Sakata la Uber na Madereva Taxi jijini Dar: Ushauri kwa RC Makonda

Binafsi nasema changamoto walio nayo madereva wa tax nchini ni bei languzi wanazokutajia kama mteja.
Mfano.. Uber kutoka posta to airport ni sh10,000 assuming hakuna foleni wakati tax ya kawaida usipungukiwe elfu 25. So madereva tax wajitathmini kabla ya hilo kwanza.
Duniani ktk nchi zilizoendelea tabia ya madereva wetu hawa hawawezi kufanya kazi kwani wao wamezoea kuvizia wateja kama sehemu huijui driver wa uber anakufikisha bila kukuyumbisha kwenye malipo lakini ikitokea kwa normal tax driver kama ni karibu basi atakuzungusha weee ili ujue ni mbali. Nakumbuka enzi nasoma kutoka njombe mjini hadi njombe sec (njoss) nauli elfu 2 lakini dereva atakuzungusha ilimradi utoe elf10.

Sasa katika hili wenzetu uber wanakaunti distance na time angalia mfano hapo kwa hiyo kwa abiria hakuna tena mda wa kujadili bei.

Pia Usalama. kama umesahau mzigo wako unakuwa salama wakati hizi tax za kawaida unakuwa huna taarifa za gari ulikuwa umepanda iliwemo namba ya dereva.

Kwa ujumla madereva wetu wana shida na wanahitaji kubadilika sana na mfumo wao wa kizamani huo lasivyo dunia itawapita .
... Well said mkuu, but uache ku quote whole text unasumbua Watumiaji wa simu.
 
Kwa nini nilipe shs 20,000 badala ya sh 10,000 kwa sababu tu nataka kulisaidia taifa? Hapa nalisaidia taifa au dereva taxi anayenigonga nauli? Nimelipa Uber shs 14,000 toka airport mpaka Ubungo saa 7 usiku wakati hapo airport taxi wangenichaji shs 40,000!!. Ma taxi drivers waache kulalamika. Ushindani ni bora kwa mtumiaji.
Afu hata issue ya mabasi ya mwendo kasi mi sikuona sababu ya kuondoa daladala za kawaida. Wangeachwa washindane katika kutoa huduma, ingekua poa sana kwetu sisi Wateja.
 
Sioni ubaya wala tatizo la Uber kuwepo nchini.

Na ningependa kuwaona na Lyft nao wakija pia.

Badala ya watu wa teksi kulalamika, ingekuwa vyema wangejiangalia na kuboresha zaidi huduma yao ili iweze kwenda sambamba na maendeleo ya kiteknolojia na hivyo kuweza kushindana na makampuni kama Uber.

Ridesharing ndo habari ya dunia kwa sababu.

So either get with the program or get the hell out.
kumbe we mbebez una upeo mdogo hivyo au kwa kuwa umehongwa hicho ki vits bas huthamini maslahi ya madereva taksi. mbebez wa bongo mna shida sana
 
Mpendwa,

Tuwe tunajitahidi kujiongeza kabla ya kuwa wajuaji wa kuwaelimisha wengine. Unadhani nimekurupuka tu kuandika hili? Aliyekuambia Uber ninsoftware tu ni nani rafiki yangu? Tumia vema hata internet tu itakusaidia kufahamu mambo kwa undani kabla ya kuwaona wenzako washamba
Sio lazima Uber,iondolewe,hata tigo wameanzisha yao inaitwa Twende,Uber inasaidia sana kwanza
1.Usalama wa abiria(kwa vile inabakisha kumbukumbu,ulipanda gari namba gani na Dereva ni Nani)
2.Hata ukisahau kitu ndani ya Taxi hizi,unajuwa ni gari namba gani ulioacha mzigo wako.
3.Wameanzisha ajira Mpya,Madwreva na Wenye Magari ni watanzania,hizo ni ajira za kumwaga.
4.Wameongeza wigo wa kodi za serekali(hapa nimepapenda sana,Hawa ni wabunifu wa kodi)
5.Wengi wa Hawa madereva ni wastaarabu,kuliko Taxi za kawaida,yaonyesha Uber wanawafatulia(ukipeleka malamiko kwa njia ya app.,yao unapata jibu kwa wakati)
Kwa nini mleta mada usilete ubunifu mwingine?Kwa kutumia app.kama kweli ni msomi,_ungeleta app ya sokoni,madukani,kwenye bucha za nyama,matunda,mbogamboga,gari za kubeba bidhaa,kama carry,shule,mahotel,Restaurant,gas za kupikia,mafundi wa Magari,mafundi ujenzi ,hospital nk.Ili mtu akiwahitaji hawa kama wako karibu yako,unamuagiza akuletee bidhaa nyumbani kwako,hata ukiwa uko ofisini au safari.Tuwe wabinifu tusisubiri wengine wabuni,halafu tuwanyang'anye ubunifu wao.
 
