Bunda. Mbali ya kuwa kivutio kikubwa pia linakuwa msaada mkubwa sana kwa watanzania wa kisiwani humo na watanzania wengine wote kwa kuwarahisishia shughuli za kiuchumi na kijamii ikiwemo matibabu ya watu wa kibara katika hospitali ya rufaa inayojengwa wilayani Ukerewe. Ndoto ya muda mrefu inaenda kutimizwa na Mama huyu shujaa, kwa hakika mama anaifungua nchi ndani na nje ya mipaka ya Tanzania. Nawasalimu kwa jina la Jamhuri, wote mnatakiwa kujibu KAZI IENDELEE. Mungu ibariki Tanzania na Mungu mbariki shujaa huyu wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan katika kutimiza ndoto hii inayoishi.
 
Ndoto iliyopitishwa!! Usiku ule nikiwa ndotoni ghafla nikaona madaraja matatu mazuri ambayo ni msaada mkubwa kwa wananchi wote; Nyerere bridge, Busisi bridge na Samia Bridge!! Daraja moja limeanzishwa na kujengwa na Mama mzaliwa wa visiwa vya Zanzibar hadi kukamilika hivyo kwa kuheshimu na kuuthamini mchango wake kwa sauti ya pamoja daraja hilo likaitwa Samia bridge ili akumbukwe kutoka kizazi hadi kizazi. Madaraja mengine yanafahamika lakini daraja la Samia ndiyo ndoto inayoishi. Daraja la Samia linaunganisha kisiwa na ni wilaya ya Ukerewe hadi wilaya ya Bunda. Mbali ya kuwa kivutio kikubwa pia linakuwa msaada mkubwa sana kwa watanzania wa kisiwani humo na watanzania wengine wote kwa kuwarahisishia shughuli za kiuchumi na kijamii ikiwemo matibabu ya watu wa kibara katika hospitali ya rufaa inayojengwa wilayani Ukerewe. Ndoto ya muda mrefu inaenda kutimizwa na Mama huyu shujaa, kwa hakika mama anaifungua nchi ndani na nje ya mipaka ya Tanzania. Nawasalimu kwa jina la Jamhuri, wote mnatakiwa kujibu KAZI IENDELEE. Mungu ibariki Tanzania na Mungu mbariki shujaa huyu wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan katika kutimiza ndoto hii inayoishi.

Tusitumie maneno kimakosa. Unaelewa maana ya shujaa?
 
Tusitumie maneno kimakosa. Unaelewa maana ya shujaa?
Shujaa ni mtu anayeweza kupambana na hatari yoyote na kuibuka mshindi kama mama Samia anavyopambana na mengi likiwemo la kuiunganisha nchi kufikika kwa urahisi na kukwamua watu kiuchumi. Ni mfano wa ushujaa wake
 
Maliza kwanza la Busisi homeboy sema ndoto nyingine ziko influenced na roho wachafu au misongo kwahiyo jaribu kuomba sana au upate chakula kizuri

Usisahau teuzi mwaka huu hatuna tena
Busisi hilo liko hatua za mwisho ili la Samia bridge lianze
 
Ndoto ni hizi hapa kuwa na njia airport
Screenshot_20231108_141556_Chrome~2.png
 
Hatua za mwisho zipi hizo nguzo zenyewe naona haziishi kila nikipita naona hakuna mabadiliko au wewe mwenzetu unaona tofauti na mimi
Huoni hatua kubwa zimefikiwa aisee?? By 2024 kitu kitazinduliwa
 
Hatua za mwisho zipi hizo nguzo zenyewe naona haziishi kila nikipita naona hakuna mabadiliko au wewe mwenzetu unaona tofauti na mimi
Ona hapo, ulipita miaka gani maana hii ni picha ya oktoba
 

Attachments

  • Screenshot_20231108_172524_Chrome.jpg
    Screenshot_20231108_172524_Chrome.jpg
    68.7 KB · Views: 3
Sina uhakika labda 2026 crane iliyokuwa inaweza zege la juu naona siku hizi imetulia tu nguzo zenyewe kuna ambazo naona bado zinasukwa kwa 2024 kuisha labda wafanye kazi 24/7
Mpaka sasa tunazungumzia zaidi ya 80% ya kazi ishakamilika.
 
Back
Top Bottom