Salva Rweyemamu SIYO Mtanzania(?)

suala ni kama yeye raia au hapana, wanaweza wakawa wamezaliwa el salvador lakini inawezekana yeye akawa mtz pipooooo !
 
I am sure this will be one of the longest threads hapa JF

Nashangaa ES mpaka sasa yuko kimya sijui vipi
 
Mzee mwanakijiji nazipenda makala zako kwenye Kulikoni lazima umlime huyu jamaa wamezidi hawa wanyamulenge. ili tunakuangalia isiwe unamuandama kwasababu ya kumuonea gele kapata cheo na anasifiwa sana kama ni mtu makini wakati wewe hujulikani kabisa. Kwanza jamaa wote wa kule uhayani kule Ngara sio wabongo.
 
Hivi wote humu jamboforums mnaohoji uraia wa watu wengine ambao maisha yao yote wameishi na kuzaliwa Tanzania na nyinyi mmewahi kujiuliza uraia wenu ni wa wapi?
 
Ndugu lazima uelewe kila anayehoji urai wa mwingine ana motivate yake wengine ni kwaajili ya kuwatenga wengine wengine ni kwaajili ya kuharibiana biashara wengine ni kwaajili ya kuharibiana nafasi za siasa wengine ni kutetea maslahi ya nchi na wengine ni gele tu mimi naona mzee mwanakijiji anatetea maslahi ya nchi ila nimemuonya kwamba isije ikawa ni gele tu maanayake Salva siku zote tuko naye lakini baada ya kupata cheo ndio anaulizwa uraia
 
Wasee wa JF,

kuna tofauti gani kati ya hii na shutuma dhidi ya miss bongo 2007??. Naona kuna watu walio simama kidete kupinga ubaguzi dhidi ya yule binti, ktk hili naona wapo upande mwingine na wana hoji kwa nguvu juu ya uraia wa huyu kiumbe...............this is DOUBLE STANDARDS, kwani tofauti ipo wapi?.

Kwanini hatutaki ku-concentrate in real problems facing our country na kujump kwenye vi-issue ambavyo havina msingi wowote???ulikuwepo wapi kusema last week au wakati anampigia debe muungwana kusema haya na una subiri tu pale anapopata ulaji??....naona kama hapa kuna "political character assassins."

Pls, wasee hii ya nani raia au sio raia sio winnable na inapoteza wakati!!!!!!.............my two cents.
 
mbona miye hata sina tatizo.. Bahati nzuri miye sijabadili upande kwenye suala hili. Nilipoliuliza swali hili mara ya kwanza ilikuwa out of logical deduction nikiwa sina sababu yoyote ya kutilia shaka.. that is why ukienda kwenye thread ya kuteuliwa kwake nimempa pongezi zake.

Nilipouliza mara ya kwanza kama ni raia nilikuwa naendeleza wazo la kuhusu Jenerali Ulimwengu kuwa "kama Generali licha ya kushika nafasi zote za serikalini na kwenye chama, lakini baadaye wakauhoji uraia wake na kumlazimisha aombe upya, je hawataweza kumgeuka huyu bwana (Rweyemamu)?" Niliuliza kwa minajili ya hoja tu.

Sasa swali hilo likafutwa ghafla na majibu yaliyofuatia yakafutwa. Hapo ndipo nilipojikuta nimepata udadisi sasa kwamba inakuwaje tusiulize uraia wa ndugu yetu huyu?

Sasa nilipoliformulate swali hili upya kwa kutumia article ya "The East African" nilitaka kuonesha kuwa "siyo ajabu kuwa Tanzania imeruhusu watu wenye uraia nje ya Tanzania kushika nafasi mbalimbali". Sasa tunapouliza kuwa kama huyu naye ni Raia si kwake binafsi, as a matter of fact, kama kuna mtu ana mashaka na Uraia wa Mwamunyange, Kallaghe, au mtu yeyote aliyeteuliwa kushika nafasi yoyote nyeti, ni lazima jibu hilo liwe la uhakika.

Nisingeendelea na mada hii kama mtu mmoja angesema tu.. "Salva alizaliwa mahali fulani, na wazazi wake walizaliwa mahali fulani".

Sasa kwa mujibu wa sheria yetu ya Uraia, Wazazi wako kama walikuwa ni raia wa Tanzania kabla ya Muungano au raia wa Tanganyika au Zanzibar basi watoto wanaozaliwa wanakuwa ni raia. Hata hivyo kama wazazi wako walikuwa na uraia wa nchi nyingine kabla ya Muungano, na wewe ukazaliwa katika Tanzania iliyoungana hauwi raia automatically, siyo kama Marekani ambao ukizaliwa katika eneo lolote la Marekani unakuwa ni raia.

Hivyo, Salva anaweza kabisa kuwa amezaliwa na kukulia Tanzania (kama ilivyokuwa Generali) lakini kama wazazi wake walikuwa hawana uraia wa TAnzania alitakiwa (kwa mujibu wa sheria) kuukana uraia wa wazazi wake alipofikisha miaka 18. Kama ameendelea kuishi na kufanya kazi kama Mtanzania na baadaye ikaja gundulika kuwa hakuwa raia, basi anayo kila sababu ya kuomba uraia wa TAnzania na akikubaliwa ana haki kama Richa Adhia na mtanzania mwingine yoyote yule.