kumbe we mbebez una upeo mdogo hivyo au kwa kuwa umehongwa hicho ki vits bas huthamini maslahi ya madereva taksi. mbebez wa bongo mna shida sana
Sio upeo mdogo,_hawa madereva wa Taxi zakawaida,walitutesa sana,kwanza hawapunguzi bei,wanaringa,hata kama una mgonjwa au mzazi,hawajui hilo.
Ukisahau mzigo,ndio basi,humpai tena.
 
Ndugu yangu,

Nipanic kwa lipi? Mjadala na kutoa mawazo? Labda lingine. Nikipanikishwa na majadala na chaki imenishinda

Mimi nimereact kwenye maoni yako kama wewe ulivyoaract kwenye yangu na ni baada ya kuona maoni yako yanajenga hoja nje ya hoja zangu. Ukisoma ujumbe wangu una mambo kama sita ambayo nilidhani wewe na wengine mwaweza kuyaona humo. Ngoja nikusaidie kukuweke summary:

MOJA: Tuna tatizo la ubora wa huduma za Taxi na ni sahihi kabia kutafuta njia za kukabiliana na hili tatizo.

PILI: Pili, pamoja na uwepo wa tatizo hili sio sahihi kuruhusu kampuni za nje kuwekeza kwenye sekta ndogo kama usafiri wa taxi ambazo zinaweza kufanywa na wazawa na kutegemewa na watu wa kipato cha chini (hili nimefananua vema kwenye ujumbe ni kwanini)

TATU: Nchi zote duniani (hasa zilizoendelea) zina sera ya kulinda ajira na biashara za watu wake. Ndio mana nimeuliza unadhani kwa nini wewe machungwa yako na maembe na maziwa huruhusiwi/huwezi kuja kuyauza Ulaya

NNE: Kwa kutumia maarifa haya haya ya uwezekano wa kuboera huduma kwa kutumia teknolojia, tunaweza kufanya hivyo kwa kuboresha usafiri wa Taxi DSM. Kwanza kuonfokana na mfumo wa kienyeji wa kumiliki na kutoa huduma na pili kutumia mifumo itakayosaidia kuongeza ufanisi na kupunguza bei. Hatuhitaji makampuni ya nje kuwekeza kwenye taxi ili tupate akili za kuwa na ushindani.

TANO: Tutumie wataalamu wetu kutengeneza mifumo ya kumanage huduma ya Taxi (na zingine pia) maana tunao na wanaweza. Na tukifanya hivyo tutakua tumefanya zaidi ya kuboresha huduma za usafiri wa taxi

SITA: Viopngozi watumie watafiti/wasomi/wagunduzi wetu kama sehemu ya mikakati yao ya kutafuta suluhisho endelevu la changamoto zetu hilo la Taxi likiwa mojawapo.

Haya nilitegemea yawe wazi kwa mtu aliyesom aujumbe wangu kabla ya kuanza kutoa lugha za sijui siifahamu Uber, sijafanya research, ni mjinga, nk.
We mbwiga ili uuze chakula ni lazima kikaguliwe na mamlaka za unaotaka kuwauzia hicho chakula. Wanalinda afya ya mwananchi wao.

Huoni wanavyochukua vipusa!!
Wanavyochukua madini!!!

Chakula sii mfano sahihi hapa.

Tunakwambia hajanyang'anywa mtu ajira.

Madereva tax wetu (cocabs) wanabei zisizo na uhalisia, na hawalipii kodi thamani ya hela tunazowalipa pundi tuwakodipo.

Tufanyizie mfano:-
Ni nani kanyang'anywa ajira na Uber.
 
unakosea, uber ni mkombozi katika huduma hii ya usafiri, inawezekana na wewe ni mmoja wa madereva tax mnaotaka kunyonya wananchi, ilifikia hatua kupanda taxi si huduma tena ni kama anasa, hatuwezi kuikimbia teknologia, sio wewe wala makonda mtazuia hili...kwani hao madereva wa uber ni wamarekani?si watanzania wenye magari yao?wanapata faida au hawapati?kodi inalipwa au hailipwi?kwanini hao madereva kama wanataka kutoa huduma nafuu wasijiunge na uber kama lengo lao ni kumsaidia mtanzania mwenzao na si kumnyonya?hii ishu ina conflict of interest...kama ukitumia taxi ya wabongo unalipa 30,000 na ukitumia uber unalipa 10,000 ni kipi bora?acheni mambo yenu kutuongezea machungu ya maisha
uber mkombozi sana, sa nyingine unajisikia vibaya unatamani kupanda taxe ila wakikutajia bei unahisi kupona na kwenda kupanda daladala.

lakini kwa uber hauna shaka unamwita anakuja anakupeleka unapokwenda kwa raha na bei nafuu.
 
Sio upeo mdogo,_hawa madereva wa Taxi zakawaida,walitutesa sana,kwanza hawapunguzi bei,wanaringa,hata kama una mgonjwa au mzazi,hawajui hilo.
Ukisahau mzigo,ndio basi,humpai tena.
we nae mbebez tu. hebu soma tena maelezo ya mtoa mada kabla hujajibu kwa haraka kama umemiss dudyu vile
 
Ndugu yangu sihitaji deal lolote na wala sina kampuni ya kuunda mifumo. Sina biashara yoyote hata ya kuuza sambuza wala ya kuendesha baiskeli. Ila ninawajibika kwa nchi yangu kutoa mchango wa mawazo na utaalamu wangu kwa ajili ya manufaa ya watu wake. Mchango wa fikra ndio jukumu kubwa tulilopewa na nchi yetu bila kujali wako wataoana ni za kipuuzi au zina mashiko. Na michango kama hii ya mijadala ni sehemu tu.

Pili michango mingi inayotolewa hapa inaonesha tuna udhaifu mkubwa sana kama jamii. Kwamba mtu hawezi kutoa maoni na ushairi wake juu ya jambo fulani hadi awe na maslahi nalo. Nazidi kumuelewa Rais JPM kwa nini anatuambia nchi ilishabadilishwa kuwa deal maana kila mtu anadhani mwingine anayongea yanatokana na maslahi binafsi. Kwa hiyo tunatakan watu waogope kutoa mawazo yao kwa sababu wataonekena wana maslahi? Ni taifa la watu gani liso na tofauti ya mawazo na mitazamo katika mambo yahusuyo maslahi ya watu wake? Munataka akina Uber tu ndio waje wawasaidie kuwaza na kuwapa solutions za matatizo yetu?