Kwa wale wanaoshangaa inakuwaje niulizie uraia wa Salva wakati nilikuwa nautetea uraia wa Richa jibu ni rahisi. Richa wazazi wake wote wawili walikuwa ni Raia wa Tanganyika, na Raia wa Jamhuri ya Zanzibar kabla ya Muungano.

Sihoji uraia wa Salva ili anyimwe nafasi fulani (kama wabaguzi wetu wa rangi walivyofanya kwenye suala la Richa) ninahoji uraia wake ili astahili nafasi hiyo, kwani kama siyo Raia wa Tanzania kumpa nafasi nyeti Ikulu ni sawa na kuwategemea wale wa kufunzi wa Chuo cha Benki na wale wa Mzumbe ambao kwa miaka nenda rudi na kwa jasho la Watanzania walisomesha na kupewa nafasi mbalimbali hata hivyo Rwanda ilipokuwa imetengamaa, wao wakaacha kazi zao wakarudi kutumikia nchi walizokuwa na utii nazo.

Ndiyo maana Mwalimu alisema msingi wa uraia wowote ni utii kwa nchi.
 
Wewe ulizaliwa wapi na wazazi wako walizaliwa wapi na wana ushahidi wa vyeti vya kuzaliwa?
 
unajua mwanakijiji sasa unaanza kunichefua, ebu angalia ulichokuwa unasema kuhusu richa, hadi ukawa-accuse watu kwa kuwaita "wabaguzi" sasa je wewe tukuite nani ?
 
mbona miye hata sina tatizo.. Bahati nzuri miye sijabadili upande kwenye suala hili. Nilipoliuliza swali hili mara ya kwanza ilikuwa out of logical deduction nikiwa sina sababu yoyote ya kutilia shaka.. that is why ukienda kwenye thread ya kuteuliwa kwake nimempa pongezi zake.

Nilipouliza mara ya kwanza kama ni raia nilikuwa naendeleza wazo la kuhusu Jenerali Ulimwengu kuwa "kama Generali licha ya kushika nafasi zote za serikalini na kwenye chama, lakini baadaye wakauhoji uraia wake na kumlazimisha aombe upya, je hawataweza kumgeuka huyu bwana (Rweyemamu)?" Niliuliza kwa minajili ya hoja tu.

Sasa swali hilo likafutwa ghafla na majibu yaliyofuatia yakafutwa. Hapo ndipo nilipojikuta nimepata udadisi sasa kwamba inakuwaje tusiulize uraia wa ndugu yetu huyu?

Sasa nilipoliformulate swali hili upya kwa kutumia article ya "The East African" nilitaka kuonesha kuwa "siyo ajabu kuwa Tanzania imeruhusu watu wenye uraia nje ya Tanzania kushika nafasi mbalimbali". Sasa tunapouliza kuwa kama huyu naye ni Raia si kwake binafsi, as a matter of fact, kama kuna mtu ana mashaka na Uraia wa Mwamunyange, Kallaghe, au mtu yeyote aliyeteuliwa kushika nafasi yoyote nyeti, ni lazima jibu hilo liwe la uhakika.

Nisingeendelea na mada hii kama mtu mmoja angesema tu.. "Salva alizaliwa mahali fulani, na wazazi wake walizaliwa mahali fulani".

Sasa kwa mujibu wa sheria yetu ya Uraia, Wazazi wako kama walikuwa ni raia wa Tanzania kabla ya Muungano au raia wa Tanganyika au Zanzibar basi watoto wanaozaliwa wanakuwa ni raia. Hata hivyo kama wazazi wako walikuwa na uraia wa nchi nyingine kabla ya Muungano, na wewe ukazaliwa katika Tanzania iliyoungana hauwi raia automatically, siyo kama Marekani ambao ukizaliwa katika eneo lolote la Marekani unakuwa ni raia.

Hivyo, Salva anaweza kabisa kuwa amezaliwa na kukulia Tanzania (kama ilivyokuwa Generali) lakini kama wazazi wake walikuwa hawana uraia wa TAnzania alitakiwa (kwa mujibu wa sheria) kuukana uraia wa wazazi wake alipofikisha miaka 18. Kama ameendelea kuishi na kufanya kazi kama Mtanzania na baadaye ikaja gundulika kuwa hakuwa raia, basi anayo kila sababu ya kuomba uraia wa TAnzania na akikubaliwa ana haki kama Richa Adhia na mtanzania mwingine yoyote yule.

Kwa wale wanaoshangaa inakuwaje niulizie uraia wa Salva wakati nilikuwa nautetea uraia wa Richa jibu ni rahisi. Richa wazazi wake wote wawili walikuwa ni Raia wa Tanganyika, na Raia wa Jamhuri ya Zanzibar kabla ya Muungano.