Bado najifunza
Mkuu mimi nimekuelewa sana. Nilikuwa najaribu kuondoa fikra potofu kwamba maslahi yako yameguswa ktk hili suala la Uber. Ndio nikatoa pendekezo kama kuna chembe yeyote ya kukutilia shaka basi ingekuwa ni kuihusisha na taaluma/fani yako. Sasa nilivyoisoma jamii ya wana JF ni kosa kubwa kusifu au kukubali jambo lolote liwe jema au baya toka kwa Paul Makonda au kwa mtu aliemteua nafasi anayoshikilia serikalini. Kama ungeanza kumponda Mh. Makonda na serikali ungepata kuungwa mkono sana na pengine ungegeuka shujaa bila kujali mantiki ya hoja zako na maslahi mapana ya taifa hasa watanzania wa hali ya chini.
Uzuri wa mjadala ni kupingana na kukubaliana acha tupate maoni. Umeanzisha mjadala mzuri wenye kufikirisha hasa kuhusu sera zetu za uwekezaji na jinsi ya kulinda wataalamu wa ndani wakati huo huo uboreshaji wa huduma za kijamii kama usafiri. Tuanzie hapa kupata ufumbuzi na sera za kudumu za jambo husika. Kila siku watu mliopo tasnia ya ualimu wa elimu ya juu mnatukanwa au kulaumiwa hamtoi mchango wenu kutatua changamoto zinazolikabili taifa. Sasa naona umejitosa kuanzisha mjadala huu ni mwanzo mzuri na rahisi kuwafikia walengwa. Pengine ungeandika chapisho flani lingebaki maktaba tu au idarani. Mara chache serikali inaenda kufuatilia machapisho na kuyafanyia kazi. Najua bado chapisho hili sio la kitaaluma kwa maana ya kwamba majibu ya tafiti rasmi lakini bado limesaidia kuweka mezani hoja ya kuijadili. Ahsante kwa mchango wako.
 
Taxi za Dar chafu
Madereva wana lugha chafu
Bei zao kubwa sana

Bora Uber unajua kabisa huibiwi
 
Sioni ubaya wala tatizo la Uber kuwepo nchini.

Na ningependa kuwaona na Lyft nao wakija pia.

Badala ya watu wa teksi kulalamika, ingekuwa vyema wangejiangalia na kuboresha zaidi huduma yao ili iweze kwenda sambamba na maendeleo ya kiteknolojia na hivyo kuweza kushindana na makampuni kama Uber.

Ridesharing ndo habari ya dunia kwa sababu.

So either get with the program or get the hell out.

Noma
 
Hawa madereva wa taxi na wao wajiinge Uber au Twende,hii pia kwa ni Usalama,kwa maana mteja aliyekokodi anajulikana kwenye app.,kwa hiyo watu wabaya hawezi kitumia taxi kwa njia za kihalifu.
 
Mkuu wa mkoa itabidi akae pembeni kwa hili kwani yale teksi bubu lazima zisajiliwe kama gari ya biashara na ipate mkanda wa wilaya yake husika. Mapato kwa serikali hayo mkuu wa mkoa hawezi kuingilia.

Mfanya biashara wa taxi atakuwa mwehu kukata huduma ya Uber ambayo inamletea wateja na harudi tupu! Nimekuwa nawauliza sana madereva wa Uber na wote wanasema mwanzoni ilikuwa ngumu lakini baadaye wamekuja kukubali kwamba its all about number if trips you make na ni afadhalibsana kupita kukaa kituoni kugombania wateja!

Wengi wamesema sasa wanaweza kujipangia kazi kiufasaha zaidi na hata kupunguza masaa ya kufanya kazi. Na ulipwaji wao benki kwa kutumia atm cards wengi wanaufurahia.

Uber ni swala la dog eat dog situation - kama huwezi kuwashinda basi ungana nao! Kwa sasa ndio habari ya jijini, na mpaka hawa wataalamu wetu watoke na competibg solution Uber itabakia kuwa the only viable solution as wote wahusika wanafaidika.

Senti mbili zangu....
 