Sihoji uraia wa Salva ili anyimwe nafasi fulani (kama wabaguzi wetu wa rangi walivyofanya kwenye suala la Richa) ninahoji uraia wake ili astahili nafasi hiyo, kwani kama siyo Raia wa Tanzania kumpa nafasi nyeti Ikulu ni sawa na kuwategemea wale wa kufunzi wa Chuo cha Benki na wale wa Mzumbe ambao kwa miaka nenda rudi na kwa jasho la Watanzania walisomesha na kupewa nafasi mbalimbali hata hivyo Rwanda ilipokuwa imetengamaa, wao wakaacha kazi zao wakarudi kutumikia nchi walizokuwa na utii nazo.

Ndiyo maana Mwalimu alisema msingi wa uraia wowote ni utii kwa nchi.

Mwkjj,

asante sana kwa jibu lako refu na lenye ufafanuzi wa kina.........nimekuelewa vyema na kama kawaida yako sipo disappointed na majibu ulotoa.

Kuna mtu huko juu alisema kwamba mtu/watu wanaleta "yengele" hili kwasababu tu huyu bwana kapata ulaji alopata,kama vile walohoji Richa kuwa miss..........the issue here ni kwamba watu hawa wote wanajulikana ktk midani zao za urembo na uhandishi wa habari respectively. lau kana watu wana matatizo na uraia wao kwanini isiwe kabla ya tukio??? hii ni sawa na kukimbilia kutoa mimba wakati ungeweza kuvaa Soksi au vidonge vya majira!!!!!!!! na hapo ndipo kuna kuwa na tatizo kwa baadhi ya watu, why now!?
 
Ngabu,
hayo ma-vyeti ya kuzaliwa bongo si unaenda tu pale uzazi na vifo una nunua na kuweka mwaka unaotaka wewe kuwa umezaliwa.........jamaa ana point anataka ku-make, tumsubiri tuone ni nini hasa hiyo point. Kwani msee mwkjj anatembea kwenye very thin line inayotenganisha watu wawili wenye tatizo la uraia ktk almost same circumstances.........interesting!!!!!!!
 
Ngabu,
hayo ma-vyeti ya kuzaliwa bongo si unaenda tu pale uzazi na vifo una nunua na kuweka mwaka unaotaka wewe kuwa umezaliwa.........jamaa ana point anataka ku-make, tumsubiri tuone ni nini hasa hiyo point. Kwani msee mwkjj anatembea kwenye very thin line inayotenganisha watu wawili wenye tatizo la uraia ktk almost same circumstances.........interesting!!!!!!!

Hata mimi nina point ninayotaka ku-make...ndio maana nimeuliza hayo maswali niliyouliza...
 
Kichwamaji
Nadhani hapa kinachoonekana ni kuwa dhambi ambayo Salva alimtendea Salim inataka kumtafuna mwenyewe, Salim kimsingi ameondoka kwenye Politics kutokana na mkono wa Salva. Na ukiangalia utakuta si watanzania wengi ambao hawana uraia wa Tanzania. Wapo wachache, lakini wakianza kusumbua wenyeji ndio wanaanza kupekuliwa uraia wao....i hate Salva. Alifanya watanzania tupoteze mtu mzuri, na matokeo yake we now have a bogus government
 
Hivi huyu kampuni yake ya ushauri ya mambo ya habari ilikuwa inashauri nini wakati kampuni yao ya Habari corp iliwashinda na kumwuuzia Rostam.G & S,inasimama Gidioni na Salva au?Vipi hawa watu bado wanamiliki Mwl Jk school?
 
Kichwamaji
Nadhani hapa kinachoonekana ni kuwa dhambi ambayo Salva alimtendea Salim inataka kumtafuna mwenyewe, Salim kimsingi ameondoka kwenye Politics kutokana na mkono wa Salva. Na ukiangalia utakuta si watanzania wengi ambao hawana uraia wa Tanzania. Wapo wachache, lakini wakianza kusumbua wenyeji ndio wanaanza kupekuliwa uraia wao....i hate Salva. Alifanya watanzania tupoteze mtu mzuri, na matokeo yake we now have a bogus government

You are moving too fast.. wale wanaouliza kwanini leo.. wangeuliza kwanini Salim baada ya kuitumikia nchi kwa muda wote huo na kuwa Waziri Mkuu na Katibu Mkuu wa OAU.. aje kuulizwa nasaba yake na utii wake kwa nchi? Kwanini Jenerali Ulimwengu baada ya kuitumikia nchi vizuri kama Mkuu wa Wilaya na Mjumbe wa NEC aje aulizwe uraia wake pale alipoanza kuikosoa serikali? Point yangu ni point ya wao walioiweka there is no cutting line.. kama waliweza kuhoji uhalali wa "mwarabu" kuwa mgombea wa nafasi ya juu ya uongozi katika nchi yetu, iweje leo washtuke watu wanapohoji uhalali wa mtu mdogo kama Salva kupewa nafasi nyeti kama hiyo Ikulu?

Swali, Salva Rweyemamu alizaliwa wapi? na wazazi wake walizaliwa wapi, je ni raia?
 
Back
Top Bottom