Jambo jema ni kuwa Mh.Makonda hajatoa maamuzi kwanza ametoa nafasi ya mjadala na mapendekezo ya wadau. Wadau wote watoa huduma na walaji/watumuaji huduma tujenge hoja. Ukweli ni kwamba Uber wamerasimisha mfumo wa biashara ya taxi. Wameondoa changamoto za bei zisizo wiana na umbali, pia wameondoa changamoto ya usalama wa abiria wa taxi na mali zake. Sasa tujikite kuangalia na matokeo hasi ya ujio wa mradi wa Uber kisha tulinganishe kipi kina maslahi kwa wengi. Je dereva taxi wasiotaka kujiunga na Uber wanayo nafasi ya kuanzisha mfumo wao washindane na Uber? Je utakuwa na faida? Je waliojiunga na Uber wanapata faida au hasara. Je taifa kiujumla linapoteza nini au linafaidika na nini?
 
Kama andiko hili ni la Mwalimu tunaempa wadogo zetu awatoe ujinga, sishangai kwanini kila mwaka idadi ya wanafunzi wanaopata zero inaongezeka....


Na walimu wa dizaini hii ndio sababu ya kwanini serikali hailipi deni lenu miaka nenda rudi...



Kutoka Ubungo mpaka mwanza niliwahi kupanda taxi kwa shilingi 25,000 ... Leo kwa umbali huo huo nilipanda uber taxi kwa shilingi 8500/=...... Ni kichaa tu ndio anaweza asione tofauti yoyote hapo....



Mlizoea kula msivyopaswa kula na acheni kulia lia kuweni wabunifu kwenye taxi zenu msitegemee Huruma ya serikali.... Nchini kenya kampuni ya uber wameweka mpaka helicopter , sijaona wanalalamika hovyo hovyo, ila tunaona daladala zao wanavyozifanyia ubunifu .. Wanaweka mpaka WiFi.... Na nyie kuweni wabunifu mwisho wa siku mteja ndio muamuzi wa mwisho kuangalia Huduma bora yenye gharama nafuu...


Ilifikia nauli ya taxi humu humu dar inazidi nauli ya kutoka dar mpaka mtwara... Tuachieni uber kama mnaona hamuwezi kuwa creative kalimeni....
 


Kama andiko hili ni la Mwalimu tunaempa wadogo zetu awatoe ujinga, sishangai kwanini kila mwaka idadi ya wanafunzi wanaopata zero inaongezeka....


Na walimu wa dizaini hii ndio sababu ya kwanini serikali hailipi deni lenu miaka nenda rudi...



Kutoka Ubungo mpaka mwenge niliwahi kupanda taxi kwa shilingi 25,000 ... Leo kwa umbali huo huo nilipanda uber taxi kwa shilingi 8500/=...... Ni kichaa tu ndio anaweza asione tofauti yoyote hapo....



Mlizoea kula msivyopaswa kula na acheni kulia lia kuweni wabunifu kwenye taxi zenu msitegemee Huruma ya serikali.... Nchini kenya kampuni ya uber wameweka mpaka helicopter , sijaona wanalalamika hovyo hovyo, ila tunaona daladala zao wanavyozifanyia ubunifu .. Wanaweka mpaka WiFi.... Na nyie kuweni wabunifu mwisho wa siku mteja ndio muamuzi wa mwisho kuangalia Huduma bora yenye gharama nafuu...


Ilifikia nauli ya taxi humu humu dar inazidi nauli ya kutoka dar mpaka mtwara... Tuachieni uber kama mnaona hamuwezi kuwa creative kalimeni....
 
Mtoa mada una mawazo mazuri lakini nashauri madereva tax wajiunge kwenye Uber hili watuudumie vizuri mfano kutoka Tegeta kwenda Airport ni Tsh 20,000/= mpaka Tsh 27,000/= kwa usafiri wa Uber,Je Tax ya kawaida kutoka Tegeta mpaka Airport si karibu mara mbili ya bei ya Uber.Mawazo yangu hao madereva tax wajiunge na Uber na wakubali ushindani na kubadilika na nashauri Uber wangeingia pia kwenye miji mikubwa kama Mwanza na Arusha.Madereva Tax wanapolalamika wakumbuke hata sisi watumiaji wa Tax tunaumia kwa gharama zao.
 
Back
Top Bottom